Mfanyabiashara Alex Msama akamatwa kwa tuhuma za Utapeli wa Viwanja vya Tsh. Milioni 800

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,383
8,132
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam kwa tuhuma za kutapeli viwanja vinne vya Beatrice Mshumbuzi, vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi milioni 800.

Msama amekabidhiwa kwa polisi leo na Waziri wa Ardhi, Jerry Silaa.

PIA SOMA
- Jerry Silaa: Alex Msama ni tapeli namba 3 wa Viwanja, ajisalimishe

---

Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama Promotion, Alex Msama, anashikiliwa na Polisi jijini hapa.

Kwa mujibu wa video iliyowekwa kwenye mtandao wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC Digital), Msama amekamatwa akiwa ofisini kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa.

Video hiyo inamwonyesha Silaa akiwa ameketi akitoa maelekezo kwa askari Polisi mwenye sare kumkamata Msama.

Silaa amesikika katika video hiyo akiuliza iwapo askari huyo ana pingu akajibiwa zipo chini.

Msama aliyekuwa amevaa fulana yenye mistari na koti lenye rangi ya kaki, ameonekana akiingia na askari kwenye gari dogo lenye rangi nyeusi lililokuwa limeegeshwa nje ya geti la jengo la Wizara ya Ardhi, lililopo Kivukoni jiji hapa.

Mbali na video hiyo, taarifa kutoka kwa watu walio karibu na Msama zimesema amekamatwa leo saa 10.00 jioni.

Mwananchi Digital imemtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro kwa simu, ambayo ilipokewa na msaidizi wake aliyeeleza yuko kikaoni.

Juhudi za kupata taarifa kutoka Jeshi la Polisi zinaendelea.

Ingawa haijawekwa wazi sababu ya kukamatwa kwa Msama, hivi karibuni Waziri Silaa alikaririwa na vyombo vya habari akimuhusisha na utapeli wa ardhi.

Mwananchi
 
3048962_IMG_20211217_181857.jpg
 
Huyu jamaa inaonekana ni tapeli mzoefu sana
Nilishasemaga humu huyu jamaa
Ni mzushi sana...
Kwa wanaomjuwa huyu jamaa
Wala hawahangaiki,dili zake issue zake nyingi ni longolongo
Ukifanya naye jambo kulipa napo
Mtihani!
Pale alipopangaga mgahawa wa food point opposite na bestbite
Napo alitaka kumletea usanii mwenye eneo pale,mama yangu mama naniii---kwenye mkataba
Msama sjui alimchukulia poa yule mama,yule mama alipomuhusisha mme wake mtu ambaye tena yuko kwenye mfumo,alimtoa baru msama pale kama mwizi
Huyu msama anajifanya pekee yake anaijuwa hela
Alafu sasa kwa kujifanya mchamungu 😄

Ova
 
Screenshot_2024-04-19-17-12-22-1.png


Promota wa Muziki wa Injili , ambaye pia ni mlokole Alex Msama , akiwa pia ni Mkurugenzi wa Msama Promotion , amekamatwa na Polisi kwa makosa ya Utapeli wa viwanja

Msama Pia ni kada Maarufu wa CCM na Mgombea wa mara kadhaa wa nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama hicho

Amedakwa leo alipoitikia wito wa Waziri wa Ardhi aliyemraka aripoti ofisini kwake kwa Mahojiano
 
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam kwa tuhuma za kutapeli viwanja vinne vya Beatrice Mshumbuzi, vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi milioni 800.

Msama amekabidhiwa kwa polisi leo na Waziri wa Ardhi, Jerry Silaa.

View attachment 2968425
Waziri Jerry Silaa hongera sana kwa kuweza kumuwajibisha huyu FEDHULI, muuza madawa na mnyang'anyi aliyejificha kwenye kivuli cha muziki wa injili.

Wakati wa Awamu ya 4 watu walimgwaya sana kwa kujifanya kuwa alikuwa karibu na Riziwani Kikwette.
 
Back
Top Bottom