Je, umeshawahi pitia maisha magumu?

Je, umeshawahi pitia maisha magumu?

Kuna watu wanatake advantage hivyo wanajaza thread kwa vihadithi vyao. Huwa najiuliza, kuwa kiongozi ni lazima utoe motivation speech? kwasababu kibaiolojia pale unachocheza nacho ni Adrenalin tu.

Shida ni kwa kila mtu, ila haimaanishi kila shida ni kubwa kuliko ingine. Mimi nimeshawahi kupresent ushuhuda wangu humu jamvini kupitis IDs tofauti na kwa maneno tofauti, kila aliyecomment alihitimisha kuwa mimi ni "Surviver". Inamaanisha shida sio shida kubwa hadti tu pale inapohatarisha uhai wako kwa miaka mingi mfulizo...hivyo wewe utaitwa survivor.

Wengi humu mmezaliws kwenye familia za wazazi wote wa pande mbili, umaskini wa familia yenu uliyopelekea kukuza kwa shida haumaanishi kuwa wewe umepitia shida, unamaanisha umekulia tu kwenye hali duni iliyopelekea iwe vigumu kufanikiwa kwenye mambo mbalimbali ya kawaida kama vile ajira, mahusiano au uchumi.

Tuulizeni tuliopitia shida.
 
Kuna watu wanatake advantage hivyo wanajaza thread kwa vihadithi vyao. Huwa najiuliza, kuwa kiongozi ni lazima utoe motivation speech? kwasababu kibaiolojia pale unachocheza nacho ni Adrenalin tu.

Shida ni kwa kila mtu, ila haimaanishi kila shida ni kubwa kuliko ingine. Mimi nimeshawahi kupresent ushuhuda wangu humu jamvini kupitis IDs tofauti na kwa maneno tofauti, kila aliyecomment alihitimisha kuwa mimi ni "Surviver". Inamaanisha shida sio shida kubwa hadti tu pale inapohatarisha uhai wako kwa miaka mingi mfulizo...hivyo wewe utaitwa survivor.

Wengi humu mmezaliws kwenye familia za wazazi wote wa pande mbili, umaskini wa familia yenu uliyopelekea kukuza kwa shida haumaanishi kuwa wewe umepitia shida, unamaanisha umekulia tu kwenye hali duni iliyopelekea iwe vigumu kufanikiwa kwenye mambo mbalimbali ya kawaida kama vile ajira, mahusiano au uchumi.

Tuulizeni tuliopitia shida.
Nawe umejaza database bure kama hao ulivyowaona wengine, cha msingi ulipaswa kutoa hiyo shida yako tutofautishe na wengine zaidi ya hapo ni wale wale tu!!

Hii thread ni maalum kwa mtu kueleza lile lilimfanya ahisi kapitia magumi (shida) nawe toa yako wacha kudharau ya wenzio!!
 
Mi kuanzia nikiwa mdogo nimepita maisha ya changamoto. Kuna wakati unaweza kulaumu family uliyozaliwa lakini haisaidii chochote.

You cant imagine family ya watu 6 baba, mama na watoto 4 wanaishi kwenye chumba kimoja for almost ten years.

Na kuna kipindi nakumbuka tuliishi na mama for almost 3 years bila baba, acha kabisa aisee masuala ya kula ugali na maharage ya mama ntilie wiki nzima ilikuwa kawaida sana halafu fikiria hapo tupo watoto na mama tu. Achana na mambo ya kula mlo mmoja kwa siku maana ilikuwa kama kawaida.

But here i am, kwa hali ile ya udogoni ya changamoto za maisha nilikuwa nikijituma sana kwenye elimu na haikunitupa mkono japo pia mazingira ya kusoma yalikuwa magumu maana ilikuwa mwendo wa koroboi mpaka natia mguu Chuo Kikuu na nafanya safari ya kwanza kuja Dar.

Hivi sasa nimeshamaliza elimu yangu lakini bado changamoto nakumbana nazo tena kubwa lakini sijafa moyo maana hakuna kigeni si kushinda wala kulala njaa zote nna uzoefu nazo na wala siogopi tena.

Ila kikubwa tu ni kwamba mimi ni mtu nisiyekufa moyo wala kukata tamaa kwa sababu tangu nimalize chuo hadi sasa nimekutana na nnaendelea kukutana na changamoto kubwa mno mno na nikifikiria nilipotoka na maisha niliyoishi ingekuwa ni kukata tamaa nisingefika hapa nilipo japo bado changamoto hazijaisha lakini kadri mda unvooenda mbele "the tough gets going"

Namshukuru tu Mungu kwa mentality na busara aliyonipa maana imekuwa silaha yangu moja kubwa sana kuweza kusurvive mpaka sasa na bado jamii inayonizunguka wananiona mi ni mtu mwenye maisha yangu ya furaha japo ukweli upo moyoni mwangu.
Hakika tunakila sababu za kumshukuru na kumtukuza Mungu... Kinacho mtengeneza mtu mzima ni mapito. Hakuna namna mtu anaweza kua mtu mzima mkomavu pasipo mapito mbalimbali tupitiayo,mtu aliepitia changamoto mbalimbali hawezi fanana na yule ambae bado hajapita

Mtu hawezi kuogelea nje ya maji,ukikuta mtu yeyote anaejua kuendesha baiskeli alijifunzia juu ya baiskeli. Ni mapito na changamoto mbalimbali yanayompa mtu viwango vya juu...

Tushukuru kwa yote,na tunapokua katika hali ngumu tuchukulie hiyo kama fursa ya sisi kusonga mbele....
 
Mimi bado napita changamoto,kuna wakati natamani mshumaa wangu uzime nipumzike,ila yote kheri,maana wote tunapita na yote yatupatayo tutayaacha,
Bwana akujibu siku ya dhiki,jina la Mungu wa Yakobo likuinue. Akupelekee msaada toka patakatifu pake na kukutegemeza toka sayuni

Akujalie kwa kadiri ya haja yamoyo wako,na kuyatimiza mashauri yako yote.... (Zab 20:1-4)
 
Salaam,
MUNGU wetu ni mwema sana, ni MUNGU anayetujali, Kuna kitu kimoja kikubwa katika maisha ambacho nimejifunza ni kutokukata tamaa, Mtu amezaliwa na uwezo mkubwa sana, uwezo wa kufanya kile anachokitaka, uwezo wa kupata kile anachokitaka,Kila unachokitamani au kukitaka kimo ndani yako. Maana yake uwezo ulio ndani yako ni mkubwa sana. Changamoto za maisha zipo, lakini tunashinda na zaidi ya kushinda tukimtumainia yeye aliye juu.
Tumezaliwa kama washindi, unapokata tamaa unaua ile nguvu ya kushinda iliyoko ndani yako, usikate tamaa, haijalishi umezaliwa katika familia gani!! Umepata shida gani??? Wewe ni mshindi, usiihesabu shida uliyoipata jana, wala hali ngumu inayokukuta leo, bali angalia unataka nini kesho. WEWE NI MSHINDI, Barikiwa na kuwa na siku njema.
 
Ndugu, ni vigumu sana kuelewa ninayopitia. Na kile ninachopata baada ya maombi.

Bila kufanya hivi , tayari ningekuwa nimeishajinyonga zamani au kufa.

Last week nilipata attack nikiwa bafuni naoga, nilianguka ghafla...damu zilitoka nyingi sana... ( nakumbuka , mchana yake kuna mtu alinitamkia atanifanya kitu kibaya - jioni nikapatwa na hali hii)
ecc23a8c060db886933b6764fb298519.jpg


Ni watu wachache sana wakianguka bafuni kama nilivyoanguka wanapona. Mara nyingi huwa wanapata stroke au kufa.

Nimenusurika kufa mara nyingi sana Ndugu. Huwezi kunielewa kwa kusoma hapa.

Ndugu pole sana hii mitihani ni yetu sote na naamini Mwenyezi Mungu bado anakupigania dunia ina majaribu mengi sana na hapa ndipo wengi tunafeli ila kama haukati tamaa kuna siku haya yote yatakwisha na utakuwa mshauri mzuri sana kwa watu waliopatwa na matatizo kama yako..Mungu wetu ni mzuri sana endelea kumtumainia.,
 
Nawe umejaza database bure kama hao ulivyowaona wengine, cha msingi ulipaswa kutoa hiyo shida yako tutofautishe na wengine zaidi ya hapo ni wale wale tu!!

Hii thread ni maalum kwa mtu kueleza lile lilimfanya ahisi kapitia magumi (shida) nawe toa yako wacha kudharau ya wenzio!!
wewe ni pumba kwasababu haupingi hoja, ika unataka tu tufikie conclusion. ukitazama andiko langu, sijageneralize lolote...nmekuwa specific, nimetoa hoja.
 
Hakika tunakila sababu za kumshukuru na kumtukuza Mungu... Kinacho mtengeneza mtu mzima ni mapito. Hakuna namna mtu anaweza kua mtu mzima mkomavu pasipo mapito mbalimbali tupitiayo,mtu aliepitia changamoto mbalimbali hawezi fanana na yule ambae bado hajapita

Mtu hawezi kuogelea nje ya maji,ukikuta mtu yeyote anaejua kuendesha baiskeli alijifunzia juu ya baiskeli. Ni mapito na changamoto mbalimbali yanayompa mtu viwango vya juu...

Tushukuru kwa yote,na tunapokua katika hali ngumu tuchukulie hiyo kama fursa ya sisi kusonga mbele....
Yah sure..
 
Salaam,
MUNGU wetu ni mwema sana, ni MUNGU anayetujali, Kuna kitu kimoja kikubwa katika maisha ambacho nimejifunza ni kutokukata tamaa, Mtu amezaliwa na uwezo mkubwa sana, uwezo wa kufanya kile anachokitaka, uwezo wa kupata kile anachokitaka,Kila unachokitamani au kukitaka kimo ndani yako. Maana yake uwezo ulio ndani yako ni mkubwa sana. Changamoto za maisha zipo, lakini tunashinda na zaidi ya kushinda tukimtumainia yeye aliye juu.
Tumezaliwa kama washindi, unapokata tamaa unaua ile nguvu ya kushinda iliyoko ndani yako, usikate tamaa, haijalishi umezaliwa katika familia gani!! Umepata shida gani??? Wewe ni mshindi, usiihesabu shida uliyoipata jana, wala hali ngumu inayokukuta leo, bali angalia unataka nini kesho. WEWE NI MSHINDI, Barikiwa na kuwa na siku njema.
Asante sana.... Maneno hayo yanatia nguvu
 
nimepitia wakat mgumu sana mwaka jana. masomo yangu hayakwenda salama. jkt sikwenda nkaja kuona jina baadae biashara zangu hazikwenda baada ya KUOKOKA NA KUMUEKA MUNGU KAMA MKOMBOZI WA MAISHA YANGU NOW NAKULA BATA NA FURAHA TELE. BINADAMU wabaya sana now naishi kiimani na kwa bahati nziri wabaya wangu nawatambua hata alienifanyia yote mwaka jna ni mke wa ...... wangu. IMANI NA MUNGU ndo msingi wa maisha. kama ni jambo baya litatokea mbelen naliona kama zuri pia naliona maisha yangu yamekua ya furaha sana na yote nlopoteza mwaka jana yanaanza kuja pole pole hap natanga niongeze jitihada zaidi nijiweke karibu na Mungu pia niache Dhambi maana ndo zinazoninyima amani[/QUOTEA
AMINA!
 
Amen sis. It is well with my soul, huu wimbo umekuwa ukitupa matumaini makubwa mnoo. His life is a living testimony

Me nina wimbo huu, kuna mwingine wa Tenzi pia unaitwa "Nipitapo Majaribu"

1. Nipitapo majaribu katikati ya miiba
Ninatosheka kwa kuwa, Unanifikiri

×××Unanifikiri mimi, waniwaza sana
Nahitaji kitu gani, wewe wanitosha

2. Masumbufu ya dunia, yasongayo moyo wangu
Mwisho yananikumbusha, unanifikiri

3. Shida zija au zisije, maisha bora au ya shida
Mwisho yananikumbusha, unanifikiri


Na kuna ule Liseme - Sarah K. Afu Nikimaliza namsikiliza Joel Osteen- Having the right perspective Aaah ni nitalia wee, Nikimaliza hapo nakuwa na hiyo amani daah, nacheka tu
Naupenda ule wa tenzi ,ujaribiwapo usitende dhambi, fululiza kiume, kwa Mungu kutiii.....
 
Bwana akujibu siku ya dhiki,jina la Mungu wa Yakobo likuinue. Akupelekee msaada toka patakatifu pake na kukutegemeza toka sayuni

Akujalie kwa kadiri ya haja yamoyo wako,na kuyatimiza mashauri yako yote.... (Zab 20:1-4)


Amen...mama mchungaji Vale. ha ha haah
 
Hapa nina maanisha kufirisika/kufulia kukosa uhakika wakupata angalau chai kwa siku kutengwa na ndugu. Kukosa kazi muda mrefu, kuugua na watu kukutenga, kukosa kodi ya nyumba/mahali pa kulala, kusingiziwa kwamba hutafuti kazi au kusemwa umelogwa ndugu kusema una laana.Kukatishwa tamaa kwamba Mungu kakuacha,kwamba unasali uongo
kudharauliwa na mambo kama hayo.

Je uliweza vipi kuchomoka katika hali hiyo?
Changamoto zipo,,,,sikua najua kuwa majani ya mnyanya ni mboga,ila nilishawah kula nikiwa mdogo tena ya kuchemsha tu.
Alhamdulillah
 
Back
Top Bottom