Je, umeshawahi pitia maisha magumu?

Je, umeshawahi pitia maisha magumu?

God (YHWH) is good all the times. His Love, Grace and Mercy are Unfailing!!! He is an Awesome & Wonderful Savior. We must become less and He must become greater, forever and always, in Jesus Christ Name!!! Shalom
Amen.
 
JEHOVAH AU MWINGINE?
Anaitwa YHWH au YAHOWAH. Sio vyema kulitamka jina hilo hovyo. Na limetokana na mtiririko huu..

Y ( gods ) YH ( Goddesses) YHW ( Images of God) and YHWH ( Almighty God)

So ukisikia watu wanaabudu JAH utaelewa.

Au YAHWEH utaelewa pia.

Kiufupi, lengo la Mungu ni kutufanya kuwa katika image yake ( YAHWEH ) but hatutakiwi kuabudiwa na watu. Mfano, wakina Paul walipokuwa wakipigiwa magoti na watu baada ya kutenda miujiza walikuwa wakikataa wasifanyiwe hivyo na walisema ' sisi ni wanadamu kama nyie" Muabuduni Mungu peke yake.

Ni Yesu Kristo pekee ambae ni Mkuu kuliko Abraham, Solomon , John etc ndiye aliyefanikiwa kufikia hatua ya YHWH. YESU NI MUNGU. Wengine ni maYahweh
 
Hayo yote uliyoyaandika , ndio nayapitia sasa. Tena yamekuwa kwa muda mrefu sana.

Ilifika mahala nikaenda SCOAN Nigeria kwa PTB Joshua kwa njia ya bara bara ( nilitumia siku 76 kufika)

Nimekuwa kiroho sana. But matatizo yapo pale pale. Na yanazidi kuongezeka mpaka kukimbiwa na watu wa karibu kabisa, uliowasomesha na kuwainua juu.

Wakwe kukuona kama mwehu, mke kukuona hufai , na kuudharau Wokovu wako.

Mara waseme sitaki Kazi, na kwamba nachagua Kazi. Wakwe wanamsisitiza mke wangu aachane na Mimi kuwa nampotezea muda, sina Kazi.

Nakuwa karibu sana na Mungu kila mara. Na ninafunga na kuomba kila mara.

Hii ni sehemu ambayo naitumia kusali mchana na Usiku..., asubuhi mchana jioni.

Usiku kabla ya saa 6 , Then saa 7-8 , na saa 9-10.

Nimetandaza vyeti vyangu vyote kuanzia chini hadi Postgraduate, na mahitaji ya watu wengine.

Natumia muda kuwaombea maadui

f077592e4c5aa05c1d2e35ac99a56ca1.jpg
Mkuu hebu elezea kidogo uliwezaje kwenda Naigeria kwa njia ya barabara?
 
Mkuu hebu elezea kidogo uliwezaje kwenda Naigeria kwa njia ya barabara?
It's a long story. Ni safari inayokutaka ujikane nafsi yako, mke, watoto, familia, jamaa, marafiki na Ndugu zako wote.

Ilikuwa ni safari ya Hatari sana. Nilikutana na maajabu na hatari nyingi sana. Nilishuhudia Uovu mwingi sana.

Nilipita Burundi , Congo, RCA, Cameroon, hadi Lagos Nigeria.

Niliwekwa mahabusu mara kadhaa na kuachiwa. Nililala sehemu za hatari sana. Nilipigwa na baridi za kila namna, jua , mvua, wadudu ..., ilifika wakati nikajiona kama kiuno kimetenguka kwasababu ya kulala chini + kutembea umbali mrefu.

Njaa ilikuwa kitu cha kawaida. Nilipendelea kula matunda katika safari yangu. Hakika Mungu wa ajabu sana... alininusuru na Magonjwa.

Nilijifunza mambo mengi sana njiani ( Rushwa+ Usalama+ Mazingira) na hata baada ya kurudi Tanzania, niliyaweka katika paper na kuyawasilisha kwenye vyombo husika ( Nilijitolea bure , nikachapisha makala na kuzigawa bure kwenye baadhi ya ofisi za mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar) . - KWA AJILI YA MAENDELEO YA TAIFA LETU
 
Nikikumbuka kula mara 1tena ugali na chunvi kukosa hata mavazi ya kubadilisha kusoma kwa tabu hakika kuliongeza bidii yangu ya kuikataa kabisa hali niliyokulia mpaka sasa sifa na utukufu zimwendee mungu pekee alinipigania katika kipindi chote kigumu asante mungu
 
Duuh sina hata cha kuandika sema leo huu wimbo umenikaa sana moyoni. My poor cousin sister has given birth to triplets, unfortunately she lost all her babies. It shall be well with her soul.....by Angel Bernard

1.Nionapo amani kama shwari
Ama nionapo shidaaa
Kwa mambo yote umenijulisha
Ni salama rohoni mwanguuu

CHORUS
Salamaa, rohoniiiii
Ni salama, rohoni mwanguuuu

2. Ingawa shetani alinitesa
Nalijipa moyo kwanii
Kristo Uliuona unyonge wangu
Ulikufa kwa roho yangu
Na dhambi zangu zote, wala si nusu
Ziliwekwa msalabani
Wala sichukui laana yake
Ni salama rohoni mwangu

××××CHORUS

Eeh Bwana himiza
Siku ya kuja
Panda itakapolia
Wala sitoogopa
Ni salama rohoni mwangu
 
Duuh sina hata cha kuandika sema leo huu wimbo umenikaa sana moyoni. My poor cousin sister has given birth to triplets, unfortunately she lost all her babies. It shall be well with her soul.....by Angel Bernard

1.Nionapo amani kama shwari
Ama nionapo shidaaa
Kwa mambo yote umenijulisha
Ni salama rohoni mwanguuu

CHORUS
Salamaa, rohoniiiii
Ni salama, rohoni mwanguuuu

2. Ingawa shetani alinitesa
Nalijipa moyo kwanii
Kristo Uliuona unyonge wangu
Ulikufa kwa roho yangu
Na dhambi zangu zote, wala si nusu
Ziliwekwa msalabani
Wala sichukui laana yake
Ni salama rohoni mwangu

××××CHORUS

Eeh Bwana himiza
Siku ya kuja
Panda itakapolia
Wala sitoogopa
Ni salama rohoni mwangu
Oh dear! Pole sana. Mpe cousin moyo. Siku nilipojua story ya mtunzi wa huu wimbo ndo niliuchukulia kwa namna ya kipekee. Ni wimbo wenye nguvu sana. "It is well with my soul". Nikipatwa na jaribu nikianza ku-panic huu wimbo unanikumbusha jaribu langu si kitu- mtunzi wa huo wimbo alipoteza mali, fedha na watoto wanne, lakini hakufa moyo; akasema ni salama rohoni mwake, na alikuja kupata mali na watoto wengine na ushuhuda wake unatujenga mpaka leo.
 
It's a long story. Ni safari inayokutaka ujikane nafsi yako, mke, watoto, familia, jamaa, marafiki na Ndugu zako wote.

Ilikuwa ni safari ya Hatari sana. Nilikutana na maajabu na hatari nyingi sana. Nilishuhudia Uovu mwingi sana.

Nilipita Burundi , Congo, RCA, Cameroon, hadi Lagos Nigeria.

Niliwekwa mahabusu mara kadhaa na kuachiwa. Nililala sehemu za hatari sana. Nilipigwa na baridi za kila namna, jua , mvua, wadudu ..., ilifika wakati nikajiona kama kiuno kimetenguka kwasababu ya kulala chini + kutembea umbali mrefu.

Njaa ilikuwa kitu cha kawaida. Nilipendelea kula matunda katika safari yangu. Hakika Mungu wa ajabu sana... alininusuru na Magonjwa.

Nilijifunza mambo mengi sana njiani ( Rushwa+ Usalama+ Mazingira) na hata baada ya kurudi Tanzania, niliyaweka katika paper na kuyawasilisha kwenye vyombo husika ( Nilijitolea bure , nikachapisha makala na kuzigawa bure kwenye baadhi ya ofisi za mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar) . - KWA AJILI YA MAENDELEO YA TAIFA LETU
Mkuu unasema ulikamatwa,ilikua nchi gani?na sababu ya msingi hasa ni nini?
 
Mkuu unasema ulikamatwa,ilikua nchi gani?na sababu ya msingi hasa ni nini?
CONGO, RCA, CAMEROON,.. reason; Visa kuexpire + kutokuwa na visa.

Wahusika kila walivyokuwa wakitaka kunipeleka ngazi za juu au mahakamani ili nifungwe jumla au kuwa deported, ; kuna vitu vilikuwa vinatokea , then wananiachia Huru au kunipa wao wenyewe msaada wa ulinzi na escort mpaka wana hakikisha navuka maeneo hatari ( baadhi ). Wakawa wananipa documents za kusafiria za muda ( sikuweza kuzitumia zote katika safari kwani nilikuwa sikaguliwi)

Na kilichonifanya kingine mpaka nikawekwa ndani ni kuomba msaada ; kwasababu ilifika mahala nikawa naenda kujisalimisha mwenyewe baada ya kuelemewa.

Huwa nashangaa sana nikiwaona wa Ethiopia wanaokamatwa Tz na kurushwa ITV. ( Mimi ilikuwa ngumu kuchanganywa na makundi ya watu wengine )
 
It's a long story. Ni safari inayokutaka ujikane nafsi yako, mke, watoto, familia, jamaa, marafiki na Ndugu zako wote.

Ilikuwa ni safari ya Hatari sana. Nilikutana na maajabu na hatari nyingi sana. Nilishuhudia Uovu mwingi sana.

Nilipita Burundi , Congo, RCA, Cameroon, hadi Lagos Nigeria.

Niliwekwa mahabusu mara kadhaa na kuachiwa. Nililala sehemu za hatari sana. Nilipigwa na baridi za kila namna, jua , mvua, wadudu ..., ilifika wakati nikajiona kama kiuno kimetenguka kwasababu ya kulala chini + kutembea umbali mrefu.

Njaa ilikuwa kitu cha kawaida. Nilipendelea kula matunda katika safari yangu. Hakika Mungu wa ajabu sana... alininusuru na Magonjwa.

Nilijifunza mambo mengi sana njiani ( Rushwa+ Usalama+ Mazingira) na hata baada ya kurudi Tanzania, niliyaweka katika paper na kuyawasilisha kwenye vyombo husika ( Nilijitolea bure , nikachapisha makala na kuzigawa bure kwenye baadhi ya ofisi za mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar) . - KWA AJILI YA MAENDELEO YA TAIFA LETU
The Meek, pamoja na upendo wako wa dhati kwa Mungu, una tatizo. Umeelemewa. Spiritual approach haikutoshi. Kuanguka kwako bafuni wala hakuhusiani na vita ya kiroho. Uko depressed. Unaweza kubisha lakini kila unapofunguka unaonyesha dalili za mtu mwenye msongo mkali. Una mkanganyo wa identity, wa lengo la kuishi na mambo mengi. Una potential kubwa sana, lakini usipoangalia inaweza kufukiwa kabla hujaifaidia dunia. Huyo YAHWYE akuwezeshe tu maana pamoja na persecution nyingi alikuwa anafanya kazi na kumtunza mama yake aliyekuwa mjane na kugharamia shughuli zake za kimisionari.
 
Kwa kweli ktk umri wangu mdogo huu nimepitia matatizo magumu mno yasiyotatulika kwa fedha ila kwa uwezo wa Mungu pekee
Miaka ya hivi karibuni hadi sasa nimekuwa nikipitia severe psychological torture na tatizo zaidi ni kukosa walau mtu wa ku share nae ila kwa kumtegemea Mungu pekee naamini atanitetea
 
Umenikumbusha siku nilivyo kuwa nalala kwenye linyumba libovu , basi mbu walikuwa wananitafuna sana , kazi sikuwa nayo pakulala hakuna , hela ya chakula hakuna , basi yaani ilikuwa ni maisha ya utata sana, Mungu alinijalia yaliisha bila hata kuiba cha mtu
 
Oh dear! Pole sana. Mpe cousin moyo. Siku nilipojua story ya mtunzi wa huu wimbo ndo niliuchukulia kwa namna ya kipekee. Ni wimbo wenye nguvu sana. "It is well with my soul". Nikipatwa na jaribu nikianza ku-panic huu wimbo unanikumbusha jaribu langu si kitu- mtunzi wa huo wimbo alipoteza mali, fedha na watoto wanne, lakini hakufa moyo; akasema ni salama rohoni mwake, na alikuja kupata mali na watoto wengine na ushuhuda wake unatujenga mpaka leo.
Amen sis. It is well with my soul, huu wimbo umekuwa ukitupa matumaini makubwa mnoo. His life is a living testimony

Me nina wimbo huu, kuna mwingine wa Tenzi pia unaitwa "Nipitapo Majaribu"

1. Nipitapo majaribu katikati ya miiba
Ninatosheka kwa kuwa, Unanifikiri

×××Unanifikiri mimi, waniwaza sana
Nahitaji kitu gani, wewe wanitosha

2. Masumbufu ya dunia, yasongayo moyo wangu
Mwisho yananikumbusha, unanifikiri

3. Shida zija au zisije, maisha bora au ya shida
Mwisho yananikumbusha, unanifikiri


Na kuna ule Liseme - Sarah K. Afu Nikimaliza namsikiliza Joel Osteen- Having the right perspective Aaah ni nitalia wee, Nikimaliza hapo nakuwa na hiyo amani daah, nacheka tu
 
Kufirisika... kudharauriwa... aisee unajuwaa kuna kipindi kinafika unajikataa... ila sasa ndio wewe na yashakukuta unashindwa kujibadilisha
 
The Meek, pamoja na upendo wako wa dhati kwa Mungu, una tatizo. Umeelemewa. Spiritual approach haikutoshi. Kuanguka kwako bafuni wala hakuhusiani na vita ya kiroho. Uko depressed. Unaweza kubisha lakini kila unapofunguka unaonyesha dalili za mtu mwenye msongo mkali. Una mkanganyo wa identity, wa lengo la kuishi na mambo mengi. Una potential kubwa sana, lakini usipoangalia inaweza kufukiwa kabla hujaifaidia dunia. Huyo YAHWYE akuwezeshe tu maana pamoja na persecution nyingi alikuwa anafanya kazi na kumtunza mama yake aliyekuwa mjane na kugharamia shughuli zake za kimisionari.
Ndugu, nashukuru kwa mawazo yako mazuri. Kiufupi ni kwamba, baadhi ya matukio mengi kabla hayajayokea huwa nayaona.

Mara nyingi sana huwa naomba yaniepuke ... mengine hutoweka kwa huruma za Mungu na mengine hutokea kama nilivyoyaona , lakini baadae nakuwa naelewa kwanini yamenitokea.

Suala la bafuni nililiona , na sikuelewa itakuwa wapi ; Kwasababu kila siku lazima niote ndoto za matukio ya mbele au kuwa na Visions ( Nina diary huwa naziandika kila siku ) .

Hata Yesu walidhani kuwa ana msongo wa Mawazo wakati ule, lakini ukweli ni kwamba mtu yeyote akiwa karibu na Mungu lazima Awe na Sober Mind ( Sober reflection) , aishi a Righteousness life + A Godly life katika Kristo Yesu. Hatua hii si kila mtu anaweza kukuelewa because, what people don't understand they always call names , and what they know they destroy
aeba8ea223fc8040505cc913ad7f471c.jpg
 
Huu uzi umenikumbusha mbali sana!! Usiombe ukafiwa na wazazi ukiwa mdogo alafu uishi na ndugu mwenye roho mbaya na hana huruma! anaweza kukutolea maneno ambayo hayawezi kufutika ktk ubongo wako! sitasahau nikiwa kidato cha pili niliomba ada kabla sijapewa niliambiwa maneno haya(wengine wazae wengine walee) niliumia sana siku ile nililia siku zima,anyway nawashukuru walinisomesha kwa masimango ila nimetoka huko kwa nguvu za Mungu,na sasa ninaishi kwa amani na furaha nikwa na familia yangu na watoto wangu.
 
Duuh sina hata cha kuandika sema leo huu wimbo umenikaa sana moyoni. My poor cousin sister has given birth to triplets, unfortunately she lost all her babies. It shall be well with her soul.....by Angel Bernard

1.Nionapo amani kama shwari
Ama nionapo shidaaa
Kwa mambo yote umenijulisha
Ni salama rohoni mwanguuu

CHORUS
Salamaa, rohoniiiii
Ni salama, rohoni mwanguuuu

2. Ingawa shetani alinitesa
Nalijipa moyo kwanii
Kristo Uliuona unyonge wangu
Ulikufa kwa roho yangu
Na dhambi zangu zote, wala si nusu
Ziliwekwa msalabani
Wala sichukui laana yake
Ni salama rohoni mwangu

××××CHORUS

Eeh Bwana himiza
Siku ya kuja
Panda itakapolia
Wala sitoogopa
Ni salama rohoni mwangu
Mpe pole sana cousin wako. Ana kipindi kigumu sana huyo, tena kwa wanawake inakuwa kumbukumbu ya mda mrefu na ni ngumu kwao kusahau. Kama mumewe hatakuwa karibu kumfariji, ni shida!!
 
Mpe pole sana cousin wako. Ana kipindi kigumu sana huyo, tena kwa wanawake inakuwa kumbukumbu ya mda mrefu na ni ngumu kwao kusahau. Kama mumewe hatakuwa karibu kumfariji, ni shida!!
Haya tunashukuru brod darling. Yani hiyo mimba yenyewe Ilivyomsumbua, hadi akawa anatutania eti harudii tena daah. Mmh Tusiongee sana, tusije tukamkufuru Mungu. Tunamshukuru yeye kwa yote, atampitisha pia katika hili, ingawa kumbukumbu yake daah.
 
Usijaribu kukata tamaa mkuu, hayo ni madogo kuna wengine wana makubwa zaidi. Kaza buti
Haya matatizo niliyopitia na ninayoendelea kuyapitia katika hii miezi ya karibuni, nimegundua kwamba, kufikwa na matatizo ni tatizo ila kukosa mtu wa kushare nae hayo matatizo (hata wa kumhadithia tu) ni tatizo zaidi!

Ila Mungu ndo kila kitu, i ll never lose hope!
 
Back
Top Bottom