JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Mastory ya bey​


Hello my people

Kuna msemo unasema aliwazalo mjinga basi humtokea,hakika hao walio Sema hakika hawajakosea kabisa

Na kuna msemo unasema ukitaka kujua tabia ya mtu basi angalia marafiki zake

Iko hivi hakika mawazo huambukiza au huathiri maisha yetu kwa namna moja au nyingine, ukiwa na marafiki ambao wanawaza kwa mlengo fulani basi maadamu upo nao kwa muda mwingi basi hakika watakuathiri kwa tabia zao

Mawazo yao yatadhihirika katika maongezi yao ya kila siku na mwisho wa siku utaathirika nayo, wakiwa marafiki wema watakuambukiza tabia nzuri, na kinyume chake wakiwa marafiki wenye tabia mbaya watakuathiri kwa tabia mbaya

The same kwa aliwazalo mjinga basi litamtokea,kwasababu mawazo ndio nishati inayo fanikisha kutokea kwa matokeo kadhaa,mfano hatufanyi jambo lolote lile ila huanzia mawazoni kwetu,kwahiyo mawazo ni nishati ambayo inabadilishwa kuwa matendo

Sasa mtu akijiwazia kuwa yeye dhaifu na hawezi kupambania jambo fulani analolitaka basi atapata matokeo hayo hayo ya kuwa dhaifu na kweli hatopata jambo analolitaka

Let me put this way kama mfano,eti home boys kama mnashindwa kuwatongoza wanawake mnao wataka mkikaa kimya na bila kuchukua hatua yoyote,mnadhani mwanamke atakuja mbele yako na kusema hi home boy do you want me?

Jibu hapana, kwahiyo ukiwaza na kuamini wewe ni mtu imara na unajiamini basi hakika utapata kile ambacho unakiamini

Kwahiyo kuwa makini sana na kile unacho kiwaza mara kwa mara,mawazo yako ndio yataendesha mfumo wako wa maisha,ukiwa chanya au positive basi yatakujenga,utajiamini na nothing can stop you, na kinyume chake ukiwa na mawazo hasi au negative yatakufanya uwe weak na usiye jiamini

Kumbuka jinsi uwazavyo na ndivyo huwavyo,think big

Ni hayo tu.
 

Ujumbe wa Leo​


🌞 Ujumbe wa Leo: Mawazo Chanya 🌞

Kila siku mpya ni nafasi ya kuanza upya. Usiruhusu mawazo hasi kukufanya ushindwe kuona uzuri ulio mbele yako. Jifunze kuangalia upande mzuri wa mambo, hata unapokutana na changamoto — kwani ndani ya kila changamoto kuna funzo na nafasi ya kukua.

Kumbuka:
✨ Unachokiwaza, ndicho kinachoelekeza hisia zako.
✨ Hisia zako, ndizo zinazoongoza matendo yako.
✨ Na matendo yako, ndiyo yanayounda maisha yako.

Chagua kufikiri kwa chanya leo — kwa sababu mawazo mazuri yana nguvu ya kubadilisha siku yako, na hatimaye maisha yako. 🌻
 

Quotes of the day​




1. 🌿 “Akili yako ni bustani; mawazo yako ni mbegu. Panda mazuri, uvune mema.” — Methali ya Kiswahili


2. 🌅 “Kila asubuhi ni mwanzo mpya. Unachofanya leo ndicho kitakachoamua kesho yako.” — Buddha (Tafsiri ya Kiswahili)


3. 💫 “Kufikiri kwa chanya si kutarajia mambo mazuri tu yatokee, bali kukubali kuwa kila kinachotokea kina kusudi.” — Mwandishi Asiyejulikana


4. 🌻 “Kaa ukiangalia mwanga wa jua, vivuli vitabaki nyuma yako.” — Walt Whitman (Tafsiri ya Kiswahili)


5. 🌈 “Unachowaza ndicho unachokuwa, unachohisi ndicho unachovutia, na unachowazia ndicho unachoumba.” — Buddha
 

Positive affirmations​




1. 💖 Ninatosha jinsi nilivyo.


2. 🌿 Nina nguvu ya kubadilisha maisha yangu kwa mawazo chanya.


3. 🌞 Kila siku inaleta fursa mpya ya ukuaji na mafanikio.


4. 🌈 Ninachagua kuwa na amani, furaha, na shukrani leo.


5. 🌺 Ninaamini safari yangu, hata pale ninapokutana na changamoto.


6. 💫 Mimi ni nuru; ninang’aa na kuvutia mema maishani mwangu.


7. 🌻 Ninastahili upendo, mafanikio, na furaha.


8. 🌸 Leo, nitaweka mawazo yangu kwenye yale ninayoweza kudhibiti — na kuyaachilia mengine.
 

Leo katika historia​


Hapa ni baadhi ya matukio ya kihistoria yaliyotokea siku kama ya leo — 7 Novemba:

Mnamo mwaka 1916, Jeannette Rankin wa Jimbo la Montana nchini Marekani alichaguliwa kuwa mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya ubunge katika Chama cha Wawakilishi (House of Representatives).

Mnamo 1917, katika nchini Urusi, makundi ya waasi wa Kihisabati (Bolshevik) yalifanikiwa kuichukua serikali ya muda chini ya Vladimir Lenin — tukio lililoashiria mapinduzi makubwa.

Mnamo 1940, daraja la angani la Tacoma Narrows Bridge katika Jimbo la Washington, Marekani lilishindwa na upepo wa kasi na kuanguka — tukio lililofundisha mengi kuhusu ushawishi wa anga kwenye miundo.

Siku hii pia huadhimishwa kama siku ya kitaifa ya International Day of Medical Physics kwa heshima ya ushauri na mchango wa wanasayansi wa fizikia ya matibabu.
 

Mastory ya bey​


hello my people

Sidney wakati huu sasa yupo kwenye wakati mgumu wa kufanya maamuzi Mazito kutoka kuwa producer wa kawaida na kuwa mkuu wa production wa MGM STUDIOS

Hii ni baada ya wadau wa MGM Studios kumtaka awe mkuu wa production,lakini kwa heshima kubwa kabisa alikataa ofa yao hiyo

Akiwa amekumbuka miaka kadhaa iliyopita alipita Studio hizo hizo ambazo zilitamba sana huko miaka 1950's na 1960's akiwa anatafuta kazi ya uandishi wa play na script.



Hapa akajikuta anamkumbuka mlinzi ambaye kila mara alipokuwa anaenda pale Getini na kumwambia natafuta kazi ya uandishi,alikuwa anamuuliza je,unaapointment?

Akajibu sina,basi yule mlinzi bila kupepesa macho alimwambia kama huna appointment basi hutamuona yoyote hapa,lakini leo hii anatakiwa kuwa mkuu wa studio hiyo hiyo ambayo kila mara alizuiwa Getini na mlinzi huyo

Kama haitoshi bwana Sidney akakumbuka jinsi alivyotaka kukatisha uhai wake kwa kunywa mvinyo pamoja na vidonge vya usingizi kama hatua ya kuepuka msongo wa mawazo ulisababishwa kwa ndoto zake kutotimia

Akiwa katika harakati za kutimiza lengo lake la kujiua,wazazi wakiwa hawapo nyumbani pamoja na ndugu zake,akiwa tayar kunywa sumu hiyo mara baba yake akarudi home akiwa amesahau kitu,ndipo akayakuta mazIngira yale.

Akamwwambia kwanini unataka kujiua akasema kila anachotaka kufanya kinafeli hivyo haoni umuhimu wa kuishi,ndipo baba akamwambia ebu twende tutembee uwanjani.

Ndipo alipomwambia mwanawe "mwanangu mbona unataka kukatisha maisha yako mapema wakati kuna page nyingi za maisha hujazifungua,kila page ina mambo yake na namna yake,hakika maisha yana siri kubwa sana na yanashangaza,kwahiyo usikatishe uhai wako kabla hujafungua page nyingi za maisha yako huenda ukapata surprise ambayo hukutarajia"

Na ni kweli kabisa akayambuka haya maneno ya baba yake ambapo leo amekuwa mtu mashuhuri akiwa mwandishi,producer wa studio kubwa kabisa kama MGM STUDIOS kama haitoshi ameteuliwa kuwa head of production ofa ambayo ameikataa.

My people hii ndio siri ya maisha ambayo wengu hatuijui,hakika siri ni ýa Mola wetu mlezi juu ya riziiki yetu na wapi hasa maisha yataelekea au kuishia, haijalishi upo katika hali gani wakati huu,unapitia magumu gani lakini hujamaliza page zote za maisha yako,there are more to come and only dear Lord knows it


Kwahiyo tusikate tamaa let us keep fighting mpaka mwisho wa maisha yetu kwani hatujui kuna neema gani ipo mbele yetu

Ni hayo tu!
 

Mastory ya bey​


Hello my people

Ni saa kumi na mbili na nusu jioni,nusu saa imepita baada ya amri ya kutotembea mida hiyo ikitolewa na nchi ya kusadikika

Mida hiyo ya hatar mwanadada akiwa na mtoto wake wa kiume wakiwa maeneo ya mabondeni,anashtushwa na mkimbio wa kijana wa kiume akielekea uelekeo wao na kuwapita kwa ghafla sana

Wakati huo huo wakati tukio la kijana kukimbia unasikika mlio wa bunduki baada ya kijana yule kukoswa na risasi,hapo mwanadada akapiga ukulele mkubwa sana

Ndipo polisi wakashuka kule bondeni wakijua huenda wameshaua hivyo wakachukue mwili wao

Mara pap wanakutana na mwanadada ambaye anatetemeka kwa hofu kubwa sana huku mwanae wa kiume akimtolea macho mwana usalama yule

Huyu mwanadada alijua amekwisha maana polisi wa nchi ya kusadikika hawana kupepesa macho linapokuja swala la kumwaga damu

To her surprise aliulizwa anafanya nini muda ule wa hatar,akasema ameshinda kutwa nzima na mwanae ndani na hakuwa na hela hivyo jioni ile ndio katumiwa shilingi elfu tano kwakuwa njaa inawauma hivyo akaamua watoke nje ili wakapate chochote

Basi yule afande akatoa shilingi elfu tano na kuwapa yule binti na mwanae na kuwataka wapotee maeneo yale,huyo mwanadada anasema alishindwa hata kusema Asante kutokana na hofu kubwa aliyoipata

Huyu ni mwanadada ambaye anafanya usafi kwenye ofisi yetu,alinisimulia haya maswaibu yake na kuahidi hii jumapili angeenda kanisani kutosa sadaka ya shukrani kwa bwana kwa kumuokoa na dhahama ile

My people hili sio tukio moja yapo mengi ya namna hii ambapo watu walitoka kwa lengo la kwenda dukani tu kupata chochote na kurudi home na kupatwa na umauti

Kuna hadithi moja ya home boy ambaye alishinda kutwa nzima ndani na ilipofika around saa moja akasema aende shop akapate soda na mkate walau apitishe usiku ule kwa kupata mlo huo ndio ikawa siku yake ya mwisho kuwa hai.

Hizi na story nyingine nyingi zinasikitisha sana hawa watu wala hawakuwa na nia ya kuandamana lakini kile kitendo cha kwenda tu kupata mahitaji ile mida hatari ndio ukawa mwisho wa maisha yao

Hakika hakuna aliyewahi kufikiria wala kuamini kwamba ipo siku mmoja nchi yetu ya kusadikika itafikia hapa tulipofikia, tunamuomba Allah atuepushe na hali hii huko siku zijazo

Ni hayo tu!
 
Back
Top Bottom