ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,597
- 21,642
Mastory ya bey
hello my peopleJana nilizungumza na dada zangu,wadogo zangu na wanangu ila leo nazungumza na kaka zangu,wadogo zangu na wanangu
Sisi wanaume tuna ile desturi ya kwenda na mwanamke wako kwa wanao au washikaji zako ili wamthaminishe,yani tuna ile ishu kwa baadhi yetu kwamba unataka upate maoni ya washikaji kuhusu mrembo wako,je anauzika au laa,analipa au laa!
Huu ni utaratibu mbaya sana ambao tuna ufanya,wahenga wanasema Kosea mambo yote lakini sio kuoa, sasa kama tunachagua mke kwa maoni ya washikaji,kama ubora wa mwanamke unaonekana mbele ya washikaji zako, je vipi kuhusu hisia zako na maono yako?
Kama washikaji zako wanamuona mwanamke bora kwa vipimo vya shepu na uzuri,je vipi ni vipaumbele vyako pale unapo mchagua soul mate wako au mke wa maisha yako?
Iko hivi mwisho wa siku ni wewe ndie unayeishi na huyo mwanamke,mambo yakienda Kombo nyumbani kwako,hutawaona washikaji zako wakishea machungu yako,pale utakapo anza kulala kwa style ya mzungu wa nne,tambua washikaji zako wao wanakula chakula cha usiku kwa raha zao pasina shaka yoyote ile
Nataka kusema nini hapa, acha kutafuta approval ya mwanamke yupi ni bora kwako kupitia washikaji zako au wanao wa kijiweni,angalia vipaumbele vyako na standard zako kwa mwanamke ambaye unamuhitaji katika maisha yako
If you ask me ni kigezo gani namba moja kwa mwanamke ambaye anafaa kuwa mke wako,jibu langu ni yule ambaye anakuheshimu na kukusikiliza,na hapo ndio utii unapopatikana,sijui mnanielewa home boys?
SIfa kubwa ya mwanamke ni utii kwa mumewe,anapokuwa mtiifu kwako basi hata heshimu itakuwepo,kwahiyo tafuta sifa hii kwa mwanamke wa maisha yako,utakuja kunishukuru baadae
Hatukatai kuwa na mwanamke mrembo kwa kipimo chako,maana uzuri wa kitu upo machoni mwa mtu lakini usiridhike na mwonekano wa nje tu bali na ndani yake pia,na huo ndio uzuri wa kudumu...sijui mnanielewa home boys?
Hopefully you have heard me loud and clear
Ni hayo tu!