JamiiForums Usiku wa manane
...Hebu ngoja kwanza kijana!, unakwenda wapi?, wapi kitambulidho cha mkaazi, na mbona umelewa?
 
...Na hiyo uliyoshika ni nini?, kijana unavuta bangee!, aroo wewe twende kituoni, haya songaaa!(Paaaah kofi heavy la mgongo).
 
...Kijana hebu changia serikali haraka haraka uendee, huwezi kulewa halafu uniambie eti huna pesaa!, na siku nyingine uwe unachukua uber!, haya potea hapa upesi(Puuuh, buti la ugoko na kwenzi la kisogoni)
 
...Enheh, na nyie wasichana mnafanyanini saa hii, hamjui raia wote wanatakiwa kulala ni jeshi tu ndo tunafaa tuwe macho saivi?
 
...Wewe mweupe mweupe hebu njoo hapa mbele, hebu taja namba yako upesi upesi..au unataka tuzurule wote leo?
 
...0436, Hii kazi ngumu, yaani napishana na walevi tuu na mabaamedi, ila ngoja kuna baro baro mmoja namuona kwa mbali subiri nikamzingue
 
...Aroo kijana mbona umesimama hapa, unasubiri nini?, wewe ni jinsia gani mbona umevaa hereni!, unafanya kazi gani?..nini!? eti boda boda! hiyo iphone umetoa wapi?, nyie ndio vibaka, reo utanieleza vizuri...
 
...Asee, ngoja nifunge lindo..yule baro baro kumbe ni mlinzi mwenzangu sema yeye ni kwa level za nchi, amenionesha kitambulisho chake nimetetemeka!, watu hawalali kuhakikisha wewe unalala, usiku mrefu kuliko mchana!
 
Back
Top Bottom