Hawa ndio askari wetu wenye jukumu la ulinzi wa mali na raia wetu tanzania ,askari anapovishwa uniform za askari hujisahau na kuona wako juu ya kila kitu baadhi ni waadilifu wengine si waadilifu mfano huyu aliyebaka angepaswa atoe msaada kwa msichana huyu na kumuonyesha njia badala yake amembaka ,hapa utaona taswira ya askari wasiowaadilifu walivyo na hulka za ajabu ,kutumia uaskari kama utambulisho na kujipatia mali au chochote ni kosa kubwa sana ,mfano wewe ni askari wa barabarani mshahara wako unafahamika kutokana na kukosa maadili ya kazi baada ya miaka 5 ana nyumba ,gari ,vimada ,hili ni kosa umetumia dhamani uliyopewa na serikalli kulinda mali na raia kujipatia fedha isivyo halali unastahili upelekwe mahakamani ujielleze kwanini usifukuzwe kazi,,na serikali inayojali utawala bora lazima ione hili ni tatizo na kuchukua hatua zinazostahiki ,,askari hawa wa aina hii tunao wengi ni wakati sasa wa kuona haya na serikali ichukue hatua madhubuti kwa askari yeyote aliyekiuka maadili na uadlifu wa kazi ya uaskari .mkoa wa arusha uwe wa mfano kwa tanzania yote .maadili yameporoka sana tuamke tukomeshe tabia hii na kwa kufanya hivi rushwa tutakuwa na uwezo mkubwa wa kupambana nayo .haihitaji ushahidi kuona hali halisi angalia maisha halisi ya baadhi ya askari hayalingani na utumishi wa serikali wanaoitumikia ,angalia trafiki wanatumia gari zao na kujazana humu na kutafuta njia panda na kuegesha gari pembeni ,hapa masurufu yatakayokusanywa kwanza watamjali aliyewabeba kwaleta pale ,pili watajiangalia wao ,tatu kama chenji zimebaki watawasilisha kituoni,.Huu si utaratibu mzuri wa serikali wa kukusanya pesa barabarani,unalea tabia ya rushwa .