chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 12,009
- 20,684
Watu kadhaa waliondoka nchini kusalimisha maisha yao, na wamekuwa na hofu kwamba watu waliowasababishia madhila hawajachukuliwa hatua, wako mtaani, na wamekuwa wakitoa wito wa kuhakikishiwa usalama ili warudi.
Baada ya kumwaga maji mengi kwenye shimo la nguchiro, hewa imekata, nguchiro mmoja kaamua isiwe tabu, akaibuka kutoka shimoni na kusema "wasaidizi" wa JPM wanalengwa, kwanza najiuliza, Kuna wasaidizi wa JPM zaidi ya mama Samia na Majaliwa? Yeye "alimsaidia" nini hasa? Na anasema Kuna tetesi kwamba, kupitia "usaidizi" aliotoa kwa JPM, anaweza kufikishwa mahakamani.
Ni "Msaidizi" huyu pekee ambaye alikuwa anazunguka na kikosi Cha watu wenye silaha, na mmoja kati anayehofu kurudi nchini, alishambuliwa na kikosi Cha watu wenye silaha, ni huyu ndugu ambaye, japo alivamia kituo Cha redio na kikosi Cha watu wenye silaha, hakuchukuliwa, hatua, na pia kikosi Cha wenye silaha kilichofurumusha marisasi pale dodoma hakijachukuliwa hatua. Je imetokea tu kwa bahati kikosi hakichukuliwi hatua mara mbili?.
Kwa nini ana hofu?
Baada ya kumwaga maji mengi kwenye shimo la nguchiro, hewa imekata, nguchiro mmoja kaamua isiwe tabu, akaibuka kutoka shimoni na kusema "wasaidizi" wa JPM wanalengwa, kwanza najiuliza, Kuna wasaidizi wa JPM zaidi ya mama Samia na Majaliwa? Yeye "alimsaidia" nini hasa? Na anasema Kuna tetesi kwamba, kupitia "usaidizi" aliotoa kwa JPM, anaweza kufikishwa mahakamani.
Ni "Msaidizi" huyu pekee ambaye alikuwa anazunguka na kikosi Cha watu wenye silaha, na mmoja kati anayehofu kurudi nchini, alishambuliwa na kikosi Cha watu wenye silaha, ni huyu ndugu ambaye, japo alivamia kituo Cha redio na kikosi Cha watu wenye silaha, hakuchukuliwa, hatua, na pia kikosi Cha wenye silaha kilichofurumusha marisasi pale dodoma hakijachukuliwa hatua. Je imetokea tu kwa bahati kikosi hakichukuliwi hatua mara mbili?.
Kwa nini ana hofu?