In Edward Lowassa, I trust...

In Edward Lowassa, I trust...

naungana na wewe wakikusulubu wewe na mimi wanisulubu..EL ni kiongozi shupavu sana...ni shupavu .yes i said it
sina hakika kama ni watanzania ninyi, maana mnaonesha watu wenye matatizo ya kusoma alama za nyakati, haiwezekani nchi yenye idadi zaidi ya watu 37 milion, jumlisha na wasiyojitambua imtegemee mtu mmoja tena mwenye tabia za unyonyaji? mna lenu kama mmetumwa, hamjatukuta, au mmepandwa na pepo????
 
Kutokana na malalamiko kuwa nchi hii haiendi, tunahitaji kiongozi mwajibikaji, decision taker and hardworking. Na jibu letu ni Eddy Lowassa in 2015!.
Kwanini anafaa:
1. ni mchapa kazi. yeye ndo amesimamia mpango wa ujenzi wa madarasa na shughli nyingi za maendeleo wakati JK akipasua anga.
2. Ni mtu ambaye anayesimamia kazi kwa karibu na ambaye hachelei kuchukua maamuzi iwapo anaoa watu wanaboronga.
3. Amesoma vizuri and he is still energetic.

Sasa watu watasema eti ni fisadi, amejilimbikizia mali, etc. Lakini kiongozi gani ambaye ni 100% perfect? Tuchukue mfano wa Ge. Paul Kagame ambaye wengi wanamsifia kwenye JF. Huyu raisi anapenda vita na amesababisha maafa Congo, etc. Lakini licha ya upungufu wake wa Human Rights na kupigana vita, anaendesha nchi vizuri na nchi inapiga hatua.
Kwahiyo tumchukulie Lowassa kama Kagame, wote ni watu wanaochapa kazi licha ya kwamba wana mapungufu. Na tukitaka kiongozi wa kutupa new push, we have to look beyond personal weaknesses.
Good ideas
Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu na mpenda nchi yake na pia mwenye kuona mbali , suala la kumhitaji Lowasa halipingiki kabisa.Angalia kazi aliyoifanya kipindi cha JK, nadhani hahitaji kupiga kelele ifano ipo hai na inajieleza kabisa.Worse enough kipindi huyo mkuu ameachia ngazi, kuna baadhi ya viongozi walifanya sherehe, je huoni kuwa kipindi chake walikalia kuti kavu, ilikuwa ni maendeleo kwa mbele. leo hii utasikia mara kijiji kimekataa kuchangia maendeleo, maana hivi.
Kwa nchi yetu bado Lowasa anahitajika sana zaidi ya unavyoweza kufikiria.
 
Good ideas
Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu na mpenda nchi yake na pia mwenye kuona mbali , suala la kumhitaji Lowasa halipingiki kabisa.Angalia kazi aliyoifanya kipindi cha JK, nadhani hahitaji kupiga kelele ifano ipo hai na inajieleza kabisa.Worse enough kipindi huyo mkuu ameachia ngazi, kuna baadhi ya viongozi walifanya sherehe, je huoni kuwa kipindi chake walikalia kuti kavu, ilikuwa ni maendeleo kwa mbele. leo hii utasikia mara kijiji kimekataa kuchangia maendeleo, maana hivi.
Kwa nchi yetu bado Lowasa anahitajika sana zaidi ya unavyoweza kufikiria.

Nilitegemea mtu kama wewe kuwa na mtizamo wa maana kuhusu nchi...hii uwezo mdogo wa kufikiri na kuweza kutype ofisini.Sikutegemea kama ungeweza kuandika haya bila kuweka mifano mitatu minne..unaishia na hoja juu juu..kweli home of great thinker wewe haupo,.
 
Tunamuhitaji afanye nini? K@#$$%%^^&^&*()((**&&&^^^%%%$$o. Tunamuombea apumzike kwa amani nyumbani kwake. HATUMTAKI. Halafu jamani angalieni mada za kututumia hapa we Ruta kuwa serious infact we don't want kumwona because of all the bad things ametufanyia sisi kama Tanzanian citizens.You know bwana some of us have already confessed our chuki na uchungu kwa mafisadi so when you keep on unarudiarudia kuwaintatein hawa jamaa I can't undaerstand you. Huyu Lowassa ni KUNYONGWA TU. in other words he must be hunged. Shwaini!
 
Kutokana na malalamiko kuwa nchi hii haiendi, tunahitaji kiongozi mwajibikaji, decision taker and hardworking. Na jibu letu ni Eddy Lowassa in 2015!.
Kwanini anafaa:
1. ni mchapa kazi. yeye ndo amesimamia mpango wa ujenzi wa madarasa na shughli nyingi za maendeleo wakati JK akipasua anga.
2. Ni mtu ambaye anayesimamia kazi kwa karibu na ambaye hachelei kuchukua maamuzi iwapo anaoa watu wanaboronga.
3. Amesoma vizuri and he is still energetic.

Sasa watu watasema eti ni fisadi, amejilimbikizia mali, etc. Lakini kiongozi gani ambaye ni 100% perfect? Tuchukue mfano wa Ge. Paul Kagame ambaye wengi wanamsifia kwenye JF. Huyu raisi anapenda vita na amesababisha maafa Congo, etc. Lakini licha ya upungufu wake wa Human Rights na kupigana vita, anaendesha nchi vizuri na nchi inapiga hatua.
Kwahiyo tumchukulie Lowassa kama Kagame, wote ni watu wanaochapa kazi licha ya kwamba wana mapungufu. Na tukitaka kiongozi wa kutupa new push, we have to look beyond personal weaknesses.

Kuwa mchapakazi na msimamizi mzuri kutakuwa na manufaa endapo maamuzi yanayotangulia kabla yatakuwa na mantiki na yenye maslahi kwa wote (umma). Sasa huyu mtu wangu, yaani anaamua kuiingiza nchi kwenye gharama ya kuwalipa watu wachache wanufaike chini ya Mradi wa RICHMONDULI atatufaa kivipi? Uzalendo siyo tu kuwa mzimamizi na mchapakazi, je, unachapa kazi zipi? Kwa ajili ya nani? Na kazi hizo ni vipaumbele vya nani? Watanzania kwenye giza mwaka 2006 walihitaji umeme na ndugu huyu kwa nguvu zake na uchapakazi wake akajibidisha kusimamia na kuhakikisha vimemo vyake vimefanikisha adhima mradi wa kuzalisha umeme wa dharula wanapewa hawa RICHMONDULI. Utasemaje awatufaa watanzania?

Tunahitaji mtu anayejua matatizo ya watanzania, na namna ya kuyapunguza kwa kuweka vipaumbele vyenye masilahi hayo. Sifa za kusimamia na kutekeleza ni za watanzania wenyewe. Tanzania inakosa watu wa kutoa maamuzi makubwa, maamuzi ya kubadilisha maisha yetu kuwa maisha ya neema kwa kutumia rasilimali zetu tulizopewa na Mungu.

Huyu mtu hawezi kufananishwa na Eddy Lowassa hata kidogo. Maana huyu jamaa, kwa uzoefu wangu mdogo tangu nimfahamu ni mkurupukaji. Tanzania inahitaji watoa maamuzi yanayotokana na tafiti za kisayansi. Tofauti na hapo, tutazidi kuendelea kuimba wimbo wa nani awe rais hadi mwisho wa kizazi chetu na vingine vitakavyofuata.

Tunahitaji mtu anayesitahili kuitwa kiongozi. Nafikiri wana JF mtanielewa nikitumia nili neno "KIONGOZI" maana lina maana yake halisi. Kuwaongoza watu kutoka sehemu fulani kuwafikisha sehemu ya pili. Hivyo, kututoa kwenye umasikini kwa kutumia silaha ya maamuzi sahihi ili kutupeleka sehemu ya pili ambayo ni maendeleo.

Eddy Lowassa hata huwezi tu ukamlingalisha na Kagame kiutendaji. Nakushauri mtake radhi bwana Kagame ndugu yangu kumfananisha na Eddy Lowassa.
 
Lowasa kajenga shule za kata sawa. Pinda naye anasimamia Kilimo Kwanza. Hatuli madarasa. Lakini kilimo kwanza tutapata msosi halafu nyingine tunauza ili tuwanunulie watoto wetu uniforms za shule ambazo wataenda kusoma huko kwenye kata ambazo zilijengwa na Lowasa. SO?
Tunahitaji maamuzi yanayozingatia vipaumbele sahihi vya kuwaondolea watanzania umaskini. Hivyo, kilimo kwanza ni mojawapo wa maamuzi sahihi kama utasimamiwa vizuri. Angekuwa LE maamuzi yake yangesukumwa kwanza na nini nitakipata mimi binafsi kwa kutekeleza hilo? Sasa huyu utamuongelea tena kuwaongoza watu kuwatoa kwenye umasikini? Aibu sisi kama tunashindwa hata kung'amua nani anatufaa kututoa hapa shimoni.

Bidii za EL ni penye masilahi binafsi, kujitangaza kwa umma kwa kutaka kujionyesha kinafiki ndiyo maana maamuzi yake yote aliyowahi kuyafanya makubwa yalikuwa ya kukurupuka kabisa ili umma umuone anavyochapa kazi. Je, unachapa kazi hiyo kwa ajili ya nani? Je, ni wakati mwafaka kuchapa kati kwa kusimamia hilo liunalolipigania ama kuna mengine umeyaacha nyumba ambayo yalitakiwa yatangulie kwanza kabla ya hilo unalolitekeleza leo? Lowassa jamani hafai!!
 
Tunahitaji maamuzi yanayozingatia vipaumbele sahihi vya kuwaondolea watanzania umaskini. Hivyo, kilimo kwanza ni mojawapo wa maamuzi sahihi kama utasimamiwa vizuri. Angekuwa LE maamuzi yake yangesukumwa kwanza na nini nitakipata mimi binafsi kwa kutekeleza hilo? Sasa huyu utamuongelea tena kuwaongoza watu kuwatoa kwenye umasikini? Aibu sisi kama tunashindwa hata kung'amua nani anatufaa kututoa hapa shimoni.

Bidii za EL ni penye masilahi binafsi, kujitangaza kwa umma kwa kutaka kujionyesha kinafiki ndiyo maana maamuzi yake yote aliyowahi kuyafanya makubwa yalikuwa ya kukurupuka kabisa ili umma umuone anavyochapa kazi. Je, unachapa kazi hiyo kwa ajili ya nani? Je, ni wakati mwafaka kuchapa kati kwa kusimamia hilo liunalolipigania ama kuna mengine umeyaacha nyumba ambayo yalitakiwa yatangulie kwanza kabla ya hilo unalolitekeleza leo? Lowassa jamani hafai!!

Hakuna cha kilimo kwanza wala kilimo mbili wote hao ni wababaishaji tu heri ya EL mara kumi tatizo lake lilikuwa ni chenji tu haimpiti mbali

JK wakati anaingia alikuwa na ambition njema tu ila masikini hakujua waliokuwa wanampamba na kumpigia kampeni ndio wabaya wake akaja kugundua too late amezungukwa na wana mtandao kumwondoa EL pekee hakukutosha

Tanzania ya leo inahitaji kiongozi dikteta kama Mseveni maana hata tukipata kiongozi mzuri kiasi gani kama malaika kwa system tuliyo nayo atalazimika ku spin kwenye same orbit na kufanya madudu yale yale
 
Balozi%2B128.jpg


- Huyoooo mzee wa Richomonduli!

Respect.


FMEs!
 
naungana na wewe wakikusulubu wewe na mimi wanisulubu..EL ni kiongozi shupavu sana...ni shupavu .yes i said it
Unanikumbusha Sophia Simba (aka Nasma Hamis) alivyosema "Hakuna mwanaume kama Lowasa" hahahhhaaa
 
Lowasa anahitajika kwenye nchi ilio na sheria zinazofanya kazi. Nchi yetu hii yenye watendaji wenye nidhamu za woga, hawamuwezi.

Ni kweli ni mchapa kazi, anaonekana kufikia malengo ya kazi anazopewa, anaonekana si mwoga wa maamuzi na kuyasimamia.

Pia anajulikana kwa kuwa na mahusiano yasiofuata sheria (bubu) za nchi yetu.

Je atakapoanza kufanya madude yake kama yuleeee tutafanyaje? Tutaendelea kuandika humu JF weeee, na yule akisema JF isionekane wenye nidhamu za woga wote watatoka humu.

Mi hata sijafanya uamuzi kama namtaka au la, ila najua wenye nchi yao wakiamua kumuweka watamuweka tu. Wakiamua kutokumuweka hata nimtakeje hatawekwa!

Ninahisi nataka kuacha kuwa passionate kwenye siasa za kitanzania, zinachosha sana.
 
Kwangu mimi ishu si kama Lowassa anafaa au hafai. Muhimu kwangu ni je, tukishampa madaraka tutaweza kuhakikisha anaweka maslahi ya waTanzania mbele? Tutaweza kumrudisha kwenye mstari akianza kuboronga? Tutaweza kumtoa madarakani akionesha dhahiri kwamba kazi imemshinda??

Vivyo hivyo kwa wote wanaotaka nafasi yoyote ya uongozi ndani ya nchi yetu.

Itabidi tufike mahali tuache ushabiki wa kijinga, tuwe makini na tuanze kuwajibishana. Ebo!!
 
ni mtawala , siyo kiongozi.......tatizo kubwa litakuwa kila kitu kitaingia 'kwa mufuko wake'
 
Ndani ya serikali yao kuwa naye yeye (EL) ni bora zaidii kulikoo waliokaliaa nafasii hizoo kwa sasa. Pamoja na mapungufu yake bado ni kiongozi imara na mtendajii..
 
mkuu uwe unafikiria kabla ya kutoa mada kama hii, hii nchi licha ya kuhitaji mtu mchapakazi lakini kikubwa katika uongozi ni uadilifu, na huwezi kuwa mtendaji mzuri bila kuwa muadilifu na katika hilo EL hatufai watanzania
Uadilifu unaanzia ndani na nakuambia hata Marehemu Nyerere hakuwa muadilifu 100% kwa sababu hakuheshimu haki za binadamu, watu wengi walikuwa kwenye vifungo vya ndani, wengine walipotea tu na wengine pia walilimbikizia mali, watu wengi walikufa wakati wa kuanzisha vijiji, kesi nyingi kama sio zote za ardhi imetokana na sera ya vijiji, n.k. kuna vitu vingi lukuki. Lakini ukimwangalia yeye na wengine waliofuata alikuwa better off. Kwa EL, it is the same, he can perform, he can decide, he can make difficult decision, he can follow through, he can execute!! We need a leader who can do all this, who can dare to say even if he becomes indifferent with other leaders!! Surely we need someone like EL or we need him.
Hata wengi mnaondika na kuchangia hapa siyo waadilifu. Uadilifu hauanzi ukiwa kwenye madaraka ya juu, hata hayo madongo uliyonayo sasa je wewe ni mwadilifu? hujawahi kuidanganya uhusiano wake na mwenzi wako? hujawahi kumwibia mwajiri wako muda? hujawahi kusupply kwa super profit kwa Watanzania wenzako through serikali, au watu na makampuni binafsi? kuna vitu vingi sana. Na sisi sote hakuna hata muadilifu hata mmoja, ni kama vile msengenyaji anavyojifanya hana dhambi kwa kuwa hajazini au hajaiba, etc.....!!!!
 
TK,

Kigongo chao ni maadili-Richmond,PTL,KIWIRA,EPA,TANGOLD,DEEPGREEN.THAI RAINS, ULAGHAI,BUZWAGI,MINING CONTRACTS---,Sasa wapimeni,oh bado-kuuza silaha DRC,Pembe za ndovu Vietnam,on and on.Sema tukusikie!!!!
 
I thought we were supposed to talk about getting him out of Parliament and not thinking of him coming back to ministries, leave alone presidency. Ni vizuri kama tukiwa tunapiga hatua, na kutafuta mtu anayeweza kutusaidia kuendeleza nchi kuliko anayeota kujiendeleza mwenyewe.
 
Rev. Hapo nipo pamoja na wewe

Let us call a spade a spade and not a big spoon. Jamaa ni mtendaji mzuri, oh jamaa jambazi, mara fisadi who can prove that?

Haya report ya richmond ndio hiyo jana imezikwa rasmi. Nani aliweza kusimamia kidete isipokuwa Dr. Slaa and Ole Sendaka, wengine kimya from Mwakyembe and his fellows. This means the guy is perfect. Let him be our president.
 
Ndani ya serikali yao kuwa naye yeye (EL) ni bora zaidii kulikoo waliokaliaa nafasii hizoo kwa sasa. Pamoja na mapungufu yake bado ni kiongozi imara na mtendajii..
Kwa nini tusiseme tu kuwa hiyo serikali ya JK haifai kuliko kuikubali endapo tu itakuwa na mla rushwa In Chief? Tamaa yetu ya maendeleo isitufanye tukawakubali wala rushwa kwa vile tu wana baadhi ya sifa zilizo bora kuliko waliopo. Tukifanya hivyo, hiyo tabia itatuzoea. Ndani ya CCM kuna wazuri na bora wengi, wapewe nafasi badala ya JK, EL n.k.
 
uNAFIKI HAULIPI WANA JF!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! MUACHENI APUMZIKE WALIOMTENDA WATAJUANA NA MUNGU WAO VIVYO HIVYO KWAKE.
JINA LA BWANA LIHIMIDIWE
 
Back
Top Bottom