Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,220
Hujawahi kuiona Serikali iliyofisika usingesema hayo. Ulikuwepo wakati tunapanga foleni ya unga wa njano wa msaada kutoka Merekani? ulikuwepo wakati tunavaa vitambaa vya "kirimplini"? ikiwa joto mpaka unaisikia inaungua mwilini, ikiwa baridi inaongeza kibaridi.
Hujawahi wewe kukesha kwenye foleni ya sukari, halafu unakuta wenzako wamepanga mawe kukuwahi na ukifika zamu yako unakuta kumbe sio sukari ni foleni ya mafuta ya nazi.
Hii nchi kijana, ilifilisika wakati wa Nyerere, tulikuwa wote kama wagonjwa kwa kukosa lishe bora.
Gilasi za kunywea maji hakuna madukani, tunatumia vifuu. Hujaiona wewe Serikali iliyofilisika na utajiri inao.
Mkuu hakuna maana yoyote kuposha mwelekeo wa mada. Sidhani kama kuna busara kuilinganisha Tanzania ya sasa na ya Nyerere. Wengine hatukuwepo kipindi hicho. Kwa hiyo unaposema kukesha kwenye foleni ya sukari, sijui Krimplin, hatuelewi, lakini ni kutokana na watanzania kukataa ujinga ndio maana hali ilibadilika. Hivi sasa wanakataa ujinga pia wa kuendesha uchumi kitoto kama serikali yetu inavyofanya. Tunafahamu kuwa wakati wa utawala wa awamu iliyopita kulikuwa na discpline kwenye borrowing and spending, the government was also serious in collecting taxes. Sasa hivi hayo hakuna. Kulikuwa na sound economic plans and implementations, we do not have them now. Sasa kinachoonekana ni kuwa tupo katika incremental mode, kwa lugha nyepesi ni hali ya kuendesha uchumi kwa staili ya "mkono uende kinywani"