Imani yetu kwa serikali ya Kikwete

Bado una imani na serikali ya Kikwete?

  • NDIYO (YES)

    Votes: 215 19.4%
  • HAPANA (NO)

    Votes: 834 75.1%
  • Sijui (Undecided!)

    Votes: 64 5.8%

  • Total voters
    1,111
Mambo yanayotokea sasa Tz yananikumbusha miaka ile ambapo masheik na maaskofu walikuwa wanapeana zamu za kutoa "matamko". Wakitoa maaskofu tamko dhidi ya serikali, masheikh nao wanainuka kutoa tamko kupinga lile la maaskofu.

Nakumbuka kipindi fulani hata Rais aliibuka na kuhutubia "wazee wa Jiji la Dar es salaam" kujibu waraka wa baraza la maaskofu, akiwakumbusha kutenganisha ya "Mungu na Kaizari", lakini hapohapo hadhira yake ikimwitikia kwa vibwagizo vya "takbiir!"

Mkuu hapo kwenye red, nimechecka sana!!!
Umenifanya nijiulize ikiwa rais na makamu wangekuwa ni wakristo miaka yote kumi kama ilivyo sasa takbiiir zingekuwa ngapi mitaani.
 
Nashindwa kupiga hii kura. Hili linatokana na swali lenyewe...linasababisha hata kuchagua sijui (undecided) inakuwa ngumu. Swali linasema Bado una imani na serikali ya Kikwete? Sijawahi kuwa na imani na hiyo serikali, sasa hii bado inanipa utata! Mwongozo tafadhali
 
ni kuamua tu wanainchi,ingawa itachukua muda sana waTz kuamka na kuchukua hatua.kwa sababu ni wachache sana wenye uwezo wa kukataa uasi na kudhubutu kujaribu

ila siku tutafika tu...kivipi sijui!!
 
Kaisomeni katika ya nchi vizuri...Bunge linaweza kupiga kura ya kutokuwa na imani na raisi. Ikifanya hivyo rais atavyunja bunge na uchaguzi mpya utafanyika..Kwa hiyo ndugu yangu mwanakijiji kapitie katiba vizuri..Shida iliyopo hapa ni kwamba wabunge wengi ni CCm sasa hata waambie wale makonokono mradi kutetea chama kuliko nchi watakubali...Hivyo ni wajibu wa Watanzania kuamka na kucahgua wabunge wengi wa upinzani ila waka ihalalishe sheria hiyo... Kenya na nchi nyingine kama Israel na Japan imewezekana kwa kuwa bunge lao angalau ni BALANCED yaani nusu kwa nusu.
 
JK ni rais bora kuliko marais wote waliopita, hakuna haja ya mjadala wa kum-uondoa ...takwimu za kiuchumi siyo hoja za kina mwanakijiji na ki-waraka waraka ziwekwe kuanzia rais wa kwanza mpaka JK utaona alivyo bora kupita wote..acheni rongo rongo zenu.
 
JK hafai kabisa kuwa kiongozi wa kututoa kwenye matatizo tuliyonayo. JK ni zao la mafisadi na atatuumiza sana miaka 5 ijayo. Tujiandae kuumia kwa sababu wenye kuona hatufai tupo wachache na hii inaweza kuonekana bayana kwenye kura hizi za kwenye mtandao, ambapo hadi sasa ni watanzania wachache wameshiriki. SINA IMANI NA JK
 
Nakumbuka maneno ya mzee mwinyi alipomwambia mkapa 1995 ya kwamba mwanume mzuri siku zote kabla haujaoa. Sasa nimeamini, jk alivyokua akipendwa na wananchi wote lakini sasa ameprove feilia, namshauri apunguzwe uswahiba na watu wake wa chini katika kazi. Aache kuchekacheka hasa akiona videmu, otherwise miaka mitano anayo ya kurekebisha makosa yake, ila mimi kura yangu hapati hasa nikikumbuka hotuba aliyomkusudia babu yetu mgaya
 
TAMBUA KABLA; AWAMU IJAYO WABUNGE NA MAWAZIRI WTALIPWA MSHAHARA MDOGO,
WATUMISHI WOTE WA UMMA.
Akigombea huyo tutajua kama hategemei maajabu.
atawazia kuuza viwanja vya wazi.
sio ataomba sadaka kwa kuchangisha huduma anazotoa.
hapana atatishia kukomesha madhambi ili apewe chochote.
YOTE HAYAPO/. NANI ATA TANGAZA NIA?

Ahsante Babu. kumbe nimekosa mambo mengi matamu. sasa naona. nilikua kwenye giza nene sana.
kweli kuona sio kujua: nasema.
WAWEKEZAJI WENYE MANUFAA KWA TAIFA NI WAZAWA TU.

MAAJABU YA VIONGOZI WETU?

Tumbo kutangulia vingine.
Macho kuangalia kabeba nini.
Miguu kukimbilia kubwa kuliko.
Mikono kubeba hata lenye hatari.
Mdomo ndiyo bila kuchoka.

Samahani najua sieleweki, ufafanuzi wa maajabu haya yahitaji hekima ya hali yajuu sana.
Kanini wapigania kuwa viongozi wakati wanajua hawawezi kutumikia/?
 
"Naunga mkono hoja hiyo kama njia mbadala ya kuiepusha nchi katika vita.
Raisi kashindwa kwa baadhi ya mambo yafuatayo yanayomfanya apoteze sifa za kuwa Raisi mwenye hadhi.

1.Ameshindwa kulinda umoja wa watanzania kwa kupitia hoja ya kadhi na OIC na kuwagawa watanzania kwenye makundi makubwa mno yenye mkinzano mkali wa ugomvi na hivyo kuvunja ahadi yake aliyoapa ya kulinda umoja wa watanzania.Kwa sababu ameshindwa hilo hastahili kabisa kuendelea kuongoza.Hata kama amefanya mazuri yepi kuvuja umoja ni kosa lisilosameheka inabidi afunge virago.

2.Ameshindwa kulinda katiba aliyoapa kuilinda kwa kugeuza ofisi za serikali zitumike kuendesha mihadhara ya kidini kwa kuteua maofisa wa serikali wazunguke nchi nzima kuendesha mihadhara ya kidini ya kuuliza kama watu wanataka kadhi wa kiislamu au hawataki.Kazi ya Raisi si kusimamia mihadhara ya kidini kwa gharama za walipa kodi.

Raisi amekuwa mtumiaji mbaya wa pesa na mali za serikalikama pesa za serikali,magari ya serikali na ofisi za serikali na za walipa kodi kwa kuzitumia kulipia ya mambo yanayohusu hoja ya kadhi wa kiislamu wakati wakizunguka kushughulikia mihadhara ya kuhusu kadhi wa kiislamu.

3.Raisi amekuwa mtumiaji mbaya wa madaraka kwa kutokemea wizara ya sheria na katiba isijihusishe na mambo ya kidini yanayohusu kadhi bali amekuwa akitumia ubabe wa kijinga kuburuza na kushinikiza maafisa wa serikali waendelee na hoja ya kadhi kinyume na matakwa ya taaluma yao ya katiba kwa maagizo mbalimbali mara kwa mara.

4.Raisi kama mhimili muhimu wa utawala katika nchi na mlinzi wa katiba ilibidi azuie hoja ya kadhi isiende bungeni kwani kufanya hivyo ni ukiukaji wa katiba.Lakini bila aibu wala haya aliachia iende bungeni na kuligeuza bunge liwe mahali pa mhadhara wa kiislamu wa kujadili kuwepo au kutokuwepo kwa kadhi wa dini ya kiislamu.Tunaamini Raisi ndiye kaligeuza bunge kiwe kijiwe cha wahuni wa mihadhara ya kiislamu ambao wanafanya bunge ni kijiwe cha mhadhara wa kujadili mambo ya kadhi wa kiislamu jambo ambalo ni la kidini kabisa.Raisi kaligeuza bunge kuwa eneo la mihadhara ya kidini ya mambo ya kadhi wa kiislamu kwa kulipelekea hoja ya kidini.

Bunge letu kwa kuwa nalo limejaa mabwege likaanza mhadhara wa kidini wa kadhi bungeni badala ya kupiga marufuku mhadhara huo usikanyage bungeni.Bunge letu limejaa watu mabwege wasiojali katiba bali posho tu ndio maana wao hawajali kuangalia katiba inasemaje kabla ya kuijadili ndiyo maana hoja ya kadhi ilipenya sababu serikali inajua bunge limejaa mabwege wasiojua katiba au hawaitilii maanani.

Ufumbuzi wa kwanza wa kuepusha vita ni kuwa bunge lipige kura ya kutokuwa na imani ili kuepusha hasira ya wananchi wasizushe vita. Wamwite Raisi bungeni wamwambie aondoe hoja zote za kidini na wampe karipio na onyo kali yeye na serikali yake asirudie tena na wamwandikie barua kuwa hawaridhishwi na utendaji wake kama wawakilishi wa wananchi na wampe karipio kali la kimaandishi kuwa arekebishe utendaji wake kama Raisi kama atakubaliana nao.

Kama Raisi atakataa kutii maagizo ya bunge kwa jeuri basi mahakama ambaye ni muhimili wa tatu itoe amri ya kumtaka Raisi aondoke madarakani kwa sababu ya kuvunja katiba kwa kuingiza hoja za kidini katika serikali na bunge hivyo ni mhalifu mkuu wa kikatiba asiyetakakiwa kuendelea kuongoza nchi.
Kama akikataa kutii hata amri ya mahakama basi Jeshi itabidi liingilie kati kumtimua kwa kuwa bunge na mahakama havina imani na utendaji wake.Endapo Jeshi litashindwa kufanya wajibu wake huo hapo sasa wananchi ruksa kuingia mitaani kufanya chochote wanachoona kinafaa wakifanye.


Kama wabunge watakataa kumchukulia hatua Raisi wakajifanya vichwa ngumu wakakataa kuondoa hoja za kadhi na OIC bungeni na kuendelea kuzijadili hivyo kuendeleza ujeuri wao wa kuivunja katiba iliyopo basi wananchi itabidi waingie hatua ya kulizingira jengo la bunge kwa siku kadhaa wabunge wakiwemo ndani kwenye kikao na kuwashinikiza wabunge wote waliomo ndani ya jingo la bunge wajiuzulu na watangazie taifa hivyo wao wenyewe kutoka humo ndani kujiuzulu kwao na kutamka kuwa uchaguzi mpya uitishwe. Kuzingira mabunge mapumbavu ni njia mbadala kuliko kuanzisha vita inayoweza maliza raia wasio na hatia.

Bunge likishindwa kulinda katiba ambayo lenyewe limeitunga halina budi nalo litimuliwe. Na kama halitaki kuondoka wananchi wana haki ya kuwashinikiza wajiuzulu kwa kulizingira jengo la bunge.Wakiendelea kugoma hata baada ya kuzingirwa basi kinachofuata hapo mimi sitakuwepo nitakuwa nawahi Moscow kwenye mtaa wa machinga wa silaha kuuliza kama bunduki za AK 47 za mitumba wanazo na zinauzwa bei gani na zaweza wasili kwenye jengo la bunge lini na kwa usafiri upi wa haraka.

Yatakayofuata sijui naachia walenga shabaha walenge chochote wanachoweza kulenga kile ambacho roho zao zinapenda kulenga.Shenzi type. "


Huyo mchangiaji ana chuki binafsi,hivi wewe kadhi na OIC ndo iliyo kugusa tu,hao mafisadi waliotawala hapa huwaoni tena wanatumia kodi za walalahoi na pia inaonekana wewe si mtanzania,au huijui katiba ya Tanzania ndo maana unayasema hayo .

Hebu tafuta vya kuchangia ambavyo vimeleta madhara makubwa kwa taifa letu,haswa kiuchumi,pesa nyingi zimepotelea mikononi mwa watu wachache.
 
hivi ni mbuge gani kutoka ccm anaweza kuthubutu walau hata kuwaza kutoa hoja hiyo? sasa hivi ni mchakato wa uchaguzi na pamoja na kuwa na sheria mpya juu ya gharama za uchaguzi bado wanatoa rushwa tena kwa kasi ya ajabu. miaka miwili ya mwanzo itakuwa ni ya kurudisha gharama ilyitumika. miaka miwili itakayofuatia itakuwa ni ya kujifunza taratibu za bunge. nusu ya mwaka wa mwisho ni wa kuhoji kusu matatizo ya jimbo na nusu ya mwisho ni ya kuzinduka na kuanza kuwahadaa wapiga kura. ni wakti gani watawaza kumuwajibisha rais? kama hoja ya richmond walioshikia bango ilikufakifo cha aibu, ni wapi tena watakako ibukia na hoja zao? kama mpaka leo bado wanaomuona Edward Lowasa ni shujaa na kwamba hakupaswa kujiuzulu, vipi juu ya kumuwajibisha rais? sioni dalili nasitaki hata kujaribu kukiumiza kichwa changu kuwaza juu ya impossibles. kwa mazingira na siasa za Tanzania haiwezekeni.
 
Katika yote hayo masikitiko tuliyo nayo watanzania, wazalendo asilimia zaidi ya 70 wamefunga mikanda ya umaskini, magonjwa, njaa, kutokugusa kabisa elimu, demokrasia iliyochakachuliwa kuliko za gas stations, na mengineyo mengi. Hao hao ndio wanaojitokeza eti kumdhamini kwa kishindo na kutanda mitaani kumshangaa!!! samahani kumshangilia! Ni wale wale ambao asilimia 30 matumbo yao yameshiba, hospitali ni nje ya nchi, wenye fedha na nguvu ya kuchangia uchaguzi, watoto wao na wao wenyewe wamesoma, tena nje ya nchi, wale ambao wameikalia demokrasia ndio waliompitisha bila kupingwa na kumwacha eti awe mgombea pekee, eti wanasema ni chaguo la Mungu kama yule kiongozi wa dini mfa maji alivyosema "Kikwete ni Chaguo la Mungu". Ni Mungu gani huyo? Tusicheze na jina la Mungu bure.
 
karibuni tulisikia kauli ya kiongozi wanchi akisema (namnukuu)… “SIHITAJI KURA ZA WAFANYAKAZI” Na hadi leo sijasikia kama amebadili kauli yake ile au kuomba radhi wafanyakazi wa Tanzania. Mimi najiuliza maswali haya;-
“Je, wafanyakazi wana haja ya kumchagua mtu aliyewakana?”
“Je; Kuna haja ya kumchagua mtu ambaye kwa kauli yake ameonesha kutokujali mchango wa wafanyakazi katika ujenzi wa taifa hili?”
mail

HUNA HAJA YA KUMCHAGUA MSALITI, TUNAYE MTU MAKINI, TUNAYE MTU MBADALA
MCHAGUE SLAA AWE RAIS 2010


Mtumie mzalendo mwingine mwenye uchungu na nchii hii ili tulikomboe taifa letu
MNASEMAJE WANAFORUM??????
 
kuna vitu vingi ki ukweli vinakwaza sana lakini pia tunahitaji hekima ya Mungu katika kila tuamualo
 
ndio bado ninaimani ya kutosha na serikari ya kikwete kwani kwa mengi aliyoyafanya katika miaka yake mitano ya uongozi . tukiangalia ktkt swla la maundombinu ameweza kujenga miundombinu na kuzikamilisha na badhii ya nyingine ziko mbioni kukamilika kwa mfano barabara ya manyoni -- dodoma , manyoni--singida , mkuranga -- kibiti .... amejenga vivuko kwa mfano MV misungi, MV pangani, nk ... pia upande wa viwanja vya ndege kiwanja cha ndege kipya cha mbeya ,


UPANDE WA KILIMO

serikali imeanzisha program ya ASPD ( agricultural sector development) ,, matumizi ya mbolea yameongezeka kutokana na kutolewa kwa ruzuku. kutoka 2005-2009 matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka tani 51629-141050 imewafikia wakulima 15,000,000 .

idadi ya matrecta imeongezeka kwa kiasi cha kuridhisha na inatia matumaini kwa miaka ijayo



SECTOA YA ELIMU
serikali amewezesha kila mtoto kupa elimu ya msingi . na kwa upande wa sekondali imeweza kuongeza idadi kubwa ya wanafunzi wanao primary kwenda secondari na pia serikari bado inampango wa kuongeza ufanisi wa shule hizo kwa kuzipatia maabara na walimu wa kutosha ili kuboresha elimu ... pia serikali imeongeza vyuo vya uwalimu ili kupata walimu wa kutosha .. serikali yetu kwa upane wa vyuo vikuu imejenga chuo kikuu cha dodoma kitakachoweza kuchukua wa elfu 40 kila mwaka na pia serikali upatikanaji wa elimu ya watu wa zima

AFYA
Serikali imefanikisha kupunguza vifo kwa mama na mtoto ,, imeimarisha vita zidi ya ukimwi na mapambano zidi ya malaria kwa kutoa vyandarua kwa watoto chini ya miaka mitano... serikali imeweza kufanikisha ukarabati na upanuzi wa majengo ya afya na kuboresha upatikanaji wa haki za mtoto ; walemavu na wazee


VIWANDA; BIASHAR NA MASOKO

nchi imeweza kuimarisha uhusiano baina ya nchi wanachama SADC, EAC ( east africa community ) WTO ( world trading center) pamoja na nchi nyinginev kama china , japan, marekani na korea , serikali imewaza kuvutia mazingira ya uwezekezaji kwa kuanzisha viwanda kama viwanda vya nguo , mbolea ,saruji, chuma na lemikali nk
 
Back
Top Bottom