Imani yetu kwa serikali ya Kikwete

Bado una imani na serikali ya Kikwete?

  • NDIYO (YES)

    Votes: 215 19.4%
  • HAPANA (NO)

    Votes: 834 75.1%
  • Sijui (Undecided!)

    Votes: 64 5.8%

  • Total voters
    1,111
ama kweli nyerere aliona mbali mi nikajua kuwa kigezo kilikuwa ni umri kumbe?! Kweli nimeyaona
 
Watanzania wengi walikuwa na imani na Rais Kikwete alipoingia madarakani 2005,wazliamini yeye ndo atakuwa rais bora kuliko walitangulia baada ya nyerere.Lakini imekuwa tofauti na matarajio ya wengi ndo maana wakamtosa kumpa kura 2010 lakini akachakachua! Ila wengi wanaamini Kikwete ni rais mzuri tatizo amaezidiwa kete na matajiri waliomuweka madarakani hivo anatoa maamuzi kwa maslahi yao.
Je wana JF hili mnalionaje?:playball:
Hakuna cha kuzidiwa kete na wenzake ni mpumbavu tu
 
I just wish this guy and his gang were reading. He has been the most lucky president, to be advised peacefully for all these years. What is next is accurately predictable
 
Maisha yanazidi kuwa magumu kila kukicha hiyo imani itoke wapi!!Serikali imeshindwa kusimamia Rasilimali zake kwa faida na maslahi ya wananchi wake matokeo yake wiliopewa dhamana ndo wamegawana kifisadi nakukumbatia wawekezaji huku mwananchi akiachwa asijue chakufanya.
 
Haki ya Mungu huu mwaka ukiisha huku hali ya sisi walala hoi ikiendelea kuwa duni kiasi hiki,tutatafuta mbadala wa maisha msitulaumu.WE HAVE NOTHING TO LOOSE.
 
Jk ukijichanganya kwenye 18 zangu nakula zote bora nife na wewe kuliko mwenyewe,tumewachoka sana nyie maisha poa sisi bora ya jana.
 
CNN,BBC na vyombo vingine vikubwa vya Television watapa ta fursa ya kuja na kureport matukio yatakayokuwa na majibu kwani Ccm na Serikali yake imesababisha kwa miaka 50,dunia itapata simanzi lakini itakuwa fundisho kwa vizazi vijavyo kwani hata Upinzani wanatulaghai tuu hakuna jipya wala ukombozi kupitia wao.
 
kadri watanzania tunavyozidi kufarakana kwa tofauti za vyama ndo tunawapa mafisadi nafasi ya kuendelea kukaa madarakani! kwa nini tusiungane na kuichukua nchi yetu kabla haijatafunwa hata mifupa iliyobaki
 
Japokuwa ninaweza kuwa nimepitwa na wakati katika kuyasema haya hasa kwa kuwa aliyasema siku nyingi sana, napenda kukubaliana Msemaji aliyetangulia {Nd. Kitia) katika karibu kila jambo alilogusia. Lakini kwa kuongezea tu ni kwamba inasikitisha namna ambavyo WATANZANIA, walio wengi wanavyojitenga na SIASA. Ukiuliza mitaani watu wengi watakujibu, "mimi na siasa mbali mbali." Watu kama hawa, ukifuatilia, utakuta hawana muda hata kidogo wa kujifunza hata mambo ya msingi ya husuyo nchi hali ya kuwa ni wananchi na ndio nchi inawategemea katika kuijenga.

Mtu wa aina niliyoisema awali, pamoja na jibu lake la kutojihusisha na siasa, kwa kiasi kikubwa anategemea UONGOZI uliopo madarakani katika kujiletea maendeleo binafsi & kuliletea maendeo taifa kwa ujumla. Lakini mtu huyu hashiriki katika kuuweka madarakani uongozi huo, hali inayoweza kutoa mwanya kwa kiongozi asiye na sifa kuingia madarakani, kiongozi ambaye watu wote, pamoja na wale wasiomchagua watalazimika kumtii kwa mujibu wa sheria. Inapotokea mtu wa aina hiyo niliyoitaja awali (asiyejihusisha ma siasa) akaamua kuitumia fursa na haki yake ya kikatiba, anaweza kumchagua mtu kwa kuangalia picha inayovutia machoni maana ndio kigezo pekee anachoweza kutumia. Lakini pia ikiwepo mifumo iliyo HAI ambayo inaweza kuhakikisha viongozi wote, waliochaguliwa na kuteuliwa wanasimamiwa na kutathminiwa kiutendaji ili kuona kama wanaweza kuondolewa katika nyadhfa wanazoshika {Hata Rais mwenyewe} iwapo hawatoshi katika nafasi walizo nazo, hali isingekuwa ilivyo sasa. Kwa nchi kama Marekani ambapo kila Mwananchi, kwa nafasi yake anashiriki kikamilifu katika MCHAKATO wa kumchagua Rais ambaye anaamini ataleta maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla, kutokuwa na imani na RAIS ama uongozi ulio madarakani ni SWALA LENYE MAANA KUBWA kikatiba na huanzia katika kura kama hizi tunazopiga humu lakini katika kiwango tofauti cha UMUHIMU na hata MAPOKEO na mifumo ya UFUATILIAJI wa matokeo yenyewe. Ipo siku mambo yatabadilika japo siku hiyo haijulikani leo.
 
Back
Top Bottom