Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Hivi nyie mnataka Zitto aache kutekeleza kazi zake za uenyekiti ya Kamati ya Mahesabu ya mashirika ya UMMa na kubagua wananchi wanaotaka kumuona na kumpa shida zake eti kwa sababu ni mbunge kutoka Chadema au naibu katibu mkuu Chadema nadhani mungeangalia hii thread ni ya lini na muanzisha thread alikuwa na maana gani, alikuwa anakionya chama kutokuwa na mtu mmoja ambaye anaonekana kama nyota pekee.

Kitu ambacho nadhani Chadema wameweza kukifanya ukiangalia sasa hivi unaona kuwa wabunge kwa viongozi wa chadema kila mtu ana nafasi yake katika chama. Zitto endelea kutekeleza majukumu yako chama wanajua unafanya nini achana na akina nini hii wanaongoja mkono undondoke kama Fisi
 
Mimi sioni cha ajabu, maana Mwalimu Nyerere alikuwa maarufu kuliko TANU na hatimaye CCM, Clinton alikuwa maarufu kuliko Democratic party, hivyo Zitto kuwa maarufu kuliko CHADEMA halijaharibika neno!

Zitto kwa sasa si maarufu kuliko CHADEMA hata akihama sioni tishio lolote.
 
Zitto akiamua kujiunga na CCM au akaamua kuachana na siasa CHADEMA itakuwa imara tu. Itayumba kidogo sana labda asilimia 10% lakini 90% itakuwa fiti. Ndio maana mmeshuhudia mikutano mingi ya hivi karibuni hajashiriki lakini nyomi ....ya ajabu!
 
Ataendelea kuwa mbunge wa Kigoma Kaskaz ndiyo kwa kuwa wananji wa huko kwao wanamkubali. Ata mimi namkubali.

Lakini umaarufu ma heshima aliyojijengea akiwa kwenye chama chetu chadema atavisikia kwenye taarifa ya habari. CCM kila kitu ni vululu-vululu.

Wewe tizama. Kijana mdogo na smart kama Nape anaonekana mzee aliyechoka kifikra kwa kulazimika kuhubiri unafiki!


Nape kijana mdogo asiye na fikra mbadala; anaamini akiondoka ccm ndiyo mwisho wa maisha.
 
Mimi sioni kama zito ni maarufu kuliko Chadema, labda ungesema Dr. Slaa au Mbowe. Lakini pia naukumbuka umaarufu wa Dr. Amani Walid Kaborou, yuko wapi sasa hivi?
 
We never work with imagination ideas Mr Man.
 
Ahame tu: Aende zake CCM. Si tunajua kwamba huyo Z itto anatumiwa na kina Zoka kuhujumu Chadema?bwana anatumiwaZ
 
Kama mdau wa karibu wa Chadema kuhama kwa Zitto, kungepunguza matatizo mengi sana ya Chadema. Zitto amehusishwa sana kuwa na ukaribu mkubwa sana na usalama wa Taifa magazetingini - eg Mwanahalisi na hajajibu.Akahusishwa na Rostam Azizi na gazeti hilo hilo kwa ushahidi wa maongezi ya simu - hajajibu. Zitto ni chanzo cha kuvunjika kwa uchaguzi wa Bavicha baadaye ya kupenyeza Rushwa ndani ya umoja huo hadi Kamati kuu wakaahirisha uchaguzi. Zitto anatabia ya kugawa makundi ndani ya Chama.Kwa mfano alikuwa anatumia kuwagawa wabunge wa Chadema KWA MISINGI YA UDINI ili wasimpinge Rais JK Ameshindwa. Chadema hatumkubali JK si kwa dini yake bali kwa Kushindwa kwake kudhibiti Mafisadi ambao wengi wao ni wakristo lakini maswahiba wake.Nimesikia anataka kuwa mkiti wa Taifa wa Chadema mwaka 2013. Ajaribu kama hajaumbuka. Mimi simkubali kabisa zitto.
Suffering from ZITTOPHOBIASIS??kuku hafi kwa utitiri!ulitakiwa umwelewe mwanzisha mada kuwa kaanzisha kiuzabinazabina ili wazabinazabina waingizwe kingi!mkuu fikiri kwa makini kabla ya kuanza kujibu!la sivyo usije ukampa Kikwete kazi ya kutibu Ufisadi,ohooo!!
 
kwa nini mnaleta thread ya zitto utadhani ni maarufu sana kwenye chama?!!!wewe uliyeleta hoja ungesema hivi: Imagine dr slaa akijiondoa chadema, cdm itakuwaje??sio zitto..ni mtu wa kawaida mno ndani ya cdm!
 
Atakuwa amepotea na nitamshauri aachane na siasa kabisa aende akajiunge na kakobe kueneza injili-itamlipa zaidi.Just IMAGINE YALE MASADAKA YOOOOOOTE YAWE YAKE!? Ata posho nakataa mie
 
kwa nini mnaleta thread ya zitto utadhani ni maarufu sana kwenye chama?!!!wewe uliyeleta hoja ungesema hivi: Imagine dr slaa akijiondoa chadema, cdm itakuwaje??sio zitto..ni mtu wa kawaida mno ndani ya cdm!
Sisimizi
 
Mara nyingi nimekwepa sana kujadili personality katika jamii forum lakini kwa kuwa mwanzilishi wa hii thread ama kwa kutumiwa au kufikiri kwa njia iliyohasimu kibusara, basi si vibaya leo nikachangia angalau kidogo katika hili la umaarufu wa Zito ambalo mimi sijawahi kuliona hata siku moja katika maisha yangu, naomba niseme tena kwa wale wanaosikiliza kwa ubongo walitafakari, na hili si kwa Zito pekeee bali kwa watu wote wanaoweza kuwa na sifa za umaarufu.

Umaarufu katika siasa sio umarufu wa uzuri wa sura, mwanasiasa yeyote duniani ni maarufu kwa sababu ya mambo ambayo anayasimamia hakuna kitu kingine, uwezo wa kujenga hoja unachangia kuongeza mvuto na si vinginevyo. Leo hii ukimwondoa Zito CDM na si Zito tu, hata Mbowe, Slaa, Mnyika na wengine wengi ukawapeleka Chama kingine chochote hoja hizo hizo ambazo wanazizungumzia CHADEMA hazitawafanya wawe maarufu, wanapohama sehemu waliokuwa wamejichimbia na kwenda sehemu nyingine inawalazimu watumie muda mwingi kujenga imani ya kwa nini wako sehemu mpya, lakini kibaya zaidi wanaongeza idadi ya mashambulizi kuelekea kwao, they are vulnerable and suceptible to political assault, badala ya kujenga hoja they become defensive hii ndio hatari yao wote.


Lakini ukihama kwa sababu wamekufitina unawakuta watu wamekuandalia pa kufikia na kwa hiyo inakuwa rahisi kuimba wimbo wako wa kisiasa mfano ni kwa akina dr slaa, Shibuda na wengine wengi waliowahi kufitiniwa na wananchi wakawalazimisha kuhama, wao walinufaika na mfumo huo lakini sio uhame eti wewe ni maarufu kuliko chama siku mbili watakusindikiza na baadaye wataanza kurudi mmoja mmoja mwishowe utabaki peke yako na wachache ambao ni diehards.

Hakuna mtu ni maarufu kupita CDM viongozi wanakiongezea chama umaarufu kwa kusimamia ipasavyo kuondoa au kuyasemea mambo yanayowakera wananchi. Ni vigumu sana watu ambao sasa wanadhani ni maarufu CCM wakaja CDM na umaarufu ule wakauendeleza hivyo, wakitaka kufanikiwa angalau kwa kuanzia waanzishe mtafaruku ndani ya chama chao na ajenda inayowaondoa iwe ni tofauti ya kimtizamo ambayo wanadhani chama chao kimefikia ukomo wa kufikiri na kutenda. Kwa maana hiyo kwao suluhisho ni kuhama ili wakatekeleze misingi ya yale wanayoaamini ambayo ni lazima yaendane na kutetea masilahi ya watu ndani na nje ya Chama chao.

Kwa misingi hiyo hiyo ndiyo maana hata Sita na Mwakyambe walisita kuhama wakachagua kupambana wakiwa ndani. Zito ndani ya CDM ataendelea kuwa maarufu na hii inatokana na namna CDM inavyofanya kazi na ilivyomlea na kumpa heshima stahili. Nje ya CDM ni samaki nje ya maji kama kuna mtu anapinga ajifanye guineapig

No matter how big or important or popular an individual is, the institution he/she belong will always be superior to him/her. The rule of exceptional is applicable only when the diference is on social evils and justice. If an individual is fighting against social evils the win is emenent regardless of size or importance in the institution.
 
zito akitoka CHADEMA NA kwenda CCM unaonaje nadhani atakuwa amejiua kisiasa. ila yapasa kujua umaarufu wa cdm sio zito wala hata Slaa, Mbowe, n.k. Kwani umaarufu wa CCM ni nani jk, magufuli, sitta,....? Umaarufu wa vyama hivi ni sera na action za vyama kwa wananchi. Akitoka Zito mwendo mdundo kama kawa atatoka na wajinga wachache lakini wengi wataendelea na harakati
 
yaaaaan! chadema kuna vichwa zaid ya ujuavyo ndugu yangu. sidhani kama kiu ya ngamia yaweza kausha mto labda kiwe kijito
 
Baada ya kupata taarifa rasmi kuwa ZZK amevuliwa nafasi zote za uongozi ndani ya CHADEMA, Vyama vinne vinamsaka ili ajiunge navyo na kujiongezea nguvu..

1. CCM
CCM ina kiu ya kumpata ZITTO ili iweze kunyakua majimbo ya KIGOMA... Matumaini ya makada wa CCM ni kumpata Zitto na baadaye Kafulila (swahiba muhimu wa Zitto) kugeuza chuki ya wana Kigoma dhidi ya CCM... MMoja kati ya watu nilioongea naye ni mpinzani mkuu wa Jenista Mhagama - Peramiho - ndani ya CCM (ambaye ni msomi mwenye PHD)... kwa maoni yake Zitto hawezi kupata nafasi za juu ndani ya CCM kwa miaka 15 ijayo ila ni mtu muhimu katika kuirudisha CCM kigoma... "Nafasi ya urais ina watu wengi sana, hawezi kupata".... Ubunge nafasi iko wazi.

2. NCCR Mageuzi
Nimepata maoni ya wafuasi wachache wa NCCR Mageuzi - mmoja ni mfuasi wake aliyekuwa kiongozi wa CDM mkoa wa Mbeya na sasa amehamia Dar kikazi na zaidi ya yote ni mwanachama wa NCCR Mageuzi... Yeye anasema, "tulijua yatatokea haya, tuna matumaini makubwa sana ataungana nasi.... Akija NCCR Mageuzi, ukanda magharibi wote kuanzia Katavi hadi kagera, Mwanza na Shinyanga tunachukua"... Anaongeza kwa kusema, uenyekiti kwa sasa hawezi kupata, ila kugombea urais nafasi iko wazi.

3. CHAUMA
Chama hiki kinaongozwa na Hashim Rungwe (mtu wa Kigoma). Pia kuna taarifa kuwa kuanzishwa kwake kuna mkono wa Kafulila na Zitto Kabwe (wote kutoka mwisho wa Reli)... Chama hiki kinamatumaini makubwa ya kumpata ZITTO... ingawa wanakiri kuwa ni kazi ngumu kukikuza chama hiki kwa muda mfupi uliobaki. "Nafasi yoyote akitaka tunampa"
...

4. CUF
Chama hiki kina mtaka kwa udi na uvumba.. mmoja wa viongozi niliyeongea naye leo - Buguruni.. ameniambia kuwa wanatarajia kupeleka ujumbe rasmi kuonana naye ndani ya wiki hii...... Tukimpata tunaweza kujiimarisha zaidi.
 
Bado ni hisia tu. Tusubiri kauli yake rasmi.
 
Baada ya kupata taarifa rasmi kuwa ZZK amevuliwa nafasi zote za uongozi ndani ya CHADEMA, Vyama vinne vinamsaka ili ajiunge navyo na kujiongezea nguvu..

1. CCM
CCM ina kiu ya kumpata ZITTO ili iweze kunyakua majimbo ya KIGOMA... Matumaini ya makada wa CCM ni kumpata Zitto na baadaye Kafulila (swahiba muhimu wa Zitto) kugeuza chuki ya wana Kigoma dhidi ya CCM... MMoja kati ya watu nilioongea naye ni mpinzani mkuu wa Jenista Mhagama - Peramiho - ndani ya CCM (ambaye ni msomi mwenye PHD)... kwa maoni yake Zitto hawezi kupata nafasi za juu ndani ya CCM kwa miaka 15 ijayo ila ni mtu muhimu katika kuirudisha CCM kigoma... "Nafasi ya urais ina watu wengi sana, hawezi kupata".... Ubunge nafasi iko wazi.

2. NCCR Mageuzi
Nimepata maoni ya wafuasi wachache wa NCCR Mageuzi - mmoja ni mfuasi wake aliyekuwa kiongozi wa CDM mkoa wa Mbeya na sasa amehamia Dar kikazi na zaidi ya yote ni mwanachama wa NCCR Mageuzi... Yeye anasema, "tulijua yatatokea haya, tuna matumaini makubwa sana ataungana nasi.... Akija NCCR Mageuzi, ukanda magharibi wote kuanzia Katavi hadi kagera, Mwanza na Shinyanga tunachukua"... Anaongeza kwa kusema, uenyekiti kwa sasa hawezi kupata, ila kugombea urais nafasi iko wazi.

3. CHAUMA
Chama hiki kinaongozwa na Hashim Rungwe (mtu wa Kigoma). Pia kuna taarifa kuwa kuanzishwa kwake kuna mkono wa Kafulila na Zitto Kabwe (wote kutoka mwisho wa Reli)... Chama hiki kinamatumaini makubwa ya kumpata ZITTO... ingawa wanakiri kuwa ni kazi ngumu kukikuza chama hiki kwa muda mfupi uliobaki. "Nafasi yoyote akitaka tunampa"
...

4. CUF
Chama hiki kina mtaka kwa udi na uvumba.. mmoja wa viongozi niliyeongea naye leo - Buguruni.. ameniambia kuwa wanatarajia kupeleka ujumbe rasmi kuonana naye ndani ya wiki hii...... Tukimpata tunaweza kujiimarisha zaidi.

Kwa nini walisubiri hadi akafukuzwa? Wangemwahi kabka angekuwa kwenye chati. Sasa hana uzito amebaki kuwa nyepesi.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom