Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.

Tatizo la huyu Bwana Edward anataka kumlazimisha Zitto kufikiri kama yeye atakavyo.Edward amenithibitishia kuwa ni mshabiki tu asiyetaka kuyapima mambo kwa undani,Uamuzi wa Zitto kuamua kumsaidia Kafulila haujajengwa katika misingi ya kuwa kwenye chama fulani, Kuna wakati unafika watu wanaangalia uwezo wa mtu na sio uwezo wa chama.

Na hayo mengine anayoogopa kusema sasa kama si fitina ni nini?
 
kiukweli, ukiangalia kiundani Zito anashangazia tena sana na msimamo wake haueleweki, lakini wakuu jamani wahenga wetu walisema ivumayo haidumu au ngoma ikilia sana hupasuka ndo yanayomkuta huyu Zito hizo credibility alizopata anafikiri atazipata marazote yani kila mara anaibuka kusema, anafikiri anakubalika kiasi cha kugombea urais, na tujue kuwa CHADEMA hakuko shwari huyo Zito yupo tu, tusubiri yatakayojiri.

mmhhh na wewe ndala 2 unamatatizo tena makubwa na nafikiri we ni memba wa Zito ndo mana hutaki kujenga hoja unan'gan'gania uchaga, huyu mwandishi ameandika ya ukweli mtupu tena ni mchambuzi mzuri sana big up Kinabo.
 


Ushauri wa Bure huu Zitto. Uamuzi wako kusuka au kunyoa.


By the way yupo wapi Sheikh Salum Msabaha?
 
ni lazima tuhoji aina ya mwandishi na aina ya makala....
alichokifanya kinabo hapo ni kutoa maoni na msimamo wake kama vile ambavyo Zitto alifanya kwa Kafulila...
nashindwa kuona umuhimu wa nidhamu anaouzungumzia kinabo dhidi ya kafulila anaoutaka zitto auangalie wakati ushahidi unaonesha kuwa kinabo alitofautiana na ZITTO TANGU ALIPOONYESHA NIA YA KUTAKA KUMPIGA CHINI MCHAGA MWENZIE MBOWE...
kama ndo hivyo basi Hapo CHADEMA chama kizima hakina nidhamu........
ni nidhamu gani ilitumika kumnyang'anya zitto haki yake ya kugombea uenyekiti?...
ni nidhamu gani ilyotumika kumshughulikia JOHN HECHE ambaye ni KIBARAKA wa MBOWE aliyetishia kumpiga makofi Zitto na kutukana matusi ya nguoni viongozi Huku akijua ni Naibu katibu mkuu wake na ndiye selling picture ya chama?..
ni nidhamu gani aliyeitumia huyo MANGI- 'kinabo' kujidai mchambuzi huku akimchonganisha naibu katibu mkuu wake na watanzania?..
hivi kinabo unadhani sisi sote humu ndani tunaakili za kushikiwa kama wachaga wanaoogopa wenzako ambao hata DEMOKRASIA wanaiogopa?..
Mbona wewe kinabo ni mwanachama wa CHADEMA, sasa iweje umjadili kiongozi wako mkubwa wa chama Gazetini?..tena katika gazeti la bosi wako?...
kama kafulila hana nidhamu kwa kuwasema viongozi wake magazetini, wewe pia vipi?...acha ushabiki MANGI.....
kunya anye kuku akinya bata kaharisha
 
Ukitazama sana, kwa undani kabisa utaona bado kuna tatizo kwetu sote!!! Hakuna mtu aliye huru humu, kila mtu anavutwa na aidha mapenzi ama itikadi. Hatujapata wachangiaji huru....
 
Dr Slaaa fukuza zito kabwe huyo kwenye chama ni mtovu wa nidhamu na amelewa sifa na umaarufu hana lolote.

Pale mlimani alikuwa akifuzwa chuo kila mwaka kutokana na utovu wake wa nidhamu

Wama siasa aina ya zito wamepitwa na wakati inatakiwa abadilishe stlye
 

Mkuu una uhakika na unayoyaandika, manake hatukuelewi. ulitakiwa ujibu hoja za msingi za mwandishi ila wewe umetoa shutma tu kwamba jamaa mchaga, ana kibarua hana kazi, njaa kali sasa sisi ungangaji njaa wa mwandishi unatuhusu nini, tunataka majibu ya hoja zake ili kupembue mchele upi na pumba ni zipi chief.

alutaa....
 
Mtamuua Zitto Mwaka huu.

amewakosea nini?mfukuzeni na yeye
 
Kanda2,
Tatizo lako ni nini? Mwenye ukabila ni wewe. Badala ya kujadilia issues unajadilia messenger. Tafuta viatu.

Umemweleza ukweli, tukiwa na watu kama hawa hatufiki tutakua tunalialia tu. Kanda2, wachaga walikufanya nini? mbona unaweweseka.
 
Mtamuua Zitto Mwaka huu.

amewakosea nini?mfukuzeni na yeye
Zitto anawanyima usingizi,nakuhakikishia hawamwezi kumuua kwa maneno yao.Zitto achana nao hao walikimbia umande wewe endelea kukata book tu,watakusha shitukia kumekucha kumbe wao wanapinga usingizi tu.
 
Ninaamini kuwa Mh. zitto ana hoja ya kujibu kwetu sisi Watanganyika. ingekuwa vyema tukasikia toka kwake kwani siasa za chadema katika mkoa wa Kigoma zina historia ya muda mrefu.

Sijawa na uhakika wa nini Kafulila anaenda kuwaambia wanachama wa Chadema huko Kigoma Kusini lakini ameripotiwa akitamba kuwa hatabaki mwanachama hata mmoja wa Chadema huko Kigoma. Mimi sipendi kuamini na wala siwezi kuamini kuwa Watu wa Kigoma (watani wangu Waha) ni wajinga kiasi hicho kuwa wanajiunga na chama kwa kumfuata Kafulila au Zitto Kabwe na siyo Sera za chama.

Ninasubiri kuona uelewa na upambanuzi wa watu wa Kigoma. Tutajua ujinga au uelewa wao baada ya ziara ya Kafulia. Hapo ninajua nini cha kufanya na kushauri!!!

Mh. Zitto anapaswa kuwa na hoja muhimu za kujenga nchi na siyo tumshabikie tu hata anapokosea. Utumwa huu wa mawazo ni mbaya sana kuliko dhambi ya kuua. Mh.Zitto tunakusubiri kwa heshima ujibu hoja !
 
Ushauri wa Bure huu Zitto. Uamuzi wako kusuka au kunyoa.


By the way yupo wapi Sheikh Salum Msabaha?


I do not think Zitto has any future with Chadema. Sidhani kama anaweza kufanya kazi na viongozi wenzie wa juu wa chama kwa amani na kuaminiana. It is a pity that he will end up that way!!!
 

Watu wengine bwana!!! utamwelewaje wakati hata dalili ya kueleweka huna wewe mwandishi!!??

Umeandika weee mpaka umepoteza maana
Umeuliza wee mpaka umejijibu
Ume-biase wee mpaka ukabalance hoja hewa

Utamwelewa vipi Zitto wakati uandishi wako wenyewe uko shagalabagala? Mimi nadhani kwa style yako it will take you forever kumelewa
 
huyu ni ripota sio mwandishi,alikuwa gazeti gani kabla ya kuchukuliwa na MBOWE? hakuwahi kuandikia chombo chochote zaidi ya IN HOUSE TRAINING YA KIBANDA.hajui akiandikacho.
 
Ukitazama sana, kwa undani kabisa utaona bado kuna tatizo kwetu sote!!! Hakuna mtu aliye huru humu, kila mtu anavutwa na aidha mapenzi ama itikadi. Hatujapata wachangiaji huru....


Mimi hapa nipo huru
 
Sasa naanza kuamini maneno ya rafiki yangu Yusuph aliyezamia huku ulaya akisema siasa za Tanzania hata Mungu kazichoka, hivi ni lini sisi watanzania tutaacha kufanya siasa za uzandiki, uwongo, ubinafsi, chuki na unafiki? Hiki chadema tulichokuwa tunakiamini kama chama mbadala kinachotarajiwa ( angalau miaka hiyooo ijayo kumbe na chenyewe kina uvundo unatokota ndani, jamani hao watu tunaowaamini, sijui ndio mnaita wenye akili na ma-philosopher tukiwachunguza kwa undani tutagundua tu dhamira zao za ndani, JAMANI TUAMKE TUACHANE NA SIASA ZA KUFUATA WATU, LEO HATUTAMWELEWA ZITTO, KESHO USISHANGAE TUSIPOMWELEWA HATA SLAA, MI SINA IMANI KABISA NA WANASIASA WOTE WA HAPO BONGO, WANAHITAJI KUBADILIKA NA KUACHA UNAFIKI NA USANII, KAFULILA NI MOJA YA MAZAO LA HIYO SIASA CHAFU. HIVI HAKUNA SHUGHULI NYINGINE ZA KUFANYA MPAKA MTU UAMUE KUJIFANYA MWANASIASA KISA UNAJUA KUONGEA SANA, SIASA SAFI NI ZAIDI YA UJUZI WA KUONGEA.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…