Ijue sayansi ya chanjo hizi na chimbuko la wasiwasi wake. Hata Ulaya ni 5% tu ndiyo wamechanja katika miezi 3. Je, wanatusubiri sisi?

Huu utopolo wote ni kutaka kuhalalisha sisi kuendelea kufa kwa uzembe wa kutopokea chanjo zilizopo?

View attachment 1718867

Chanjo zilizopo zipo vizuri na habari thabiti kukuhusu iliyopo ni hii;



Mtajishaua sana na vi websites mnavyovinukuu nje ya mada. Utakuwa chanjo uko ndani ya wiki za mwanzo mlitegemea 100% ya watu kuwa vaccinated tayari?

Kwamba zingine za hivi pelekeeni wajinga.
Kwani kuchanja mtu mmoja inachujua muda gani mpaka sasa iwe 5% kwa zaidi ya mwezi?
Kama kupiga kura watu wanapiga kura mamilioni na matokeo yanatoka ndani ya masaa au siku mbili itakuwa kuchanjwa kasindano kamoja kisha unatokomea?
Hata wao huko wamezira ila ujinga wenu ndo mnabaki kulazimisha tu

Watu milioni mia tatu huko marekani wakitaka kuchanjwa ni mwezi mmoja wote wameisha kwa kuwa kila nyenzo wanayo
Na kutokana na vifo vinavyo wakumba wasingesubili kufa bali wangeenda kuzuia kifo.
 
Kwani kuchanja mtu mmoja inachujua muda gani mpaka sasa iwe 5% kwa zaidi ya mwezi?
Kama kupiga kura watu wanapiga kura mamilioni na matokeo yanatoka ndani ya masaa au siku mbili itakuwa kuchanjwa kasindano amoja kisha unatokomea?
Hata wao huko wamezira ila ujinga wenu ndo mnabaki kulazimisha tu

Watu milioni mia tatu huko marekani wakitaka kuchanjwa ni mwezi mmoja wote wameisha kwa kuwa kika nyenzo wanayo
Na kutokana na vifo vinavyo wakumba wasingesubili kufa bali wangeenda kuzuia kifo.
China ambako idadi ya watu ni bilioni 1.5 karibu wote wamechanjwa na chanjo yao salama isiyo na makando kando ya genetic engineering. Hakuna tena reports ya vifo kutokana na covid-19 kwa kipindi cha miezi 3 hadi sasa. Wazungu hawaamini takwimu hizi. Tuachane nao.
 
Kwani kuchanja mtu mmoja inachujua muda gani mpaka sasa iwe 5% kwa zaidi ya mwezi?
Kama kupiga kura watu wanapiga kura mamilioni na matokeo yanatoka ndani ya masaa au siku mbili itakuwa kuchanjwa kasindano amoja kisha unatokomea?
Hata wao huko wamezira ila ujinga wenu ndo mnabaki kulazimisha tu

Watu milioni mia tatu huko marekani wakitaka kuchanjwa ni mwezi mmoja wote wameisha kwa kuwa kika nyenzo wanayo
Na kutokana na vifo vinavyo wakumba wasingesubili kufa bali wangeenda kuzuia kifo.

Kwani mtu anajichanja mwenyewe kama anavyopiga kura mwenyewe?

Kwani chanjo zipo za kutosha at hand kwa watu wote tayari hata kwa USA tu?

Uongo mbuzi design hii mbona kwao ni chattle vijijini?

Kwani watumishi wanaofanya hiyo kazi ya kuchanja watu ni wangapi?

Mnavyokaa kuiba kura mkihesabu kura milioni 1 Zanzibar kwa wiki nzima na kura milioni 10 kwa wiki nzima bara, mnadhani kote ni wizi wizi tu?

Hivi shilingi milioni 10 inakuchukua wewe au inamchukua mwanafunzi wa darasa la saba muda gani kuzihesabu?

Msidhani kwa vile ninyi ni majizi basi kila mtu ni kama nyie.

Vile vile msidhani kwa vile tumenyamaza hatujui kuwa katika majizi nyinyi ni mamama au mababa zao.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
China ambako idadi ya watu ni bilioni 1.5 karibu wote wamechanjwa na chanjo yao salama isiyo na makando kando ya genetic engineering. Hakuna tena reports ya vifo kutokana na covid-19 kwa kipindi cha miezi 3 hadi sasa. Wazungu hawaamini takwimu hizi. Tuachane nao.

Vita ya kiuchumi dhidi ya Tanzania ghafla imepotelea wapi?

Hiiiiii bagosha.

Kumbe kuna ugonjwa watu wanakufa chanjo zipo na huyu bwana ndiyo kamwachia Mungu maisha yetu?

IMG_20210218_173848_589.jpg
 
Kwani mtu anajichanja mwenyewe kama anavyopiga kura mwenyewe?

Kwani chanjo zipo za kutosha at hand kwa watu wote tayari hata kwa USA tu?

Kwani watumishi wanaofanya hiyo kazi ya kuchanja watu ni wangapi?

Mnavyokaa kuiba kura mkihesabu kura milioni 1 Zanzibar kwa wiki nzima na kura milioni 10 kwa wiki nzima bara, mnadhani kote ni wizi wizi tu?

Hivi shilingi milioni 10 inakuchukua wewe au inamchukua mwanafunzi wa darasa la saba muda gani kuzihesabu?

Msidhani kwa vile ninyi ni majizi basi kila mtu ni kama nyie.

Vile vile msidhani kwa vile tumenyamaza hatujui kuwa katika majizi nyinyi ni mamama au mababa zao.

Au nasema uongo ndugu zangu?
Unauliza maswali ya kitoto sana,
Wewe hata kupeleka mtoto hospitali au kuumwa hujawahi ili uone hata wanavyochanja watoto?
Kuhusu idadi ya wachanjaji, unadhani marekani wana wahudumu wa afya wachache kama hapa kwetu?
Unadhani 5% ya wamarekani ni watu wangapi?
Unadhani wanaweza kushindwa kuwa na uwezo wa kumiliki chanjo milioni mia wakitaka?
Je wingi wa maambukizi hayo na vifo ni furaha kwao kuliko ghalama ya kuwachanja?
Tumia akiri dogo inaomekana hata bado hujapata mwanamke ndo.maana hujui mambo.
 
Unauliza maswali ya kitoto sana,
Wewe hata kupeleka mtoto hospitali au kuumwa hujawahi ili uone hata wanavyochanja watoto?
Kuhusu idadi ya wachanjaji, unadhani marekani wana wahudumu wa afya wachache kama hapa kwetu?
Unadhani 5% ya wamarekani ni watu wangapi?
Unadhani wanaweza kushindwa kuwa na uwezo wa kumiliki chanjo milioni mia wakitaka?
Je wingi wa maambukizi hayo na vifo ni furaha kwao kuliko ghalama ya kuwachanja?
Tumia akiri dogo inaomekana hata bado hujapata mwanamke ndo.maana hujui mambo.

Huna lolote jombi.

Hivi vi propaganda uchwara kwao chattle vijijini. Hata pale mjini vitaboomer.

Kwani marekani wasiotaka chanjo hawapo?

Chanjo ni suala binafsi.

Tusilazimishane kuchanjwa au kutochanjwa. Ndiyo ustaarabu au vipi?

Kwanini kutuzungumzia tulioko hatarini wakati nyie haiwahusu?

Mambo ya ngoswe yanawahusu nini nyie?
 
Sidhani Kama DNA zao zinafika bilioni 3. Huenda zikawa buku tu.
Hahahaaa. Tundu Lisu atakuwa alishawadonolea na ku fly nazo to Belgium na kumpatia Robert Amsterdam ambaye naye alishazipeleka mahakama ya ICC kama kithibiti!!!
 
Ugonjwa umetengenezwa na wachina ili wawe super power halafu wewe unasema tukachukue chanjo kwao?

May I be the last one to believe that the Chinese did this to themselves! (Fact itakayo nisaidia kuelewa ni September 11 ya Wamerekani!) Maybe......and only Maybe!

Otherwise I think all this C19 BS is part of the World Wide Cold War taking place as we converse, and us, the ‘Third World Countries “ are being used as pawns in the game!

My opinion; Let’s get back to our roots ASAP! Mcheza kwao Hutunzwa/Hutuzwa!
 
Duuh ndo uwaambie NIMR wazame maabara waje na chanjo.....bora waache kazi
 
Huu utopolo wote ni kutaka kuhalalisha sisi kuendelea kufa kwa uzembe wa kutopokea chanjo zilizopo?

View attachment 1718867

Chanjo zilizopo zipo vizuri na habari thabiti kukuhusu iliyopo ni hii;



Mtajishaua sana na vi websites mnavyovinukuu nje ya mada. Utakuwa chanjo uko ndani ya wiki za mwanzo mlitegemea 100% ya watu kuwa vaccinated tayari?

Kwamba zingine za hivi pelekeeni wajinga.


You sound like you’re high on something Chief!

No offense meant!
 
Duuh ndo uwaambie NIMR wazame maabara waje na chanjo.....bora waache kazi
Uchumi wetu utakapofikia kiwango cha high middle income country mwaka 2025 bila shaka tutakuwa na maabara zetu wenyewe za uhandisi wa vinasaba (genetical engineering laboratories) za kiwango cha kimataifa kama zile za BioNTech ya ujerumani iliyohusika kutengeneza chanjo ya Pfizer au ile ya Oxford University iliyohusika kutengeneza ile chanjo ya AstraZeneca. Ngoja kwanza tumalize bwawa la umeme la Nyerere na SGR ya umeme. Yanayokuja yanafurahisha. Vuta subira. Roma haikujengwa siku moja. Ngosha bado tunaye.
 
Bro hizo statistics za vaccination umotoa wapi? Israel ndio inaongoza kwa vaccination 92% ya ppn inamaana hao wote wameathirika. Instead of criticizing others come up with a practical solution for Africans. Source of african problems is the african themselves. We are damn enough to accept vaccination from the rest world instead of us developing our own Rate of COVID-19 vaccination by country 2021 | Statista
 
Hili ndiyo tatizo. Yaani watu wanadhani elimu inapatikana kwenye kampuni ya wamarekani inayoitwa google badala ya shuleni na vyuoni. Wao ni ku google tu na cho chote watakachokipata huko google wanaamini ndiyo ukweli.
Wako kama wew unayeamini jiwe anajua kila kitu mpaka umemkabidhi ubongo wako
 
Unauliza maswali ya kitoto sana,
Wewe hata kupeleka mtoto hospitali au kuumwa hujawahi ili uone hata wanavyochanja watoto?
Kuhusu idadi ya wachanjaji, unadhani marekani wana wahudumu wa afya wachache kama hapa kwetu?
Unadhani 5% ya wamarekani ni watu wangapi?
Unadhani wanaweza kushindwa kuwa na uwezo wa kumiliki chanjo milioni mia wakitaka?
Je wingi wa maambukizi hayo na vifo ni furaha kwao kuliko ghalama ya kuwachanja?
Tumia akiri dogo inaomekana hata bado hujapata mwanamke ndo.maana hujui mambo.
Yani hata neno akili hujui linavyoandikwa lakini unamwambia mwenzako atumie akili!! Sasa watu kama wewe ndiyo washauri wa jiwe hapo unategemea nini cha maana?
 
Nitajaribu kuieleza sayansi hii kwa njia na lugha nyepesi ili jamii ipate mwanga suala hili ambalo kisayansi ni complex. Lengo ni kuelimishana ili kupunguza mihemuko na mivurugano tunayoishuhudia kwa sasa hasa kwa baadhi ya wanasiasa na viongozi mbali mbali wa kijamii na wenye taaluma ya habari.

Atakayeweza kusoma nakala hii ndefu anakaribishwa.

1. Nitaanza na vinasaba (genes):
Miili ya viumbe hai ina undwa na chembe chembe ndogo sana zinazoitwa seli (cells). Binadamu ana matrillion ya seli. Seli hizi zinafanya kazi mbali mbali za kuwesha kuishi (metabolism). Kila seli ina nukleasi iliyozungukwa na saitoplasm. Kwenye nukleas kuna molecules za Deoxyriboncleic acid - kifupi chake DNA. Kila seli ya binadamu ina DNA zipatazo billion 3 zilizobebwa kwenye mikufu (chromosomes) 46 ndani ya nukleas.

Taarifa zote za jinsi miili yetu inavyojengeka na kufanya kazi inabebwa kwenye hizo DNA. Kazi zote za miili yetu inafanyika kwenye saitoplasm ya seli zetu. Yaani kwenye saitoplasm ndiko kwenye viwanda mbali mbali vya kuiwezesha miili yetu iishi na kufanya kazi zote vizuri.

Kazi zote zinazofanyika kwenye kwenye saitoplasm zinafanyika kwa maelekezo na usimamizi wa DNA. Ili DNA iweze kusimamia kazi inayofanyika kwenye saitoplasm huwa inatengeneza molecule ya Ribonucleic acid - kwa kifupi RNA na kuituma huko kwenye saitoplasm kwenda kusimamia kazi husika. Hivyo inaitwa messenger RNA - kwa ufupi mRNA.

DNA ilivyumbuliwa mwaka 1953. Huu ulikuwa ni uvumbuzi wa siri ya maisha kwani siri zote za uhai na jinsi kila seli ya mwili inavyofanya kazi zimebebwa kwenye DNA. Baada ya sayansi mpya ya uhandisi wa vinasaba (genetical engineering) kuendelea (advance), kwa kipindi cha miaka 13 kuanzia mwaka 1990 hadi 2003 wanasayansi toka sehemu mbali mbali duniani walifanikiwa kuzing'amua (decode) siri zote za DNA zote billion tatu zilizoko kwenye seli za mwili wa binadamu. The entire human genetic code was decoded/ revealed. Ziko kwenye ving'amuzi vya maabara mbali mbali za uhandisi wa vinasaba.

Kuanzia hapo wanasayansi wameendelea kucheza na hizo vinasaba vya DNA ili kuweza kuangamiza baadhi ya magonjwa kwenye seli za binadamu hususani ya saratani kama ya kongosho (pancreas cancer) na ya baadhi ya virusi kama virusi vya Zika vilivyogundulika huko Uganda mwaka 1947 kwenye msitu wa Zita vikienezwa na mbu Aedes.

Pamoja na kuonesha matokeo mazuri sana katika tiba za maradhi haya, hadi sasa kwa kipindi cha mwongo mmoja mamlaka za FDAs zilishindwa kuzipa kibali tafiti hizi kuendelea na phase 2 ya clinical trials za watu wengi zaidi. Wasi wasi ukiwa ni athari ya muda mrefu ambayo inaweza kutokea kwenye vinasaba (DNA) ya seli ya binadamu.

2. Virusi ni vitu gani:
Virusi ni vimifuko ya vipande vidogo sana ya vinasaba (genes). Kuna virusi ambavyo genetic material yake ni DNA tupu na zingine ambazo ni za RNA tupu. Kirusi cha ukimwi ni cha RNA chenye genetic code 9 tu. Kirusi cha coronavirus nacho ni cha RNA na kina genetic codes 56.

Seli ya kirusi haina saitoplasm. Yaani hizo RNA au DNA zake zimehifadhiwa kwenye gamba (envelope) la protein. Kwa coronavirus gamba hili la protein ni la duara lenye miiba midogo midogo mingi (spike protein). Maji ya sabuni (soapy water) huweza kulisambaratisha (denature) gamba hili kwa urahisi na kukiua kirusi hiki. Ndiyo sababu ya kuwashauri watu kunawa mikono yao kwa sabuni mara kwa mara. Pia joto la nyuzi 45 hadi 56 C kwenye mazingira ya unyevunyevu huweza kulisarambaratisha gamba hili. Hii nayo ndiyo sababu ya tafiti mbali mbali duniani ambazo zimeweza kuonesha faida ya steam inhalation therapy ambao kwetu tunaita kujifukuzia.

Kwa kuwa virusi havina saitoplasm ili viweze kuzaliana zinahitaji kuingia kwenye seli za kiumbe kingine chenye saitoplasm. Hivyo zinaingia kwenye seli ya binadamu kwa lengo la kwenda kuzaliana. Kikishaingia kwenye seli ya binadamu genes ya virusi hivi huchukua kamandi ya maelekezo na usimamizi wa viwanda vya saitoplasm. Vinaamurishwa kufanya kazi ya kuzalisha virusi tu. Kazi zingine zinasitishwa. Hivyo seli zizovamiwa na virusi hivi zinageuzwa kuwa viwanda vya kufyatua virusi tu na vikishafyatuliwa vinavyamia seli zingine. Seli za askari wa mwili (immune cells - B lymhocytes, T lymphocytes, macrophages, Killer cells, cd4 cells etc) zinaingia vitani ambayo matokeo yake ni kifo au kupona.

3. Chimbuko la chanjo za SARS-CoV-2
Baada ya mlipuko mkubwa wa SARS (kiswahili chake Changamoto la Upumuaji) wa kirusi cha CoV-2 au coronavirus wa pili huko Wuhen, China mwezi Nov 2019 wahandisi mahiri wa vinasaba waliingia kazini kumchakata huyu kirusi. Hadi March 2020 wakawa wameweza ku decode the entire genetic code ya kiumbe hiki kidogo ambacho hadi wakati huo hakuna aliyekuwa anazijua hapa duniani. Mchina angeweza kukaa na king'amuzi hicho kwa siri peke yake maana ilikuwa ni uvumbuzi mkubwa wa siri ya maisha ya kirusi hiki. Lakini kwa upendo wa kipekee aliamua kuwasambazia bure maabara zote kubwa za genetic engineering ulimwenguni. Maabara hizi zilipokea kwa furaha ving'amuzi hivi na mara moja kuanza kucheza na vinasaba za kirusi hiki ili kupata dawa au chanjo ya kumwangamiza.

Bahati mbaya au nzuri zilijielekeza zaidi kwenye genetic code ya gamba la mdudu huyu - the spike protein genome. Ziliona hapo ndipo rahisi kummaliza mdudu huyu. Clinical trials zikafanyika haraka haraka. Ilikuwa ni fursa kwa tafiti zao za tiba kwa njia ya vinasaba zilizokuwa zimekwamishwa na FDAs zao kwa miaka mingi sasa kupewa ruhusa angalao ya dharura. Hadi kufikia December 2020 zikawa zimepata hiyo emergency approval na kuanza mass vaccination ya watu wote duniani kama phase IV clinical trial.

Cha kushangaza Mchina ambaye ugunduzi wake wa vinasaba ndiyo ulipelekea utengenezaji wa hizo chanjo, yeye chanjo yake haikutumia teknolojia hiyo. Yeye chanjo yake inatumia kirusi chote (the whole virus with its entire structure including the entire genome intact) kilichopunguzwa makali kama ambavyo zilivyo chanjo za magonjwa mengine tulizozizoea.

Chanjo hizi za wengine ni kama ifuatavyo:

- Pfizer na Modern: Hizi saitoplasma ya seli za binadamu inaingiziwa mRNA kuiamuru izalishe magamba (spike proteins) ya virus vya corona. Unapata kinga dhidi ya magamba yake na hivyo hataweza kuingia tena mwilini mwako kama ataendelea kubaki na gamba lile lile. Ndani ya muda mfupi imeonekana kwamba gamba la kirusi hiki ni kama la kinyonga. Hujibadilisha mara kwa mara kutegemea na mazingira. Kwa muda mfupi zaidi ya aina 7 ya magamba haya yamegundulika - kuna South Africa variant, UK variant, Brazil variant, na majuzi Kenya variant na kadhalika.

Chanjo hizi za mRNA ni ngumu kuzitunza kwani zinahitaji ubaridi wa -20 C kwa Moderna na -70 C kwa Pfizer.

- Johnson & Johson, AstraZeneca na Gamaleya (Spunik V from Russia):
Ili kutatua tatizo la uhifadhi, chanjo hizi zinatumia DNA adenoviruses zilizofanyiwa engineering kubeba ndani yake gene ya spike protein ya CoV-2. Tofauti kati yake ni aina za hizo adenovirus zilizotumika kama kibebeo. Ile ya Astra Zeneca inatumia kirusi cha mafua ya sokwe (chimpanzee flue virus). Ile ya Urusi ina viral vector mbili (Ad26 na Ad5). Ile ya J & J ina viral vector Ad26.

- Efficacy ya chanjo hizi kwa matokeo ya phase III clinical trials: Moderna 94%, Pfizer 95%, Gamaleya 91.4%, AstraZeneca 62%, Johnson & Johnson 62%.

4. Coverage ya chanjo huko ughaibuni:
Zoezi la chanjo huko ughaibuni na america lilianza mwanzoni mwa mwezi December 2020. Lilienga kuanza kwa wale waliokwenye hatari zaidi ya kupoteza maisha kwa gonjwa hili ambao ni wanaohudumia wagonjwa hawa mahospitalini, wazee wenye umri zaidi ya miaka 70 na wenye magonjwa hatarishi km kisukari, magonjwa ya moyo au figo au maini, saratani na ukimwi.

Hadi kufikia tarehe 4 March ni wastani wa asilimia 5 tu ndiyo walioweza kuchanjwa ndani ya muda huo wote wa miezi mitatu pamoja na hamasa kubwa iliyofanyika na inayoendelea kufanyika. Sababu kubwa ni wasi wasi walionao wananchi pamoja na baadhi ya wanasayansi wao kuhusu chanjo hizo zinazocheza na vinasaba za genes zao. Bado kuna vitu vingi havijajulikana kisayansi. Kwa mfano unaambiwa hata ukichanja lockdown, kuvaa barakoa na mambo mengine unaendelea nayo kama awali. Yaani hata hiyo efficacy yake hawaiamini.

Halafu wanaona kabisa licha ya kuchanja gonjwa hili badala ya kupungua huko kwao limekuwa likiongezeka. Kwa nini?
Vaccination coverage kwa baadhi ya nchi zao ni kama ifuatavyo:

USA 7.7%, Belgium 7.2%, Italy 7.8%, France 7.1%, Netherland 5.9%, Russia 3.7%, Bulgaria 3.5%, Sweden 8.1%, Germany 8.1%, Spain 8.6%, Portugal 8.8%, Greece 9.5%,

5. Huu upendo kwa nchi za Afrika umetokea wapi?:
Wakati kasi ya coverage ya chanjo kwenye nchi zao zimekuwa za kusuasua, sisi wametuandama tuchanjane haraka. Wametupa au kutuahidi kutupa chanjo bure zinazotosheleza kuchanja watu laki 5 kila nchi ya Afrika. Masharti ya chanjo hizi za bure ni kwamba zichanje watu wenye afya nzuri walio na umri wa miaka 18 hadi 45. Wasiwe na magonjwa mengine ye yote including morbid obesity. Wamediliki hata kutuamuru kuwa watu hawa wawe ni walimu na polisi wetu.

Kwa nini wanataka watu wa aina hii ndiyo tuwachanje wakati watu wa aina hii miili yao iko imara kukabili virusi vya corona kwa asilimia 99.9%?
Kwa mjanja atagundua kuwa wanataka kuwafanyia a phase IV clinical trial watu hawa ambayo matokeo yake yanaweza kuondoa wasi wasi walionao watu wao huko ughaibuni kuhusu hizi chanjo.

Wanatusubiri sisi tuchanjane. Hadi sasa nchi 10 za Afrika zimekubali 'msaada' huu na faster faster zimepelekewa hizo chanjo na wameanza kuchanjana.

Nchi inayokataa au kusuasua kupokea 'msaada' huu inaandamwa kinoma na inachukuliwa kama adui. Sisi hatujaukataa bali tumewaambia watupe muda wa wanasayansi wetu kufanya uchambuzi na utafiti. Loo ona mashinikizo tunayoyapata hadi kutoka kwa watu tunaowaheshimu sana. Tupeni muda kidogo. Uamuzi tutatoa bila kushinikizwa tuzitoe wapi na tumchanje nani.

6. Ushauri wangu: Tuangalie zaidi chanjo ya Sinopharm ambayo imeiwezesha China kuudhibiti vizuri sana ugonjwa huu.



Aiseee Mibongo ni mipwenge kabisa umeijaza ujinga, yote inakusujudia
Anzisha kanisa hapa, utakuwa na unatembelea VOGUE kama kina Gwaji

USA 7.7%, Belgium 7.2%, Italy 7.8%, France 7.1%, Netherland 5.9%, Russia 3.7%, Bulgaria 3.5%, Sweden 8.1%, Germany 8.1%, Spain 8.6%, Portugal 8.8%, Greece 9.5%
Hizi nchi zote wanakabana koo wenyewe kwa wenyewe kwa upungufu wa chanjo.
Halafu unaleta utopolo ambao uko shallow kuzidi utopolo wenyewe,
Mbona hamna mabingwa wa tiba duniani UK kwenye hii pumba listi yako , unajuwa idadi ya waliochanjwa
Au nikuwekee cheti changu hapa uamini
 
Chanjo yangu naenda kupata jumatano,wala sina doubt..even if ingekua inafanya kazi 20% ningechukua....
 
You sound like you’re high on something Chief!

No offense meant!

You sound like you're high on something. That makes the two of us!

No offense meant chief!

Nyani kuona kundule umnunulie kioo:

IMG_20210218_174254_207.jpg


Akili ndogo sana! Kama yule Daktari.

Bitter that you can't fool all the people all the time, uh?

Relax.

Take it easy.
 
Back
Top Bottom