Kwa ujumla huyo ziro hajitambui, hajielewi, amejawa na unafiki. Hakuna anachosimamia, ziidi ya unafikiView attachment 1896435
Nakumbuka Makonda amewahi kuwaagiza polisi kumkamata Mbowe baada ya kumtaja kwenye orodha ya madawa ya kulevya. Sirro hakusubiri maandishi. Makonda huyohuyo akaagiza Aabdul Nondo akamatwe kwa tuhuma za kujiteka. Sirro hakusubiri maandishi, licha ya kwamba yalikua maelekezo ya Mkuu wa mkoa tu. Leo Waziri katoa maelekezo anasema anasubiri maandishi?
Anyway ni barua gani Sirro alipewa kuwakamata vijana wa Chadema waliokua ibadani huko Mwanza juzi jumapili? Je Sirro alipewa barua na nani kumkamata Askofu Mwamakula na Prof.Azavel Lwaitama usiku wa manane hotelini kama majambazi na kuwaweka rumande bila hatia? Sirro alipewa barua na nani kuwakamata vijana wanaokwenda mahakamani kufuatilia kesi ya Mwenyekiti Mbowe? Why these double standards?
Credit: Malisa GJ