Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Kuna msemo maarufu usemao: "To judge a leader, look at the organisation ten years later"
 
TzPride,

With due respect, we have been tolerant for 45yrs, slowly waTz are losing patience especially when they see things moving in a wrong direction. There has been so much crap of late eg mining contracts, IPTL, you name it all. So do you want WaTz kukaa kimya while some segments of the comminities (watawala and their cronies) seem to siphon all the goodies from those shady deals? We acha na sisi tupigie makelele rather than just sitting idle kama mwanakondoo anayenyolewa!
 
Ndugu zangu haya ni matokeo ya mfumo mbovu, tusipo chukua hatua tutaendelea kupiga kelele wakati manyang'au wakiendelea kutuingiza mkenge.

Mfumo wa uchaguzi, hapa kuna tatizo kubwa, tukianza na chakato wa kumpata mgombea ndani ya chama hapa ni fujo, kila mmoja anatamba kwa wingi wa fedha kuwashawishi wapambe, hizi pesa wanapata wapi? isije ikawa kuna maspeculator ambao wanatoa hizi pesa na ikitokea mgombea akashinda inabidi kutoa fadhila ya mkitaba minono bila kuangalia maslahi ya taifa.

Mfumo wa sheria, inashangaza kuona kuwa sheria zetu zinawapa viongozi wetu nguvu kubwa ambayo hupelekea kuwa na kiburi, kulingana na katiba yetu rais hawezi kushitakiwa kwa lolote afanyalo akiwa madarakani, hii ni hatari kubwa kwa mustakabali wa taifa.

Mfumo wa uteuzi wa viongozi, hapa kuna tatizo, rais anamamlaka makubwa kwani huchagua viongozi wawe mawaziri n.k kwa utashi wake mwenyewe na watu wake wa karibu [chama] hapa ndugu zangu unategemea nini kama si mazingira ya kubebana. je? tunayo miiko ya viongozi

Ninaheshimu mwazo yene wana foram, ila inabidi tubadili mikakati, tuna haki ya kulaumu na kupiga kelele kuwa imani kwa raisi wetu inapungua, tupige kelele maradufu tuhakikishe tunakuwa na mifumo thabiti ya nchi yeti ili manyan'au wasi take advantage.

Vyama vya siasa vimelala mara zote hukurupuka uchaguzi ukikalibia na mara zote huwa wamechelea.
 
TzPride
"Mchanga wa dhahabu mtu mmoja anaongelea hajui kabisa nini hicho kama ukitaka undani wake niulize uone kwa nini unapelekwa huko."

Ndugu TzPride, naomba unieleze kwa nini mchanga unapelekwa huko...
 
TzPride.

Mijadala ya hapa haitegemei Wakenya wamesema nini, Wanabodi hapa wako MAKINI wana akili zao na wako hapa kujadili issues zinazo husu Taifa letu na kwa faida yetu. Kenya yaweza chukuliwa kama mfano kwa jinsi walivyo serious kudumisha uchumi wao kwa faida ya wananchi wao. Wanabodi kuikosoa serikali ni kwasababu wanaitakia mema Tanzania period. Issues hapa zinamwagwa ni kwa sababu Wanabodi wengi wana VISION yenye mlengo wa maendeleo.

kwa taarifa yako, wanabodi hapa pamoja na ku-criticise, wakati mwingine wanatoa solutions, na tumeshuhudia zingine zikifanyiwa kazi na serikali yetu. Mfano Mwanakijiji alipendekeza kule BCS mfumo kwa Polisi jinsi ya ku-curb crime ambao sasa unatumika DSM kama model.

Wewe umeona majenereta RDC kufungwa ndio ushindi!!, Hata IPTL mitambo yao nayo ilifungwa........hivi hilo nalo hulioni.

Idea ya kupata alternative source of power (electricity) ni Nzuri, Tunachopiga kelele hapa ni njia zitumikazo kupata hizo alternative source na hatima yake ambayo siku zote imekuwa unnecessary mzigo kwa mwananchi wa kawaida. Jaribu kusoma zile post(najua hujazisoma) za Mkandara kuhusu IPTL pamoja na Mwanabodi mwingine aliyetoa data kuhusu Ufeki wa RDC na jinsi walivyo-inflate price za hayo majenereta yako unayoyashangilia.

Tafadhali, usitulazimishe wengine kufikiri kuwa unaelekea kuwa 0.5Ngw
 
Wazee!


This is a wake up call! there is a very strong need to curb the ever growing trend of "ufisadi" in our country before it lands us in even more serious trouble. As we encourage more foreign investors, we are also exposing our "uozo" in our society. Our neighbours are already in for it! http://news.bbc.co.uk/1/hi/uk_politics/6135244.stm
 
Rais wetu JK ktk hutuba yake ya kwanza Bungeni aliahidi mambo mengi muhimu sana... Je, tumefika wapi leo hii!...Mwaka ndio umeshakatika hivyooo!

Ebu tujikumbushe upya baadhi ya ahadi zake ktk lugha ya kigeni!... ALITO AHADI hivi:-

Let me now address the central tasks of the Fourth Phase Government.
The CCM Election Manifesto for the 2005 General Elections identified two central tasks.
First, to take Tanzania out of the morass of a still backward and dependent economy, and modernise it.
Second, to include more Tanzanians in the national economy, and empower them to fight poverty.
Honourable Speaker:
In performing these central tasks, I should like the people of Tanzania to expect action on the following ten core issues:
The Fourth Phase Government will ensure peace, stability and unity;
The Fourth Phase Government will protect and promote all the successes attained during all the previous three phases of government;
The Fourth Phase government will carry forward the war on poverty, illiteracy and disease, with new vigour, new zeal and new speed;
The Fourth Phase Government will fulfil its governance and development responsibilities, and will focus on good governance and accountability; the rule of law and respect for the human rights of all people;
The Fourth Phase Government will enhance its capacity to maintain law and order, and protect people’s lives and property. We will resolutely fight crime, and stop armed robbers from operating with impurity;
The Fourth Phase Government will ensure our national borders remain secure and inviolable. We will not allow anyone or any country to infringe on our territory, or our freedom;
The Fourth Phase Government will do all in its power to maintain good relations with all countries and with regional and international organisations;
The Fourth Phase government will pay special attention to the needs of disadvantaged groups, including women, youth, children, the disabled and orphans;
The Fourth Phase Government will lead a new initiative on environmental conservation so that future generations may inherit a beautiful country with a secure base for sustainable development; and
The Fourth Phase Government will promote sports, as
well as cultural and other forms of entertainment.
 
Ingawa JK hajapiga hatua kubwa sana ila kulingana na ahadi zake hizo kume ameshafanikiwa kidogo kama ifuatavyo:


(a) The Fourth Phase Government will ensure peace, stability and unity;
Baada ya Nyerere kufanya kazi ya kujenga National Unity, hakuna serikali itakayokuja na kuahidi kufanya jambo hili. Nadhani angeahidi kuwa " ... will not disturb the existing peace, stability and unity". Kwa hilo serikali inatakiwa ku-maintain status quo tu kama alivyofanya, an hivyo amefanikiwa.


(b) The Fourth Phase Government will protect and promote all the successes attained during all the previous three phases of government;

Huu mkataba ya Richmond ni dalili tosha kuwa ana "promote" yaliyofanywa na BWM. Halafu kuendelea kutunza mikataba feki kama ITPL na mikataba ya madini inaonyesha kabisa kuwa ana "protect" yaliyofanywa na BWM. Kwa hiyo kulingana na ahadi hiyo naona kama kuna mafanikio kdiogo katika utekelezaji wake.


(c) The Fourth Phase government will carry forward the war on poverty, illiteracy and disease, with new vigour, new zeal and new speed;

Hapa iko ngoma. Probably kama mapambano hayo ni kwa faida ya wateule wa serikali na watoto wao amabo ndio wanaopata contract nono za kuwaondolea umaskini, ndio wanaopata nafasi za kusoma na kutibiwa nje wakati wale wa kawaida wanasota na kugomagoma pale bongo kwa kukosa mikopo ya serikali kulipia masomo yao. Hospitali tena ndiyo basi tu. Nadhani kipengele hiki Mzee hajakifikia kuanza kushughulikia watanzani wote. Kwa sasa hivi ni hakuna lolote tunaloweza kutathmini.


(d) The Fourth Phase Government will fulfil its governance and development responsibilities, and will focus on good governance and accountability; the rule of law and respect for the human rights of all people;

Hapa kuna mawazo mchanganyiko. Kufukuzwa kazi Brother Dito inawezeakana kuchukuliwa kuwa ni sehemu ya accountability ingawa sioni kama kulikuwa na njia nyingine wakati jamaa yuko lupango. Ila kule kuhamisha mawaziri nadhani mzee alichemsha; kulikuwa hakuna accoutability yoyote. Dili ya Richmond limeweka doa kubwa sana katika record ya good governance. Rule of law inafanya kazi kwa Brother Dito ingawa kuruhusu Mzee Mkono amtetee wakati ni mbunge kunaleta dosari kidogo. Angalau angeacha kampuni yake ifanye kazi hiyo lakini siyo yeye personally.


(e) The Fourth Phase Government will enhance its capacity to maintain law and order, and protect people's lives and property. We will resolutely fight crime, and stop armed robbers from operating with impurity;

Hii kwa kweli mzee kajitahidi sana. Kama bado kuna ujambazi siyo kosa la serikali yake ila labda ni kutoka na usugu wa tatizo hili. Kwa kupambana na ujambazi kweli nampa 98%


(f) The Fourth Phase Government will ensure our national borders remain secure and inviolable. We will not allow anyone or any country to infringe on our territory, or our freedom;

Inawezekana kuwa nia ya kufanya hivi ipo lakini sioni kama serikali ina mkakati wowote wa kulitekeleza. Wakati huu ambao serikali inaonekana kujiachia kuwa mambo yote ndani EAC, na mashirika yote ni mali ya South Afrika, sioni kama serikali inaweza kuzuia watu kutoka SA kuja kufanya kazi pale kwetu na hata kuingilia uhuru wetu: vivyo hivyo kwa Kenya na Uganda. In general hakuna kilichokwisha fanyika cha maana kwa mfano kuwasaka walioko nchini kinyume cha sheria na kuwandoa kwa nguvu.


(g)The Fourth Phase Government will do all in its power to maintain good relations with all countries and with regional and international organisations;

Ni vigumu kupima mafanikio kwenye lengo hili kwa sababu ni lengo trivial kabisa. Ni Idi Amin tu aneyeweza kushindwa kulitekeleza hili. Hata hivyo serikali ingehakiki upya upangaji wa mabalozi wake wasiwe skewed upande mmja wa dunia. South America na nchi za Pacific hatuna uwakilishi mzuri


(h)The Fourth Phase government will pay special attention to the needs of disadvantaged groups, including women, youth, children, the disabled and orphans;

Bila kuwa na tafasiri bayana ya "needs of disadvataged groups" huwezi kupima mafanikio yoyote hapa. Ila jamaa mmoja aliwahi kuandika kuwa "needs of women have been addressed;" kuna mawaziri wengi wa kike kuliko serikali yoyote iliyotangulia. Vile vile wanawake wanapata upendeleo maalumu kuonana na viongozi kueleza matatizo yao.


(i)The Fourth Phase Government will lead a new initiative on environmental conservation so that future generations may inherit a beautiful country with a secure base for sustainable development.

Serikali ilirithi uozo kabisa katika swala la kutunza mazingira na rasilimali za asili za nchi. Mikataba ya uwindaji na uchimbaji madini vyoote vinachangia kuharibu mazingira. Serikali haijafanya lolote kurekebisha mikataba mibovu iliyorithiwa kutoka serikali zilizotangulia. Kwa hiyo tathmini ya ahadi hii ni inaonyesha mapungufu katika utekelazaji


(j) The Fourth Phase Government will promote sports, as well as cultural and other forms of entertainment.

Hapa kwa kweli serikali imefanya makubwa sana hadi Taifa Stars ikawa siyo tena kichwa cha mwenda wazimu.
 
Mzee Bob,

Kuna hela za kuleta maendeleo mikoani kwa ajili ya kuanzisha ajira kwa vijana shillingi Billioni moja, kwa kila mkoa!
 
Wazee Donors wanaanza kuwa dissappointed na hii "new vigour, new zeal and new speed", je tutafika?

Ububu wa serikali washtua mataifa makubwa ya Ulaya
HATUA ya Serikali ya Awamu ya Nne kukaa kimya pasipo kuweka bayana hatua zozote za wazi dhidi ya tuhuma kadhaa zinazoelekezwa kwa taasisi kadhaa za umma na watendaji wake, sasa zinaonekana kuanza kuishtua jumuiya ya kimataifa...http://www.freemedia.co.tz/daima/2006/11/25/habari1.php
 
Kichuguu,
Awamu ya nne haina interest kabisa kuendeleza ya Nyerere. Ukimsikiliza rais kwa makini yeye kajifunika kanga walizovaa akina Mwinyi na Mkapa. Period. Hawa ndio mfano wake, kwa kasi mpya na ari mpya. Kwa hiyo usishangae ya Richmond.
 
Kichuguu,

Kama kawaida, umeangalia kila kitu kwa makini. That is very good.

Tukumbuke msemo kwamba "talk is cheap". JK anapenda kusema kwa namna ya kufurahisha wasikilizaji, na wako wengi ambao wanamshangilia kama mpira, bila kujiuliza atatekelezaje ahadi zake.

Dar es Salaam ni kitovu cha taifa. Mwananchi wa kawaida aliyeko Dar hana maji, hana umeme na ana shida hata ya fedha za daladala. Na akipata nauli, usafiri wenyewe ni wa shida ajabu. Mtu wa kawaida Dar kwa sasa ana maisha ya shida kama yale ya 1980 - 1985. Ule unafuu uliopatikana wakati wa Mzee Ruksa na wa Nchee Nkapa haupo tena.

Maneno ya serikali ni mengi, matendo hakuna. Yako maneno ya kuleta usafiri wa haraka wa mabsi makubwa, ya "shida ya meme itaisha karibuni", na hata ya kujaza Bwawa la Mtera kwa mvua za kutengeneza. Usanii mtupu huu!

Serikali ya JK ni ya maneno mengi, matendo machache. Ya Mkapa ilikuwa ya maneno hakuna, ni matendo tu. I liked it. Kwa maoni yangu, serikali ya sasa ni ya kitapeli mno.

Augustine Moshi
 
FUKUZA WALA RUSHWA

JK atatupeleka pabaya – kwa maoni yangu huyu jamaa ni hatari na inabidi ajifunze kwa haraka sana na kuwa makini – ni kwanini anajikombakomba sana kwa M7. Ni mara ya ngapi amekwenda hapo Uganda tangu awe rais. Matatizo ya bongo hayawezi kutatuliwa kutoka kwa M7 na kukaa kimya bila kufukuza wala rushwa.

Kitu ambacho mpaka sasa ameweza ni kusafiri nje – swali ni je bado anaendelea kuwa foreign affairs minister?

Acha hilo angalia jinsi alivyokuwa anamsujudia mfalme wa Japan? Na press ya TZ walivyowajinga wakaiweka kwenye front pages. Hajafahamu kwamba yeye sasa ni kiongozi wa watu zaidi ya millioni 40 chunguza hiyo picha na zile zinazopigwa akikutana na viongozi wengine. Ni aibu tupu? Hata balozi wa Tanzania alipokutana na malkia wa Uingereza ilikuwa tofauti na ni lazima aache kukutana na matapeli uchwara ambao sasa wamefanya Ikulu ni nyumbani kwao – huyu jamaa ni limbukeni kweli kweli.

Na mtu anayempangia hizi safari sijui naona amelogwa au ni yeye mwenyewe haambiliki – kuna nchi hapa duniani wamekuwa ni marafiki wakubwa wa Tanzania tangu tupate uhuru ambazo ndio marafiki wa kweli, yeye cha kwanza aliona Marekani na Uarabuni ndiko kwa kwenda. Sasa priority yake iko wapi?

Ndio sababu utaona matatizo lukuki ambayo sasa hivi yanaiandama serikali yake kwa sababu waliomzunguka wameisha mjulia na hawana wasiwasi naye. Majority ni wezi.

[TANZANIA INA HESHIMA YAKE, SASA TUMEMCHAGUA KUWA RAIS KAMA HAWEZI KAZI BASI AJIUZULU].

_______________________________
Dua la kuku halimapati mwewe
 
Mkandara: umetoa ahadi zile tu alizozitoa pale bungeni. Lakini kuna zile ahadi lukuki alizozitoa katika kampeni. Nafikiri hizi nazo akumbushwe. Nitazitafuta, nikizipata nitazipost hapa.
 
Wazalendo;

Kwa kifupi ni kwamba, kwa mwendo huu sioni AMANI WALA UMASKINI kututoweka. Sijui kama utasema kuwa TZ tuna amani wakati wananchi wanashindwa kuhudumia familia zao. RAIS kila siku KIGUU NA NJIA wahitimu wanashindwa kwenda VYUONI, UMEME, MAJI, na matatizo mengine mengi. Nafikiri inabidi AMANI tusiichukulie tu kwamba WANANCHI HAWAJABEBA MAPANGA basi tuna amani. Hawa viongozi wanazidi kujineemesha wao wenyewe bila kujali hali ya wananchi.

PONGEZI KWA CHUO KIKUU KWA KUANZA KUCHAMBUA HALI YA UCHUMI HASA YA MWANANCHI WA KAWAIDA PAMOJA NA KUANZA KULETA MJADALA WA ZABUNI AMBAZO SERIKALI INA-SIGN MAJUMBANI KWAO BILA KUELEZA WANANCHI UKWELI WA MAMBO KWA UWAZI. NAFAHAMU UDSM BADO NI MKONO WA SERIKALI LAKINI NATEGEMEA WATAENDELEA NA CHANGAMOTO HIYO.
 
KWA KIASI KIKUBWA AHADI NYINGI ZA KIKWETE ZILIKUWA ZINATOKA BILA MANTIKI YOYOTE. MOJAWAPO NI HILI LA KUTENGENEZA AJIRA WAKTI SERIKALI IMESHAUZA MASHIRIKA YOTE NA KUJITOA KATIKA BIASAHARA YA AINA YOYOTE. AHADI NYINGINE AMBAYO NINAITAZAMA KWA MAKINI NI ILE YA KUJENGA SHULE ZA SEKONDARI 500 KILA MWAKA.

=====================


Kikwete Atahadharishwa


*ILO yasema ajira milioni moja kufikiwa ni kazi
*Yasema njia bora ni kuimarisha uchumi wa nchi

Na Mkombe Zanda, Morogoro

SHIRIKA la Kazi Duniani (ILO), limeitaka Serikali ya Tanzania kuchukua tahadhari kubwa katika mpango wake wa kuzalisha ajira milioni moja nchini, kwa kuimarisha kwanza uchumi wake, kwani bila kufanya hivyo kamwe mpango huo hautafanikiwa.

Mshauri wa Ufundi wa ILO, Profesa Vremudia Diejomaoh, aliitaka Serikali kutambua kuwa mpango huo hauwezi kufanikiwa wala kuwa endelevu na wenye manufaa kwa wananchi wa kawaida nchini, endapo uchumi wa Taifa hautakuwa imara na wenye uwezo wa kukabiliana na mahitaji halisi ya uanzishaji wa ajira hizo.

Profesa Diejomaoh alisema ili ajira hizo ziweze kupatikana ni lazima kwanza Tanzania iwe na uchumi madhubuti utakaokuwa na uwezo wa kutoa fursa za upatikanaji wa kipato cha uhakika kwa wananchi, hali ambayo pia itatoa fursa ya kuanzishwa kwa ajira nyingine za kuwasaidia Watanzania.

Alisema uchumi imara ndiyo njia pekee ya kuimarisha na kuzalisha zaidi ajira kwa wananchi wa kawaida, hivyo aliitaka Serikali kuzingatia kwanza msingi huo katika utekelezaji wa mpango wake.

Profesa Diejomaoh alitoa tahadhari hiyo juzi mjini hapa katika mkutano wa siku mbili wa vyama vya wafanyakazi nchini, wa kujadili upatikanaji ajira.

Kimsingi aliitaka Tanzania kutambua kuwa mazingira yaliyopo hivi sasa nchini, hayatoi fursa nzuri katika utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya kimataifa, kuhusu upatikanaji wa ajira nyingi kwa wananchi wa kawaida, hali ambayo imeendelea kuwa vikwazo katika utengenezaji wa ajira kwa wananchi.

Aidha, Profesa Diejomaoh aliishauri Serikali kuipa kipaumbele zaidi sekta binafsi kwenye utekelezaji wa mpango huo, kwani hiyo ndiyo sehemu inayomiliki soko kubwa la ajira nchini.

Kutokana na hali hiyo, aliitaka Serikali kurekebisha kasoro hizo ili kuhakikisha Tanzania inakuwa na fursa nzuri zaidi katika kuwawezesha raia wake kujipatia ajira mbalimbali zenye uwezo wa kuwakwamua kimaisha.

Miongoni mwa marekebisho hayo, Profesa Diejomaoh aliyataja kuwa ni kukuza fursa za kiuchumi na biashara, kuboresha mfumo wa utawala bora, kuboresha miundombinu hasa vijijini, kupunguza masharti ya uwekezaji na kuboresha mfumo wa elimu kwa raia wake.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA), Bw. Nestory Ngulla, aliitaka Serikali kuhakikisha kuwa mpango wa ajira milioni moja unatilia mkazo zaidi katika utengenezaji wa ajira zenye uwezo wa kumkwamua mwananchi wa kawaida, kutoka kwenye hali duni ya kiuchumi aliyonayo hivi sasa.

“Ni lazima tuhakikishe mpango wa ajira milioni moja unatengeneza ajira bora na si bora ajira. Tunataka ajira zenye kumwezesha Mtanzania kukabiliana na changamoto za sayansi na teknolojia zilizopo hivi sasa, ili aweze kujikwamua kiuchumi.

Mkutano huo wa siku mbili unatarajiwa kutoa mapendekezo kwa Serikali kuhusu namna ya upatikanaji wa ajira kupitia sekta binafsi nchini.

Kabla na baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Rais Jakaya Kikwete, alitoa ahadi za Serikali yake kutengeneza ajira milioni moja katika kipindi cha miakamitano ya uongozi wake.

Wakati huo huo, Ramadhan Libenanga anaripoti kwamba Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya vijana Kapteni mstaafu John Chiligati, amesema Serikali katika utekelezaji wa ahadi zake kwa wananchi, tayari kwa kipindi kifupi imetoa jumla ya sh. bilioni 10.5 kati ya sh. bilioni 21 zilizotengwa kwa kila mkoa, kupewa sh. bilioni moja na
tayari zimewasilishwa katika Benki za CRDB na NMB nchini.

Waziri Chiligati alisema Serikali pia imeanzisha utaratibu wa kutambua na kurasimisha rasilimali na biashara za Watanzania wanyonge walio katika sekta iliyo rasmi kupitia mpango wa MKURABITA wenye lengo la kuandikisha na kutoa vyeti vya umiliki kwa rasilimali hizo na kutumiwa kwa vyeti hivyo kama dhamana na ya mikopo kwenye mabenki.

Akifungua mkutano wa Jumuiya za Wafanyakazi kuhusu Programu ya Ajira ya
Taifa mjini hapa jana, Waziri alisema hiyo ni moja ya jitihada za Serikali iliyopo madarakani kutekeleza ahadi yake iliyotolewa na Rais Kikwete wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka jana kuhusu kutoa ajira milioni moja kwa kipindi cha miaka mitano 2006-2010.

Alisema Serikali, imechukua hatua mbalimbali za kusaidia kukua kwa uchumi na hivyo kuongeza ajira ikiwamo kuanzishwa kwa mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo (ASDP) ambapo wakulima wadogo watapewa pembejeo, zana za kilimo na masoko.

Kwa mujibu wa Waziri Chiligati kuwa katika mpango huo, jumla ya sh. trilioni 2. 5 zimetengwa katika bajeti ya mwaka huu kwa ajili hiyo.

Mbali na hayo Waziri Chiligati alisema ukosefu wa ajira ni tatizo sugu na linaloleta kero kwa nchi zote zinazoendelea ikiwamo Tanzania.

Alisema kulingana na taarifa za utafiti wa nguvukazi uliokuwa ukifanywa, mwaka 2000 na 2001 kiwango cha ukosefu wa kazi nchini kilikuwa ni asilimia 12.9 na ulibainisha kwamba kila mwaka watu wapatao 700,000 huingia katika soko la ajira na kundi linaloathirika zaidi ni vijana na wanawake.

Waziri Chiligati alisema tatizo linalochangia kupunguza kasi ya kukuza ajira ni uwekezaji finyu kwenye sekta zenye uwezo mkubwa wa kukuza ajira kama vile kilimo.

Aidha, alisema hivi sasa asilimia 82 ya Watanzania wote wanategemea kilimo kwa maisha yao na kwa ajira ambapo suluhisho ni namna ya kuboresha kilimo na sekta iliyorasmi ili nafasi nyingi zaidi ziweza kupatikana.

Chiligati alisema kuwa njia nyingine ya kukuza uchumi ni kuwekeza zaidi katika maeneo ambayo yatahitaji nguvu kazi kubwa kama shughuli za viwanda, ujenzi wa barabara, nyumba viwanja vya ndege na mabwawa.

Alisema suala la kukuza uchumi na kuongeza ajira linahusu jamii yote na hasa sekta binafsi ambayo ndiyo sekta itakayotoa asilimia kubwa ya ajira nchini
 
The Fourth Phase Government will fulfil its governance and development responsibilities, and will focus on good governance and accountability; the rule of law and respect for the human rights of all people;
.

Hapa kafanya Kinyume

Kupitishwa mswadwa wa kuruhusu waziri wa TAMISEMI kuchagua madiwani wa watatu katika halmashauri,ililenga kudamaza utawala bora na sio kuboresha.

Kuteua wabunge kuwa wakuu wa mikoa ni kituko kingine cha utawala bora.

Ameshindwa kuainisha vizuri vipaumbaule vya serekali yake. Mwaka wake wa kwanza umejaa usaniii na sanaa za maonyesho.Amejisahau kabisa, ameendelea kufanya kampeni kwa kutoa ahadi kem kem.Asopobadilika na akiendelea na mwenendo huu,Tz itakuwa na hali mbaya 2010.

Taifa Stars ni moja ya maeneo adimu ambayo ameng'ara.
 
Back
Top Bottom