Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Ina maana Msabaha huko africa mashariki ndiko atakakoweza!!!?


Hivi hasa ni LAANA GANI HII JAMANI? NI KWA NINI RAIS WA TANZANIA NAKUWA HANA UWEZO WA KUWAFUKUZA KAZI MAWAZIRI/WATU ALIOWATEUA?

YAANI UMETEUWE MTU KUFANYA KAZI KWA MANUFAA YA UMMA HALAFU MTU HUYO AIBE NA KUVURUGA, UKAMUACHA AU UNAMBADILISHA TOKA HAPA KWENDA KWINGINE!

KAMA RAIS ANAONA AMEISHWIWA WATANZANIA WANAOWEZA KUWA MAWAZIRI

SI AENDE MAREKANI AU NCHI NYINGINE AKAAZIME WATU ILI AWATEU KULIKO KUFANYA HII RECYCLING YA AJABU!

KALAMAGI NA MEMBE WATAIWEZA HIYO WIZARA YA MADINI?
 
serikali yote (mawaziri na raisna wakuu wa mikoa na wilaya) wapo kwenye kampeni tu za 2010. hawatulii unadhani wanaleta nini? mbona mpaka lowasa afike mahali ndo mambo yanaibuka je unadhani hakuna waziri alifika kilindi kabla ya lowasa kuona barabara haifai?

JK haaminiki na anapata sifa za bure na zinai[peleka pabaya Tanzania na mwisho ni hali mbaya isisyosemeka. subiri tupo na tutaona.

I CAN'T TRUST JK EVER
 
Mimi nawashangaa sana mnasema JK ana baraza la wasanii. Hivi kama wewe si mzinzi unaweza kuwa na marafiki wazinzi? JK ni msanii ndiyo maana anatafuta wasanii wenziwe .JK hivi mnampa sifa zipi na za nini ? Tangia kaanza kuzunguka mikaoni , nje ya Nchi , magerezani na mahospitalini na kuondoka kumekuwa na mabadiliko gani ? Jiulizeni halafu mnieleze kwama tangia aingie Ukonga na Segerea kumekuwa na mabadiliko gani na pia Muhimbili kaweka nini pale . Maana hata ku chekiwa afya alienda Ujerumani sasa mnasemaje ?
 
Hata ule mktataba wa billi gate na kikwete waliosaini dodoma utalifikisha taifa hili pabaya hapo baadaye.

Bilii gate atanufaika sana na atakuwa anakusanya hela nyingi san toka serikalini.

Ni afadhali uangalie upya. Ni afadhalia asiingie naye mkataba na kuna wataalam watakuwepo siku za karibuni ili kuweza kufanya mikakati ya Linux badala ya Windows. Au tuendelee kama ilivyokuwa zamani. Huyu bilii gate wamuombe tu achangie hela za ujenzi wa chuo kama anataka.

After ten years tutakuwa watumwa wa microsoft na bill gate.
 
Mzee Rufiji,

Maneno mazito hayo, lakini kumbuka kuwa mzee SAS ni basha huyo tena moto wa kuotea mbali huyo!
 
Mzee ES kweli SAS basha or just mudslinging?
 
Duh,

Haya yananikumbusha ya yule mtu-nyoka pale Buguruni Polisi ile miaka ya thamanini ambaye pamoja ya kudaiwa kuwa alikuwa pale polisi kila aliyetakiwa athibitishe madai yake hayo aliishia "aambiwa" na "wapo waliomuona". Ni akina nani hao? Jibu lilikuwa kimyaaaaa!!!! always. We are hearing similar stories again today.

Mzee Es said:
Mzee wangu wewe ni mbongo kweli?, Maana huku bongo sio siri tena na waliohusika wapo!
 
Duh, waheshimiwa humu karibu wataifanya hii forum iwe ni ya NYEPESI NYEPESI, na wazee wa data sasa wanakuwa wazee wa kuropokwa.

Anyway.. Mzee Mwanakijiji aliwahi kuusia humu ... kila mara nnaukumbuka usia ule .. 'read at your own perill'.
 
Hewala mzee wangu, tuendelee na mjadala ila utakapopata nafasi ulizia ya msaidizi wake yule luteni wa jeshi letu alikufaje kule Addis?

Hii forum hata siku moja haiwezi kuwa nyepesi nyepesi maana yote yanayoandikwa hapa huwa yanakuja kuthibitishwa, kama huyafahamu uliza kwanza kabla ya kurukia mambo,

zile kampeni za rais Dodoma zingeendelea for at least one more week yote yangetoka, na hata yeye mzee SAS, alishaambiwa mapema ndio maana mtandao walikuwa wamemsubiri tu baada ya uchaguzi Dodoma ajichuuze kulia hadharani ili wayafungulie, kama walivyomfanyia ya kumuua Karume, je kabla ya ule uchaguzi mtu angekwambia kuwa huyu mzee alihusika na kifo cha Karume, ungesemaje?

Wakati umefika wa wananchi kufanya utafiti wa kina juu ya hasa what mtandao did ili kuupata urais inaonekana kwamba wananchi hawafahamu kabisa, mzee wangu muombe mungu siku moja ulione faili la Ben, ambalo lilifanyiwa kazi na mtandao na lililomfanya akubali kuwaachia mtandao ngazi!

Huenda mbinu za mtandao zilikuwa chafu, lakini ninawaheshimu kwa jinsi walivyoweza kukusanya ukweli, ambao hata usalama wa nchi yetu umeshindwa kuukusanya, yale mafaili yamaadili ya CCM ambayo yalikuwa nahabari nyingi zakutoka usalama, yalikuwa yamejaa unafiki mtupu, mafaili ya kweli yalitengenezwa na Mtandao, ndio maana viongozi wote waliotengenezewa walifyata mkia, maana hawa mtandao wangeyafungulia wengine ingekuwa ndio mwisho wao wa siasa, ila ninaamini somewhere somehow kuna siku haya mafaili yatakuja ku-leak, ndipo wananchi watajionea wenyewe kuhusu viongozi uchwara tulionao!
 
Mzee Es,
SAS basha?... Mashaallah.. huyu ndiye anatakiwa kuwashughulikia viongozi wote wazembe serikalini. Nadgani viongozi watakaza misuri yao maanake sasa hivi wanachofanya viongozi wetu ni usenge mtupu.... ombaomba umalaya wa kuomba misaada, tunafungiwa kanyaboya kwa kila mradi... hii nini hii kwani watu hawa hawakusoma!
Wanahitaji basha kama Idd amin Dada alivyokuwa jambazi!...Hakuna haja ya kuwaua ila wapate aibu na adhabu ya kiume!
Tuyaache hayo, unajua nimejaribu kufikiri kwa nini JK kafanya mabadiliko ya mawaziri bila kumfukuza mtu. Na jibu rahisi nililopata ni kwamba. Hawa mawaziri wote na manaibu wake ni wale waliompigia kura CCM kule Chimwaga, sasa akiwaondoa uongozi ina maana kapunguza nguvu ya kura zake mwaka 2010. Na hiyo itaacha mwanya mkubwa kwa EL ambaye nasikia pia mwaka 2010 anataka kushika inkosikazi. JK ingawa ana nafasi kubwa kushika awamu ya pili kirahisi bila upinzani kulingana na katiba yao lakini naona sasa hivi CHUKUA CHAKO MAPEMA imefika hatua nyingine kabisa.
Kwa hiyo, yawezekana kabisa huko CCM kuna moto sasa hivi na JK kafanya hayo mabadilisho kuwakumbusha tu - who is in charge!
 
Msabaha kupelekwa Afrika Mashariki ni kuwasaidia Warundi wenzie wajiunge na jumuiya haraka.

Membe kwenye nishati na madini namuaminia babake.

JK kaona aibu kuwatema mawaziri kwa sababu wapinzani wangembeza, kwa hiyo kaua soo kimtindo. Lakini naamini baada ya muda ya muda mrefu kuna baadhi yao watajiuzulu "kwa sababu za afya"! We twende tu!
 
Mzee Bob,

Ilifikia mahali kwamba ni lazima afanye mabadiliko maana ni wazi kuwa kuna baadhi ya mawaziri wameshindwa kufanya kazi, na kwenye kikao cha kamati kuu alishaambiwa wazi kuwa issue ya umeme inapunguza heshima ya serikali yake,

akaambiwa kuwa awafukuze wazee wote kule nishati, lakini kutokana na moto unaoendelea kuwaka huko ndani sasa hivi akaogopa kupunguza wafuasi wake, mzee Mkandara labda nikuandikie kwenye PM, kuhusu kinachoendelea sasa hivi!
 
Kikwete: Vigogo wa dawa za kulevya jisamilisheni

Na Ramadhan Semtawa, Songea

SIKU chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa ana majina ya vigogo wa dawa za kulevya nchini, amewataka wanaojihusisha na biashara hiyo kujisamilisha vinginevyo watanaswa na msako mkali utakaoanzishwa dhidi yao.

Akihutubia katika kilele cha Mwenge na hitimisho la wiki ya Vijana Taifa juzi, Rais Kikwete alisema msako wa vigogo hao utakuwa mkali kuliko ule ambao unaendeshwa dhidi majambazi.

Alisema dawa ya vigogo hao ni kujisalimisha kwa kuacha biashara hiyo au vinginevyo watakabiliana na mkono mrefu wa dola.

Alisema sasa umefika wakati kwa 'Wazungu wa Unga' kuamua kujisalimisha kwa kuachana na biashara hiyo au wakabiliane na mkono wa dola.

"Naomba vijana muache kukubali kutumiwa, mkikataa mtakuwa mmesaidia serikali kuukata mzizi wa fitana wa 'wazungu wa unga', naomba nichukue fursa hii kuwaonya kwamba, tutawaendeshea operesheni kama ile dhidi ya majambazi," alionya Rais na kuongeza.

"Ni jukumu lao kuamua kuacha au kukabiliana na nguvu za dola, hawa ni watu hatari, lakini vita hii tutaweza kufanikiwa ikiwa vijana mtashirikiana na serikali yenu, ungeni mkono serikali," alisisitiza Rais.

Alisema vijana wengi ambao ni nguvu kazi ya taifa wanaathirika kutokana na matumizi ya dawa za kulevya na kuonya kwamba serikali haitakaa kimya kukubali hali hiyo iendelee.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete imeungwa mkono na Kamishna wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Christopher Shekiondo ambaye amesema sambamba na mpango huo kuna mkakati wa kubadili sheria ya dawa za kulevya ili kuwabana zaidi vigogo wa mihadarati.

Shekiondo alisema sheria ya sasa ina upungufu kwani inatoa mwanya na kwa wafanyabiashara wakubwa kuendelea kufanya biashara ya dawa za kulevya bila kukamatwa na ushahidi ingawa majina yao yanaweza kupatikana.

Kwa mujibu wa Shekiondo, udhaifu uliopo katika sheria ya sasa unatokana na adhabu ya faini kwa watuhumiwa ambao mara nyingi si vigogo wenyewe bali ni wale waliotumwa hivyo huwa rahisi kwa vigogo wakubwa kulipa faini hizo.

Shekiondo alifafanua kwamba, wafanyabiashara wakubwa au vigogo wanapotuma vijana wao kwenda nje au kuuza katika soko la ndani huwasisitizia kwamba hata wakikamatwa wasithubutu kuwataja kwani watatolewa kwa dhamana hivyo wakiwataja watakosa watu wa kuwatoa kwa dhamana.

"Ni kweli dawa za kulevya huingizwa nchini na wafanyabiashara wakubwa, lakini inakuwa vigumu kuwakatamata hawa, hawa hutumiwa vijana wao, lakini huwaeleza kabisa kwamba hata wakikamatwa wasithubutu kuwataja kwani wao ndiyo watakaowatoa kwa dhamana," alisema Shekiondo na kuongeza:

"Sasa ndiyo maana unaona kijana anakamtwa na mzigo kutoka nje lakini hamtaji bosi wake kwa sababu anajua atatolewa kwa dhamana, ni kweli kama mtu ana mzigo wa Sh100milioni na kijana wake anatakiwa kutolewa kwa dhamana ya Sh10milioni unafikiria atashindwa kumtoa."?

"Haya ni mapungufu ndiyo maana tunaangalia jinsi ya kupendekeza kuwepo mabadiliko katika sheria hii ili iwe na meno zaidi iwabane wafanyabaishara wakubwa na wanaotumiwa hasa kwa kuangalia masharti ya dhamana kuyafanya kuwa magumu zaidi."

Shekiondo alifafanua kwamba, dawa za kulevya bado ni tatizo kubwa nchini kiuchumi na kijamii na kuongeza kwamba hivi sasa kuna changamoto kubwa ya kudhibiti matumizi na biashara ya dawa hizo hasa kuwa makini na biashara hiyo kutoka Marekani ya Kusini kuelekea Afrika Magharibi.

Kamishna huyo alisema hivi sasa kuna wimbi kubwa la uingizaji dawa za kulevya kutoka Marekani ya Kusini kuingia Afrika Magharibi hasa kwa dawa za viwandani kama heroine, coceine na mandrax na kuongeza kwamba ingawa dawa hizo zinalengwa kupelekwa Ulaya lakini hata nchi za Afrika Mashariki zinaweza kukumbwa na hatari hiyo.

Akizungumza na wahahariri Ikulu hivi karibuni Rais Kikwete alikiri kupokea barua ya majina ya vigogo 58 wa dawa za kulevya iliyoandikwa na vijana 15 wazalendo.

Alisema mbali ya kuyapokea majina pia vyombo vya dola vimeaanza kuyafanyia kazi


Wala rushwa walipewa muda wa kubadili tabia,sasa wazungu wa unga wanaombwa wajisalimishe.This President can't be serious,can he?
 
JK anaonekana ana huruma!! na roho nzuri!!

lakini amezidisha kwa kuwafanyia wala rushwa, mawaziri wahuni kama Dr Msabaha! Hili bomu Msabaha ninaliombea ili baada ya 2010 lisiwemo barazani.

Tena nimesoma humu wanasemea kumbe huyo Dr. Msabaha ni ana udini na ukabila! HAFAI HUYO NA HANA NAFASI KATIKA NCHI YETU TUNAYOITAKA/ITEGEMEA.

Karamagi tulisikia humu na kwenye news kuwa ndoa yake imemshinda. Tatizo la umeme wa tanzania na la mikataba ya madini ninadhani ni kubwa kuliko hata la ndoa! Je ataweza! huko KUNA MAJARIBU MAKUBWA MNO! MTU ANAWEZA KUWA BILIONEA KWA SEKUNDE MOJA TU, KINACHOTAKIWA NI SAHIHI YAKE TU! NA HASA WAZIRI AKIJUA KUWA RAIS HATAMFUKUZA KAZI AU KUMFUNGULIA MASHITAKA.


Sasa JK roho yako nzuri na huruma yako ilelekeze kwa hawa maskini na walalahoi ambao ndio tunaoumizwa na hayo manguchiro! wezi.

Na waliokupa kura ni hawa wanaomumizwa na wamekupa wakijua jukumu lako ni kupambana na waovu ili walalahoi walale hai!

UKIZIDISHA HURUMA KWA WEZI,MAJAMBAZI, WALA RUSHWA TUENDELEE KUKUELEWAJE!?
 
Yes, I can still trust this President. I believe we will see more and hear more from him and the country will change for the better.

Just imagine, we did not distrust or did we a president who made us queue for sugar, etc. which were no where to be seen. If that happened today, would we trust that president, yet we seem to trust him until today despite all that hardship. Those days we wouldn't know if there was no power because we did not have bulbs - and there was nothing, not even reliable power and the situation was at its worst towards the end of his term in office. Yet some in this forum seem to praise Mwalim JKN at the top of their voices; but condemn JK with all vigour well knowing that the guy has been there for less than a year. Majambo yakushangaza haya!!
 
Dont forget that a multitude of praises showered to Mwalimu were largely hypocritical,or rather compulsive.Braza,we were living in the era of "ndio mzee,zidumu fikra sahihi za nyerere,etc."Asikudanganye mtu kwamba Watanzania walikuwa wanafurahia maumivu ya kujipanga kwenye maduka ya kaya for a kilo of sugar or getting couple of bottles of beers at a mercy of an RTC staff.Ilikuwa inawauma because we are not made of steel.What could we do while living in a police state?Only way to survive as a politician was to praise Mwalimu in every possible way,only way to join university was to join Umoja wa Vijana,and your immediate semi-God was balozi wa nyumba kumi wa CCM (a local spymaster to safeguard the so-called party hegemony).

Do you sincerely think people wouldnt express their dissatisfaction had there been semi-free media as we currently have?By the way,with complete no access to what's happening beyond Tanzanian borders how on earth could bongolanders know that they were missing?The only rags we were allowed to read were Uhuru,Mzalendo,Daily News and Sunday News which were only reporting the rulers' speeches,and only comments you could have found were praises to such leaders.

Jk should be thankful to those who criticize him because as nilivyowahi kusimuliwa hadithi flani,mfalme hakujua kuwa yuko uchi mpaka pale mwanae alipomwambia "baba,kuna kitu kama nyoka kina-swing katikati mapaja yako..."
 
Mlalahoi, nakubaliana nawe. Nyakati za Nyerere hazipo na hazirudi tena. Hatuwezi kuhalalisha uzembe kwa kutumia mambo ya kale. Nyerere alikuwa na kipindi chake na changamoto zake.Hatuwezi kumchekea JK anapafanya madudu kwa kuwa tu kulikuwa na ukimya wakati wa Nyerere. Kwanza ni kituko kuwafananisha Nyerere na JK,hawafanani kabisa.

Tuache kumpaka rangi JK,imetosha apige mzigo sasa. Anaongea mno,mikwara mingi hamna lolote ambalo linatokea.Cha kushangaza kila akipata wasaa wa kuzungumza,anatoa ahadi. Baraza la mawaziri pamoja na kuwa na watendaji wabovu ni kubwa mno. Gharama za kuiendesha serekali kuu ni kubwa na hivyo tutaendelea kuzinyima rasilimali serekali za mitaa!

Sina imani nae
 
humu tunajua wamo ambao wanataka serikali iendelee kufanya madudu ili wanufaike!

ndiyo maana sioni ajabu kwa mtu kuja hapa aksema eti kwa kuwa tulikuwa kimya wakati wa nyerere sasa tusiongee!!

Kwanza wengine tulikuwa wadogo saaaana!

cha maana hapa ni kuwa ingelitakiwa Mwniyo afanye VIZURI KULIKO NYERERE NA HAPO TUNGESONGA MBELE. NA PIA MKAPA ANGETAKIWA KUFANYA VIZURI ZAIDI KULIKO NYERERE NA MWINYI. NA KWA SASA TUNAMTAKA KIKWETE AFANYE VIZURI KULIKO WOTE TENA YEYE SASA ANAONGOZA WATANZANIA WENGI WAO WAKIWA NA MADGREE KIBAO! DIPLOMA USISEME!

SASA HUYO ANAYEKUJA NA UHNI WAKE ETI TUKAE KIMYA ANA MAANA GANI HUYO?!

HUMU WENGINE TUNAJUA MNTAKA UDINI UTAWALE ILI MUENDELEE KUPTA ULAJI AU MNATAKA UKABILA UTAWALE ILI MUENDELEE KUJINEEMESHA!

WAMO WAKWELI NA TUNAWAONA TU WAKITOA MAJAMBOSI HUMU!

SAS HIVI TUNATAKA KIONGOZI ANGALIE MBELE MBELE KWA MAENDELEO ZAIDI. PIA AREKEBISHE PALE AKINA NYERERE, MWINYI NA MKAPA WAMEHARIBU ILI TUSONGE MBELE!

WEWE UNAYETUTISHA ACHA UHNI WAKO!
 
Ama kweli CCM yaani wamekaa wakaona kwamba Umeme tu ndiyo shame kwa serikali ya JK ? Kuna madawa ya kulevya anawaachia hawa jamaa ambao aidha ni wakubwa na wengine ndiyo wanao ichangia CCM ama hata walichangia kampeni zake .Kuna madini na mikataba hovyo na mengine mengine .Sasa JK ndiyo haswa anaonyesha ni aina gani ya kiongozi .
 
Back
Top Bottom