Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Jizaledo said:
Kichuguu,
Katika kuthamini ubinadamu Mwalim alikuwa msitari wa mbele sana lakini kamwe hakujali tahadhari yakujihusisha katika mambo ya watu wengine kwa uchumi wetu.
Ni kweli kuwa kuna mambo mengi tu ya kiuchumu ambayo Nyerere alikuwa too utopian kwa kuchanganya sana siasa za kimataifa na uchumi wa nchi changa kama Tanzania. Alitakiwa awe makini sana. Vita siyo lelemama, hata leo Marekani wanajutia kujihusiha na vita ya Iraki. Tanzania ilijihusiha na vita nyingi sana katika eneo hilo la afrika kuanzia mwaka 1968 hadi 1980.

A Brief Background:

(a) Baada ya uhuru, effort ya viongozi wa kwanza wa afrika ilikuwa ni kuungansiha bara la afrika ili taifa moja kubwa (USAfrica).

(b) Tanzania, Zambia na Zaire zilikuwa ni nchi pekee za Afrika mabazo zilikuwa zinapakana na makoloni, na kulikuwa na kero zake hasa kuhudumia wakimbizi na mambo kama hayo; kwa mfano mwishoni mwa miaka ya sitini tulikuwa tunapigwa mabomu na Wareno kule Ruvuma mara kwa mara.

(c) Baada ya mapinduzi Zanzibar ilijenga na uhusiano na Ujerumani ya Mashariki wakati bara ilikuwa ikisaidiwa na Ujerumani Magharibu kujenga barabara, hospitali ya ocean road na sikumbuki sawasawa kama ilikuwa ni pamoja na nkurumah hall ile ya chuo kikuu. Ulipofika wakati wa Muungano, ambao kuna maandiko yanayoonyesha kuwa ulikuwa umetengezwa zaidi na mataifa ya magharibi ili kupunguza kasi ya ukominist kuingia sehemu hiyo ya dunia, nchi za Magharibi zilimuambia Nyerere kuwa fukuza ujerumani mashariki ama sivyo sisi hatutakusaidia. Hii ilikuwa ni dharau ambayo mchonga hakuivumilia; akawaambia kuwa chukueni mali zenu muondoke. Wajerumani wale walibomoa sehemu ya barabara lami ambayo walikuwa wameshweka na kuna taarifa kuwa Nkurmah hall haikumalizika.

Sasa basi mchanganyiko wa mambo haya ulisababisha Nyerere (a) kuthamini sana africanism (b) kupunguza imani kwa mataifa ya nje na ndiyo maana akaja na sera za kujitegemea; huu ndio ulikuwa mwazo wa siasa za Ujamaa na Kujitegemea:- Nyerere aliyesomea Uingereza hakuwa na background yoyote ya Ujamaa kabla ya hapo, (c) kuyachukia mataifa ya magharibi ambayo yalikuwa yanashirikiana na makaburu na wareno against Africanism, na hivyo kupigana nayo.

Inawezekana kabisa mazingira yalimlazimisha kufanya hivyo, ilia yeye alizidi sana. Waswahili wanasema wema usizidi uwezo. Niliwahi kuishi na watu kutoka Zimbabwe ambako Nyerere aliwahi kupeleka batallion nzima kupigana na smith; wala hawakumbuki kuwa kuna askari wa Tanzania waliwahi kupoteza masiha yao kwa ajili ya uhuru wao. In fact wanacheka sana kuwa Tanzania pamoja na kupata uhuru miaka mingi bado haijafanya lolote la maendeleao. Jamaa wa afrika ya kusini ndiyo wacha kabisa. wanasema Tanzani ni "third world." wengi wao hawajui kama Tanzania ilisadia chochote katika uhuru wao. Kwa hiyo investament yetu kwa uhuru wao haikuleta faida yoyote kwetu sisi.

In general, Nyerere hakuwa na restraint ya kuhakikisha kuwa hamalizi resources za nchi katika vita zake za ukombozi ingawa vita hizo zilikuwa za halali
Hebu jaribu kufanya uchunguzi kwa Wananchi wa kawaida, ambao ndio wanaomatter hapa wakuambie ni awamu ya Raisi yupi maisha yao yalikuwa na nafuu; na ninakuhakikishia Mzee Ruksa chati yake utaiona iko juu kiasi gani.


Mimi siyo mmoja "mwananchi wa kawaida" kwa sababu naangalia maendeleo kwa maana halisi siyo kwa maana artificial. Watu alimwita Mwinyi ruksa kwa vile alipopata pesa za mkopo akazitupa mitaani bila uangalizi wowote hivyo kutoa ruksa kuzitumia; hivyo kila mtu alaweza kujipatia kwa namna moja au nyingine. Nilikuwa nakutana na watu kwenye baa wakiwa na shiling milioni kumi mfukoni kwa ajili ya kulewea wakijua kuwa kesho yake wangepata nyingine.

Hata akipatikana mwendwazimu asiye kuwa na plani yoyote ya wapi anataka kuipeleka nchi, lakini akawa anagawa hela hovyo hovyo kwa kila mtu, utashangaa kuwa kuna waswahili wengi watampenda.

Hicho huwezi kukitumia kuwa ni kipimo cha uongozi mzuri. Ametelemsha sana hadhi ya Tanzania. Wakati Mwinyi anapokea nchi Tanzania ilikuwa ya 18 kutoka chini. Wakati yeye anaondoka madarakani aliiacha Tanzania ikiwa ya 8 kutoka chini, yaani kila mwaka ilikuwa ikishuka daraja. Mkapa amepokea ikiwa ya 8 na kuiacha ikiwa ya 4; alipinguza kidogo sipidi ya kuporomka labda kwa vile nchi ilishafika bondeni tayari.
 
Mkandara,

Heshima yako.

Tafadhali soma yanayolumbanwa ndani ya mada yakuongoze jinsi ya kujibu. Wewe unaashiria kuwa wa kulaumiwa kwa kushuka shillingi ni Mungu wakati wenzako wanasema ni Mwinyi na mimi ninalumbana kutafuta kati ya Mwinyi na Nyerere ni nani anayestahili kulaumiwa kwa kudorora shilingi. Sasa wewe kumleta Mungu au mzungu unakwenda nje ya mkondo wa malumbano.

Nimekudokeza tu ili uyalete maswali yako vizuri ili tupate la kukujibu.

Ahsante,

Mkandara said:
ManjuMakuti,
kwanza karibu kijiwe hiki na itabidi ukafanye utafiti wa nguvu kuweza kutuvuta.
Ningependa tu kukuuliza maswali mawili ambayo yamekita ktk kila hoja yako...Hii ALIYEANZA..
Aliyeanza kuanguka kwa shilingi, sijui Rushwa na Ujambazi ni Nyerere imetoka wapi?... Mbona vyote hivyo vilikuwepo toka dunia iumbwe na labda labda kwa urahisi zaidi niseme toka mkoloni! je, tumlaumu Mungu au mkoloni kwa kuwepo vitu hivyo?
Nyerere hakutoa mishahara midogo laah hasha. Graduate wa UDSM alikuwa akichukua Tsh.1750/- mwaka 1975 hali nyumba ya msajili bada ya utaifishaji ni chini ya Tsh. 200 sijui (that's about 10% ya mshahara..damn!). Uliona wapi dunia hii! haya kima cha chini kilikuwa 450 kwa hiyo nao waliweza kuapnga chumba kimoja...Achaa mzee Ukiruka hadi mwaka 1980 mishara ilipanda hadi kufikia kitu kama Tsh. 2040/- kwa graduate. Maisha nayo yalipanda lakini bado wasomi waliweza kuyakabiri maisha.
Na ushahidi mkubwa ni kwamba wazazi wetu sisi wote humu wanazo nyumba zao yaani waliweza kujenga nyumba kwa kutegemea ajira wakati wa Nyerere!...(hata iwe ya vyumba sita). Walioshindwa kujenga walikuwa wamelemazwa na nyumba za bure za serikali. Acha mbali maswala ya usafiri wa UDA wa shilingi 1, kila idara na mashika yake walikuwa na usafiri wao. Jangwani hakuna kabisa kuona mfanyakazi anayekatisha kwa mguu. Leo hii mshikaji kukatiza jangwani imekuwa ibada ya kila mfanyakazi.
Kisha swali la Pili ni hii KUIGA..
Mshikaji ELIMU ya kitu sio KUIGA, jaribu kutofautisha vitu hivi. Hivi kweli dunia ya leo unaweza kuanzisha kitu ambacho hakikugusiwa na mtu yeyote kabisa!.. yaani wewe ndio uwe mwanzilishi, sidhani tena dunia ya tatu mmmh!..ndoto.
Hakuna kati yetu anayeweza zuka na mfumo wa siasa, uchumi, sayansi wala dini ambayo haijawahi kuandikwa sehemu. Huo utakuwa ni UTUME tena.
Vyote tunasoma vitabu na ku-apply haina maana tunaiga. Ujamaa hakuuanzisha Mao nae kaukuta. Hao akina Shakespear na Caesar, wametumiwa na viongozi kibao wa dunia hii ktk hotuba zao, mifumo ya bunge,senate ktk uongozi n.k. Hii sio kuiga mshikaji sidhani Mwinyi alikuja na zake kama sii kufuta akina Kandoro na Shaaban Robert.
Nakuomba usome kitabu cha Nyerere kinachoitwa UJAMAA na utakuta tofauti nyingi sana na huyo MAO.
Mwache mzee wa watu wewe dollar tumebadilisha sisi na tunafahamu kabisa kwamba mwaka 1975, bei za mazao yetu zilishushwa mara mbili na hao westerners hali bidhaa zao ikiwa ni pamoja na mafuta (OIL) vilipanda bei mara mbili. Kwa hiyo hata kama uchumi wetu ungekuwa mzuri kiasi gani... pingamizi zilikuwa nyingi sana mbali kabisa na ukame, vita, vikwazo vya kiuchumi n.k.
Vita baridi mshikaji ilikuwa kuwaangusha wote waliokuwa wakifuata UJAMAA na TZ haikuwa tofauti na nchi nyinginezo.
 
ManjiMakuti,
Mshikaji nimekuelewa vizuri sanahoja yako kuhusu shilingi kushuka. Watu wamemlaumu Mwinyi kwa sababu mara ya kwanza tumeingia ktk economic reform ni mwaka 1986 chini ya support ya IMF na World bank ambao kitu cha kwanza walichodai ni kuishusha thamani shilingi yetu. Nyerere alikataa katakata kushusha thamani ya shilingi yetu kulingana na thaminisho lao. Na sababu kubwa ambayo JKN aliisema ktk hotuba zake ni kwamba tukishusha thamani ya fedha yetu kama wanavyotaka hawa IMF itatughalimu sisi mazao zaidi ili kununua kitu kilekile. Yaani kama kununua trekta ni magunia 100 ya kahawa basi itatughalimu magunia 150 kwa trekta lilelile...kumbuka Manji bei za mazao yetu wanaozipanga ni hawa wazungu sio sisi. Hawaihitaji fedha yetu ya madafu ktk soko lao bali wanaitimia thamani ya shilingi yetu ktk ununuzi wa mali zetu.
Mathlan, mwaka 1990 kilo moja ya sangara mvuvi wetu alilipwa Tsh 300 (chini ya dola moja) wakati sangara huyohuyo alipofika Ulaya aliuzwa ktk soko lao kwa bei ya Usd 5 kwa kilo. Leo hii nina hakika sangara hana faida tena kwa mvuvi wetu kwani huko Ulaya sangara ananunuliwa kwa USd 3.50. yaani kashuka bei toka 5 hadi 3.50 wakati huohuo thamani ya shilingi yetu pia imeshuka mara mbili ya thamani ile ya mwaka 1990. Lakini huyohuyo sangara wakati wa Nyerere alikuwa akiuzwa Japan,tena wakichukua na gills zake kwa Usd 2.50 moja kwa moja toka kwa mfanyabiashara - Mtanzania. Majongoo pia ilikuwa biashara safi sana Japan lakini mzungu alipoishtukia tu tukawekwa sawa ktk mkataba na EU kwa hiyo hakuna kinachotoka kuuzwa Ulaya bila idhini yao na kisingizi kikubwa ni hizo standard kumbe wao ni middlemen tu. Wafanya biashara na hasa walanguzi toka Dar wakawa hawana tena sauti wala soko. Kwa sababu kama hizi ndio maana Nyerere alidai sisi tupange bei za bidhaa zetu, jambo ambalo leo hii kila kiongozi wa Afrika anaona kijiko kudai huko UN ama anapokutana na viongozi wa G8.
Kwa hiyo bob, kila tunapojisifu kuwa tumeweza kuuza (exports) vizuri zaidi kuliko mwaka uliopita ina maana tumechuma zaidi mali zetu na kibaya kuliko yote hatufahamu jinsi ya kupandikiza mbegu kufidia kile kilichovunwa.
Dhahabu, Tanzanite,samaki hata miti yetu nahasa mpingo (vinyago) vinapotea!..itakuwa historia hivi karibuni kuwa tulikuwa navyo.
Kifupi, haikuniingia akilini kwa sababu ushukaji wa thamani ya fedha ni mbinu ya kiuchumi ili kuuza zaidi. Na kama unakumbuka baada ya Mwinyi kushusha thamani ya shilingi tuliweza kuuza nje (exports) zaidi kwa bei ya jioni. Ni mchanganyiko wa soko huru (RUKSA) kuchangia ktk uchumi wetu kupata sura mpya baada ya negative economic growth kati ya 1980 and 1985. Kwa hiyo hata Mwinyi kulikuwa na mazuri yake lakini nadhani wanachosema ni kwamba mzani wa thamani ya shilingi yetu ulielemea uzito zaidi ktk mabaya.
 
Mkandara,

Inaonekana wazi kuwa elimu yako ya uchumi imekuzwa vizuri na fikira za Nyerere na darasa za jukwaani. Sasa ujuwe kuwa Nyerere si mchumi kabisa hivyo inakubidi usomee uchumi vizuri. Pia Nyerere ni mtu aliyekuwa akikwepa ukweli na mwenye chuki za kibinafsi. Alipokuwa akiambiwa ukweli aling'aka eti hawezi kugeuka jiwe. Uliza wachumi akina Mtei walishauri nini kuhusu matakwa ya IMF na kwa nini. Je shilingi inavyoanguka sasa hivi ni IMF gani aliyesema tuishushe thamini yake? Shilingi ilikuwa inaporomoka nyenyewe kama nilivyokuonyesha hapo awali na ingezidi kufanya hivyo utake usitake. La muhimu ambalo unajaribu kulikwepa ambalo halikwepeki ni kuwa kuanguka kwa shilingi ya Tanzania chanzo chake alikuwa Nyerere na wala usingewaona IMF kutowa ushauri wowote kama shilingi ingekuwa imara in the first place.

Tatizo la Nyerere ni kuwa alijifanya mtaalam wa kila kitu asiyetaka ushauri - mzee aambiliki na aliposhauriwa na wataalamu na akakataa kusikia aliishia kuwaadhibu watu kwa kuwafukuza kazi. Na mambo yalipogharibika zaidi aliishia kulaumu taasisi za kimataifa kwa hoja za mitaani zisizokuwa na utaalamu wowote.

Kweli apendae chongo huita kengeza. Jana tu ulikuja juu na kudai kuwa kuanguka shilingi na vitu vingine vilikuwepo tangu mwanzo wa dunia katika kumtetea jitihadi zako za kumtetea Nyerere na unapoonyeshwa kuwa fikra zako hizo zina walakini na haziendani na malambano yaliyopo hapa basi unazitupa upesi upesi na kuanza kumkariri Nyerere kuhusu chuki zake na IMF. Sasa mimi nitalumbana na wewe kwa misingi ipi kwani unaonekana wazi kuwa huna uhakika na unachoandika.

[/B]Quote:
Originally Posted by Mkandara
ManjuMakuti,
kwanza karibu kijiwe hiki na itabidi ukafanye utafiti wa nguvu kuweza kutuvuta.
Ningependa tu kukuuliza maswali mawili ambayo yamekita ktk kila hoja yako...Hii ALIYEANZA..
Aliyeanza kuanguka kwa shilingi, sijui Rushwa na Ujambazi ni Nyerere imetoka wapi?... Mbona vyote hivyo vilikuwepo toka dunia iumbwe na labda labda kwa urahisi zaidi niseme toka mkoloni! je, tumlaumu Mungu au mkoloni kwa kuwepo vitu hivyo? [/B]


Mkandara said:
ManjiMakuti,
Mshikaji nimekuelewa vizuri sanahoja yako kuhusu shilingi kushuka. Watu wamemlaumu Mwinyi kwa sababu mara ya kwanza tumeingia ktk economic reform ni mwaka 1986 chini ya support ya IMF na World bank ambao kitu cha kwanza walichodai ni kuishusha thamani shilingi yetu. Nyerere alikataa katakata kushusha thamani ya shilingi yetu kulingana na thaminisho lao. Na sababu kubwa ambayo JKN aliisema ktk hotuba zake ni kwamba tukishusha thamani ya fedha yetu kama wanavyotaka hawa IMF itatughalimu sisi mazao zaidi ili kununua kitu kilekile. Yaani kama kununua trekta ni magunia 100 ya kahawa basi itatughalimu magunia 150 kwa trekta lilelile...kumbuka Manji bei za mazao yetu wanaozipanga ni hawa wazungu sio sisi. Hawaihitaji fedha yetu ya madafu ktk soko lao bali wanaitimia thamani ya shilingi yetu ktk ununuzi wa mali zetu.
Mathlan, mwaka 1990 kilo moja ya sangara mvuvi wetu alilipwa Tsh 300 (chini ya dola moja) wakati sangara huyohuyo alipofika Ulaya aliuzwa ktk soko lao kwa bei ya Usd 5 kwa kilo. Leo hii nina hakika sangara hana faida tena kwa mvuvi wetu kwani huko Ulaya sangara ananunuliwa kwa USd 3.50. yaani kashuka bei toka 5 hadi 3.50 wakati huohuo thamani ya shilingi yetu pia imeshuka mara mbili ya thamani ile ya mwaka 1990. Lakini huyohuyo sangara wakati wa Nyerere alikuwa akiuzwa Japan,tena wakichukua na gills zake kwa Usd 2.50 moja kwa moja toka kwa mfanyabiashara - Mtanzania. Majongoo pia ilikuwa biashara safi sana Japan lakini mzungu alipoishtukia tu tukawekwa sawa ktk mkataba na EU kwa hiyo hakuna kinachotoka kuuzwa Ulaya bila idhini yao na kisingizi kikubwa ni hizo standard kumbe wao ni middlemen tu. Wafanya biashara na hasa walanguzi toka Dar wakawa hawana tena sauti wala soko. Kwa sababu kama hizi ndio maana Nyerere alidai sisi tupange bei za bidhaa zetu, jambo ambalo leo hii kila kiongozi wa Afrika anaona kijiko kudai huko UN ama anapokutana na viongozi wa G8.
Kwa hiyo bob, kila tunapojisifu kuwa tumeweza kuuza (exports) vizuri zaidi kuliko mwaka uliopita ina maana tumechuma zaidi mali zetu na kibaya kuliko yote hatufahamu jinsi ya kupandikiza mbegu kufidia kile kilichovunwa.
Dhahabu, Tanzanite,samaki hata miti yetu nahasa mpingo (vinyago) vinapotea!..itakuwa historia hivi karibuni kuwa tulikuwa navyo.
Kifupi, haikuniingia akilini kwa sababu ushukaji wa thamani ya fedha ni mbinu ya kiuchumi ili kuuza zaidi. Na kama unakumbuka baada ya Mwinyi kushusha thamani ya shilingi tuliweza kuuza nje (exports) zaidi kwa bei ya jioni. Ni mchanganyiko wa soko huru (RUKSA) kuchangia ktk uchumi wetu kupata sura mpya baada ya negative economic growth kati ya 1980 and 1985. Kwa hiyo hata Mwinyi kulikuwa na mazuri yake lakini nadhani wanachosema ni kwamba mzani wa thamani ya shilingi yetu ulielemea uzito zaidi ktk mabaya.
 
Loooh Manji umekanyaga pabaya ndugu yangu.
Uchumi ndio mahala pangu na uwanja wazi kabisaaa lete vitu!....
Kwanza nadhani wewe mgumu sana kuelewa na yawezekana sababu ni uandishi wangu mwenyewe lakini lugha niliyotumia hapa nyepesi sana.

Nitarudia kusema huwezi kumlaumu Nyerere kwa kushuka kwa shilingi wakati wa Mwinyi ati kwa sababu shilingi ilikuwa ikishuka toka wakati wa Nyerere.
Hili darasa bovu kabisa! Na kiuchumi ni mtazamo wa mfa maji...
Nchi haiwezi kwenda mbele ikiwa utatazama shilingi ilishuka wapi na kuwa ndio sababu. Mbona Uganda shilingi yao ilishuka wakati wa Obote na Idd Imin leo hii ime-pick up!...mbona lugha yako sii ya kichumi kabisa!..Unaposema Nyerere hakuwa mchumi una maana gani?..sielewi kabisa bob yaani mchumi kwako ni yule anayefanikiwa kukuza uchumi ama?
Kifupi unachojaribu kusema hapa ni kuwa haiwezekani Mwinyi kuweza kuipa thamani fedha yetu kwa sababu Nyerere alikwisha haribu.
Na kama huo ndio mtazamo wako nakuuliza wewe tena nambie ni wakati gani shilingi haikushuka thamani toka ile ya east Afrika!..Hapa nikiwa na maana hata Nyerere anaweza dai kuwa sii yeye aliyenza kushusha thamani... kisha wakati wa Nyerere na Mwinyi ni vitu viwili tofauti kabisa.. mifumo ya kiuchumi tofauti. Labda tuzungumzie wakati wa Mwinyi, Mkapa na JK...waliopo ktk mfumo mmoja.
Hilo swali la IMF gani aliyesema sijui una maana gani kwani IMF sii jina la mtu! na ikiwa unataka nikupe data zinazohusu mapendekezo ya IMF wakati wa Mwinyi nitakupa. Rushwa lilianza toka wakati wa Nyerere! sasa hii hadithi gani isiyoeleweka!..
 
Mchumi Mkandara,

Mzee, wewe hodari sana kuchambuwa matatizo ya uchumi kwa kusisitiza kuwa yalikuwapo tangu "hapo mwanzo". Sasa huu uchumi wako wa rushwa, kuanguka kwa shillingi n.k unavyovieleza "kiuchumi" kuwa vilikuwapo tangu hapo mwanzo kama ulivyoandika awali kama ninavyokukariri hapa chini. Ila pia inaonekana wazi kuwa huo mwanzo wako huna uhakika nao na umebaki unauyumbishayumbisha. Eh sasa imekuwa mwanzo ni shillingi ya Afrika Mashariki. Hebu tueleze nayo ilishuka thamani vipi na kwa kiwango gani?

By the way, hivi ni nani amesema IMF ni jina la mtu, au Kiswahili pia kinatatiza kuhusu neno "gani" na matumizi yake mengi? Simuoni Manju Makuti kusema hayo.

[/b]Quote:
Originally Posted by Mkandara
ManjuMakuti,

Ningependa tu kukuuliza maswali mawili ambayo yamekita ktk kila hoja yako...Hii ALIYEANZA..
Aliyeanza kuanguka kwa shilingi, sijui Rushwa na Ujambazi ni Nyerere imetoka wapi?... Mbona vyote hivyo vilikuwepo toka dunia iumbwe na labda labda kwa urahisi zaidi niseme toka mkoloni! je, tumlaumu Mungu au mkoloni kwa kuwepo vitu hivyo? [/b]
 
Jizaledo,

Nawe umeungana ktk kutoelewa?..
Jamani vipi!.. nimesema ya kwamba kila kiongozi lazima awe responsible na uongozi wa kile alichokikuta!.. Ukikuta fedha imeanguka thamani ni jukumu lako kulinda ama kurekebisha na sio kusingizia nyuma tulikotoka. Ukikuta Rushwa ni jukumu la kiongozi kuondoa rushwa. Sababu yoyote ile ya kuendeleza sins ama uharibifu kwa visingizio vilikuwepo kabla yake ina maana moja tu... sii kosa la kiongozi anayehusika!
Kama ndivyo basi kila kiongozi anaweza kusema kakuta kitu kile kipo chini ama kimeanguka!..Je, kwa nini umechukua jukumu la kuongoza ikiwa utaacha kila kitu kibaki kama ulivyokikuta.
Kwa hiyo jibu sahihi la Utawala wa Nyerere ni maelezo ya ndugu yetu Kichuguu...
Amesema:- Wakati Mwinyi anapokea nchi Tanzania ilikuwa ya 18 kutoka chini. Wakati yeye anaondoka madarakani aliiacha Tanzania ikiwa ya 8 kutoka chini, yaani kila mwaka ilikuwa ikishuka daraja. Mkapa amepokea ikiwa ya 8 na kuiacha ikiwa ya 4; alipinguza kidogo sipidi ya kuporomka labda kwa vile nchi ilishafika bondeni tayari.
Kulingana na majibu ya ManjiMakuti inaonyesha wazi kuwa hatuwezi kuwalaumu viongozi waliopita kwa kuzidi kuiporomosha nchi ikiwa wao wameikuta Tanzania ikiwa ya 18 toka chini. Well, jibu langu kwenu mbon Maleysia, Ethiopia, Uganda na hata Rwanda zilikuwa chini yetu zimeweza ku-pick up hali pia uchumi na fedha yao ilikuwa chini. Swala hapa sii kushuka kwa thamani ya fedha tu ila kushuka huko kunahusiana na kuzidi kwa Umaskini. Tazama CIA fact book kuhusu exchange rates ama site hii hapa....http://www.theodora.com/wfb1991/tanzania/tanzania_economy.html
Inasema hivi:- Exchange rates: Tanzanian shillings (TSh) per US$1--196.60 (January 1991), 195.06 (1990), 143.377 (1989), 99.292 (1988), 64.260 (1987), 32.698 (1986), 17.472 (1985). Sasa kwa kuwa shilingi ilikuwa 17.472 basi ni makosa ya Nyerere leo hii kuwa Elfu na upuuzi?


Swala la IMF. Jizaledo sio neno - "Gani" isipokuwa neno "Aliyesema".
ManjiMakuti kaandika hivi ktk hoja yake iliyopita:-
Uliza wachumi akina Mtei walishauri nini kuhusu matakwa ya IMF na kwa nini. Je shilingi inavyoanguka sasa hivi ni IMF gani aliyesema tuishushe thamini yake?..
Ni IMF gani aliyesema... sijui hapa wewe umeelewa vipi?
 
Mkandara,

Nimekuelewa na ninakuunga mkno moja kwa moja tuwe tunaangalia mbele na kutaraji viongozi waliopo na wajao waendeleze uchumi mbele. Lakini pia tukubali kuwa kazi hii inataka kasi mpya kwani kwa takwimu ulizotowa nchi yetu imekuwa inadidimia kwenye safu za chini katika kila awamu. Sasa ni kweli yaliyopita sindwele, tugange yaliyopo na yajayo lakini inabidi tujuwe asili ya matatizo yetu ili tupate dawa yake. Kama mtu alifurunda "foundation" inabidi tujuwe kufurunda huko tuweze kusawazisha barabara ama sivyo tutagusa juu juu tu.

Naona Manju Makuti ameamuwa kutojibu au anabuy time; bali sidhani IMF kwake ni mtu, ila lugha ya Kiswahili huwa na utamu wa asili yake na mimi huwa najifunza kwayo daima pamoja na personification zake na huwa ninafuatia matumizi ya lugha zaidi na upeo wa matumizi ya maneno kuliko vitu vilivyowazi kama wanabodi humu kuwa wote wanajuwa ni nani (oops!) IMF.

Niseme tu hii topic imetuweka pema katika kuelewa matatizo yanayotusibu. Kazi njema wazee!

Mkandara said:
Jizaledo,

Nawe umeungana ktk kutoelewa?..
Jamani vipi!.. nimesema ya kwamba kila kiongozi lazima awe responsible na uongozi wa kile alichokikuta!.. Ukikuta fedha imeanguka thamani ni jukumu lako kulinda ama kurekebisha na sio kusingizia nyuma tulikotoka. Ukikuta Rushwa ni jukumu la kiongozi kuondoa rushwa. Sababu yoyote ile ya kuendeleza sins ama uharibifu kwa visingizio vilikuwepo kabla yake ina maana moja tu... sii kosa la kiongozi anayehusika!
Kama ndivyo basi kila kiongozi anaweza kusema kakuta kitu kile kipo chini ama kimeanguka!..Je, kwa nini umechukua jukumu la kuongoza ikiwa utaacha kila kitu kibaki kama ulivyokikuta.
Kwa hiyo jibu sahihi la Utawala wa Nyerere ni maelezo ya ndugu yetu Kichuguu...
Amesema:- Wakati Mwinyi anapokea nchi Tanzania ilikuwa ya 18 kutoka chini. Wakati yeye anaondoka madarakani aliiacha Tanzania ikiwa ya 8 kutoka chini, yaani kila mwaka ilikuwa ikishuka daraja. Mkapa amepokea ikiwa ya 8 na kuiacha ikiwa ya 4; alipinguza kidogo sipidi ya kuporomka labda kwa vile nchi ilishafika bondeni tayari.
Kulingana na majibu ya ManjiMakuti inaonyesha wazi kuwa hatuwezi kuwalaumu viongozi waliopita kwa kuzidi kuiporomosha nchi ikiwa wao wameikuta Tanzania ikiwa ya 18 toka chini. Well, jibu langu kwenu mbon Maleysia, Ethiopia, Uganda na hata Rwanda zilikuwa chini yetu zimeweza ku-pick up hali pia uchumi na fedha yao ilikuwa chini. Swala hapa sii kushuka kwa thamani ya fedha tu ila kushuka huko kunahusiana na kuzidi kwa Umaskini. Tazama CIA fact book kuhusu exchange rates ama site hii hapa....http://www.theodora.com/wfb1991/tanzania/tanzania_economy.html
Inasema hivi:- Exchange rates: Tanzanian shillings (TSh) per US$1--196.60 (January 1991), 195.06 (1990), 143.377 (1989), 99.292 (1988), 64.260 (1987), 32.698 (1986), 17.472 (1985). Sasa kwa kuwa shilingi ilikuwa 17.472 basi ni makosa ya Nyerere leo hii kuwa Elfu na upuuzi?


Swala la IMF. Jizaledo sio neno - "Gani" isipokuwa neno "Aliyesema".
ManjiMakuti kaandika hivi ktk hoja yake iliyopita:-
Uliza wachumi akina Mtei walishauri nini kuhusu matakwa ya IMF na kwa nini. Je shilingi inavyoanguka sasa hivi ni IMF gani aliyesema tuishushe thamini yake?..
Ni IMF gani aliyesema... sijui hapa wewe umeelewa vipi?
 
Jizaledo,
Shukran,
Najishtukia kuwa mimi kipenzi cha JKN na mara nyingi namtetea sana hasa pale watu wanapokuja na madongo ambayo kusema kweli hayamhusu. Nyerer alikuwa na MAKOSA kibao lakini binafsi sijaweza kuona MAPUNGUFU yake ktk uongozi zaidi kuwa Ujamaa ulimwangusha. Na kama mchonga angechukua Ubepari mzee yule alikuwa kichwa kibaya sana....sijui tungekuwa wapi!...
Nyerere aliweza kabisa ku-LEAD kundi la watu na mkafanya kazi kama mapunda bila kulaumu na dunia yote wanafahamu sii Egypt, South, Ghana wala Somalia... nani asiyemfahamu! Nyerer alikuwa tuzo kwa nchi na ndiye pekee anajulikana kuliko hata mlima Kilimanjaro!... WHY?
Hata hivyo Jizaledo, nakuapia hakuna hata mtu mmoja humu anayefahamu Tanzania ilikuwa wapi tulipopata uhuru! Yaani Nyerere alipokabidhiwa nchi tanzania ilikuwa imesimama wapi hadi tuseme yeye kaishusha hadi kufikia nchi ya 18 toka chini. Inawezekana sana kuwa Tanzania ilikuwa labda ya 5 ama 6 toka chini na Nyerere akaweza kutupandisha hadi 18.
halafu msingi wa nchi zote zilizotawaliwa umejengwa na Mkoloni, viongozi wengi Afrika wameendeleza yale waliyoyakuta na labda muhimu wenzetu wamekuwa na displine ktk maintainance.. Mtazame Kenyatta hakufanya kitu Kenya zaidi ya uhuru wa bendera, hivyo hivyo nchi Kibao hawana mpya kabisa toka mkoloni aondoke, labda nikiacha Ivory Coast... lakini Tanzania mshikaji kuna mengi kayaweka Nyerere ambayo hayakuwepo hasa Miundo mbinu isipokuwa maintanace ilitupiga chenga na bado inaendelea kutupiga chenga. Yote haya yanayotukuta leo hii yanatokana na uzembe wetu ktk kufanya Ukarabati... hatuna tamaduni hiyo hata ktk tafsiri ya kamusi!..labda nikuulizeni, navyofahamu mimi - Ukarabati maana yake ni kufanya service.. Je, maintainance inaitwa nini ktk lugha yetu?
Wewe unakumbuka ile Oceanshore ya pale posta ya zamani enzi za 70s?...bustani yake ilikuwa kiboko, taa zilikuwa zikiwaka usiku na ma-bench kibao ya watu kukaa jioni uafikiri upo ktk mji wa Ulaya.. Vijana wote yalikuwa ndio makutano yao jioni baada ya shule..siku hizi kumejaa vifaru!...
Wewe hata tunapoona wafagia barabara tunashangaa (michuzi anazitoa ktk site yake) kwa sababu ustaarabu huo ulikwisha toka enzi za Punda Wengi Duniani (PWD). Na sababu haijulikani
 
Kikwete lives in utopian world as Tanzanians wallow in problems --------------------------------------------------------------------------------
Standard Newspaper, Sunday 22 October, 2006.

By Ernest Mpinganjira,

Ordinary Tanzanians reacted with indifference to last week's Cabinet reshuffle in which 10 ministers and eight deputies swapped places.

The business community and opposition parties dismissed the changes, implemented by President Jakaya Kikwete, as cosmetic and "too little too late". They accused the president of attempting to mask massive graft allegations that have dogged his nascent administration since he came to power 10 months ago. Ordinary Tanzanians were surprised by Kikwete's hand-in-glove handling of the economic downturn that threatens to explode into a socio-political crisis.

Growing criticism of poor economic management was delivered, albeit veiled, when experts revealed on Wednesday that the government's debt stock had ballooned by $302 million between January and last month and stood at $9.383 billion. This is attributed to unrestricted domestic borrowing and unnecessary foreign debts.

Prof Marjorie Mbilinyi from the Tanzania Gender Networking Programme (TGNP) warned this does not augur well for the government. She cautioned the trend is likely to wipe out gains from the foreign waiver of $4 billion last July, which the World Bank and International Monetary Fund recommended be converted to investments in the water and energy sectors.

The verdict of the majority is that the president lives in utopia as his populist approach to serious national issues has brought the economy to its knees.

They accuse the president of playing to the gallery rather than taking pragmatic steps to curb runaway graft, civil service incompetence and general ineptitude in the management of public affairs.

With the manufacturing sector virtually grounded and other key areas of the economy on the downspin, Kikwete's 10-month-old administration has come under severe criticism for sustaining and entrenching cronyism inherited from the previous government.

The president responded to the allegations by reshuffling the Cabinet.

The highlights were the changes in the ministries of Energy, Water and Minerals. These ministries have been under the spotlight for incompetence and prevarication, leading to the perception that Kikwete was out of touch with reality.

The reshuffle came amid revelations that a fictitious firm that claims to be incorporated in the US, Richmond Development Company, had been picked by Kikwete's henchmen to supply $172 million worth of equipment to add 100 megawatts to the national grid. Richmond, it turned out, was after all briefcase outfit owned by Tanzanians who call the shots at State House.

Initial investigations link Richmond Development - whose operations are quite similar to Kenya's infamous Anglo Leasing - to an Arusha-based tycoon. He is said to have bankrolled Kikwete's presidential campaigns when his party appeared to be wavering.

In spite of the changes, the reshuffle did not provide fixes to the ailing economy. Executive Secretary of the Tanzania Private Sector Foundation, Mr Lous Accaro, scoffed at the reshuffle, terming it incompetent.

"The Ministry of Energy and the Cabinet in general have let down the president. The Energy minister and his team failed to find solutions to the prevailing power crisis, which has been compounded by dubious contracts," Accaro said. He told reporters last week: "The ministers fooled the president into making empty promises that the current power problems would be over by October. This is a shame."

Kikwete promised the country early October that the Government was in the final phase of fixing the power crisis. However, two weeks after the promise, it came to light that Richmond Development Company was a fictitious outfit without a physical address in North Carolina, US, where it is purported to have been incorporated.

It also emerged the directors of the briefcase company had sold to the state-owned Tanzania Electric Supply Company's (Tanesco) an unserviceable second-hand Boeing 707 engines purporting to be new power equipment.

Opposition party leader and loser in last December president poll, Mr John Mbatia, described the reshuffle as "too little too late and raised more questions about the government's ability to deliver" in the context of the current economic slowdown unleashed by the power crisis. Mbatia, who vied for presidency on NCCR-Reforms party, said the president should have purged half the Cabinet and brought in fresh blood to turnaround the economy, which has been on the back-foot since Kikwete came to power 10 months ago.

"I wish the president had made more substantial changes by dropping half the Cabinet and bringing on board new faces. I don't think the changes will have any positive impact on the president himself or Tanzania in general," he said.

The Cabinet changes, described by analysts as the first major reshuffle since independence, targeted the ministries of Energy, Minerals and Infrastructure, where the immediate former holders of the portfolios have in the past one month been implicated in suspect deals that run into hundreds of millions of dollars.

The former Minister for Energy, Dr Ibrahim Msabaha, has moved to the less prestigious East African Community Affairs portfolio. Msabaha was a fortnight ago accused of hiring a fictitious firm - with an address in the US - in a $172 million deal to supply power equipment to Tanesco.

The swindle became known when Richmond Development failed to deliver the equipment that was supposed to add 100 megawatts to national power greed.

Tanzania is experiencing crippling power deficits, with power experts having warned that the country's main hydropower generating plants face imminent closure in two weeks.

On Thursday, Tanesco announced one of the main hydropower generation plants, Kidatu dam, which generates nearly 80 megawatts, had ceased operations due to low water levels, while the Mtera and Kihansi that make up the Mtera dam power system may close any time.

The exposure of the graft and incompetence went beyond the power sector.

Former Minister for Infrastructure Development, Mr Basil Mramba, has been linked to a suspect deal in which the government lost two thirds of the royalties accruing from mineral exports to Alex Stewart Assayers mineral auditing firm in which his son, Mr George Kandoah, owns a substantial stake. Mramba reportedly executed the deal when he was Finance minister in Benjamin Mkapa's regime.

Tanzanians view the reshuffle as intended to restore credibility, with the president having failed to live up to his pre-election promise to root out corruption and create employment in a country, where more than 60 per cent live on less than a dollar per day.

*******
empinganjira@yahoo.com

http://www.eastandard.net/archives/sunday/hm_news/news.php?articleid=1143959936
 
Majibu ya "serikali" ndiyo hapa...
Lakini yote kwa yote, kwa ujumla Jumuiya ya Afrika Mashariki imo mashakani.

Give us a break
Editor
Daily News; Friday,October 27, 2006 @00:01

CYNICS have been passing harsh judgement on Tanzania's economic performance in the wake of electricity shortage, which resulted from drought and late arrival of this year's long rains.
Expectedly, a Kenyan newspaper, which is obsessed with
Tanzania's immensely popular fourth president, seized the opportunity to carry yet another opinionated, highly libellous article last weekend, proclaiming the dawning of doomsday for this country.

The tabloid, whose relish for mudslinging the new Tanzanian government must now be critically interrogated, maintains that the country faces imminent "socio-political crisis."

The sick author of the article cites unspecified "runaway graft," incompetent civil service and "general ineptitude in the management of public affairs" as the factors that have brought the Tanzanian economy "to its knees."

Quoting nobodies, the prophet of doom trivialises the recent cabinet reshuffle, which he, however, acknowledges to be the biggest since independence.

In the first place, it is not worth our breath, let alone that of the presidency, to address the malicious, sweeping allegations carried by the Kenyan tabloid. We will leave it to the ministers assaulted personally by the article to decide what to do.

Tanzanians gave President Jakaya Kikwete near unanimous mandate to lead them only 10 months ago and they have endorsed every measure he has taken in his quest to improve their standard of life.

The disparaging, false propaganda against him, which puts journalism in the neighbouring country to great shame, can best be dismissed with the contempt it deserves.

The Governor of the Bank of Tanzania (BoT), which is the custodian of the national economy, Mr Daudi Ballali, reassured the people yesterday that the economy remains on course despite the shocks associated with high oil price, drought and power shortage.

According to Mr Ballali, the economy has been able to withstand the shocks because of macro level gains pegged on sound monetary and fiscal policies and structural reforms in the last decade.

That is far from saying the economy is not on trial, but it is an authoritative statement on the state of the economy. Of course, the government knows that the power shortage must quickly be brought to an end. New exports should be promoted urgently to balance international trade and BoT has to tighten monitoring of economic performance with timely intervention to reverse negative trends. Tanzanian economists have absolutely nothing to learn from the posturing rag in Nairobi.
 
Hii article nzuri sana. Raisi Kikwete soma hapa na ufanyie kazi please. Nchi unaipeleka wapi??????. Hatuna sababu za kuwa maskini Tanzania. Ni uzembe wa marafiki zako.
 
Wanachofanya waandishi wa Kenya ni kuandika kile ambacho waandishi wetu wangeandika. Lakini waandishi wetu ndo hao tena, acha wenzao wazibe pengo. Lakini ndohivyo wanatuchafua sana machoni pa wakenya na waafrika wengine. Wanachotucheka ni kwamba mambo yanakwenda vibaya lakini ndo kwanza tunazidi kumchekea na kumshangilia rais wetu! Ndo mtu moja akiniuliza 'watanzania hata kununa tu hamuwezi?'
 
Maneno mazito haya na ni kweli watanzania sijui tume rogwa ama kuna kitu gani kinatokea .Yaani hali ni mbaya bado tuna angalia .Kazi kubwa mno tunayo mbeleni .
 
Mtalii wetu JK sasa hivi anaelekea Asia na Falme za kiarabu. Ataimaliza dunia hivi karibuni. Habari yenyewe ndo hii hapa. Kwa mtindo huu, ni vigumu kumwamini


Kikwete ziarani ughaibuni kwa wi ki mbili

Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete anaondoka leo nchini kuelekea nchi kadhaa za Asia, Falme za Kiarabu ambako atakuwa na ziara ya zaidi ya wiki mbili.

Taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana ilieleza kuwa ziara hiyo ambayo ni kutokana n a mwaliko wa viongozi wa nchi hizo.

Ziara hiyo, ambayo ni mfululizo wa safari zake, itamfikisha Japan, China, Korea Kusini pamoja na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE). Rais atarejea nchini Novemba 13.

Katika ziara hiyo Rais Kikwete ataongoza na mkewe, Salma, Waziri wa Mipango, Uchumi, Uwezeshaji, Dk Juma Ngasongwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Zanzibar (Fedha na Uchumi), Mwinyihaji Makame .

Wengine ni Naibu Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo na Mbunge wa Muhambwe, Felix Kijiko.
 
Huyu jamaa nadhani ana hisia kwamba bado ni waziri wa mambo ya nje ya Tanzania na si rais wa Watanzania .Tunayo kazi kubwa sana .
 
Jamani kinachofanya mmbeze hivyo rais wenu ni nini? Yaani mnangoja muambiwe na wakenya kumnunnia rais wenu!
JK hajashuka leo, ni kijana wetu kakuliwa hapa, kalitumikia taifa tukaamua kumchagua wenyewe. Leo watu wengine wakuambie ati mnamshabikia Jk, nanyi ati ..ooh tumelogwa? Muacheni ajaribu kutumia ubunifu wake awaletee maendeleo, vuteni subira huku mkifanya wajibu wenu wa kujiletea maendeleo. Msitegemee kumchgua na kesho yake awaleteee maendeleo. Kwa sasa zungumzeni juu ya Ben tu, kwani Jk bado mdaq mfupi sasa kupima mafanikio yake. safari za nje ni mikakati yake wengi hamjui nini hasa anatafuta. au kama mtz unaona kenya mambo yao yanaenda vyema, hebu nenda uone kama mama Kibaki hatakulamba kibao kama alivyowatwanga waanahabari wa huko. Msiige hamaki za wakenya, wao wanaangalia mambo kikabila zaidi ndo maana wanakuwa na chuki na viongozi wao. waandishi wa Kenya wanataka sana mambo ya namna hiyo yawe Tz pia. Charles Onyango-Obo ni mmoja wa watu anmbaye haachi kuiandika vibaya Tz.Mlisema majenerata ya RDC hayatakuja lakini sasa aibu tupu kwa walalmisha yameshaanza kufungwa.
Mchanga wa dhahabu mtu mmoja anaongelea hajui kabisa nini hicho kama ukitaka undani wake niulize uone kwa nini unapelekwa huko.

Tusiige kutoka Kenya tutapotoshwaaaaaaaa..serikali yetu inahitaji zaidi support na sio criticism. Mnajua mapigano ya kooo na koo huko kenya husababishwa na nani? Uchochezi wa vyombo vya habari na viongozi wenye maslahi ya kibabila.
 
Back
Top Bottom