Uzima Tele
JF-Expert Member
- Jan 20, 2023
- 1,104
- 2,345
Ni kwa sababu, haiingii akili hata chembe kwa yeyote mwenye akili timamu kuamini sababu ya kupotea kwa VP siku zaidi 30 bila taarifa yoyote rasmi ya serikali kule aliko na anafanya nini.
Baada ya muda, eti serikali inajitokeza na kudai kuwa VP alikuwa mahali fulani (hapatajwi) na alikuwa kwenye kilichopewa jina la "kazi maalumu" isiyotajwa.
La kujiuliza ni hili kuwa, hivi, ni kazi gani maalumu yenye maslahi kwa nchi hii isiyo na jina aliyokwenda kufanya VP kwa siku 30..?
Kinachofanya tujiulize swali hili ni wajihi na mwonekano wa VP baada ya kujitokeza. Anaonekana ni mtu mnyonge sana. Ni mtu mwenye mawazo mengi (troubled person). Ni kama vile kweli alikuwa anaumwa na labda alikuwa anapata matibabu sehemu.
Lakini kama alikuwa anaumwa na alikuwa anapata matibabu sehemu fulani hapahapa nchini au nje ya nchi, iweje taarifa za kuumwa kwake ziwe siri?
Kwanini haisemwi alikuwa anaumwa badala yake tunaambiwa alikuwa kwenye kazi maalumu? Kunafichwa nini?
Kuumwa mtu (kiongozi VP akiwemo) hakuwezi kufichika jamani. Ambacho si lazima kijulikane ni ugonjwa anaoumwa mtu. Hili linaweza kufichwa na haina shida yoyote...
Kuna hisia kali zinazoweza kuthibitika muda si mrefu kuwa lipo tatizo huko serikalini. Kuna Kila viashiria kuwa huyu mtu alikuwa hatarini na aidha alifichwa au alijificha mahali mwenyewe (Kwa ruhusa ya deep state) ili kujiokoa..!
Lakini kwanini kiongozi mkuu wa level ya VP awe hatarini? Kuna nini ndani ya serikali hii?
Wakati utasema tu, TUSUBIRI.
Baada ya muda, eti serikali inajitokeza na kudai kuwa VP alikuwa mahali fulani (hapatajwi) na alikuwa kwenye kilichopewa jina la "kazi maalumu" isiyotajwa.
La kujiuliza ni hili kuwa, hivi, ni kazi gani maalumu yenye maslahi kwa nchi hii isiyo na jina aliyokwenda kufanya VP kwa siku 30..?
Kinachofanya tujiulize swali hili ni wajihi na mwonekano wa VP baada ya kujitokeza. Anaonekana ni mtu mnyonge sana. Ni mtu mwenye mawazo mengi (troubled person). Ni kama vile kweli alikuwa anaumwa na labda alikuwa anapata matibabu sehemu.
Lakini kama alikuwa anaumwa na alikuwa anapata matibabu sehemu fulani hapahapa nchini au nje ya nchi, iweje taarifa za kuumwa kwake ziwe siri?
Kwanini haisemwi alikuwa anaumwa badala yake tunaambiwa alikuwa kwenye kazi maalumu? Kunafichwa nini?
Kuumwa mtu (kiongozi VP akiwemo) hakuwezi kufichika jamani. Ambacho si lazima kijulikane ni ugonjwa anaoumwa mtu. Hili linaweza kufichwa na haina shida yoyote...
Kuna hisia kali zinazoweza kuthibitika muda si mrefu kuwa lipo tatizo huko serikalini. Kuna Kila viashiria kuwa huyu mtu alikuwa hatarini na aidha alifichwa au alijificha mahali mwenyewe (Kwa ruhusa ya deep state) ili kujiokoa..!
Lakini kwanini kiongozi mkuu wa level ya VP awe hatarini? Kuna nini ndani ya serikali hii?
Wakati utasema tu, TUSUBIRI.