Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 26,107
- 52,832
85 Years Ago to date, Sunday, 10 October 1938 Soviet Union, Moscow Siku hii anazaliwa mtoto mwenye akili nyingi sana Jijini Moscow Urusi, Hawa ndio wale watoto ambao huzaliwa mara moja Baada ya miongo kadhaa.
Kwa kuwa alikuwa ni mtoto mwenye akili nyingi, alifanikiwa kusoma kwenye shuke za vipaji hadi chuo kikuu cha Moscow akisoma mahusiano ya kimataifa. Pia alikuwa anaimudu vizuri lugha ya kijerumani. Alipomaliza chuo akapangiwa kazi katika ubalozi wa ujerumani Mashariki mwaka 1961 Mwaka 1961 alirudi Moscow na kujiunga na idara ya ujasusi KGB ambako alipata mafunzo ya utimamu wa mwili, kujihami, ujasusi na matumizi ya silaha.
Mwaka 1966 akapangiwa kazi katika ubalozi wa Denmark jijini Copenhagen. Mwaka 1968 Akiwa Denmark kukatokea maandamano makubwa yakitaka mabadiliko katika nchi ya kijamaa ya Czechoslovakia. Maandamano haya yaliitwa “Plague springs” Umoja wa nchi za kijamaa USSR wenye makao yake makuu jijini Moscow ukaingilia kati kuwatawanya waandamani wale. Nguvu kubwa iliyotumiwa na nchi yake dhidi ya waandamani haikumfuraisha Kachero huyu hivyo akawa ameingia roho ya uasi dhidi ya taifa lake.
Akaanza kutuma ishara kwa mashirika ya kijasusi ya Denmark na Uingeleza kuwa amejitolea kuwafanyia Counter Intelligence dhidi ya Urusi Alijaribu kutuma ishara ya kwanza kwa kumpigia simu mke wake aliyeitwa Yelena ambaye naye alikuwa ni KGB Akiwa na uhakika kuwa serikali ya Denmark ilikuwa ikizifatilia simu za ubalozi wao, akaanza kuongea maneno mengi ya kuishitumu serikali yake ya Urusi na sera zao za kijamaa. Mkewe akawa anampinga huku yeye akishikilia msimamo wake.
Aliamini kama maafisa wa Denmark watakuwa wamesikiliza mazungumzo yale basi watamtafuta.Ishara hii haikuweza kueleweka na majasusi wa Denmark. Majasusi wa Denmark nao walijikuta wanamhitaji kachero huyu baada ya kubaini lazima atakuwa sio afisa tu wakawaida wa ubalozi wa Urusi.
Bahati mbaya nao walimtumia ishara ambazo kachero hakuweza kuzibaini. Maafisa hao walikosea kwa kuhisi huenda Mtu huyu anajihusisha na mapenzi ya jinsia moja hivyo wakamtumia “Shoga” mmoja ambaye alimuomba kachero huyu wapange miadi ya kunywa pombe pamoja kwenye pub fulani. Nia yao ikiwa akikubali kukutana nae ndiye wamshawishi awe mole wao.
Kachero akamtolea nje! Wakati haya yanaendelea, mashushushu wa Uingeleza wakawa wamepewa sifa nzuri kumhusu mtu huyu kupitia mmoja wa wanafunzi aliyesoma naye Moscow. Mwanafunzi huyu aliewaeleza maafisa wa MI6 kuwa kachero huyu anachukizwa sana na sera ya ujamaa Taarifa zake kikawavutia Ukawekwa mtego kumnasa kwa kumtumia mwadadada mrembo mwanafunzi wa udaktari wa meno ambeye alikuwa mchezaji mashuhuri wa vinyoya(badmiton) mcheo ulipendwa sana na kachero huyu.
Kachero huyu alikuwa akinywa, akichati na hata kutoa out na mwanadada huyu lakini hakuwa anamuonyesha hisia zozote za kimapenzi. Hivyo mpango huu haukuzaa matunda. Ikabidi mkuu wa MI6 pale Denmark asonge front mwenyewe.
Mwaka 1974 shirika la kijasusi la Uingeleza MI6 (Military Intelligence Section 6) kupitia mkuu wake nchini Denmark, akamfata binafsi na kumuomba waongee faragha. Akakubali Huu ndio ukawa mwanzo wa mtu huyu ambaye anadaiwa alikuwa na uwezo wa ajabu wa kukumbuka kuanza kazi kama Mole wa MI6 ndani ya KGB ambaye alipewa jina la uficho la SUNBEAM,
Kwa wakati huo ilikuwa ni kazi ngumu sana kumpata afisa wa KGB ambaye angekubali kuuza siri za taifa lake. Ilikuwa ni sawa na kumpeleka mpelezi akafanye upelelezi ndani ya sayari ya Mars. Hii ilikuwa ni kalata iliyochezwa vizuri na mataifa ya magharibi. Taarifa alizokuwa akituma SUNBEAM, ziliishia mikononi wa rais wa Marekani Ronald Reagan zikitoka kwa waziri mkuu wa Uingeleza Margaret Thatcher ambao saa nyingine aliwasiliana nao directly bila kupitia MI6 JINSI ALIVYOKUWA ANAVUJISHA TAARIFA Wakati ule maelekezo kutoka KGB Moscow yalikuwa yakitumwa kwenda Copenhagen kwa njia ya “microfilm” iliyokuwa inawekwa kwenye “diplomatic pouch” Microfilm ni kifaa kama ule mkanda wa picha uliokuwa unatumika kwenye kamera za zamani.
Pia diplomatic bag ni mfuko au begi linalotumika kusafilishia nyaraka za kidiplomasia kuingia au kutoka ndani ya nchi. Kwa sheria za kimataifa begi hili haliruhusiwi kusachiwa.
Kwa njia hii ndio KGB walikuwa wakituma maelekezo ya kijasusi kwenye ubalozi wa Denmark.
Wakati wa mapuziko kwa ajili ya chakula cha mchana, ndani ya nusu saa, kachero huyu angechukua microfilm iliyoletwa na kwenda kumpatia agent wa MI6 ambaye alikuwa akisimama nje ya ubalozi kwa utulivu usiotia mashaka. Agent huyu alikuwa akichukua microfilm na kwenda kuikopi kwenye kifaa maalumu kilichoandaliwa maalumu kwa kazi hii kwenye safe house yao ya karibu. Baada ya kazi hii Agent aliirudisha original microfilm kwa kachero kisha naye angeirudisha mahali pake bila kushtukiwa ikiwa imeshanakiliwa. Kwa njia hii MI6 na CIA waliweza kupata maelfu ya taarifa nyeti za Urusi kuhusu Denmark kama vile majina ya uficho ya operations zao, maelekezo na uchunguzi wao wa siri.
Pia kachero huyu alikuwa anapeleka taarifa binafsi kwenye safe house ya MI6 alipokuwa akienda mwenyewe. Hapa ndipo Sunbeam aliwashangaza mashushushu kwa uwezo wake wa kutunza kumbukumbu kwani alikuwa akifika bila file lolote lakini alikuwa anashuka data toka kichwani kwa uwezo wa hali ya juu.
Alikuwa anakumbuka maongezi aliyofanya na majasusi wenzake na maudhui yake huku akifafanua kwa taaluma ya hali ya juu. Akapewa jina la utani la “Operation download” Miula yake miwili ya kufanya kazi nchini Denmark iliisha mwaka 1978 hivyo akarudi nchini kwake Urusi jijini Moscow.
I will be back, ni ndefu sana.- I mean no malice to nobody.
Kipande Kinachoendelea
Kwa kuwa alikuwa ni mtoto mwenye akili nyingi, alifanikiwa kusoma kwenye shuke za vipaji hadi chuo kikuu cha Moscow akisoma mahusiano ya kimataifa. Pia alikuwa anaimudu vizuri lugha ya kijerumani. Alipomaliza chuo akapangiwa kazi katika ubalozi wa ujerumani Mashariki mwaka 1961 Mwaka 1961 alirudi Moscow na kujiunga na idara ya ujasusi KGB ambako alipata mafunzo ya utimamu wa mwili, kujihami, ujasusi na matumizi ya silaha.
Mwaka 1966 akapangiwa kazi katika ubalozi wa Denmark jijini Copenhagen. Mwaka 1968 Akiwa Denmark kukatokea maandamano makubwa yakitaka mabadiliko katika nchi ya kijamaa ya Czechoslovakia. Maandamano haya yaliitwa “Plague springs” Umoja wa nchi za kijamaa USSR wenye makao yake makuu jijini Moscow ukaingilia kati kuwatawanya waandamani wale. Nguvu kubwa iliyotumiwa na nchi yake dhidi ya waandamani haikumfuraisha Kachero huyu hivyo akawa ameingia roho ya uasi dhidi ya taifa lake.
Akaanza kutuma ishara kwa mashirika ya kijasusi ya Denmark na Uingeleza kuwa amejitolea kuwafanyia Counter Intelligence dhidi ya Urusi Alijaribu kutuma ishara ya kwanza kwa kumpigia simu mke wake aliyeitwa Yelena ambaye naye alikuwa ni KGB Akiwa na uhakika kuwa serikali ya Denmark ilikuwa ikizifatilia simu za ubalozi wao, akaanza kuongea maneno mengi ya kuishitumu serikali yake ya Urusi na sera zao za kijamaa. Mkewe akawa anampinga huku yeye akishikilia msimamo wake.
Aliamini kama maafisa wa Denmark watakuwa wamesikiliza mazungumzo yale basi watamtafuta.Ishara hii haikuweza kueleweka na majasusi wa Denmark. Majasusi wa Denmark nao walijikuta wanamhitaji kachero huyu baada ya kubaini lazima atakuwa sio afisa tu wakawaida wa ubalozi wa Urusi.
Bahati mbaya nao walimtumia ishara ambazo kachero hakuweza kuzibaini. Maafisa hao walikosea kwa kuhisi huenda Mtu huyu anajihusisha na mapenzi ya jinsia moja hivyo wakamtumia “Shoga” mmoja ambaye alimuomba kachero huyu wapange miadi ya kunywa pombe pamoja kwenye pub fulani. Nia yao ikiwa akikubali kukutana nae ndiye wamshawishi awe mole wao.
Kachero akamtolea nje! Wakati haya yanaendelea, mashushushu wa Uingeleza wakawa wamepewa sifa nzuri kumhusu mtu huyu kupitia mmoja wa wanafunzi aliyesoma naye Moscow. Mwanafunzi huyu aliewaeleza maafisa wa MI6 kuwa kachero huyu anachukizwa sana na sera ya ujamaa Taarifa zake kikawavutia Ukawekwa mtego kumnasa kwa kumtumia mwadadada mrembo mwanafunzi wa udaktari wa meno ambeye alikuwa mchezaji mashuhuri wa vinyoya(badmiton) mcheo ulipendwa sana na kachero huyu.
Kachero huyu alikuwa akinywa, akichati na hata kutoa out na mwanadada huyu lakini hakuwa anamuonyesha hisia zozote za kimapenzi. Hivyo mpango huu haukuzaa matunda. Ikabidi mkuu wa MI6 pale Denmark asonge front mwenyewe.
Mwaka 1974 shirika la kijasusi la Uingeleza MI6 (Military Intelligence Section 6) kupitia mkuu wake nchini Denmark, akamfata binafsi na kumuomba waongee faragha. Akakubali Huu ndio ukawa mwanzo wa mtu huyu ambaye anadaiwa alikuwa na uwezo wa ajabu wa kukumbuka kuanza kazi kama Mole wa MI6 ndani ya KGB ambaye alipewa jina la uficho la SUNBEAM,
Kwa wakati huo ilikuwa ni kazi ngumu sana kumpata afisa wa KGB ambaye angekubali kuuza siri za taifa lake. Ilikuwa ni sawa na kumpeleka mpelezi akafanye upelelezi ndani ya sayari ya Mars. Hii ilikuwa ni kalata iliyochezwa vizuri na mataifa ya magharibi. Taarifa alizokuwa akituma SUNBEAM, ziliishia mikononi wa rais wa Marekani Ronald Reagan zikitoka kwa waziri mkuu wa Uingeleza Margaret Thatcher ambao saa nyingine aliwasiliana nao directly bila kupitia MI6 JINSI ALIVYOKUWA ANAVUJISHA TAARIFA Wakati ule maelekezo kutoka KGB Moscow yalikuwa yakitumwa kwenda Copenhagen kwa njia ya “microfilm” iliyokuwa inawekwa kwenye “diplomatic pouch” Microfilm ni kifaa kama ule mkanda wa picha uliokuwa unatumika kwenye kamera za zamani.
Pia diplomatic bag ni mfuko au begi linalotumika kusafilishia nyaraka za kidiplomasia kuingia au kutoka ndani ya nchi. Kwa sheria za kimataifa begi hili haliruhusiwi kusachiwa.
Kwa njia hii ndio KGB walikuwa wakituma maelekezo ya kijasusi kwenye ubalozi wa Denmark.
Wakati wa mapuziko kwa ajili ya chakula cha mchana, ndani ya nusu saa, kachero huyu angechukua microfilm iliyoletwa na kwenda kumpatia agent wa MI6 ambaye alikuwa akisimama nje ya ubalozi kwa utulivu usiotia mashaka. Agent huyu alikuwa akichukua microfilm na kwenda kuikopi kwenye kifaa maalumu kilichoandaliwa maalumu kwa kazi hii kwenye safe house yao ya karibu. Baada ya kazi hii Agent aliirudisha original microfilm kwa kachero kisha naye angeirudisha mahali pake bila kushtukiwa ikiwa imeshanakiliwa. Kwa njia hii MI6 na CIA waliweza kupata maelfu ya taarifa nyeti za Urusi kuhusu Denmark kama vile majina ya uficho ya operations zao, maelekezo na uchunguzi wao wa siri.
Pia kachero huyu alikuwa anapeleka taarifa binafsi kwenye safe house ya MI6 alipokuwa akienda mwenyewe. Hapa ndipo Sunbeam aliwashangaza mashushushu kwa uwezo wake wa kutunza kumbukumbu kwani alikuwa akifika bila file lolote lakini alikuwa anashuka data toka kichwani kwa uwezo wa hali ya juu.
Alikuwa anakumbuka maongezi aliyofanya na majasusi wenzake na maudhui yake huku akifafanua kwa taaluma ya hali ya juu. Akapewa jina la utani la “Operation download” Miula yake miwili ya kufanya kazi nchini Denmark iliisha mwaka 1978 hivyo akarudi nchini kwake Urusi jijini Moscow.
I will be back, ni ndefu sana.- I mean no malice to nobody.
Kipande Kinachoendelea