Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,993
Haina maana mimi tu ndio nitumie hapana.
Wala hatutakiwi kumkubali kirahisi tu kwa sababu alikuwa Mchungaji na Wachungaji wamemkubali.
Atumie jina la Yesu, lakini afundishe watu, waelewe na kumkubali Bwana Yesu, kama bwana na Mwokozi wa Maisha yao.
Awafundishe kuabudu katika jina la Yesu, halafu awape dawa wa pone.
Inakuwaje unamwambia mtu nimekuponya kwa jina Yesu anaondoka wala hasemi habari za Yesu anasema habari za Kikombe na Babu mwenyewe.
Hayo ni maswli ambayo yananifanya nishindwe kuikubali na kuiamnini.
Kwa upande mwingine, Njia za Mungu zipo nyingi, kutokana na hilo ndo maana na sema TUOMBE UKWELI UJULIKANE.
Yawezekana mmenilewa vibaya au nimejieleza vibaya hapo juu, ila lengo langu ni kwamba. NIngemwelewa Babu kama asingemhusisha Mungu kwa Jina la Yesu, katika hiyo dawa yake, ikajulikana tu kuna Dawa imegunduliwa na babu inaponya watu, wa DINI zote, kabila zote, na Rangi zote, iwe unamwamini Yesu au humwamini pia. We amini kikombe na Babu mwenyewe basi.
Unaposema Kikombe kina ponya kwa jina La Yesu, wakati kuna watu hawataki kulisikia hata hilo jina la Yesu, lakini wanakwenda kwa sababu ya magonjwa na Mateso tu, mimi nakuwa sielewe. Ndio maana nikasema Basi yeye atibu tu, kwa mti na maji kama hana nafasi ya kufundisha habari za Yesu aache kulitumia hilo jina.
Tuendelee kuweka Imani yetu, kwenye Hayo maji na huo mti.
Mbarikiwe.
Babu hawezi kuacha kulitumia jina la YESU kwakuwa tu kuna watu hawapendi kulisikia, na wasiopenda kusikia jina la YESU likitajwa wakokila mahali si kwa babu wa loiondo pekee.
Isitoshe watu wasiopenda kulisikia jina la YESU likitajwa na babu wa loliodo ni pamoja na wewe. Yesu alipomuamuru mkoma akajitose mto jordani mara saba hakuacha kulitaja jina la Mungu baba,vinginevyo YESU angeendelea tu kuponya watu pasipo kutaja jina la Mungu kwa kuwa wengine walikuwa hawamjui Mungu bali walisukumwa na mateso ya magonjwa waliyokuwa nayo.