Kwahiyo wewe tu ndo unaruhusiwa kulitumia jina la YESU lakini mchungaji mstaafu aliyetumia muda wa maisha yake kumhubiri YESU kristo sasa haruhusiwi tena kulitaja jina kla YESU kwenye huduma yake kwa kuwa tu hupendi?? kazi bado mbichi kwa kweli, unakwenda mbele hatua tano kisha unarudi nyuma hatua kumi!!
Haina maana mimi tu ndio nitumie hapana.
Wala hatutakiwi kumkubali kirahisi tu kwa sababu alikuwa Mchungaji na Wachungaji wamemkubali.
Atumie jina la Yesu, lakini afundishe watu, waelewe na kumkubali Bwana Yesu, kama bwana na Mwokozi wa Maisha yao.
Awafundishe kuabudu katika jina la Yesu, halafu awape dawa wa pone.
Inakuwaje unamwambia mtu nimekuponya kwa jina Yesu anaondoka wala hasemi habari za Yesu anasema habari za Kikombe na Babu mwenyewe.
Hayo ni maswli ambayo yananifanya nishindwe kuikubali na kuiamnini.
Kwa upande mwingine, Njia za Mungu zipo nyingi, kutokana na hilo ndo maana na sema TUOMBE UKWELI UJULIKANE.
Yawezekana mmenilewa vibaya au nimejieleza vibaya hapo juu, ila lengo langu ni kwamba. NIngemwelewa Babu kama asingemhusisha Mungu kwa Jina la Yesu, katika hiyo dawa yake, ikajulikana tu kuna Dawa imegunduliwa na babu inaponya watu, wa DINI zote, kabila zote, na Rangi zote, iwe unamwamini Yesu au humwamini pia. We amini kikombe na Babu mwenyewe basi.
Unaposema Kikombe kina ponya kwa jina La Yesu, wakati kuna watu hawataki kulisikia hata hilo jina la Yesu, lakini wanakwenda kwa sababu ya magonjwa na Mateso tu, mimi nakuwa sielewe. Ndio maana nikasema Basi yeye atibu tu, kwa mti na maji kama hana nafasi ya kufundisha habari za Yesu aache kulitumia hilo jina.
Tuendelee kuweka Imani yetu, kwenye Hayo maji na huo mti.
Mbarikiwe.