Hoja ya Shossi juu ya sh. 500/- ya babu

Hoja ya Shossi juu ya sh. 500/- ya babu

Naomba niweke wazi kitu kimoja hiyo mia tano inayoonekana kama tunaipinga kwa wivu si kweli kwani kama matumizi yake ni kusaidia wajane na masikini biblia imesema "[FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu, [/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.[/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]" Luka 12:32-33[/FONT]

Mimi na wewe Miss Judith tunachokipinga ni kuwapa "kikombe" bila kuwapa neno la Mungu hata biblia imesema [FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]"Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana".[/FONT] Luka 12:34 ndio maana mimi na wewe tunampinga babu si kwa kuwa anapokea mia tano ila kwakuwa hawapi watu chakula cha roho hafanyi anavyotakiwa kufanya!
 
Naomba niweke wazi kitu kimoja hiyo mia tano inayoonekana kama tunaipinga kwa wivu si kweli kwani kama matumizi yake ni kusaidia wajane na masikini biblia imesema "[FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu, [/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.[/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]" Luka 12:32-33[/FONT]

Mimi na wewe Miss Judith tunachokipinga ni kuwapa "kikombe" bila kuwapa neno la Mungu hata biblia imesema [FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]"Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana".[/FONT] Luka 12:34 ndio maana mimi na wewe tunampinga babu si kwa kuwa anapokea mia tano ila kwakuwa hawapi watu chakula cha roho hafanyi anavyotakiwa kufanya!

unahangaika sana ku-judge waliokuhusu

Ungejiangalia wewe na utimilifu wako na ufitini wako... basi tanzania inekua mbali sana

dogo unantia shaka sana kama uko straight aisee
 
Miss Judith may i know where you worship? I means your church
 
Naomba niweke wazi kitu kimoja hiyo mia tano inayoonekana kama tunaipinga kwa wivu si kweli kwani kama matumizi yake ni kusaidia wajane na masikini biblia imesema "[FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu, [/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.[/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]" Luka 12:32-33[/FONT]

Mimi na wewe Miss Judith tunachokipinga ni kuwapa "kikombe" bila kuwapa neno la Mungu hata biblia imesema [FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]"Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana".[/FONT] Luka 12:34 ndio maana mimi na wewe tunampinga babu si kwa kuwa anapokea mia tano ila kwakuwa hawapi watu chakula cha roho hafanyi anavyotakiwa kufanya!

tuko pamoja mkuu,

watu wanasema tuna wivu na biashara ya babu, mara wengine wanauliza kuwa hatuwaoni akina mwingira, kakobe, rwakatale, gwajima nk. hawakioni tunachokihoji. hawazingatii misingi ya maandiko tunayonukuu wala hawajali kama hata wachawi, wanga, wala rushwa, makahaba, majambazi nk wanakunywa dawa na kurudi kufanya maasi yao kama siku zote. na wengine wamepewa wakiwa ndani ya magari na kisha kugeuza magari yao na kupotea bila walau maneno mawili matatu ya kiroho! hapo lazima mtu yoyote ajuaye maana ya dini ajiulize mara mbili kuwa hii nihuduma ya aina gani?

Mungu apange bei ya karama yake ya uponyaji na asijihusishe kwa kiwango chochote na uponyaji wa roho! hakuna jina la Yesu linalotajwa pale zaidi ya jina la babu mwenyewe na jina la mti wake wa tiba.

kwa kweli kuna mengi sana ya kuhoji na nakushukuru sana kwa kuendelea kutafakari bila kuchoka kuhusu hili suala. tuko katika nyakati za hatari sana mpendwa

ila nashukuru wapo baadhi wameanza kuelewa tunachokongea, wapo waliokuwa wanaogopa kusema waziwazi lakini baadaye nao wameonyesha waziwazi kutokubaliana na mpamgilio mzima wa mambo huko kijjini na kuyahusianisha na Yesu ama dini, tena wengine wameongeza sana uzito wa kimaandiko na umekuwa msaada na mwangaza mkubwa sana.

kwa kweli nawashukuru sana wapendwa wote waliochukua muda wao kusoma maandiko, kuyatafakari na kutushirikisha hapa jamvini kwa faida ya wote. mbarikiwe sana wapendwa.

safari ni ndefu mpendwa lakini naamini hatimaye kweli itashinda

nakutakia siku njema na tafakari njema

asante na Mungu akubariki sana
 
Naomba niweke wazi kitu kimoja hiyo mia tano inayoonekana kama tunaipinga kwa wivu si kweli kwani kama matumizi yake ni kusaidia wajane na masikini biblia imesema "[FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu, [/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.[/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]" Luka 12:32-33[/FONT]

Mimi na wewe Miss Judith tunachokipinga ni kuwapa "kikombe" bila kuwapa neno la Mungu hata biblia imesema [FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]"Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana".[/FONT] Luka 12:34 ndio maana mimi na wewe tunampinga babu si kwa kuwa anapokea mia tano ila kwakuwa hawapi watu chakula cha roho hafanyi anavyotakiwa kufanya!

Carnal mind,

Andiko huua bali Roho huhuisha.
 
tuko pamoja mkuu,

watu wanasema tuna wivu na biashara ya babu, mara wengine wanauliza kuwa hatuwaoni akina mwingira, kakobe, rwakatale, gwajima nk. hawakioni tunachokihoji. hawazingatii misingi ya maandiko tunayonukuu wala hawajali kama hata wachawi, wanga, wala rushwa, makahaba, majambazi nk wanakunywa dawa na kurudi kufanya maasi yao kama siku zote. na wengine wamepewa wakiwa ndani ya magari na kisha kugeuza magari yao na kupotea bila walau maneno mawili matatu ya kiroho! hapo lazima mtu yoyote ajuaye maana ya dini ajiulize mara mbili kuwa hii nihuduma ya aina gani?

Mungu apange bei ya karama yake ya uponyaji na asijihusishe kwa kiwango chochote na uponyaji wa roho! hakuna jina la Yesu linalotajwa pale zaidi ya jina la babu mwenyewe na jina la mti wake wa tiba.

kwa kweli kuna mengi sana ya kuhoji na nakushukuru sana kwa kuendelea kutafakari bila kuchoka kuhusu hili suala. tuko katika nyakati za hatari sana mpendwa

ila nashukuru wapo baadhi wameanza kuelewa tunachokongea, wapo waliokuwa wanaogopa kusema waziwazi lakini baadaye nao wameonyesha waziwazi kutokubaliana na mpamgilio mzima wa mambo huko kijjini na kuyahusianisha na Yesu ama dini, tena wengine wameongeza sana uzito wa kimaandiko na umekuwa msaada na mwangaza mkubwa sana.

kwa kweli nawashukuru sana wapendwa wote waliochukua muda wao kusoma maandiko, kuyatafakari na kutushirikisha hapa jamvini kwa faida ya wote. mbarikiwe sana wapendwa.

safari ni ndefu mpendwa lakini naamini hatimaye kweli itashinda

nakutakia siku njema na tafakari njema

asante na Mungu akubariki sana


Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi. Yohane 2:1
 
Miss Judith may i know where you worship? I means your church

Ingawaje aliwahi kujibu yeye ni mlutheran lakin mwenendo wake unaonyesha sio lutheran.
Yaani ukiangalia wengi wanaompinga Babu ni watu wa madhehebu tofauti na Babu, hasa hasa wale wa Efatha, FBFC kwa kakobe na type zingine kama hizo ndio wanaongoza kwa kutapatapa.
Yaani Babu amewatikisa kisawasawa na wao si tu kwamba wametikisika, bali wamepukutika mpaka manyoya, sasa wako uchi wanatafuta nguo za kujisitiri hapa JF
 
Miss Judith, toka mwanzo unampinga sana huyo babu, ushayri mfupi tu, waache wenye matatizo waende wakatibiwe, hospitali unalipa kiasi gani that ulalame sh 500? Na 500 yenyewe inayoenda kanisani huoni hata haya kusema eti masharti? Dada amini unachoamini na wengine waamini wanachokiamini acha kulalama ovyo kila siku, so far una hakika gani unachoamini ndo sahihi zaidi kuliko wengine huh??Acha watu wanaoteseka na magonjwa wakatibiwe km dawa inatibu acha maswali ya kipuuzi eti kuchemshwa..so unatala watafune mzizi km ulivyo?? I guess utakuwa wa mlokole wa makanisa binafsi wewe ndo huwa wako so selfish!!

Judith hija yake ni kuwa wanaoenda kwa babu baada ya kupata kikombe hawapati neno la Mungu isije ikawa ni tamaa ya kupata matibabu kwa pesa ndogo kwani hata bilia inasema "Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo. Yakobo 1:15".
 
Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi. Yohane 2:1

Kaka hivi injili umeanza lini kuihubiri maana pale CBE tulikujua uko upande wa pili.

Au ndiyo mambo ya Balaam asipomtii Mungu, punda anaongea (numbers 22:28).

I'm beginning to like this drama
 
Judith hija yake ni kuwa wanaoenda kwa babu baada ya kupata kikombe hawapati neno la Mungu isije ikawa ni tamaa ya kupata matibabu kwa pesa ndogo kwani hata bilia inasema "Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo. Yakobo 1:15".

Kaka hata hujui hoja ya dada Judith, isome tena maana issue sio wanaokwenda bali ni anayetoa huduma.
Usiquote maandiko ambayo ni irrelevant.
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Si kawaida yangu kurejea kwenye mada niliyoichangia lakini baada ya kuipitia tena na kusikiliza maneno ya mitaani nimeona si vibaya nikarejea tena kuchangia hii mada.

Mwanzo nilisema wanaopinga huduma ya Babu wa Loliondo wa wanasumbuliwa na wivu hawana hoja za maana za kumshawishi mtu mwenye akili zake ambaye hajawahi kusumbuliwa na magonjwa ya akili kuacha kufuata huduma ya Babu.

Nimegundua mambo mengi kwanini wapo wapinzani wengi wa huduma ya Babu.

[1] Tofauti za kimadhehebu ni sababu kubwa inayotumuiwa na baadhi ya viongozi wa madhehebu ya kikristo kuwatisha waumini wao wasiende kupata tiba ya Babu.Madhehebu mengi hasa Assambless of God waumini wake wengi walikuwa wakiabudu aidha Catholic,Lutheran au Anglican.Waumini wamejazwa ujinga kwamba uponyaji kamwe hauwezi kupatikana nje ya dhehebu lao yaani Pentecoste/Assembless of God.kwakuwa Babu wa Loliondo ni mchungaji mstaafu wa Kilutheri dhana kwamba hakuna upako au uponyaji inaendelezwa sana na kukuzwa.

Nitatoa mfano mmoja kukazia hoja yangu,Mwalimu C Mwakasege ni muumini wa kanisa la Lutherani wakati anaanzisha huduma yake [Maana] alikumbana na upinzania mkali kweli kwanini hajahama dhehebu la Lutheran ambako hakuna upako /Yesu na nk.Mwalimu Mwakasege alikuwa akiwajibu vizuri sana baadhi ya wakosoaji wake wakubwa kwamba Yesu hakai kwenye Madhehebu wala hakuna dhehebu liloanzishwa na Yesu kila mtu anayeokoka abaki kwenye dhehebu lake.Ukishangaa kwanini Askofu Mtume na Nabii Mwingira anamwandama Babu utakuta ni dhana ile ile ya haya madhehebu kudhani Mungu yuko kwenye madhebu yao tu mengine ni wasindikizaji tu.

Nilihudhuria mkutano wa Injili wiki iliyopita nilishangaa mhubiri alikuwa akitumia muda mwingi kumkosoa Babu badala ya kumuubiri Kristo.Kila kipengele kuhusiana na babu kilichambuliwa kwa namna ya ushabiki wa ajabu kiasi waumini/wasikilizaji wakakosa amani ya kuendelea kumsikiliza mhubiri.Shilingi mia tano anayotoza Babu ilijadiliwa kiasi kwamba hata wenye sadaka ya 500 walishindwa kutoa eg ina alama ya nyoka na nk.

Mwisho Babu wa Loliondo hajamlazimisha mtu au watu wamfuate ikiwa moyo wako unakukataza kwenda kupata tiba sawa lakini habari za kumzushia Babu ni vyema zikaachwa kabisa watu,ndugu na jamaa wamekwenda wamepata tiba/kikombe wamepona magonjwa sugu yaliyowasumbua na kuwatesa kwa muda mrefu chuki za nini mbona mlikuwa mnanunua vitambaa vya Mama G Lwakatare,Mlikuwa mkombewa na Mzee wa Upako mkatia fedha nyingi kwenye A/C yake binafsi haikuwa nongwa.Babu habagui anatoa kikombe kwa watu wote Waislamu kwa wakristo bila kukulazimisha kufuata dini anayoiamini punguzeni chuki maana najua kuacha kabisa haiwezekani.

Wiki ijayo mvua ikipungua nakwenda kupata kikombe cha Babu !!!!!!!.

Ngoja nikuhubirie brother Ngongo. Shetani ni mjanja sana anapoanzisha kitu anajua jinsi ya kuwapata wote wanaoamini na wasioamini ili tu jina la Yesu litukanwe na nguvu ya roho mtakatifu isitende kazi katikati ya wanadamu. Sasa unachosema kuhusu hao wahubiri wa makanisa ya kiroho yana ukweli wa kishetani lakini ashukuriwe Mungu ambaye hekima yake yashinda uovu wote. Sasa nifafanue namaanisha nini; wahubiri wakihubiri kuhusu makanisa, dini au chochote kinachohusu wao bila kumpa Mungu utukufu wanaingia katika mtego wa shetani na kutoka nje ya neema ya Mungu, na hilo likitokea shetani anapata nafasi ya kuwatandika kwa njia mbalimbali kama vile mapato yao kushuka. Napia anajua wale wasiolijua neno nirahisi kuvutwa na miujiza so kote kote anakuwa amejipatia utukufu.

Lakini ebu tuone neema ya Mungu inavyofanya kazi; hao wahubiri wakingia katika misuko suko watarudi kwenye magoti yao na kumuuliza Mungu ni wapi wamepotea? Nao watajifunza na katika kujifunza wanaingia katika level nyingine ya kumjua Mungu na utendaji wake na hivyo kuongezewa upako mara dufu. Na wale waliopotea kwa kunywa dawa za mganga wa Jadi kwa kulitumia vibaya Jina la Yesu watapokea uponyaji na hiyo itakuwa ni sehemu ya wao kuanza kuliamini jina la Yesu na kwa neema ya Mungu wataanza kusikiliza neno na hatimaye baadaye kugundua walikosea kwani ule uponyaji wakwanza haukuwa permanent lakini huu wa kulijua hasa jina la Yesu ndiyo hasa unaoleta uponyaji kami unaoambatana na amani na satisfaction in personal desires. Watapata nafasi ya kujua tofauti ya huo utapeli wa mwanzo na kugundua kweli ambayo bila huo uwongo pengine wasingekuja jua the real Jesus.

Utaniuliza how do you know? Simple through the word of God; Ebu tafakari haya yafuatayo. Mungu alipokuja duniani kwa mfano wa mwanadamu na kuitwa Emanuel/Yesu shetani alimjua kuwa ni nani japo wanadamu hawakumjua maana shetani alikuwa na Mungu kabla ya mwanadamu. Lakini alijua kuwa kwavile umungu wake haupo ndani yake basi akifa ndiyo mwisho wake for anajua principle zote za kiroho na mwili. Kitu ambacho hakukijua ni Wisdom of God ambayo ni roho mtakatifu tu ndo anayeijua. So akataka kumuua kupitia herode ikashindikana maana bado wanadamu walikua hawajapata kujua. Alipopata nafasi ya kumuua ukubwani akajua amemaliza kazi na ushindi ni wake bila kujua kuwa yote aliyoyafanya ndiyo hasa plan ya Mungu ya kumwokoa binadamu. Maana bila dhambi hakuna kifo ndiyo maana ilibidi Yesu achukue dhambi zetu ili aweze kufa maana Mungu hawezi kuitizama dhambi na macho ya Mungu (roho mtakatifu) yanapoondoka kwako tayari unakufa automatically. Lakini pia bila kifo Yesu asingeweza kufika kuzimu maana ni kwa njia ya kifo tu ndipo mtu unaweza kufika kuzimu ndiyo maana neno la Mungu linasema wote wasio na roho wa Mungu wameshakufa japo kuwa wanaonekana ni hai. Na Kama Yesu asingeenda kuzimu asinge pata nafasi ya kukutana na shetani na kumnyang'anya nguvu zake alizopewa na mwanadamu kwa hiari yao wenyewe kwa kukosa utii na kumtii shetani. Na kufumba na kufumbua Mungu aka create a new beggining yaani Yesu kufufuka katika wafu; it was the first thing to happen ambacho shetani alikuwa hakijui na kwa design hii basi akatengenezwa Adam mpya ambaye hajazaliwa kwa mwili wa damu na nyama bali kwa nguvu ya roho Mtakatifu; neno la mungu linasema "ile ile nguvu ya roho iliyomfufua Yesu kaburini inakaa ndani yenu na hivyo kuwafanya ninyi kuwa viumbe vipya si kwa mfano wa Adamu wa kwanza bali kwa Adamu wa pili ambaye hakuzaliwa na corruptible body. So shetani kwa mara nyingine akagundua kwa mikono yake ametengeneza ukombozi wa mwanadamu na Mungu akabakia kuwa mwenye haki. Maana anajua kabisa hapo Mungu hakuhusika bali yeye mwenyewe kwa mikono yake.

It is gud to meditate and know the word of God, bila hilo tutakuwa victim wa shetani kilasiku japo kwa neema Mungu hutuokoa na hayo yote. Sasa kwa mkristo mwenye kujua neno kama mimi nikienda kwa babu basi ndiyo nimeshajipeleka jehanamu milele maana neema ya Mungu nimeikataa kwa utashi wangu mwenyewe. Lakini kwaasiyelijua neno la Mungu bado inaweza pia ikawa njia ya kumpeleka kwenye uwokovu kamili. Inanipasa mimi niliyefunuliwa kuwafundisha wengine ili wasipotee na nisipofanya hivyo tayari natenda dhambi. Lakini pia nimepewa angalizo kwamba wale tu ambao kwa hakika hajui walitendalo hata kama ni waamini tayari. Lakini wale ambao wameamua kumtumikia shetani kwakupenda huku wakijua wanachokifanya ni dhambi basi hao nijitenge nao maana wanafanya kazi pampja na shetani nao wanahukumu yao ambapo Mungu anawaambia ole wao. Hili tunalisoma katika Timotheo zote mbili. So God has His own ways of dealing with things na sisi hatuna sababu ya kuhukumu maana hukumu ni yake yeye. We preach the gospel thats it and leave the rest for him to do huku tukiendelea kujinyenyekesha chini ya mkono wake wenye nguvu na kumrudishia sifa na utukufu yeye na siyo makanisa, dini zetu au vyeo vyetu mf. pastor, mtume, nabii etc.

Mbarikiwe na bwana!
 
watu wanahangaika sana na umaarufu wa duniani

Haya bana
 
kama huiamini tiba yake stay back and mind your own stuffs! He is not forcing anyone not even advertised! Sasa kama wewe huitaki so what? Kill him then....!

Badala yake wao ndio wanam-advertise makanisani, JF na kwingineko.
Babu wa watu kama angekuwa anasoma JF nadhani angetamka laana maana umri wake tu unastahili heshima fulani ktk jamii much more kwamba alikuwa mtumishi wa Mungu.
 
ndugu pakajimmy,

hatukejeli wanaopata faraja huko kwa babu kutokana na magonjwa na madhaifu mbalimbali, la hasha. tunawashauri wapendwa wetu wasome na kufahamu ukweli juu ya nini yaliyo mapenzi na makusudi ya Mungu kama yalivyobainishwa ndani ya biblia na wapime na kujaribu kila roho kama inatokana na Mungu.

hivi kuna mtu huko samunge aliyepata majaribu kumshinda ayubu? mbona ayubu alikataa kumkufuru Mungu? iweje maelfu huko samunge wawe tayari kumdhihaki Mungu kwa sababu ya BP, cancer, ukimwi nk, eti kwa kupokea kikombe cha mchungaji mstaafu!

mwenye imani ya kweli na iliyojengwa kwenye neno (siyo iliyojengwa kwenye miujiza) atamtukuza Mungu hata apate mateso kiasi gani. atamtukuza Mungu hata katikati ya mateso, naam hata kama atamiminwa damu na kufa kama shahidi (martyr). imani yenu iko wapi sasa?

mimi niko tayri kuishi na majaribu ya ukimwi na mengineyo sugu lakini sio kumkufuru Mungu kiasi hicho cha samunge. ee Mwenyezi Mungu naomba nisaidie

Glory to God
Kumbuka shida haina adabu. Waliojaa kwenye Makanisa ya kina Kakobe, Rwakatare, Fernandes, Mzee wa upako "Mitume" na "Manabii" ni watu walioelemewa na msalaba kiasi cha kuitafuta ahueni popote. Walikimbilia kwenye makanisa hayo kusaka miujiza wenye nayo wanayoinadi, miujiza ambayo baadae waligundua ni hila na ulaghai na usanii kibao wakiambulia kukombwa mamilioni na baadhi kufilisika.
Kumbe shida zao zilitumika kama vitega uchumi wa "Wachungaji" walaghai hawa. Ndiyo maana wanalalama baada ya kuona wafuasi wao wanakimbilia kwa Babu na huko wanapokea uponyi usio na hila, gharama, ulaghai vitisho wala kulazimishwa uhamie dhehebu la Babu.
Mwacheni Babu aendeleze utume wake kwa vile kama kazi si ya Mungu itajishuhudia.
 
Ingawaje aliwahi kujibu yeye ni mlutheran lakin mwenendo wake unaonyesha sio lutheran.
Yaani ukiangalia wengi wanaompinga Babu ni watu wa madhehebu tofauti na Babu, hasa hasa wale wa Efatha, FBFC kwa kakobe na type zingine kama hizo ndio wanaongoza kwa kutapatapa.
Yaani Babu amewatikisa kisawasawa na wao si tu kwamba wametikisika, bali wamepukutika mpaka manyoya, sasa wako uchi wanatafuta nguo za kujisitiri hapa JF

Nitashangaa kama Wapentekoste watakuwa wametikiswa na huduma ya babu. Lengo kuu la Upentekoste ni kuokoa na kuponya roho za watu zimrejee Bwana na kuufikia uzima wa milele. Upentekoste unaongozwa na roho aliye hai - ni zaidi ya mwili ulio hai. Uponyaji wa mwili ni jambo/lengo la muda mfupi kwa ajili ya kudhihirisha utukufu wa Mungu tu na si mwisho wa yote. Ndio maana miujiza si huduma kuu katika Ukristo (ingawa wako wanaoona hivyo). Sasa kama kweli huduma ya kiroho itazidiwa na huduma ya uponyaji wa mwili basi suala la kujiuliza ni kama kweli kazi ya Bwana inafanywa katika kweli yake badala ya kulinganishwa na biashara za kidunia zinazopimwa na ukubwa wa soko (idadi ya wafuasi) bila kujali "thamani halisi" ya soko hilo. Hapo Babu anaweza kuwa amepatia kuwaambia baadhi ya viongozi wa dini kwamba wako kibiashara zaidi.
 
hivi kama ana watu zaidi ya elfu 4 wanaosubiri kutibiwa unatarajia akianza kutia neno kwa mmoja mmoja anamaliza lini? Its so very clear toka mwanzo babu anaongelea tiba na imani, sasa mnataka hadi mahubiri mpewe, mnayohubiriwa kila jumapili hayawatoshi? The fact is dawa ameiombea so unapokunywa kwa imani that mungu amekuponya unapona..whats so complicated hapo? Acheni kujudge imani za watu, miss judith hata siku ya hukumu sisi walimwengu unaotusikitikia tutakupungia mkono ukiwa unaingia jehanam na bikira yako, na sie peponi including babu...

Mkuu tatizo ni kuwa watu wanakunywa kwa imani ipi? kama kuna imani mbona hakuna kuitangaza kabla au baada ya kunywa dawa? kinachoangaliwa una mia tano unapewa kikombe inavyoonyesha imani si mali kitu kwa babu ila "mia tano" ndio mpango mzima. Ngoja nikupe neno la Mungu jioni ya leo.....

Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake.Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwa mwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia. Kisha mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya.Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu.Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi Yohane 10:11-14

Tumeona kuwa mchungaji mwema yupo tayari kufa kwa ajili ya kondoo wake, na yule mchungaji anaejali "jero jero" anaweza kuwakimbia kondoo wanapovamiwa na mbwa mwitu!
 
Nitashangaa kama Wapentekoste watakuwa wametikiswa na huduma ya babu. Lengo kuu la Upentekoste ni kuokoa na kuponya roho za watu zimrejee Bwana na kuufikia uzima wa milele. Upentekoste unaongozwa na roho aliye hai - ni zaidi ya mwili ulio hai. Uponyaji wa mwili ni jambo/lengo la muda mfupi kwa ajili ya kudhihirisha utukufu wa Mungu tu na si mwisho wa yote. Ndio maana miujiza si huduma kuu katika Ukristo (ingawa wako wanaoona hivyo). Sasa kama kweli huduma ya kiroho itazidiwa na huduma ya uponyaji wa mwili basi suala la kujiuliza ni kama kweli kazi ya Bwana inafanywa katika kweli yake badala ya kulinganishwa na biashara za kidunia zinazopimwa na ukubwa wa soko (idadi ya wafuasi) bila kujali "thamani halisi" ya soko hilo. Hapo Babu anaweza kuwa amepatia kuwaambia baadhi ya viongozi wa dini kwamba wako kibiashara zaidi.

Makwazo hayana budi kuja lakini ole wake yule ambaye yaja kupitia yeye, japo kuwa Yuda Iskariote alikuwa katika kutimiza adhima kuu ya ukombozi lakini kwakua alikubali kumtumikia shetani ilimpasa kukosa neema ya Mungu Ole kwa Babu mwenye kuzipoteza roho za wadogo hawa huku akiijua kweli yote ingekuwa heri kwake kama asingezaliwa. Asifiwe Yesu wa msalaba maana hata baada ya kuwapoteza kupitia kwazo lake wengi wataokolewa na kuufikilia ukweli na kwahilo jina la Yesu litabaki likiabudiwa mbinguni na dunia. Kama wingi wa watu ndiyo kipimo cha huduma Yesu aliwaambia wale maelfu siku ile baada ya jana yake kufanya miujiza ya mkate na samaki kuwa leo wanaenda kula mwili wake na kunywa damu yake; wote wakarudi nyuma na kumwacha na tangu siku ile hawakuambatana naye tena. Akawageukia mitume kumi na mbili nakuwauliza kama na wao wanalifuata kundi lilomwacha; Petro akawaokoa akasema tuende wapi bwana WEWE UNA MANENO YA UZIMA; hakusema wewe unatenda miujiza. Lakini kule Efeso the word of God grew mightly and prevailed na hapo mamilioni wakawa converted. So its for Glory of God sometimes uwongo/makwazo yaje ili jina lake liinuliwe zaidi baada ya uwongo kujulikana.

Last week Pr. Chris amefanya night of Blis South Africa kwenye World Soccer Stadium ule umati na technology iliyotumika haijapata tokea kwenye christian gatherings hata world occasions isipokuwa kwenye soccer ambayo ndiyo gathering ya garama duniani na huandaliwa na mataifa mengi; lakini miezi michache tu huyu Pr. alirushiwa tuhuma nzito na zenye kuvunja moyo. Mungu amejibu kwa moto and most of souls were saved vilema walipona, viziwi walisikia, magonjwa yaliponywa na Mamilioni walitoa maisha yao kwa Kristo. Kabla ya kristo kurudi dunia inaenda kushuhudia uwezo na nguvu za roho mtakatifu kwajinsi isivyo weza kuelezeka kwa maneno ya binadamu lakini hii ni ili injili ihubiriwe kwa kila kiumbe ili asijetokea yeyote atakaye sema hakusikia neno la Mungu. Baada ya hapo roho mtakatifu ataondoka ili wale walio wadunia hii na kiongozi wao mkuu shetani waiitawale dunia kabla ya Yesu kurudi na watakatifu kuja kuweka mwisho wa utawala wa Ibilisi na ma urget wake na kuikunja dunia kama karatasi huku akianzisha ufalme upya wa Yerusalemu mpya ambapo hatutahitaji mwanga wa Jua na Mwezi bali yeye ndiye atakuwa mwanga wa milele.

Kila sikio linalosikia hili linapewa wito wa kuikimbilia neema na kuachana na mambo ya ulimwengu huu. Haijalishi wewe ni dini gani, race gani, jinsia ipi na status gani. Wokovu siyo dini wala kanisa bali ni kumkubali Yesu kutawala maisha yako ili upate nguvu ya roho mtakatifu uweze kuishinda dhambi maana kwa mwili wa damu na nyama dhambi huwezi kuikwepa na dhambi kubwa ni kukataa neema na kukumbatia giza. Silazima uhame dhehebu unaweza baki hapo hapo la msingi ukubali kwa moyo bila unafiki na uanze kukiri Lordship of Jesus hadharani kwa kinywa chako hii ndiyo design ya kupata wokovu, yaani kuamini moyoni na kukiri kwa kinywa. Mungu alipoumba dunia roho ya Mungu ili tulia juu ya maji na kisha akatamka mwanga nau ukawa akaita mwanga mchana na giza usiku...Hii inaonyesha hiyo design, aliamini (Roho wa Mungu kutuliajuu) na kwa mdomo akatamka (Kukiri kwa kinywa) hii ni principal na design ya uumbaji. Maana kwakufanya hivyo unaumba mtu mpya aliyezaliwa kwa imani (Roho ya Mungu) na Kuhuishwa na mdomo ambacho ni visible thing. Msipotoshwe na binadamu wanohubiri makanisa, dini ama vyeo vyao hao nao wanathawabu yao lakini kuwa kiumbe kipya ni sharti lakumwona Mungu bila roho wake kuwa ndani yake ile ya shetani lazima ife na kuelekea kuzimu. Unaweza kuwa kiumbe kipya na kuendelea na dini yako shida nikuwa hiyo dini kama haifundishi neno la Mungu basi shetani atakutesa sana lakini ukivumilia mateso utamwona Mungu. Ila ukipata sehemu ya kukua kiroho basi shetani hawezi kukugusa so unaanza kufurahia maisha yako ya umilele hapa hapa duniani.
 
Padri Wa Kanisa Katoliki Ashauri Watanzania Kujiuliza Maswali 4 Kabla Ya Kwenda Loliondo

Posted by Mjengwa | Monday, March 21, 2011

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Tanzania Kadinali Pengo
Kiongozi mmoja wa kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam jana alielezea msimamo wa kanisa Katoliki kuhusu tiba ya Loliondo inayotolewa na Mchungaji Ambikile Mwaisapile kuwa kabla mtu yeyote hajapata tiba hiyo lazima ajiulize maswali manne kwanza kabla ya kuamua kuitumia.
Akihutubia katika Ibada ya Jumapili katika Kigango cha Mt. Yohane wa Msalaba Parokoa ya Mbezi Luis, Paroko wa parikoa hiyo Padre Vivian alisema, "Sina chuki wala tatizo lolote na tiba ya Loliondo, lakini kama unataka kwenda lazima ujiulize maswali manne yafuatayo.
"Kwanza, tiba inayotokana na miujiza ya Mungu lazima iwe endelevu isiwepo kwa kipindi kifupi tu," alisema.
Swali la pili alilotaka watu wajiulize ni kuwa tiba inayokuja kama muujiza kutoka kwa Mungu huwa na masharti? Swali la tatu alilolitaja Paroko huyo ambaye ni Padre wa Shirika la Wakalmeli ni kuwa, Kama tiba hiyo inafanyakazi ndani ya Loliondo, kwanini isifanyekazi Dar es Salaam na kwingineko?
Na swali lake la mwisho alilotaka watu wajiulize kuhusu tiba hiyo ya magonjwa sugu ukiwemo UKIMWI ni je, Mungu aliwaumba wanadamu na kisha kuamua kuwaangamiza? Au wanadamu wanaangamia kutokana na vitendo vyao vya ujanja ujanja?
"Ukiisha jiuliza maswali hayo na kujiridhisha kwa majibu utakayopata unawea kufanya maamuzi ya kwenda Loliondo. Hivyo ukiliona basi limeegeshwa katika stendi ya Mbezi au mahali pengine na ukasikia wapigadebe wanaita Loliondo Loliondo Loliondo, basi panda ukapate kikombe cha Babu," aliongeza kusema.
Katika siku za hivi karibuni Mchungaji Mwaisapile ameutikisa Ulimwengu baada ya kutangaza kuwa anatibu magonjwa sugu kwa kutoa dozi ya kikombe kimoja cha dawa ya kienyeji kwa gharama ya shilingi 500/ kwa Watanzania na Tsh 1,000/= kwa wageni.
Viongozi mbalimbali wa siasa na dini wakiwemo maaskofu wa madhehebu ya Kikristo wamekuwa wakitoa ushuhuda wa ukweli wa tiba hiyo na kuwashauri wananchi wenye magonjwa sugu kwenda kijijini Samonge mkoani Arusha kupata tiba.Hata hivyo kwa upande mwingine, baadhi ya viongozi wa makanisa hayo akiwemo Askofu Zakaria Kakobe wa kanisa la FGBF na Mchungaji Christopher Mtikila wamekuwa wakiipinga vikali tiba hiyo.
 
Back
Top Bottom