Hoja ya Shossi juu ya sh. 500/- ya babu

Hoja ya Shossi juu ya sh. 500/- ya babu

Yaani ukiangalia wengi wanaompinga Babu ni watu wa madhehebu tofauti na Babu, hasa hasa wale wa Efatha, FBFC kwa kakobe na type zingine kama hizo ndio wanaongoza kwa kutapatapa.

Yaani ndugu yangu unafikiri kweli tuko hapa kushindana na babu ili iweje? Wewe unafikiri mambo yote tunayo changia hapa ni kwasababu ya chuki? Mwombe Mungu akupe ufahamu kuelewe jinsi shetani alivyo mwongo.

Unajua shetani hupenda sana kutupumbaza na mambo ya kidunia ili tusiutafute ufalme wake, kwasababu anajua fika kwamba kama tutajua kweli basi mtaji wake (roho zetu) umekwisha. Kwahiyo anatufanya tulumbane kwenye mambo mabalimbali mfano dhehebu lipi ni bora ili tupumbazwe. Ndiyo maana ni vizuri kusoma maandiko nakujua hila zake.

kwa taarifa yako shetani ni mwerevu sana anatumia hila ambazo ziko "so innocent" yaani huwezi kujua wakati mwingine kama uko mtegoni anapokuja shituka "it's too late". Ndiyo maana Yesu aliseme tukeshe tukiomba.

Jua ya kwamba shetani halali yeye yuko macho 24-7 kwasababu anajua he is running out of time.

Nikupe mfano mmoja tuu, wewe unafikiri ni kwanini waumini wengi hujisikia uchovu (kusinzia) wakiwa kanisani? Yaani wakati woote wanakuwa ok lakini ikifika wakati wa neno tuu, miayo inaanza. Au unafikiri ni kwanini watoto hulialia kwenye nyumba za ibada, unafikiri kwasababu ni kawaida yao kulia?

Ni kwasabau shetani hataki watu wa Mungu walisikie neno lake ili waokolewe kwahiyo anawavuruga (distract) kwakuleta kelele.

Kwahiyo ndugu achana na mambo ya madhehebu bali soma maandiko ili uelewe wokovu wa kweli ni nini. Soma nyaraka za mtume Paulo upate picha kamili ya kuishi maisha ya kikristo.

Yaani Babu amewatikisa kisawasawa na wao si tu kwamba wametikisika, bali wamepukutika mpaka manyoya, sasa wako uchi wanatafuta nguo za kujisitiri hapa JF

Kwakweli sijui ni nani huyo aliyetikisika hata mimi nampa pole, kwasabau si sahihi kumuogopa binadamu wenzako.
 
Wapendwa katika Bwana,

mambo mengi yalijitokea katika thread hii na nyingine nilzoanzisha kumhusu babu wa loliondo. nilipanga kuhitimisha leo mjadala huu kwa upande wangu ila kwa kuwa ndugu Mohamedi Shossi ameiona leo na nimeona ni yema nimpe fursa kwenye thread hii naye aweze kujadiliana na wanaJF wengine leo na kesho kabla sijahitimisha. kwa sababu hii, nimeahirisha kuihitimisha hadi kesho jioni baada ya saa za kazi.

labda niwaweke wazi kuwa hitimisho lenyewe litafafanua kila eneo ambalo yaliibuka maswali katia mada hii. maeneo niliyoyaona ni haya:

1.
Ni bora tukamwacha babu aendelee na kazi zake
2.
Tumwache kila mtu afuate imani yake
3.
Tusihukumu tusije tukahukumiwa
4.
Mambo ya imani magumu kueleweka
5.
tuiache huduma ya babu itajidhihirisha mbele ya safari kwani kama ni ya uongo atakwama tu
6.
Hata Yesu aliponya watu kwa kutumia tope, naaman mshamu aliponywa kwa kujichovya mara saba mto yordani
7.
Watu wameteseka sana na maradhi na Mungu amekuja kuwafariji na kuwarejeshea matumaini ya afya njema
8.
Sh. 500/- anazotoza babu si kitu ukilinganisha na baraka na faraja ya uponyaji wa magonjwa sugu kama ukimwi, kansa, kisukari, shinikizo la damu nk wanayopata. tena wengi wako tayari kutoa zaidi ila babu ndiye anawazuia
9.
Kwa nini hatupingi huduma za akina kakobe, mwingira, rwakatale, fernandes, lusekelo, gwajima gamnywa nk ambazo hutoza pesa nyimgi sana kwa kisingizoio cha sadaka na michango mbalimbali kama mafungu ya kumi, ujenzi, shukrani nk.
10.
Sisi tunaotilia shaka huduma hii tuna wivu na huenda ni mawakala au waendeshaji wa huduma nyingine zilizozidiwa ushindani na huduma ya babu
11.
tuaotilia shaka huduma hii tuna kiburi cha uzima na kuwa kuna kila uwezekano kuwa hatujapatwa na magonjwa sugu na kujua jinsi yanavyowatesa watu
12.
Muhimu ni kupona na sio zaidi
13.
Ubikira wa Miss Judith na kuwa miss Judith ana-attract attention ya watu bila ulazima wowote
14.
mwenendo wa Miss Judith hapa JF kikristo unatia shaka kwa mfano amewahi kuanzisha topic inayofundisha watu kutongoza na nyingine kadhaa kwenye majukwaa ya MMU na lile la "at your own risk"
15.
thread kuhamishiwa chit-chat forum kunaonyesha kuwa imepelekwa kijiweni na hivyo sio mjadala wa maana
16.
mengineyo ambayo nimesahau mnikumbushe

nawaahidi kuwa nitatoa majibu na maelezo mazuri yaliyojitosheleza juu ya haya pamoja na mengine mengi hapo kesho kama saa kumi jioni. kila mwenye dukuduku na aliyeuliza swali lake jana na hakupata jubu, basi unakaribishwa kujisomea amwenyewe jibu lako. majibu yanaweza kuwa marefu lakini usichoke kabla hujapata jibu lako.

Mungu awabariki nyote

Glory to God
 
Naomba niweke wazi kitu kimoja hiyo mia tano inayoonekana kama tunaipinga kwa wivu si kweli kwani kama matumizi yake ni kusaidia wajane na masikini biblia imesema "[FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu, [/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.[/FONT][FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]" Luka 12:32-33[/FONT]

Mimi na wewe Miss Judith tunachokipinga ni kuwapa "kikombe" bila kuwapa neno la Mungu hata biblia imesema [FONT=Bookman Old Style, Times New Roman, Times Roman, Serif]"Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana".[/FONT] Luka 12:34 ndio maana mimi na wewe tunampinga babu si kwa kuwa anapokea mia tano ila kwakuwa hawapi watu chakula cha roho hafanyi anavyotakiwa kufanya!
Naona tatizo la wachangiaji wengi wa mada hii ni kuchangia bila kufanya ufuatiliaji au hata ka utafit kadogo ka kufika kwa babu physically hata kama si kwa kunywa dawa.
Kila asubuhi saa moja babu hutoa briefing kwa wanaokuwepo. Nilishuhudia watu wakitoka kwenye magari hata yaliyokuwa umbali wa kilometa 8 kuja kusikiliza briefing ya babu. Kwa kifupi siku ya tarehe 18/3/2011 katika briefing alisema yafuatayo (mimi nilikuwepo):
Dawa hiyo ameoteshwa kutibu magonjwa matano yasiyo na dawa za kawaida nayo ni Ukimwi, kisukari, kansa, pumu, na kifafa. Lakini alisema kuna watu wametoa ushuhuda kuwa wamepona magonjwa tofauti na hayo; kuna waliokuja na kipofu akapona na wengine kiwete akatembea. Huo ni ushuhuda wa watu
Kwa wenye HIV, ndani ya muda wa siku saba vidudu vitakuwa vimefungwa na haviwezi kukushambulia, na baada ya mwezi mmoja vitakuwa havipo tena, hivyo aliwashauri wanaopima baada ya kunywa kikombe wasiwe na waswasi ikiwa watapima ndani ya siku 7 na wakaambiwa vidudu bado vimo. Alitoa tahadhari ya kutokwenda kuendekeza tena kale kamchezo kwani dawa inanywewa mara moja tu; hivyo ukipata tena ugonjwa haitakusaidia.
Dawa si ya dhehebu wala dini fulani; hivyo aliwaasa viongozi wa makanisa mbalimbali na dini mbalimbali wasiwazuie waumini wao kuja kuponywa.
Kuhusu watu wanaotafuta hiyo mizizi ya mti huo ili waondoke nayo, alisema haitawasaidia kwani ameoteshwa dawa aitoe yeye mwenyewe kwa mkono wake na inywewe pale pale. Akasema hajui kama Mungu kamteua mtu mwingine wa kutoa dawa hiyo.
Alisema yeye si mganga na hivyo yeye hatibu; kinachotibu ni neno la Mungu aliloweka kwenye huo mti, yeye ni wakala tu wa kuunganisha mgonjwa na neno hilo.
Kuhusu watu wanaochakachua foleni kuwa wakinywa wanakunywa juisi au maji alisema yeye hajasema hayo, yeye anachotoa ni dawa, ila hiyo isiwe kigezo cha kuvuruga foleni kwani nyote miacha magari yenu mkajirundika hapa, hamtaweza kuhudumiwa.
Kwa magonjwa mengine (yale manne) alisema matokeo utayaona mapema zaidi kama pumu, kisukari, kifafa na kansa. wa kansa kama iko kwa nje utaona mabadiliko ndani ya siku tatu tu!
(Alitulaumu eti tumezuia vyombo vya kuchemshia dawa kwani kuna gari limevibeba lakini tunainyima njia ya kupita)
Kama kawaida, aliruhusu maswali:
Wa kwanza aliuliza juu ya mwanae kuwa na kisukari kwa miaka 6; umati ulihamaki na kumjibu kuwa huyo atapona usiwe na hofu. Niliona babu akiongea naye kwa sauti ya chini sikusikia alichomweleza.
wa pili alisema niko katika ndoa kwa muda mrefu lakini sijapata mtoto; je dawa itanisaidia? Babu alianza kwa kumpa pole; kisha akamwambia - watoto hutoka kwa Mungu na dawa imetoka kwa Mungu, hivyo kunywa dawa huku ukiomba bila shaka Mungu atakusaidia.
Swali lililofuata lilihusu wagonjwa mahututi, au wasio na uwezo wa kufika hapo alipo babu kwamba anaonaje akiwapa hiyo dawa wakawapelekea ali mradi yeye ameshaibariki? Aliwajibu kuwa yeye ameelelezwa kuwa dawa itanywewa pale na hajaelekezwa vinginevyo, hivyo wafanye bidii wawalete. "Kama nitaelekezwa vinginevyo basi nitafanya kulingana na maelekezo"
Mimi nilimuuliza swali: Kwa mfano nimekuja hapo nina ukimwi, nimekunywa dawa na kupona, nimerudi nyumbani lakini kwa bahati mbaya nikapata kisukari, je naweza kuja kunywa dawa mara ya pili kwa ugonjwa huu mpya? Alisema "sina jibu" Kwa kadri nilivyooteshwa mtu atakunywa dawa hii mara moja tu; kwamba sasa uje mara ya pili kwa ugonjwa tofauti - sina jibu. Lakini Mungu si wa hivyo - yaani leo uje na ugonjwa sugu unywe dawa upone halafu upate tena ugonjwa mwingine sugu? Hakika Mungu si wa hivyo - ila ikitokea hivyo - sina jibu!
Mama mmoja aliuliza kuwa mwanae haeleweki - mara ni wa kike mara ni wa kiume. Kwa kweli wengi au labda niseme mimi sikumwelewa alimaanisha nini, ila babu alimweleza hivi - hakika Mungu hushinda nguvu zote za giza.
Baada ya hapo yalianza maswali ya kurudia ikionekana kuwa wanouliza walichelewa - Babu alifunga kipindi hicho kwa sala fupi akituombea wote tuliosafiri kuja pale ili tuweza kuponywa hayo mateso tuliyokuja nayo na hatimaye turudi nyumbani salama tukimtukuza Mungu kwani ndiye muweza wa yote.
umati uliomba tutawanyike ili tuweze kupewa dawa. Tulirudu kwenye mgari yetu na kuendelea kupokea kikombe na kuondoka.
Kati ya watu 10 tuliokuwa kwenye gari, aliyepata nafuu ya haraka ni wa pumu. Wakati tuanaenda alikuwa amevaa jaketi na khanga ili asidhurike sana lakini baada ya kunywa dawa aliweza kuachia jaketi kuvaa nguo za kuacha mabega nje licha ya mawingu, mvua na baridi iliyokuwepo! Wengine matatizo yetu yatachukua muda zaidi ili kuthibitisha uponaji wetu.
Huyo ndiye babu - nisingeweza kuandika neno kwa neno kwa yote aliyosema; hayo ni kwa ufupi tu. Safari yetu tulifika kijijini Samunge jumatano saa 12.05 jioni, tukapata kikombe ijumaa saa 2 asubuhi. Mvua iliyonyesha kwa wingi siku ya alhamisi ililowesha kuni na hivyo dawa kuchemshwa kidogo mchana na kuisha saa moja jioni ambapo babu alisitisha huduma yake hadi kesho yake. Kama angetoa dawa kama kawaida hadi saa tatu usiku, tungekunywa siku hiyo.
 
.............. hayo ni kwa ufupi tu. Safari yetu tulifika kijijini Samunge jumatano saa 12.05 jioni, tukapata kikombe ijumaa saa 2 asubuhi. Mvua iliyonyesha kwa wingi siku ya alhamisi ililowesha kuni na hivyo dawa kuchemshwa kidogo mchana na kuisha saa moja jioni ambapo babu alisitisha huduma yake hadi kesho yake. Kama angetoa dawa kama kawaida hadi saa tatu usiku, tungekunywa siku hiyo.

pole sana mpendwa kwa misukosuko ya samunge.

Bwana anasema njooni kwangu wote wenye kulemewa na mizigo ya dhambi nami nitawapumzisha. jifunzeni kwangu kwa maana mimi ni mpole na myenyekevu wa moyo, nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi. ulihangaika hivyo kwa kuwa ulienda kwa Babu samunge, hakika kwa Bwana Yesu aliye mahali pote, usingeteseka kiasi hicho. ukiijiua kweli, hiyo itakuweka huru

nakuombea afya njema na ubarikiwe sana na Bwana

Glory to God
 
Yaani ndugu yangu unafikiri kweli tuko hapa kushindana na babu ili iweje? Wewe unafikiri mambo yote tunayo changia hapa ni kwasababu ya chuki? Mwombe Mungu akupe ufahamu kuelewe jinsi shetani alivyo mwongo.

Unajua shetani hupenda sana kutupumbaza na mambo ya kidunia ili tusiutafute ufalme wake, kwasababu anajua fika kwamba kama tutajua kweli basi mtaji wake (roho zetu) umekwisha. Kwahiyo anatufanya tulumbane kwenye mambo mabalimbali mfano dhehebu lipi ni bora ili tupumbazwe. Ndiyo maana ni vizuri kusoma maandiko nakujua hila zake.

kwa taarifa yako shetani ni mwerevu sana anatumia hila ambazo ziko "so innocent" yaani huwezi kujua wakati mwingine kama uko mtegoni anapokuja shituka "it's too late". Ndiyo maana Yesu aliseme tukeshe tukiomba.

Jua ya kwamba shetani halali yeye yuko macho 24-7 kwasababu anajua he is running out of time.

Nikupe mfano mmoja tuu, wewe unafikiri ni kwanini waumini wengi hujisikia uchovu (kusinzia) wakiwa kanisani? Yaani wakati woote wanakuwa ok lakini ikifika wakati wa neno tuu, miayo inaanza. Au unafikiri ni kwanini watoto hulialia kwenye nyumba za ibada, unafikiri kwasababu ni kawaida yao kulia?

Ni kwasabau shetani hataki watu wa Mungu walisikie neno lake ili waokolewe kwahiyo anawavuruga (distract) kwakuleta kelele.

Kwahiyo ndugu achana na mambo ya madhehebu bali soma maandiko ili uelewe wokovu wa kweli ni nini. Soma nyaraka za mtume Paulo upate picha kamili ya kuishi maisha ya kikristo.



Kwakweli sijui ni nani huyo aliyetikisika hata mimi nampa pole, kwasabau si sahihi kumuogopa binadamu wenzako.


Kama hamko kushindana na Babu basi mwacheni afanye kazi yake, acheni kumtungia thread hapa JF za kumsema sema. Wewe usie amini achana nae, wapo wengine wanamuamini na tiba zake. Zungumzeni kudumisha imani zenu, acheni kuingilia imani za wengine na kuzihukumu sio sahihi. Babu ataendelea na imani yake aliyokuwa nayo mpaka siku ya mwisho ya uhai wake, hata tikisika na watu kumtungia majungu hapa JF.
 
Wapendwa katika Bwana,

mambo mengi yalijitokea katika thread hii na nyingine nilzoanzisha kumhusu babu wa loliondo. nilipanga kuhitimisha leo mjadala huu kwa upande wangu ila kwa kuwa ndugu Mohamedi Shossi ameiona leo na nimeona ni yema nimpe fursa kwenye thread hii naye aweze kujadiliana na wanaJF wengine leo na kesho kabla sijahitimisha. kwa sababu hii, nimeahirisha kuihitimisha hadi kesho jioni baada ya saa za kazi.

labda niwaweke wazi kuwa hitimisho lenyewe litafafanua kila eneo ambalo yaliibuka maswali katia mada hii. maeneo niliyoyaona ni haya:

1.
Ni bora tukamwacha babu aendelee na kazi zake
2.
Tumwache kila mtu afuate imani yake
3.
Tusihukumu tusije tukahukumiwa
4.
Mambo ya imani magumu kueleweka
5.
tuiache huduma ya babu itajidhihirisha mbele ya safari kwani kama ni ya uongo atakwama tu
6.
Hata Yesu aliponya watu kwa kutumia tope, naaman mshamu aliponywa kwa kujichovya mara saba mto yordani
7.
Watu wameteseka sana na maradhi na Mungu amekuja kuwafariji na kuwarejeshea matumaini ya afya njema
8.
Sh. 500/- anazotoza babu si kitu ukilinganisha na baraka na faraja ya uponyaji wa magonjwa sugu kama ukimwi, kansa, kisukari, shinikizo la damu nk wanayopata. tena wengi wako tayari kutoa zaidi ila babu ndiye anawazuia
9.
Kwa nini hatupingi huduma za akina kakobe, mwingira, rwakatale, fernandes, lusekelo, gwajima gamnywa nk ambazo hutoza pesa nyimgi sana kwa kisingizoio cha sadaka na michango mbalimbali kama mafungu ya kumi, ujenzi, shukrani nk.
10.
Sisi tunaotilia shaka huduma hii tuna wivu na huenda ni mawakala au waendeshaji wa huduma nyingine zilizozidiwa ushindani na huduma ya babu
11.
tuaotilia shaka huduma hii tuna kiburi cha uzima na kuwa kuna kila uwezekano kuwa hatujapatwa na magonjwa sugu na kujua jinsi yanavyowatesa watu
12.
Muhimu ni kupona na sio zaidi
13.
Ubikira wa Miss Judith na kuwa miss Judith ana-attract attention ya watu bila ulazima wowote
14.
mwenendo wa Miss Judith hapa JF kikristo unatia shaka kwa mfano amewahi kuanzisha topic inayofundisha watu kutongoza na nyingine kadhaa kwenye majukwaa ya MMU na lile la "at your own risk"
15.
thread kuhamishiwa chit-chat forum kunaonyesha kuwa imepelekwa kijiweni na hivyo sio mjadala wa maana
16.
mengineyo ambayo nimesahau mnikumbushe

nawaahidi kuwa nitatoa majibu na maelezo mazuri yaliyojitosheleza juu ya haya pamoja na mengine mengi hapo kesho kama saa kumi jioni. kila mwenye dukuduku na aliyeuliza swali lake jana na hakupata jubu, basi unakaribishwa kujisomea amwenyewe jibu lako. majibu yanaweza kuwa marefu lakini usichoke kabla hujapata jibu lako.

Mungu awabariki nyote

Glory to God

Hivi ukiacha kutunga thread zenye kuzungumzia Tiba za Babu na imani yake utapungukiwa nini??
Kwa nini kila dakika udai NITALETA MENGINE KUHUSU BABU KESHO, huna mengine ya kutuletea hapa???
Achana na Babu bwana, komaa na imani yako, za wengine waachie wenyewe, HUZIWEZI

:smash::smash::smash::smash::smash::smash:

Watu wengine bana
 
Miss Judith,thank you very much for this useful thread. But for as long as nimeshafika kwa babu na kupata kikombe kinachonipa ahueni kubwa ya maradhi 'niliyokuwa' nayo, sitahoji lolote kuhusu hiyo mia tano. Infact natamani ningeweza kulipa zaidi

Loo! Kumbe umepata ahueni tu? Mbona babu anasema dawa hiyo inaponya kabisa? Hapo ndipo ushetani wa babu unapodhihirika.
 
Nitashangaa kama Wapentekoste watakuwa wametikiswa na huduma ya babu. Lengo kuu la Upentekoste ni kuokoa na kuponya roho za watu zimrejee Bwana na kuufikia uzima wa milele. Upentekoste unaongozwa na roho aliye hai - ni zaidi ya mwili ulio hai. Uponyaji wa mwili ni jambo/lengo la muda mfupi kwa ajili ya kudhihirisha utukufu wa Mungu tu na si mwisho wa yote. Ndio maana miujiza si huduma kuu katika Ukristo (ingawa wako wanaoona hivyo). Sasa kama kweli huduma ya kiroho itazidiwa na huduma ya uponyaji wa mwili basi suala la kujiuliza ni kama kweli kazi ya Bwana inafanywa katika kweli yake badala ya kulinganishwa na biashara za kidunia zinazopimwa na ukubwa wa soko (idadi ya wafuasi) bila kujali "thamani halisi" ya soko hilo. Hapo Babu anaweza kuwa amepatia kuwaambia baadhi ya viongozi wa dini kwamba wako kibiashara zaidi.

Acheni kuzigeuza mada imani zisizo wahusu
Tulieni na tangazeni imani zenu
Kama Babu unamuona anatibu kwa nguvu za shetani au anafanya biashara basi achana nae
Fanya yako yanayokupendeza wewe na Muumba wako
Na yeye atafanya yake na Muumba wake na wote waliopamoja nae
Komaeni na imani zenu
 
Hivi ukiacha kutunga thread zenye kuzungumzia Tiba za Babu na imani yake utapungukiwa nini??
Kwa nini kila dakika udai NITALETA MENGINE KUHUSU BABU KESHO, huna mengine ya kutuletea hapa???
Achana na Babu bwana, komaa na imani yako, za wengine waachie wenyewe, HUZIWEZI
Watu wengine bana

Endelea Miss Judith. Mpinge shetani anayetenda kazi ndani ya babu kwa kadri uwezavyo.
 
Acheni kuzigeuza mada imani zisizo wahusu
Tulieni na tangazeni imani zenu
Kama Babu unamuona anatibu kwa nguvu za shetani au anafanya biashara basi achana nae
Fanya yako yanayokupendeza wewe na Muumba wako
Na yeye atafanya yake na Muumba wake na wote waliopamoja nae
Komaeni na imani zenu
Imani hizo zinatuhusu kwa namna moja au nyingine. Lazima tuseme. Wanaokwenda huko wengine ni marafiki zetu, wajomba zetu, wafanyakazi wenzetu, hatuwezi kukaa kimya huku tunaona wanapotea bure. LAZIMA TUSEME NA TUTAENDELEA KUSEMAAAAA!!
 
Kama hamko kushindana na Babu basi mwacheni afanye kazi yake, acheni kumtungia thread hapa JF za kumsema sema. Wewe usie amini achana nae, wapo wengine wanamuamini na tiba zake. Zungumzeni kudumisha imani zenu, acheni kuingilia imani za wengine na kuzihukumu sio sahihi. Babu ataendelea na imani yake aliyokuwa nayo mpaka siku ya mwisho ya uhai wake, hata tikisika na watu kumtungia majungu hapa JF.
Hatuwezi kukaa kimya huku tunaendelea kumwona babu akifanya kazi za shetani. Lazima tuwatahadharishe watu. Na watu wana akili, wanajua kupima ukweli na ubaya. Angalia idadi ya waliounga mkono thread hii, ndio utajua kumbe kazi anayofanya Miss Judith ni muhimu. Keep it up Miss Judith.
 
Hatuwezi kukaa kimya huku tunaendelea kumwona babu akifanya kazi za shetani. Lazima tuwatahadharishe watu. Na watu wana akili, wanajua kupima ukweli na ubaya. Angalia idadi ya waliounga mkono thread hii, ndio utajua kumbe kazi anayofanya Miss Judith ni muhimu. Keep it up Miss Judith.

Sheikh Yahya, Dr ndodi, Mama Lwakatre, Kakobe, Mwingingira & co, na mtahama hapa mjini mwaka huu, babu lazima awauwe na njaa nyinyi wezi wakubwa. na bado tunampelekea msaada wa hali na mali aendelee kutoa huduma za kweli. nyambafu kabisa.
 
Mkuu tatizo ni kuwa watu wanakunywa kwa imani ipi? kama kuna imani mbona hakuna kuitangaza kabla au baada ya kunywa dawa? kinachoangaliwa una mia tano unapewa kikombe inavyoonyesha imani si mali kitu kwa babu ila "mia tano" ndio mpango mzima. Ngoja nikupe neno la Mungu jioni ya leo.....

Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake.Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwa mwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia. Kisha mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya.Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu.Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi Yohane 10:11-14

Tumeona kuwa mchungaji mwema yupo tayari kufa kwa ajili ya kondoo wake, na yule mchungaji anaejali "jero jero" anaweza kuwakimbia kondoo wanapovamiwa na mbwa mwitu!

Wewe na Miss Judy mnataka kujipachika uungu ungu fulani na mnataka kila mtu mwanadamu aishi nje ya mwili. Nyinyi wenyewe hoja zenu ni za macho ya kibinadamu. Sasa naamini hamna hata chembe ya macho ya kiroho ya kusoma maandiko matakatifu.

Tukiacha hayo mbona nyinyi hamuendi kumkabili huyo mchungaji mkajua kinachojili maana yeye atawapa jibu la kuwatosheleza na mnaweza kuwa na hoja nzito zaidi ya hizi za kumbeza.

Nasikikita kuwadharau. Malaika na mashetani wote ni viumbe wa Mungu. Kwa hiyo mnaweza kujichunguza mko kundi gani. "Tumeona kuwa mchungaji mwema yupo tayari kufa kwa ajili ya kondoo wake" Dhihaka ya mwenye kukosa maarifa.
 
Hatuwezi kukaa kimya huku tunaendelea kumwona babu akifanya kazi za shetani. Lazima tuwatahadharishe watu. Na watu wana akili, wanajua kupima ukweli na ubaya. Angalia idadi ya waliounga mkono thread hii, ndio utajua kumbe kazi anayofanya Miss Judith ni muhimu. Keep it up Miss Judith.

Narudia jichunguzeni kama nyinyi na mitume wenu siyo mapepo
 
Imani hizo zinatuhusu kwa namna moja au nyingine. Lazima tuseme. Wanaokwenda huko wengine ni marafiki zetu, wajomba zetu, wafanyakazi wenzetu, hatuwezi kukaa kimya huku tunaona wanapotea bure. LAZIMA TUSEME NA TUTAENDELEA KUSEMAAAAA!!

Endelea Miss Judith. Mpinge shetani anayetenda kazi ndani ya babu kwa kadri uwezavyo.

Hatuwezi kukaa kimya huku tunaendelea kumwona babu akifanya kazi za shetani. Lazima tuwatahadharishe watu. Na watu wana akili, wanajua kupima ukweli na ubaya. Angalia idadi ya waliounga mkono thread hii, ndio utajua kumbe kazi anayofanya Miss Judith ni muhimu. Keep it up Miss Judith.

imgres
hyena-laughing.jpg
 
Kama hamko kushindana na Babu basi mwacheni afanye kazi yake, acheni kumtungia thread hapa JF za kumsema sema. Wewe usie amini achana nae, wapo wengine wanamuamini na tiba zake. Zungumzeni kudumisha imani zenu, acheni kuingilia imani za wengine na kuzihukumu sio sahihi. Babu ataendelea na imani yake aliyokuwa nayo mpaka siku ya mwisho ya uhai wake, hata tikisika na watu kumtungia majungu hapa JF.

Hatuwezi kunyamaza na lazima tuseme ukweli kwasababu kama kuna uwalakini kwanini tukae kimya? Hii mada si kwaajili ya babu bali ni kwaajili ya wana JF ili waweze kutambua kwamba si vyote vin'gaavyo ni dhahabu.
 
Jajajajajaaa..bite it girl! you're BORING!!! babu babu babu..kama unamuota kamsaidie.. get the hell out of here with your fake virginity!

Virginity is precious thing and strong weapon to a christian lady. If that could not make a difference Mary mother of Jesus could not qualify to carry the mission of God to this world. Through virginity one is able to get a precious husband according to the perfect will of God. I treasure my wife since I met her virgin; I am proud of her and it makes me feel a real man to be the first to enter her. Kuna wanaume ambao hawajabahatika kupata virgin woman hata mmoja pamoja na kupractice sexual relation hata kabla ya ndoa zao kwani shetani aliwajeruhi mapema partners wao. To them who have lost it please you can still get the husband/wife according to the perfect will of God if you will sincerely confess and abstain from sexual relations; may God have mercy on you. Wanaume wengi wamepoteza destiny zao kwakuamua ku go with women before their marriage hao ndio ambao wana mpigia kelele Miss Judith. Dont you know that whoever connects himself with a hallot is connecting His spirit to the devil? Can a devil give you a good destiny? Its not late either there is blood of Jesus and the Holly spirit who can recreate you and be a new creature born of spirit na hivyo vyote kuwa renewd basi come to the throne of grace where you will find a rest.
 
Conclusion :

  • Babu aendelee na tiba.
  • Watu wanaopata kikombe cha babu wamshukuru Mungu na waendelee na imani yao
  • Tanzania kuna waganga wengi sana wa kienyeji na ambao wanamtumia shetani. Kama dawa ya babu imeletwa na shetani basi tunatarajia atajitokeza mganga mwingine ambaye atatumia mti huo huo kutibia, kwa kuwa tunajua waganga wanazidiana. Ila kama tiba imetoka kwa Mungu itaendelea kuwepo hata kama kuna watu hawaipendi
 
....1) Sina hakika na imani ya huyu ndugu yetu Mohamedi Shossi, sijui kama ni mwislamu, mkristo ama muumini wa dini nyinginezo.

2) Mungu wetu afikie mahali apange bei!! tena ya huduma itokanayo na karama aliyotoa mwenyewe? kweli hapo pagumu kuingia akilini. tena mungu wake huyo akampa na mchanganuo wa namna atakavyozigawa hizo pesa, eti 300/- kwakanisa, yatima na wajane na 200/- za wahudumu wanaomsaidia kazi! kwa kweli naona kama hizi ni kashfa kwa Mungu wetu.

3) yeye atangaze kuwa ni mganga aliyekuja na dawa ya mti wa mrigariga, afuate taratibu za serikali za kujisajili kisheria ili serikali itambue kazi zake na aweke bei yake kama wawekavyo waganga wengine na tutamchukulia kama tunavyowachukulia waganga wengine.

4) ukishaweka bei (hata kama ni sh.10/-) maana yake ni kwamba asiye nayo hapati huduma! kumbuka madukani kuna pipi za sh.10/- na usipokuwa na hiyo sh.10/- hupati hiyo pipi. ndiyo maana ya bei. sasa babu anasema kama huna sh. 500/- kaa pembeni mwenye hela aje apate kikombe!

Miss Judith majumuisho yanatakiwa yajikite kwenye hoja ya msingi hayo yatokanayo mengine ni ya kibinafsi zaidi. Wengine tunakupa heshima ya dada, sasa ukituingiza kujadili mambo yahusuyo sexual status yako hutotutendea haki, drop that please.
Ila kwa wadogo zetu ambao hawajaoa na wanamcha Mungu nadhani wanafursa ya kukuPM (natania!!).

Hayo ya kina Mwingira pia hatuyahitaji kwenye majumuisho maana yalikuwa yananogesha hoja tu wala hayakuwa hoja ya msingi. Tukiyahitaji basi ije topic mpya kuhusu wao.

Hoja ilijikite kumhusu huduma ya babu (by age) na utozaji wa sh 500 kwa mtazamo wa biblia.

Nimejaribu kuivunja hoja yako kwenye mafungu manne:

1. Huna uhakika na imani ya Mohamed Shossi. Mimi ninamjua na nimemwuliza swali "Ni lini amekuwa mhubiri wa injili ya Yesu". Unless amefanya mabadiliko hivi karibuni lakini ni dharau kuisemea dini ya mtu mwingine. Anatoa nukuu za biblia kunogesha mjadala na watu mnamsupport. Nikasema amekuwa Punda aliyezungumza baada ya Balaam kutomwona malaika wa Mungu?? Kwa hili sikuungi mkono wewe na Shossi maana mnadhihaki maandiko matakatifu.

2. Mungu kupanga bei: Unapojumuisha kama itaonekana Mungu hawezi kupanga kiwango basi ni vema utuwekee na reference ya kimaandiko ili itusaidie siku za usoni. Pia uonyeshe kwamba Mungu hawezi kutoa mchanganuo. Nikipata ushahidi mpya wa kimaandiko (sio desturi) kwamba Mungu hawezi haya basi huyu Mungu hatakuwa hai.

3. Babu atangaze kuwa ni mganga wa kienyeji: Amesha tangaza kwamba yeye si mganga wa kienyeji kwa hiyo hakuna kati yetu anaweza kubadilisha hilo. Kuna ushuhuda wa mwanaJF kwamba babu hutoa briefing asubuhi ambayo inaelekeza kwamba Mungu ndiye aponyaye, babu ni point of contact tu. Tuiachie serikali kuamua la kufanya ingawa mpaka sasa serikali yenyewe inam-support kwa kuweka miundi mbinu ya kuwasaidia wenye kufika Loliondo.

4. Hatujapata kusikia kesi ya mtu alokwenda kwa babu akakosa huduma kwa vile hana sh 500. Ingawa sh 500 ni kubwa kwa baadhi ya watanzania wenzetu (tunaishi kwa chini ya dola moja) bado watanzania ni wepesi kusaidiana iwapo kuna mmoja hatokuwa nayo. Ni mjinga tu (hata akiwa mtoto) atakwenda dukani kuomba pipi huku akijua hana hela. Mwerevu atafanya moja kati ya mawili: 1) aombe hiyo sh. 10 kwa mwenye kuwa nayo kabla hajaenda dukani au 2) aende dukani amkope mwenye duka.
Hitimisho likubali kwamba hakuna ushahidi wa aliyekosa huduma hivyo assumption hii haikuwa sahihi.

Kwenye thread yako ya "Kutana na Babu wa Eritrea" ilikuwa na lengo potofu kwa kutaka sasa kuonyesha kwamba kila anayetangaza uponyaji kama babu wa Loliondo basi tutamwita babu. Wa Eritrea hatukuambiwa kwa nini umemwita "Babu".

Ushauri: Siku nyingine usitumie up rightness yako kujaribu kuuthibitishia ulimwengu maana "Not by mighty or power BUT by His Spirit, says the Lord". Kumbuka haki yetu yote its like filth cloth in the eyes of the Lord.
 
  • Thanks
Reactions: CPU
Back
Top Bottom