Chamoto
Platinum Member
- Dec 7, 2007
- 9,883
- 22,305
Chamoto kama umesoma post zangu kabla nilisema "Binafsi sina uhakika na dawa anayotoa babu lakini sitotenda haki kuisema negatively kwa vile isije ikawa kwa kufanya hivyo ukawa unashindana na Mungu mwenyewe".
Ninapinga watu ku-conclude kwamba anachofanya yule babu si cha Mungu bila kuonyesha kimaandiko kwamba si cha Mungu. Binadamu tunadhani tunaweza kumchagulia Mungu nani amtumikie na amtumikie vipi. Ni vipi kama kweli mtu akinywa dawa na akapona undhani sifa atampa Mungu yupi hata kama hakuhubiriwa injili siku hiyo??? Kama Rahabu kahaba alikuwa ni mtumishi wa Mungu, Mchungaji mstaafu je??
Tuseme tu kwamba TUSIHUKUMU maana nani ajuaye kama afanyacho babu ni Kazi ya Mungu, ni nani yuko tayari kushindana na Muumba wake?? Eti chungu kimwambie mfinyanzi hujui kazi yako wewee... thubutuuuuu!!!!!!!!!!!!!!!!
Tupo pamoja ndugu ila tunatakiwa tuhoji kwa maandiko (mfano kwanini hawaambi walioponywa wamtukuze Mungu) na kuomba na Mungu ni mwema atatuwezeka kutambua kweli.