Hoja ya Shossi juu ya sh. 500/- ya babu

Hoja ya Shossi juu ya sh. 500/- ya babu

kuna post nyingi sana nimetoa majibu mengi sana tofauti. tatizo kuna mtu hukurupuka kuweka post bila kusoma zilizotangulia. kwa hiyo kama hoja fulani imejirudia na mimi nilishaijibu silazimiki kujijibu upya.

pia kuna wale wanaoniuliza wakinitaka nisemee mfano madhehebu yangu ya KKKT ama huduma zinazojitegemea kama za akina rwakatale, mwingira, kakobe, mwakasege, lusekelo nk, mimi si msemaji wa KKKT wala huduma nyingine yoyote ila nikiona kitu hakiendi kama maandiko yanavyosema mimi hufafanua namna maandiko yanavyotaka na si kusemea kanisa. hata huyu babu naye ni m-KKKT kama mimi, ninamkosoa kwa kuwa shughuli zake zina maswali mengi sana kwa mujibu wa maandiko.

kuna wengine wananishambulia mimi binafsi. naweza kuafafanua pale ninapoona kuna haja ya kufanya hivyo, vinginevyo naziacha tu hoja zao waendelee wenyewe.

halafu mmeona wengine wameanza kuchat na marafiki zao hapa kwenye thread kama wafanyavyo kwenye thread za jukwaa la MMU, sijui watu watabadilika lini!?

we jadili hoja nami nipo kufafanua hoja.

you are welcome.

kwa neema ya Mungu nitazikabili hoja zenu zote

Glory to God


Heshima kwako Judith,

Kwanza kabisa nataka nikukumbushe kwamba Mungu hana kigeugeu, wala njia zake hazichunguziki, akili yake na uwezo wake ukilinganisha na sisi binadamu ni sawa na umbali kati ya mbingu na ardhi.
Umesema kwamba wewe ni mlutheri lakini pia umekiri kwamba si msemaji wa KKKT, na inafahamika kwamba babu ni mchungaji mstaafu wa KKKT na huduma yake imeidhinishwa na kubarikiwa na uongozi wa kanisa la KKKT, Askofu Thomas Laizer ndiye mkuu wa KKKT dayosisi ya kaskazini alipo babu wa loliondo na ametolea tamko huduma ya babu. Sasa kama mkuu wa kanisa unalolitumikia ameshatoa kauli ya kuunga mkono huduma ya babu na wewe unakuja hapa kuipinga, basi unakwenda kinyume na msimamo wa kanisa lako ambalo msemaji wake amethibitisha kanisa lako KKKT kuunga mkono huduma hiyo. Kwa lugha nyepesi kabisa wewe ni muasi ama unataka kuanzisha uasi ndani ya kanisa la KKKT.
Kama unajiamini na unaamini kwamba unachokisema na kukisimamia ni cha ukweli, hukupaswa kuja hapa kumshambulia babu wa loliondo, ulitakiwa kwenda kuonana na uongozi wa kanisa lako na kuwaeleza dukuduku lako, kinyume na hapo naogopa kukuita msaliti.

Kitu kingine ninachokiona kwako, kama tukikubaliana na mtazamo wako kwamba huduma ya babu ni ya kishetani, si mpango ama huduma ya kiMungu,basi tutalazimika kukutazama vizuri katika angle hiyo hiyo ya unyoofu wa moyo wako na matendo yako. Tukijaribu kukumbuka kwamba Kimtokacho mtu mdomoni ndicho kiujazacho moyo wake,basi nataka turudi nyuma kidogo tu kwenye lile darasa lako la mbinu za kutongoza. Kwa jinsi ulivyoendesha lile darasa la kutongoza bila shaka wewe ni mzoefu wa kuwavua wanaume, huwezi kuwa mtaalamu wa kutongoza halafu uje kutamba kwamba wewe ni bikira, labda unataka kutufanya tufikirie hatua moja mbele kwamba unatumia mtandao wa nusu shilingi.
Lakini pia nikibaki hapo hapo kwenye mbiu za kutongoza na uaminifu wako mbele za Mungu, ninapenda nikukumbushe kwamba aliyesema usizini ndiye huyo huyo aliyesema usishuhudie uongo na ndiy huyo huyo Mungu aliyesema usiue. Maandiko matakatifu yanatukumbusha na kutufundisha kuwa ukimuangalia mwanamke/mwanamme na kumtamani moyoni mwako tayari umeshazini naye, kwahiyo unakuwa hatiani kwa kuzini. Kwahiyo kama unthubutu kutongoza wanaume kwa mujibu wa maelezo yako mwenyewe basi tayari umemtamani huyo mwanaume na kwahiyo hata kama haufiki kwenye hatua ya kuukalia mtalimbo basi tayari umeshazini na huyo mwanaume na kwahiyo unakuwa umetenda dhambi kwa kwenda kinyume na amri ya Mungu.
Kutokana na ukweli huu, sitaki kuamini kabisa kwamba unaweza kuja kujikweza hapa kwamba ni mkamilifu kwakuwa bado bikra bila kukumbuka unashiriki uzinzi myoni mwako.

Mwisho kabisa nikukumbushe kwamba Kakobe, Mwingira, Mama rwakatare na wengine tunaowafahamu wanafanya show za vipindi vya kuhubiri injili kwenye runinga kila siku na watu wanamiminika kwao kupata uponyaji, na hawa wananchi wanaokwenda kutafuta uponyaji huko nio wanaotoa sadaka na michango mbali mbali kwa majina ya sadaka ya shukrani n.k, tunashuhudia watu wakitoa shuhuda kwamba wamesafiri kutoka kona zote za nchi hii hata nje ya nchi kuja dsm kutafuta uponyaji kwa kakobe, mwigira, mama rwakatare, mzee wa upako na wengine lakini hilo halikushughulishi isipokuwa unashughulika na huduma ya babu ambayo hajawahi kuwa na kipindi cha runinga ama radio kujitangaza bali walioponywa ndio waliosambaza habari za uponywaji wao na hatimaye media zikaamua kumpa babu promo bila yeye kulipia.Kwanini hujahoji watumishi wa show za runinga kwenda kutoa uponyaji mioani badala yake wamejikita dsm tu?? kwani hao wananchi wanapokuja dar wanakuja bila kulipia nauli? au makanisa hayo ndiyo yanayowasafirisha kuja dsm?? hebu kuwa mkweli katika hili, chuki, wivu na husda ndo zinakusumbua.

Nakuomba ukatubu kwanza dhambi yako ya uzinzi na nuendelee kumtumikia Mungu pasipo kujikweza ili usije ukashushwa chini na kuaibika.
Nilikuwa napita tu kuelekea mugumu nikaona ni vizuri kukuachia ujumbe huu muhimu kwa ustawi wa imani yako.
 
Tunapima kila roho kwa maandiko na sio hisia au maelekzo ya viongozi wa dini.
Babu kapotoka wapi???? Tupeni maandiko jamani!!!!!!!!

Babu hahubiri neno, mtumishi anatakiwa kuhubiri neno ili liwaweke wasikilizao huru (Joh 8:3)
 
Watu wanachekesha saana dunia hii jamani.

Kunamtu aliumwa na JINO akiwa kwenye ndege, akawa anapiga kichwa dirisha safari nzima huku akilia na kuwaambia Wafanyakazi kwenye ndege na wakati huo wakiwa juu kuwa "NITEREMSHENI...." Watu walivunjika mbavu. Mungu bariki walimuelewa na hawakumpa kifungo cha kutokupanda ndege zao.

Mie nilikuwa naogopa sana WEMBE. Ila kuna siku niliuguwa JIPU na USIKU wa maneno likaiva, weeee!!!!! Nilikimbilia kwa mshikaji na wakati analichana, na tena kwenye Makalio (mwanaume hata aibu sina) sikusikia kabisa maumivu ya Wembe ila ya JIPU.

Huyu dada unaweza kukuta kweli ni Mfuasi wakundi fulani ambalo wana wasiwasi wa kupoteza wateja. Ila cha ajabu ni kuwa unaweza kukuta hata mwenyewe hapo na huyo mwandishi wake, walishaenda Loliondo Kimya kimya na KULAMBISHWA kikombe cha Babu. Kashapona na sasa anaangalia ULAJI uko wapi.....

Tanzania bana, kweli ni nchi ya BONGO.
 
Lakini leo hii KIKOMBE CHA BABU watu hawataki kuamini na na hawana vithibitisho au hawajafunuliwa kama babu ni wa mungu au la lna wanajaribu tu kutangaza babu siye.
Nipo kujaribu kujua ipi ni busara kama watu hawana uhakika wa haya ni haki kwao au ni dhambi kumtangaza babu vibaya au kukaa kimya?
Ikumbukwe Mungu katujalia hekima ya kupambanua mambo na kutafuta namna ya kuyapresent na kujua namana ya kucounter act na reaction za watu.
Sijawahi kusema kwamba Babu ana dhambi kwa kufanya anayoyafanya ila tunatakiwa kuwa waangalifu na kuhoji maandiko yanasemaje? Tatizo langu ni kwamba neno (injili) halihubiriwi
 
Tunapima kila roho kwa maandiko na sio hisia au maelekzo ya viongozi wa dini.
Babu kapotoka wapi???? Tupeni maandiko jamani!!!!!!!!

Ninachosema ni kuwa waangalifu kwani kama Babu anamwamini Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo basi kwanini asiwape neno kuwaelezea kwanini Yesu alikuja na kwanini hao watu wanatakiwa kumfuata yeye. Kama babu atasema yeye ni mganga mimi wala sita kuwa na shida. lakini kama ni mchungaji ni wajibu wake kuchunga kondoo wa bwana
 
Heshima kwako Judith,

Kwanza kabisa nataka nikukumbushe kwamba Mungu hana kigeugeu, wala njia zake hazichunguziki, akili yake na uwezo wake ukilinganisha na sisi binadamu ni sawa na umbali kati ya mbingu na ardhi.
Umesema kwamba wewe ni mlutheri lakini pia umekiri kwamba si msemaji wa KKKT, na inafahamika kwamba babu ni mchungaji mstaafu wa KKKT na huduma yake imeidhinishwa na kubarikiwa na uongozi wa kanisa la KKKT, Askofu Thomas Laizer ndiye mkuu wa KKKT dayosisi ya kaskazini alipo babu wa loliondo na ametolea tamko huduma ya babu. Sasa kama mkuu wa kanisa unalolitumikia ameshatoa kauli ya kuunga mkono huduma ya babu na wewe unakuja hapa kuipinga, basi unakwenda kinyume na msimamo wa kanisa lako ambalo msemaji wake amethibitisha kanisa lako KKKT kuunga mkono huduma hiyo. Kwa lugha nyepesi kabisa wewe ni muasi ama unataka kuanzisha uasi ndani ya kanisa la KKKT.
Kama unajiamini na unaamini kwamba unachokisema na kukisimamia ni cha ukweli, hukupaswa kuja hapa kumshambulia babu wa loliondo, ulitakiwa kwenda kuonana na uongozi wa kanisa lako na kuwaeleza dukuduku lako, kinyume na hapo naogopa kukuita msaliti.

Kitu kingine ninachokiona kwako, kama tukikubaliana na mtazamo wako kwamba huduma ya babu ni ya kishetani, si mpango ama huduma ya kiMungu,basi tutalazimika kukutazama vizuri katika angle hiyo hiyo ya unyoofu wa moyo wako na matendo yako. Tukijaribu kukumbuka kwamba Kimtokacho mtu mdomoni ndicho kiujazacho moyo wake,basi nataka turudi nyuma kidogo tu kwenye lile darasa lako la mbinu za kutongoza. Kwa jinsi ulivyoendesha lile darasa la kutongoza bila shaka wewe ni mzoefu wa kuwavua wanaume, huwezi kuwa mtaalamu wa kutongoza halafu uje kutamba kwamba wewe ni bikira, labda unataka kutufanya tufikirie hatua moja mbele kwamba unatumia mtandao wa nusu shilingi.
Lakini pia nikibaki hapo hapo kwenye mbiu za kutongoza na uaminifu wako mbele za Mungu, ninapenda nikukumbushe kwamba aliyesema usizini ndiye huyo huyo aliyesema usishuhudie uongo na ndiy huyo huyo Mungu aliyesema usiue. Maandiko matakatifu yanatukumbusha na kutufundisha kuwa ukimuangalia mwanamke/mwanamme na kumtamani moyoni mwako tayari umeshazini naye, kwahiyo unakuwa hatiani kwa kuzini. Kwahiyo kama unthubutu kutongoza wanaume kwa mujibu wa maelezo yako mwenyewe basi tayari umemtamani huyo mwanaume na kwahiyo hata kama haufiki kwenye hatua ya kuukalia mtalimbo basi tayari umeshazini na huyo mwanaume na kwahiyo unakuwa umetenda dhambi kwa kwenda kinyume na amri ya Mungu.
Kutokana na ukweli huu, sitaki kuamini kabisa kwamba unaweza kuja kujikweza hapa kwamba ni mkamilifu kwakuwa bado bikra bila kukumbuka unashiriki uzinzi myoni mwako.

Mwisho kabisa nikukumbushe kwamba Kakobe, Mwingira, Mama rwakatare na wengine tunaowafahamu wanafanya show za vipindi vya kuhubiri injili kwenye runinga kila siku na watu wanamiminika kwao kupata uponyaji, na hawa wananchi wanaokwenda kutafuta uponyaji huko nio wanaotoa sadaka na michango mbali mbali kwa majina ya sadaka ya shukrani n.k, tunashuhudia watu wakitoa shuhuda kwamba wamesafiri kutoka kona zote za nchi hii hata nje ya nchi kuja dsm kutafuta uponyaji kwa kakobe, mwigira, mama rwakatare, mzee wa upako na wengine lakini hilo halikushughulishi isipokuwa unashughulika na huduma ya babu ambayo hajawahi kuwa na kipindi cha runinga ama radio kujitangaza bali walioponywa ndio waliosambaza habari za uponywaji wao na hatimaye media zikaamua kumpa babu promo bila yeye kulipia.Kwanini hujahoji watumishi wa show za runinga kwenda kutoa uponyaji mioani badala yake wamejikita dsm tu?? kwani hao wananchi wanapokuja dar wanakuja bila kulipia nauli? au makanisa hayo ndiyo yanayowasafirisha kuja dsm?? hebu kuwa mkweli katika hili, chuki, wivu na husda ndo zinakusumbua.

Nakuomba ukatubu kwanza dhambi yako ya uzinzi na nuendelee kumtumikia Mungu pasipo kujikweza ili usije ukashushwa chini na kuaibika.
Nilikuwa napita tu kuelekea mugumu nikaona ni vizuri kukuachia ujumbe huu muhimu kwa ustawi wa imani yako.


Nakubaliana na haya maneno yako hasa kwenye kipengele cha kujikweza, NI kweli tunaishi kwa Neema ya Mungu tuuuuuuuu!!!
Sio kweli kwamba kama hujaanguka kwenye uzinzi kimatendo ni kwa sababu ya ujanja wako hapana ni kwa sababu ya Neema ya Mungu inayokulinda na kukuhifadhi.

Kuna watu tume/wamejikuta wanaingia kwenye mahusiano ya mapenzi bila hata kutarajia kwa sababu tuna miili na tupo duniani. Roho i radhi lakini mwili ni dhaifu. ILa tunayeweza yote katika MUNGU. Miss Judy, nyenyekea na itukuze Neema ya MUngu tuuuuu!!!

Hayo mengine ya babu, umeshasema vya kutosha.
TUOMBE SASA, cha Mungu kijulikane ni kipi.

Afu sasa na ninyi ndo nini kuhamishia thread kwenye BIKIRA jamani,
Au hoja zimeisha?
Haya kwa herini.
ILa MSIACHE KUOMBA, OMBENI BILA KUKOMA!!!
 
CPU inaonekana wewe umefika kwa babu, hebu niambie kidogo hivi anaombea kwa jina la YESU?
Watu wa dini zote wanafika pale, anawafundisha Imani ya kupona ktk jina la Yesu, wanakubali na kuamini,
Halafu anachukua maji anayaombea kwa jina la Yesu, halafu anawapa watu wanakunywa kwa Imani ya Bwana Yesu,
Halafu wanarudi, wakiwa wapepona kwenye dini zao kwa Imani ya kupona kwa JINa la YESU?
Wanaendelea na Dini zao kama kawaida, kama mpagani, anarudi kwenye upagani wake, lakini amepona kwa jina la YESU?

Au ni aje hapo? CPU nisaidie tafadhali.

Ulielekeza maswali kwa mwingine ila naomba nichangie. Kwanza ujue dini upagani ni institution za dunia. Makanisa mengi na taasisi nyingi za dini zina katiba zinazosajiliwa na mamlaka za serikali. Suala la imani ni la mtu binafsi. Mimi naamini kuwa Yesu nimjuavyo siyo lazima iwe sawa na mtu mwingine. Lakini ukinitendea jema (kwa imani kuwa umenitendea jema) nitamshukuru Mungu kwa imani yangu kuwa wewe umelifanya kwa mapenzi yake.

Babu anapofanya kila kitu kwa jina la Yesu ni sahihi kwa kuwa ni imani yake (hatujui mazingira yanayomuimanisha) kuwa litakuwa au litatimia. Kwa hekima kiimani haitakiwi hata siku moja umwambie mtu kuwa imani sahihi ni hii. Yeye mwenyewe aendele kuamini kama alivyofuata huduma kuwa ni imani yake imemuelekeza.

Somo la imani ni gumu sana sana katika maisha ya neema tuliyojaliwa na Mungu. Lakini chukulia unapanda kitandani kulala; kamwe hufikirii kuwa kitanda kitakubeba bila kuvunjika hiyo ndiyo imani isyo na shaka na kweli kitanda hakivunjiki. Basi babu anaamini kwa jina la Yesu na wewe unayepona imani iliyokuleta kunya hiyo dawa in the first place ndiyo inakuponya rudi huko huko ulikotoka ukashuhudie umepona. NDIVYO NINAVYOMUELEWA BABU. Wanaoponya kwa nguvu zao nawatilia mashaka.

NATANGULIZA KUKUOMBA MSAMAHA KAMA NIMEKUPELEKA KUSIKO
 
Ninachosema ni kuwa waangalifu kwani kama Babu anamwamini Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo basi kwanini asiwape neno kuwaelezea kwanini Yesu alikuja na kwanini hao watu wanatakiwa kumfuata yeye. Kama babu atasema yeye ni mganga mimi wala sita kuwa na shida. lakini kama ni mchungaji ni wajibu wake kuchunga kondoo wa bwana

Pengine sio job description ya babu kuhubiri neno. Alikuwa mchungaji sasa kahamishwa kitengo je, no body knows.
 
dah!
wajameni jaribuni kuweka mabandiko mafupi mafupi yaliyosheheni point tu....!


mnaandika zaidi ya wahariri wajameni!?
 
Sijawahi kusema kwamba Babu ana dhambi kwa kufanya anayoyafanya ila tunatakiwa kuwa waangalifu na kuhoji maandiko yanasemaje? Tatizo langu ni kwamba neno (injili) halihubiriwi

Usemacho cha moto ni kweli kuwa nneno hakuna kwa babu.
Tuna haki ya kuhoji kimaandiko.
Tuna nafasi ya kuijaribu roho hii, tuna muda wa kuombea taifa.
Lakini sikufurahishwa na kuona watu wakikaa kumsema vibaya babu wakati hawaonyeshi kama wana huo ufunuo, kama roho yako inasita na haina uhakika nadhani busara ni kukaa kimya na kumuomba mungu, binafsi ni muoga kuchallenge imani au roho ya mtumishi awaye yeyote hadaharani mpaka niwe na ufunuo huo pamoja na uhakika.

Wapo wamsemao Kakobe,wapo wamsemao mwingira mzee wa upako, rwakatare, maboya na wengine wengi lakini siwezi kuhoji muumini wake na kuvutia niabudupo wakati sijafunuliwa
 
Pengine sio job description ya babu kuhubiri neno. Alikuwa mchungaji sasa kahamishwa kitengo je, no body knows.
Basi asiseme ameoteshwa na Mungu kwasababu maandiko yanatufundisha kuhubiri neno. (Matayo 28:19)
 
Nakubaliana na haya maneno yako hasa kwenye kipengele cha kujikweza, NI kweli tunaishi kwa Neema ya Mungu tuuuuuuuu!!!
Sio kweli kwamba kama hujaanguka kwenye uzinzi kimatendo ni kwa sababu ya ujanja wako hapana ni kwa sababu ya Neema ya Mungu inayokulinda na kukuhifadhi.

Kuna watu tume/wamejikuta wanaingia kwenye mahusiano ya mapenzi bila hata kutarajia kwa sababu tuna miili na tupo duniani. Roho i radhi lakini mwili ni dhaifu. ILa tunayeweza yote katika MUNGU. Miss Judy, nyenyekea na itukuze Neema ya MUngu tuuuuu!!!

Hayo mengine ya babu, umeshasema vya kutosha.
TUOMBE SASA, cha Mungu kijulikane ni kipi.

Afu sasa na ninyi ndo nini kuhamishia thread kwenye BIKIRA jamani,
Au hoja zimeisha?
Haya kwa herini.
ILa MSIACHE KUOMBA, OMBENI BILA KUKOMA!!!

Nimekusoma vizuri mpendwa,

Bikira inakuwa ni muhimu kuitaja kwa kuwa ukimsoma vizuri judith utamuona kwamba anajisifia kuwa na bikira katika umri wake wa miaka 26, kwa maneno mengine ni kama anajina kwamba amemaliza kazi, yuko kwenye njia sahihi lakin akasahau kwamba muda mfupi uliopita alikuwa anatoa darasa la kidunia-kutongoza, maandiko matakatifu hayatufundishi mbinu za kutongoza, yanatufundisha kuwa wanyenyekevu na upendo kwa binadamu wenzetu. Maandiko yanatuambia tutawezaje kusema tunampenda Mungu tusiyemuona ilihali tunawachukia majirani zetu tunaowaona kila siku??

btw, tuko pamoja tuanajribu kuwekana sawa.
 
Babu hahubiri neno, mtumishi anatakiwa kuhubiri neno ili liwaweke wasikilizao huru (Joh 8:3)

There you err again, there are five fold ministries.
Kuhubiri neno la Mungu sio kipimo cha kuwa mtumishi wa Mungu. Hebu tukumbushane kidogo maana babu kaingilia huduma za watu (1Cor 12:.....New Translation)..


12:4 Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
12:5 Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
12:6 Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
12:7 Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
12:8 Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
12:9 Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
12:10 humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
12:11 Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12:12 Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
12:28 Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
12:29 Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
12:30 Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
13:2 Tena, naweza kuwa na kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, nikafahamu siri zote na kujua kila kitu; naweza kuwa na imani yote hata nikaweza kuihamisha milima, lakini kama sina upendo mimi si kitu.
 
CPU inaonekana wewe umefika kwa babu, hebu niambie kidogo hivi anaombea kwa jina la YESU?
Watu wa dini zote wanafika pale, anawafundisha Imani ya kupona ktk jina la Yesu, wanakubali na kuamini,
Halafu anachukua maji anayaombea kwa jina la Yesu, halafu anawapa watu wanakunywa kwa Imani ya Bwana Yesu,
Halafu wanarudi, wakiwa wapepona kwenye dini zao kwa Imani ya kupona kwa JINa la YESU?
Wanaendelea na Dini zao kama kawaida, kama mpagani, anarudi kwenye upagani wake, lakini amepona kwa jina la YESU?

Au ni aje hapo? CPU nisaidie tafadhali.

Maswali yako yooote yameegemea kwanza kwa KUNISEMEA NIMEFIKA KWA BABU.
Kwanza naomba usiwe unanikadiria, niulize kwanza kama nilifika Loliondo au la then ndio utaandalia validity ya hayo maswali yako

Unatakiwa ufahamu ya kwamba Babu yuko pale kutibu, sio kubadilisha imani za watu. Na hata ukipata dawa zake ukapona bado pia hakuchagulii imani. Yeye ameongozwa na Mungu akaponye watu wote wenye imani na wasio na imani.
Kwa hiyo imani inabaki kuwa ya mtu mwenyewe binafsi, kabla na baada ya kupata dawa.

Halafu then naona umeingiza Jina la Yesu hapa ili ionekane kuna utofauti.
Kwangu mimi mkristo, na hata kwa imani ya Walutheran uponyaji kwa Jina la Yesu, kwa Jina la Mungu bado ni kule kule tu.
Yaani Yesu, Mungu bado njia ni ile ile kwa Muumba wa Mbingu na Dunia. Maana Yesu ni Mwana wa Mungu, hivyo na yeye pia ni Mungu
Au wewe mwenzetu una separate vp hayo majina?????
 
Basi asiseme ameoteshwa na Mungu kwasababu maandiko yanatufundisha kuhubiri neno. (Matayo 28:19)

Yeye kaoteshwa uponyaji na sio kuhubiri neno kama maandiko yanavyowafundisha. Kumbuka yeye hajaoteshwa kupitia maandiko, ameoteshwa kupitia ndoto.

Msiwe wachoyo kwa kuona imani zenu na yale mliyofundishwa ni bora kuliko imani za wengine. Msimhukumu babu mchungaji, Mungu ndiye mwenye kujua yote na si binadamu.
 
dah!
wajameni jaribuni kuweka mabandiko mafupi mafupi yaliyosheheni point tu....!


mnaandika zaidi ya wahariri wajameni!?

Hah ha aha
Na wewe Sukari-Eksitensheni umo??
 
Lakini sikufurahishwa na kuona watu wakikaa kumsema vibaya babu wakati hawaonyeshi kama wana huo ufunuo, kama roho yako inasita na haina uhakika nadhani busara ni kukaa kimya na kumuomba mungu, binafsi ni muoga kuchallenge imani au roho ya mtumishi awaye yeyote hadaharani mpaka niwe na ufunuo huo pamoja na uhakika.
Ni kweli unayoyasema hata mimi sikutaka kujiingiza hapa lakini kunamabo yalikuwa yanapotoshwa ndiyo maana nikaja kujibu maswali.

Wapo wamsemao Kakobe,wapo wamsemao mwingira mzee wa upako, rwakatare, maboya na wengine wengi lakini siwezi kuhoji muumini wake na kuvutia niabudupo wakati sijafunuliwa

Mimi simsehei yeyote kati ya hao na wala sijawahi kwenda huko kushiriki lakini sivibaya tukahiji kwani hii ndo jukwaa la great thinkers right? Kama tunajadili mambo ya kidunia kwanini tusijadili mambo ya kiroho? Kama tukifanya hivyo basi tutakuwa ni wanafiki.
 
Back
Top Bottom