Hivi Rais Samia amewahi kuandika Makala au Paper ya utatuzi wa changamoto za jamii?

Nimelazimika kuuliza hii kitu, ni muhimu sana kujua. Makala nzito iliyojaa critical analysis na ikapatikana kwenye national au International journals. Paper fulani hivi ya kuzungumzia changamoto mtambuka za jamii yetu ya Kitanzania.

Mambo haya yanaakisi sana uwezo wa mtu. Nafikiri ana Degree na Masters, ziko wapo Research reports zake tuzifanyie Literature Review.

Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi chungu mzima. Lakini hatuoni hatuoni hata moja ikipatiwa majibu ya utatuzi. Nchi ni kama mgonjwa anayesubiri muujiza wa Baba wa Mbinguni tu.
Huwa hausomi zile nakala za uteuzi na utenguzi?
 
Nyerere hakufilisi uchumi wa nchi. Nyerere alianzisha mashirika na viwanda vingi tu lakini hakujua watanzania ni wezi na wavivu wa kutupwa. Enzi za Nyerere watu waliokuwa wanasoma bure. Hospital bure. Kulikuwa mpaka na kupewa warrant wa kusafiri kwa wanafunzi na watu wengine kama wanamuziki. Kwa kifupi watu wa kawaida ndiyo walikuwa wana-enjoy keki ya Taifa. Hebu nionyeshe katika hizi nchi za sub-Sahara African countries ni nchi ipi wananchi wake walikuwa wanaishi vizuri kama Tanzania kipindi cha Nyerere! Nyerere mpaka raslimali aliziacha kwa matumizi ya baadae. Sasa hizi wanashindana kuzipiga bei.
Hawa Watoto wamezaliwa Mkapa akiwa madarakani wanajifanya wajuaji sana,kumbe weupe!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
..Nchi ilifilisika wakati wa awamu ya kwanza.

..baadhi ya matatizo yalisababishwa na sera za kijamaa alizoziamini Mwalimu Nyerere.

..kibaya zaidi Mwalimu alikataa ushauri wa kuchukua hatua za kurekebisha uchumi mapema.

..nashauri msome vitabu vilivyoandikwa na Edwin Mtei, na Andy Chande, mtapata picha ya nini ilisababisha uchumi wetu kuanguka miaka ya 1980.

..Kwenye kitabu cha Andy Chande anaelezea jinsi Mwalimu alivyotaifisha mali za kina Chande na kuanzisha shirika la National Milling.

..tatizo ni kwamba waliopewa kuendesha hizo mali za kina Chande / National Milling hawakuwa na uzoefu wa uendeshaji wa biashara hiyo.

..Matokeo yake shirika la umma kukawa likiendeshwa kwa hasara. Serikali ya Mwalimu iliendelea kutupa fedha ktk mashirika mengi ya aina hiyo.

..Mwalimu pia alitaifisha mashamba ya mkonge. Mkonge ilikuwa moja ya mazao yanayoingiza fedha nyingi za kigeni. Matokeo ya hatua za utaifishaji za Mwalimu Nyerere ni kuanguka kwa sekta ya mkonge.

..kulikuwa na harakati nyingi za kuyasimamisha mashirika yaliyokuwa yametaifishwa, pamoja na kuanzisha mengine mengi mapya ambayo hayakuweza kusimama yenyewe.

..Mwalimu alishauriwa atafute wabia kwa mashirika na makampuni yaliyokuwa wakifanya vibaya, lakini ushauri huo haukutekelezwa.

..Watanzania waliokuwa wakitoa ushauri, au kuunga mkono mabadiliko ya sera za uchumi waliitwa WASALITI / VIBARAKA ndani ya Ccm, na walishindwa ktk chaguzi za ndani ya chama.

..Mfumo wa uendeshaji uchumi wa Mwalimu uliwakera nchi wafadhili na taasisi zilizokuwa zikitukopesha. Matokeo yake ni wafadhili na wakopeshaji kugoma kutupa fedha mpaka pale tutakapobadili sera zetu, na namna tunavyoendesha uchumi.

..Hali hiyo ndio chanzo cha mgogoro kati ya Mwalimu Nyerere na taasisi za fedha kama IMF na WB. Mwisho wa yote Mwalimu aliamua kung'atuka na kupisha wengine waje waendesha nchi.

..Tofauti ya Mwalimu Nyerere na waliomfuatia ni kwamba yeye hakuwa fisadi aliyenufaiki ktk lindi la matatizo ya kiuchumi tuliyokuwa tukikabiliana nayo. Mwalimu aliachia madaraka akiwa hana hata pensheni ya Uraisi.
Kwani Nyerere aliua Uchumi alio ujenga nani?

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Alipaswa kujua watanzania ni wavivu kabla ya kutaifisha mashirika na viwanda binafsi na kuvifanya vya serikali, matokeo yake vikawa, vinajiendesha kwa hasara hadi kujifia

Serikali kutoa vitu bure sio ujanja, serikali sio baba au mama yako, serikali inatakiwa kuweka miundombinu sahihi na sera sahihi kwa ajili ya wananchi kuzalisha na kipato na kujilipia huduma wenyewe, nchi zilizoendelea ndio zilifanya hivyo, ujamaa ni kulea uvivu
Kipindi cha Nyerere ndio kipindi wananchi waliishi maisha magumu kuliko vipindi vyote, kwa mgao wa bidhaa, udikteta, njaa
Kwani baada ya kubinafsisha Wananchi wamenufaika vipi zaidi ya kutajirisha watu wachache!!?

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Nakubaliana na ujumbe wako kuanzia hapo kwenye 'vinginevyo' upo sahihi kabisa.

Hapo kwenye sentensi ya kwanza, Mungu naomba anipe uwezo wa kunyamaza, kuna vitu vinauma sana!
Magufuli alifoji Elimu kivipi wakati ata andiko lake alilopatia PhD lilitangazwa adharani?
Wekeni ushahidi wa kutosha,alifoji kivipi ili na sisi maamuma tuelewe!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
..tafuta vitabu vya Edwin Mtei, na Andy Chande.

..naamini ukichanganya na uzoefu wako utapata full picture ya nini kiliangusha uchumi wetu.
Huyo Mtei si alikuwa kibaraka wa Wazungu!
Kilichoua Uchumi wetu ni uwizi na uvivu wa Watanzania, Mwalimu Nyerere alifanya kwa nafasi yake ila alizungukwa na wezi kama ambavyo ata sasa Rais kazungukwa na Wahuni!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Uwezo huo hana, to me samia, is "the president that was never meant to be"
Nchi hii ina bahati mbaya sana, Kikwete, Mwinyi(baba), Maghu,hawa walikuwa ajari mbaya kwa mustakabali wa TZ, madhara waliyoyafanya, itachukua miaka mingi 100+kulekebisha,
Sasa imagine, Mpango anakuwa Raisi wa nchi! Wizara tu ilimtoa kamasi,nilikutana nae kahama, yupo kwenye V8, na, bodyguards wake, wawili wana siraha, wanaibuka kwenye vituo vya kuuza mafuta, wanaanza kuulizia risiti kama zinatolewa! Wakasumbua sana mameneja wa vituo vya mafuta! Kwa ukubwa wa nchi hii, unawezaje kutumia hii mbinu kucheki kama risiti zinatolewa!
So pathetic!
 
Kwani Nyerere alirithi Uchumi gani toka kwa Wakoloni mpaka aka ufulisi?

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
Wakoloni waliacha bandari, mashamba makubwa na ranchi, viwanda, benki...vilivyokuwa vikitoa ajira na kulipa kodi kwa serikali, Nyerere alipoingia akawapora watu binafsi waliokuwa waliokuwa wakiendesha kwa ufanisi na kuwakabidhi watu wake kutoka TANU (CCM) na wakishindwa kuviendesha sababu ya elimu ndogo, rushwa na uvivu na kuviua
 
Soma vizuri historia yako kijana, Mwarabu umemkuta huku pwani kakupokea. Wewe wakuja tu. Hii unayooita bara wala hujakosea hili lote lilikuwa bara la Zenj "Zenjbar".

Huna historia huku kabisa. Tena wewe unaonesha huna hata miaka 5 huku au labda ulikuja kutenbea tu na kurudi kwenu sijuwi pori gani huko.

Wenyeji wa pwani hawaongei kijinga kama wewe. Madrassa ziliwafunguwa ubongo, wewe bado bongolala.
Kushinda kwenye bao na alkasusi ndiyo kufungua ubongo?
 
..Nchi ilifilisika wakati wa awamu ya kwanza.

..baadhi ya matatizo yalisababishwa na sera za kijamaa alizoziamini Mwalimu Nyerere.

..kibaya zaidi Mwalimu alikataa ushauri wa kuchukua hatua za kurekebisha uchumi mapema.

..nashauri msome vitabu vilivyoandikwa na Edwin Mtei, na Andy Chande, mtapata picha ya nini ilisababisha uchumi wetu kuanguka miaka ya 1980.

..Kwenye kitabu cha Andy Chande anaelezea jinsi Mwalimu alivyotaifisha mali za kina Chande na kuanzisha shirika la National Milling.

..tatizo ni kwamba waliopewa kuendesha hizo mali za kina Chande / National Milling hawakuwa na uzoefu wa uendeshaji wa biashara hiyo.

..Matokeo yake shirika la umma kukawa likiendeshwa kwa hasara. Serikali ya Mwalimu iliendelea kutupa fedha ktk mashirika mengi ya aina hiyo.

..Mwalimu pia alitaifisha mashamba ya mkonge. Mkonge ilikuwa moja ya mazao yanayoingiza fedha nyingi za kigeni. Matokeo ya hatua za utaifishaji za Mwalimu Nyerere ni kuanguka kwa sekta ya mkonge.

..kulikuwa na harakati nyingi za kuyasimamisha mashirika yaliyokuwa yametaifishwa, pamoja na kuanzisha mengine mengi mapya ambayo hayakuweza kusimama yenyewe.

..Mwalimu alishauriwa atafute wabia kwa mashirika na makampuni yaliyokuwa wakifanya vibaya, lakini ushauri huo haukutekelezwa.

..Watanzania waliokuwa wakitoa ushauri, au kuunga mkono mabadiliko ya sera za uchumi waliitwa WASALITI / VIBARAKA ndani ya Ccm, na walishindwa ktk chaguzi za ndani ya chama.

..Mfumo wa uendeshaji uchumi wa Mwalimu uliwakera nchi wafadhili na taasisi zilizokuwa zikitukopesha. Matokeo yake ni wafadhili na wakopeshaji kugoma kutupa fedha mpaka pale tutakapobadili sera zetu, na namna tunavyoendesha uchumi.

..Hali hiyo ndio chanzo cha mgogoro kati ya Mwalimu Nyerere na taasisi za fedha kama IMF na WB. Mwisho wa yote Mwalimu aliamua kung'atuka na kupisha wengine waje waendesha nchi.

..Tofauti ya Mwalimu Nyerere na waliomfuatia ni kwamba yeye hakuwa fisadi aliyenufaiki ktk lindi la matatizo ya kiuchumi tuliyokuwa tukikabiliana nayo. Mwalimu aliachia madaraka akiwa hana hata pensheni ya Uraisi.
Excellent. Kibaya zaidi katika yote haya, alitaka taasisi na mashirika yote yasimamiwe na makada wa TANU/CCM walioidhinishwa na yeye kama mwenyekiti wa chama (CC).

Hata vyama vikuu vya ushirika alivyovikuta vikiwa huru na kuwa na nguvu kubwa sana kiuchumi nchini alivivunja ili kuua nguvu na jeuri ya wenyeviti wake. Baadaye akavianzisha tena chini ya wenyeviti waliokuwa vetted na CCM! Ndio ilikuwa mwisho wa vyama makini vya ushirika na jeuri ya mkulima wa Tanzania.

Alijali sana utii (loyalty) kuliko sifa nyingine zote. Alikuwa tayari hata kuvumilia baadhi ya wezi na wala rushwa wanaomtii na kumpigia magoti kuliko weledi wanaokosoa mawazo yake. Ajabu yeye binafsi aliuchukia sana wizi na ufisadi. Lakini kukosolewa mawazo yake ilikuwa inmpandisha hasira zaidi. Hapo ndipo unafiki wa watendaji serikalini katika mnyororo wa kusimamia rasilimali za umma na uchawa (kula na wakubwa) ulipoanzia.
 
Sasa hukuona nimemuandika Tiny na LONRHO?

Nisiyoyajuwa na nimeyaishi? Unataka kusema nini ewe poyoyo.

Alikuwa na kiwanda na kilikuwa Pugu Road kama huelewi, kilikuwa kinaunganisha matrekta mdogo mdogo, wakataka kukiongezea ukubwa ndiyo Nyerere akaleta zake. Unjuwa matokeo yake au nikukumbushe?

Matokeo Tiny Rowland akaja Tanzania, akamwambia Nyerere kwa utaratibu kabisa kupitia balzi, rudisha vyote ulivyonitaifisha ulipe na gharama au umejiumiza. Nyerere akafanya ubishi.

Tokea hapo tukabaniwa kila kitu kimya kimya na nchi za magharibi. Unalijuwa hilo. Tukawa nyang'a nya'a tukasingizia vita imetutia umasikini. Voita itutie umasikini wakati sisi tyumetumiwa na Waingereza na Wayahudi tu?

Wewe wadanganye mapoyoyo, mimi nimeuisha huo wakati na nnalijuwa hilo sakata kwa details moja moja.,
Kama ungekuwa unayajua, usingehusisha Lonrho na kiwanda cha Valmet.
 
Excellent. Kibaya zaidi katika yote haya, alitaka taasisi na mashirika yote yasimamiwe na makada wa TANU/CCM walioidhinishwa na yeye kama mwenyekiti wa chama (CC).

Hata vyama vikuu vya ushirika alivyovikuta vikiwa huru na kuwa na nguvu kubwa sana kiuchumi nchini alivivunja ili kuua nguvu na jeuri ya wenyeviti wake. Baadaye akavianzisha tena chini ya wenyeviti waliokuwa vetted na CCM! Ndio ilikuwa mwisho wa vyama makini vya ushirika na jeuri ya mkulima wa Tanzania.

Alijali sana utii (loyalty) kuliko sifa nyingine zote. Alikuwa tayari hata kuvumilia baadhi ya wezi na wala rushwa wanaomtii na kumpigia magoti kuliko weledi wanaokosoa mawazo yake. Ajabu yeye binafsi aliuchukia sana wizi na ufisadi. Lakini kukosolewa mawazo yake ilikuwa inmpandisha hasira zaidi. Hapo ndipo unafiki wa watendaji serikalini katika mnyororo wa kusimamia rasilimali za umma na uchawa (kula na wakubwa) ulipoanzia.

..Mimi naamini sera za UJAMAA zilikuwa na athari kubwa kwa mashirika ya umma kuliko wizi.

..Kwa mfano, lila shirika la umma lilikuwa na tawi la Ccm, na tawi la Juwata.

..Sasa ukizingatia sera ya CHAMA KUSHIKA HATAMU ni kwamba Ccm na Juwata ktk taasisi ya umma walikuwa na uwezo wa kuingilia maamuzi ya management.

..Vilevile mashirika haya yalibebeshwa mizigo mikubwa ya huduma za kijamii kabla hata hayajaimarika.

..Haikuwa ajabu kukuta shirika la umma lina timu za mpira wa miguu, netball, bendi za muziki, mabasi ya kusafirisha wafanyakazi, etc.

..Ukiacha hayo, mashirika ya umma yalikuwa yanashindana kuwa " CHAWA " wa Ccm kwa wakati huo. Kila Mkurugenzi au Meneja Mkuu alikuwa anataka kumzidi mwenzake kwa kuchangia shughuli na mikutano ya Ccm.

..Kwa kifupi mashirika ya umma yalikuwa hayazingatii kanuni za biashara. Kukosa umakini ktk idadi ya waajiriwa ilikuwa moja ya changamoto. Na Meneja yeyote aliyejaribu kujenga hoja kwamba kampuni uendeshe kibiashara alipigwa vita kuwa analeta mambo ya ubepari, ubeberu, nk.
 
Back
Top Bottom