Rais Samia: Lita Milioni 70 za Maji kutoka Kigamboni ziingizwe Dar es Salaam kusaidia upungufu wa Maji

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Nishati Safi ya Kupikia, Leo Novemba 1, 2022



Prof. Anna Tibaijuka
Mbunge mstaafu Profesa Anna Tibaijuka amesema Watanzania wengi wanafahamu umuhimu wa gesi lakini bado wanalazimika kutumia mkaa na kuni kwa kuwa gharama za nishani safi ndio ni tatizo.

Amesema “Moja ya changamoto ya nishati safi ni gharama za vifaa, mfano gesi ndogo ilikuwa inauzwa Tsh. 18,000 sasa hivi inauzwa Tsh. 24,000 hapo ndipo tatizo linapoanzia.”

Amesema Serikali inatakiwa kuingilia na kuweka sawa suala hilo kupitia sera, pia ameshauri EWURA na mamlaka nyingine husika zitengeneze mazingira mazuri kwa watumiaji na wazalishaji wa gesi ambao ndio wawekezaji.
Samia Suluhu Hassan - Rais
Tunapoikata miti sijui uhai wetu uko wapi, ni gharama ya maradhi tunayopata.

Kwenda kutafuta nishati ya kuni kunaleta gender based violence, ukiwa huko unakutana na wachunga mbuzi (wabakaji), ukirudi nyumbani unakutana na kipigo.

Kingine ni kubadili mindset, unapojenga nyumba unajenga na jiko la nje ili utumie kuni. Tubadili hii mindset.

Katika kutafuta afua, kumekuwepo na teknolojia ya biogas, majiko ya gesi, umeme n.k

Takwimu zinasema Kaya zinazotumia gesi ni 5%, umeme ni 3%, bado tunachangamoto ya kutotumia vizuri nishati safi.

Nielekeze kwamba swala hili siyo la muda mfupi, kwamba baada ya muda mfupi watanzania wote wawe na nishati safi. Tuanze sasa, lakini twende na kasi kubwa.

Swala hili ni mtambuka, kianzishwe kikosi kazi kisicho cha kiserikali kitakacho chambua na kutoa mapendekezo ya kisera, kije na mpango kazi utakaoelekeza kwenye kutafuta suluhu ya nishati safi na endelevu.

Ni lazima twende na nishati safi ya kupikia kwa maendeleo ya nchi, jamii na kukinga haki za wanawake ambao wanafanya mambo mengi ya kujiumiza pasipo malipo. Tuwapunguzie mzigo na madhara ya kile wanachofanya tena bila malipo. Pia, tunampa muda zaidi wa kushughulika na mambo mengine ya kiuchumi.

Hadi 2032 tuwe na nishati safi ya kupikia, lengo ni kumtua mama mzigo wa kuni kichwani.

Tunasema mkaa ni rahisi lakini gharama ya mti ule ni kubwa sana. Miti tunayopanda mingi iwe ya matunda maana kukata mti wa matunda utawaza mara nne. Miti ya asili tuitumie kuzalisha asali kwa kuwa ina soko kubwa duniani.

Naipa Wizara Mwaka mzima wa 2023 nataka mjielekeze kwenye hili la taasisi kubwa kutumia nishati safi. Ikifika 2024 nataka nisimame kwa wananchi niseme nimefanikisha hilo kwa kiwango hiki.

Kuhusu Upatikanaji wa maji DSM kwanza ni mabadiliko ya hali ya hewa yenye sura 2 ambayo ni Ki Mungu na kwa sababu ya mambo yetu wenyewe, ukataji wa miti ndiyo sababu kuu, watu wanalima, wameweka vizuizi vya maji kwenda mto ruvu, watu wamejenga ponds wanafuga samaki humo humo. Mkuu wa mkoa na DAWASA nawaagiza mkasafishe mto isaidie upatikanaji wa maji.

Nataka nione lita milioni 70 kutoka kigamboni zinaingia DSM ili kupunguza changamoto ya maji.

DAWASA na Wizara ya maji itazame miundo mbinu, mingine ilijengwa zamani, kingine ni ujenzi holela wa makazi. Waziri mkuu atawasimamia.
 
Subiri kwanza tuone mzee.
Screenshot_20221101-083400.png

Wakati nimetoka kusoma post hii post ya chini yako nimekutana na hii 👆👆👆👆👆
 
Ni jambo jema

Siku Rostam alipoinunulia Kwaya ya KKKT Kinondoni vyombo vipya vya muziki nilihisi kuna jambo la kimwili zaidi!
 
Alipomchukua Lowassa CHADEMA na kwenda kumkabidhi kwa hayati Shujaa Maguful ndio nilichoka kabisa
Hiyo cha mtoto, Pale RA kwenye hilo tukio alipojifanya dereva wa Lowasa akamwendesha kwenye VXR-V8 hadi Lumumba kwa mwendazake na kupokelewa kwa bashasha nikasema bora niachane na siasa nijilimie vinyungu vyangu vya ving'amba huku Kinegembasi bila kelele na mtu
 
Nimelisikiliza kidogo ni Kingamano muruwaa sana.

Tusipokuwa makini watu milioni sitini na ushee haya mapori yataisha ndani ya miaka ishirini.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Nishati Safi ya Kupikia, Leo Novemba 1, 2022



Prof. Anna Tibaijuka
Mbunge mstaafu Profesa Anna Tibaijuka amesema Watanzania wengi wanafahamu umuhimu wa gesi lakini bado wanalazimika kutumia mkaa na kuni kwa kuwa gharama za nishani safi ndio ni tatizo.

Amesema “Moja ya changamoto ya nishati safi ni gharama za vifaa, mfano gesi ndogo ilikuwa inauzwa Tsh. 18,000 sasa hivi inauzwa Tsh. 24,000 hapo ndipo tatizo linapoanzia.”

Amesema Serikali inatakiwa kuingilia na kuweka sawa suala hilo kupitia sera, pia ameshauri EWURA na mamlaka nyingine husika zitengeneze mazingira mazuri kwa watumiaji na wazalishaji wa gesi ambao ndio wawekezaji.
Samia Suluhu Hassan - Rais
Tunapoikata miti sijui uhai wetu uko wapi, ni gharama ya maradhi tunayopata.

Kwenda kutafuta nishati ya kuni kunaleta gender based violence, ukiwa huko unakutana na wachunga mbuzi (wabakaji), ukirudi nyumbani unakutana na kipigo.

Kingine ni kubadili mindset, unapojenga nyumba unajenga na jiko la nje ili utumie kuni. Tubadili hii mindset.

Katika kutafuta afua, kumekuwepo na teknolojia ya biogas, majiko ya gesi, umeme n.k

Takwimu zinasema Kaya zinazotumia gesi ni 5%, umeme ni 3%, bado tunachangamoto ya kutotumia vizuri nishati safi.

Nielekeze kwamba swala hili siyo la muda mfupi, kwamba baada ya muda mfupi watanzania wote wawe na nishati safi. Tuanze sasa, lakini twende na kasi kubwa.

Swala hili ni mtambuka, kianzishwe kikosi kazi kisicho cha kiserikali kitakacho chambua na kutoa mapendekezo ya kisera, kije na mpango kazi utakaoelekeza kwenye kutafuta suluhu ya nishati safi na endelevu.

Ni lazima twende na nishati safi ya kupikia kwa maendeleo ya nchi, jamii na kukinga haki za wanawake ambao wanafanya mambo mengi ya kujiumiza pasipo malipo. Tuwapunguzie mzigo na madhara ya kile wanachofanya tena bila malipo. Pia, tunampa muda zaidi wa kushughulika na mambo mengine ya kiuchumi.

Hadi 2032 tuwe na nishati safi ya kupikia, lengo ni kumtua mama mzigo wa kuni kichwani.

Viva Rostam.
 
Dar 70% watumie ges asilia kupikia ziwekwe gas prepaid meters no Mkaa Dar. Pia Moro mjini Tuokoe Misitu ya Pwani na Morogoro. Vinginevyo we are doomed
Bei ya Umeme iwe chini 50% ya sasa
Bei ya Gesi iwe chini 50% ya sasa
Bei ya Mkaa iwe zaidi ya Tanzanite maeneo ya miji
Usambazaji wa Umeme na Gesi remote areas uendelee kwa kasi ya Mwanga

Kinyume cha hapo hiki kiangazi ukame cha mtoto kijacho mpaka sisimizi watakimbilia mjini
 
Back
Top Bottom