Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Nishati Safi ya Kupikia, Leo Novemba 1, 2022
Prof. Anna Tibaijuka
Mbunge mstaafu Profesa Anna Tibaijuka amesema Watanzania wengi wanafahamu umuhimu wa gesi lakini bado wanalazimika kutumia mkaa na kuni kwa kuwa gharama za nishani safi ndio ni tatizo.
Amesema “Moja ya changamoto ya nishati safi ni gharama za vifaa, mfano gesi ndogo ilikuwa inauzwa Tsh. 18,000 sasa hivi inauzwa Tsh. 24,000 hapo ndipo tatizo linapoanzia.”
Amesema Serikali inatakiwa kuingilia na kuweka sawa suala hilo kupitia sera, pia ameshauri EWURA na mamlaka nyingine husika zitengeneze mazingira mazuri kwa watumiaji na wazalishaji wa gesi ambao ndio wawekezaji.
Tunapoikata miti sijui uhai wetu uko wapi, ni gharama ya maradhi tunayopata.
Kwenda kutafuta nishati ya kuni kunaleta gender based violence, ukiwa huko unakutana na wachunga mbuzi (wabakaji), ukirudi nyumbani unakutana na kipigo.
Kingine ni kubadili mindset, unapojenga nyumba unajenga na jiko la nje ili utumie kuni. Tubadili hii mindset.
Katika kutafuta afua, kumekuwepo na teknolojia ya biogas, majiko ya gesi, umeme n.k
Takwimu zinasema Kaya zinazotumia gesi ni 5%, umeme ni 3%, bado tunachangamoto ya kutotumia vizuri nishati safi.
Nielekeze kwamba swala hili siyo la muda mfupi, kwamba baada ya muda mfupi watanzania wote wawe na nishati safi. Tuanze sasa, lakini twende na kasi kubwa.
Swala hili ni mtambuka, kianzishwe kikosi kazi kisicho cha kiserikali kitakacho chambua na kutoa mapendekezo ya kisera, kije na mpango kazi utakaoelekeza kwenye kutafuta suluhu ya nishati safi na endelevu.
Ni lazima twende na nishati safi ya kupikia kwa maendeleo ya nchi, jamii na kukinga haki za wanawake ambao wanafanya mambo mengi ya kujiumiza pasipo malipo. Tuwapunguzie mzigo na madhara ya kile wanachofanya tena bila malipo. Pia, tunampa muda zaidi wa kushughulika na mambo mengine ya kiuchumi.
Hadi 2032 tuwe na nishati safi ya kupikia, lengo ni kumtua mama mzigo wa kuni kichwani.
Tunasema mkaa ni rahisi lakini gharama ya mti ule ni kubwa sana. Miti tunayopanda mingi iwe ya matunda maana kukata mti wa matunda utawaza mara nne. Miti ya asili tuitumie kuzalisha asali kwa kuwa ina soko kubwa duniani.
Naipa Wizara Mwaka mzima wa 2023 nataka mjielekeze kwenye hili la taasisi kubwa kutumia nishati safi. Ikifika 2024 nataka nisimame kwa wananchi niseme nimefanikisha hilo kwa kiwango hiki.
Kuhusu Upatikanaji wa maji DSM kwanza ni mabadiliko ya hali ya hewa yenye sura 2 ambayo ni Ki Mungu na kwa sababu ya mambo yetu wenyewe, ukataji wa miti ndiyo sababu kuu, watu wanalima, wameweka vizuizi vya maji kwenda mto ruvu, watu wamejenga ponds wanafuga samaki humo humo. Mkuu wa mkoa na DAWASA nawaagiza mkasafishe mto isaidie upatikanaji wa maji.
Nataka nione lita milioni 70 kutoka kigamboni zinaingia DSM ili kupunguza changamoto ya maji.
DAWASA na Wizara ya maji itazame miundo mbinu, mingine ilijengwa zamani, kingine ni ujenzi holela wa makazi. Waziri mkuu atawasimamia.
Prof. Anna Tibaijuka
Mbunge mstaafu Profesa Anna Tibaijuka amesema Watanzania wengi wanafahamu umuhimu wa gesi lakini bado wanalazimika kutumia mkaa na kuni kwa kuwa gharama za nishani safi ndio ni tatizo.
Amesema “Moja ya changamoto ya nishati safi ni gharama za vifaa, mfano gesi ndogo ilikuwa inauzwa Tsh. 18,000 sasa hivi inauzwa Tsh. 24,000 hapo ndipo tatizo linapoanzia.”
Amesema Serikali inatakiwa kuingilia na kuweka sawa suala hilo kupitia sera, pia ameshauri EWURA na mamlaka nyingine husika zitengeneze mazingira mazuri kwa watumiaji na wazalishaji wa gesi ambao ndio wawekezaji.
Samia Suluhu Hassan - RaisTunapoikata miti sijui uhai wetu uko wapi, ni gharama ya maradhi tunayopata.
Kwenda kutafuta nishati ya kuni kunaleta gender based violence, ukiwa huko unakutana na wachunga mbuzi (wabakaji), ukirudi nyumbani unakutana na kipigo.
Kingine ni kubadili mindset, unapojenga nyumba unajenga na jiko la nje ili utumie kuni. Tubadili hii mindset.
Katika kutafuta afua, kumekuwepo na teknolojia ya biogas, majiko ya gesi, umeme n.k
Takwimu zinasema Kaya zinazotumia gesi ni 5%, umeme ni 3%, bado tunachangamoto ya kutotumia vizuri nishati safi.
Nielekeze kwamba swala hili siyo la muda mfupi, kwamba baada ya muda mfupi watanzania wote wawe na nishati safi. Tuanze sasa, lakini twende na kasi kubwa.
Swala hili ni mtambuka, kianzishwe kikosi kazi kisicho cha kiserikali kitakacho chambua na kutoa mapendekezo ya kisera, kije na mpango kazi utakaoelekeza kwenye kutafuta suluhu ya nishati safi na endelevu.
Ni lazima twende na nishati safi ya kupikia kwa maendeleo ya nchi, jamii na kukinga haki za wanawake ambao wanafanya mambo mengi ya kujiumiza pasipo malipo. Tuwapunguzie mzigo na madhara ya kile wanachofanya tena bila malipo. Pia, tunampa muda zaidi wa kushughulika na mambo mengine ya kiuchumi.
Hadi 2032 tuwe na nishati safi ya kupikia, lengo ni kumtua mama mzigo wa kuni kichwani.
Tunasema mkaa ni rahisi lakini gharama ya mti ule ni kubwa sana. Miti tunayopanda mingi iwe ya matunda maana kukata mti wa matunda utawaza mara nne. Miti ya asili tuitumie kuzalisha asali kwa kuwa ina soko kubwa duniani.
Naipa Wizara Mwaka mzima wa 2023 nataka mjielekeze kwenye hili la taasisi kubwa kutumia nishati safi. Ikifika 2024 nataka nisimame kwa wananchi niseme nimefanikisha hilo kwa kiwango hiki.
Kuhusu Upatikanaji wa maji DSM kwanza ni mabadiliko ya hali ya hewa yenye sura 2 ambayo ni Ki Mungu na kwa sababu ya mambo yetu wenyewe, ukataji wa miti ndiyo sababu kuu, watu wanalima, wameweka vizuizi vya maji kwenda mto ruvu, watu wamejenga ponds wanafuga samaki humo humo. Mkuu wa mkoa na DAWASA nawaagiza mkasafishe mto isaidie upatikanaji wa maji.
Nataka nione lita milioni 70 kutoka kigamboni zinaingia DSM ili kupunguza changamoto ya maji.
DAWASA na Wizara ya maji itazame miundo mbinu, mingine ilijengwa zamani, kingine ni ujenzi holela wa makazi. Waziri mkuu atawasimamia.