Hivi dini zingine hawaruhusiwi kuchinja?

Hivi dini zingine hawaruhusiwi kuchinja?

Mimi nachinja mwenyewe au Wana familia yangu. Huwa siiti muislam kuchinja. Na wakija nyumbani huwa nawapa mboga za majani na kumwambia kuwa kuku wa kienyeji kachinjwa na mkristo
 
Unauhakika haipo?
Soma Qur-aan. Hutakuta aya hata moja inayokataza kula kilichochinjwa na myahudi au mkiristo.

Bali utakuta aya inayoturuhusu kula vyakula vyao na kuwaoa wanawake wao walio wema na wabaki na dini yao
Mkuu naomba msaada ktk hili la ndoa kati ya mwanaume muislam na mwanamke mkristo/myahudi. Je, ndoa kama hyo hufungwa na sheikh na ktk misingi gani?
 
Unauhakika haipo?
Soma Qur-aan. Hutakuta aya hata moja inayokataza kula kilichochinjwa na myahudi au mkiristo.

Bali utakuta aya inayoturuhusu kula vyakula vyao na kuwaoa wanawake wao walio wema na wabaki na dini yao
Mkuu naomba msaada ktk hili la ndoa kati ya mwanaume muislam na mwanamke mkristo/myahudi. Je, ndoa kama hyo hufungwa na sheikh na ktk misingi gani?
 
Wakristo sio tu kwamba haturuhusiwi kuchinja, tunaweza na tunaruhusiwa kula chochote isipokua nyamafu tu. Tukiamua kuchinja wenyewe hakuna tatizo lolote kwa upande wetu, tatizo jamii zetu zimeingiliana na kuna ukaribu wa hali ya juu sana na ujirani kati ya waumini wa dini hizi mbili, sasa kwa wengine hawaruhusiwi kula kilichochinjwa bila kufuata taratibu zao, kuamua kuchinja wenyewe italeta kuwanyima ushiriki wa hao ndugu na jamaa zetu.

Tunafanya hivyo kwa kuweka maelewano tu na kujumuika, kuchinja tunaweza sana. Kama hatuwezi, mnyama nani hua anachinja?
exellent
 
Mkuu naomba msaada ktk hili la ndoa kati ya mwanaume muislam na mwanamke mkristo/myahudi. Je, ndoa kama hyo hufungwa na sheikh na ktk misingi gani?
Iwapo binti hana walii basi ndoa hii itafungwa na qaadh.
 
Mimi nimeishi katika jumuiya ya watu mbalimbali na wa dini zote.

Cha kushangaza inapofika sikukuu au wamenunua jogoo basi watu hutafutwa kwa ajili ya kuchinja, japokuwa wanaume wapo.

Nimekula sana shingo mchuzi hata vibawa kwa kazi hiyo. Ndio nauliza; Je, kuna madhehebu ya wakristo wanakataza kuchinja?
Naweza sema wengine katika wakristo wanaamini kuwa ni musilamu ndio anayechinja (halali) sababu ya kusema hivyo ni kuwa hapa nyumbani jirani zetu ni wakristo lkn kila wakitaka kuchinja ni lazima watuite sisi,na kuna siku mmoja wao alichinja mwenyewe mbuzi lkn amini nyama ile waligoma kuila na mmoja wa familia ile anaitwa Wema aliniambia mm nyama akichinja mkristo mwenzangu siwezi kula .nikamuuliza kwa nini?akasema moyo wangu tu unakataa kula nyama ilichinjwa na mkristo.nikabaki na mshangao tu
 
Wakristo sio tu kwamba haturuhusiwi kuchinja, tunaweza na tunaruhusiwa kula chochote isipokua nyamafu tu. Tukiamua kuchinja wenyewe hakuna tatizo lolote kwa upande wetu, tatizo jamii zetu zimeingiliana na kuna ukaribu wa hali ya juu sana na ujirani kati ya waumini wa dini hizi mbili, sasa kwa wengine hawaruhusiwi kula kilichochinjwa bila kufuata taratibu zao, kuamua kuchinja wenyewe italeta kuwanyima ushiriki wa hao ndugu na jamaa zetu.

Tunafanya hivyo kwa kuweka maelewano tu na kujumuika, kuchinja tunaweza sana. Kama hatuwezi, mnyama nani hua anachinja?
Umejibu vyema tena kwa hekima. I wish wat kwe jf wangekuwa wana respond mada design hii.
 
Hata kukata magovi tulikuwa tunapuuza, tulikuwa tunasema ni islamic thing,lakini tumegundua leo kuwa ndio njia sahihi ya kuzuia maambukizi ya ukimwi tunapanga foleni ya kuyatoa masoksi hayo,hata wajaluo wamenyoosha. maneno
Ina faida gani hii njia kuzidi njia zingine mbadala? Inapunguza maumivu kwa mchinjwaji au? Why this and not any other way?
 
Mimi sijaelewa. Hivi mnabishania juu ya nani mwenye haki ya kuua, kati ya mkristo na muislamu, kuchinja, yaani kutoa uhai wa kiumbe ndo mnabishania?????
 
[quote uid=105391 name="imhotep" post=18594161]Hivi ndio inavyotakiwa.View attachment 438083
Ina faida gani hii njia kuzidi njia zingine mbadala? Inapunguza maumivu kwa mchinjwaji au? Why this and not any other way?[/QUOTE]
Iko siri ndani yake,ni sawasawa na govi,hatukujua madhara yake mpaka ukimwi ulipoingia,uisilamu na uyahudi na umasai ulijua faida zake.
 
Uislamu ulianza ukiwa mgeni kwa watu na utarejea ktk hali ya ugeni kama ulivyoanza. Aya hiyo nimeshaweka hapo ambayo pia inaruhusu mwanaume muislamu kumuoa mwanamke mkristo au myahudi. Ni ktk muktadha gani...H/work.
Hata mwanamke wa kiislamu anaruhusiwa kuolewa na mwanume wa kiyahudi au kikiristo, watu wana complicate too. Soma Quran 2:221
 
Ujinga huo mim sina NACHINJA MWENYEWE MFUGO WANGU,, Awe Nguruwe,, Jogoo,, Mbuzi Sihitaji mfugo wangu uelekezwe Kibla nachinja TU,,

Sisi Mungu wetu siyo Kama King,amuzi kwamba lazima dish lielekee upande Fulani ndo upate Chanel,,

Sisi pande zote Mungu wetu anaona na kusikia maombi yetu.,, iwe wakt wa kuchinja,, kuombea uponyaji nk pande zote yupo TU.
alooo umetisha mkuu
 
Kwa kuongezea hapo ktk sheria ya kiislamu ni haramu kula kilichochinjwa na muislamu ambaye haswali sala tano.
Acha uongo wewe, ili nyama iwe halal ni kusomwewa jina la Mwenyezi Mungu, hata mkiristo akichinja kwa kutaja jina la Mwenyezi Mungu hiyo nyama inakuwa halal
 
Back
Top Bottom