STORY: FAKE HISTORY(Historia Batili)
WRITER: Jumaa Khatib Mdharuba(Jk)
+255 718 274 130
+255 756 274 130
EPISODE 11
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Ni siku tatu sasa tangu mwili wa Sauda upumzishwe kwa amani,Si Kulwa tu, bali hakuna hata mmoja kati ya ndugu zake pia aliyekuwa amehoji au kuulizia kuhusu kifo cha Sauda na utata ambao Kulwa alidai upo. Walishasahau.. Na ni katika siku hii hii ndio Kulwa alipigiwa simu kutoka kazini kwake na akatakiwa arudi Rwanda kwani yeye alikua mtu muhimu sana pale benki..Akiondoka kuna mambo mengi sana yanasimama yakimsubiri yeye..Na kwakuwa walishazika, akawa hana namna bali kuondoka tu. Alipanga aondoke kesho yake asubuhi sana..
Mjomba nataka nkwambie kitu ambacho kitakusaidia maishani mwako.. Alianza kuongea Mzee J4 baada ya kumwita pembeni Kulwa, hii ni baada ya kuagwa safari na mjomba wake huyu..
Kwenye haya maisha kuwa makini sana mjomba, usidhani kila kitu unachofikiri unaweza kufanya basi ukakurupuka kukifanya, UTAUMBUKA.. Alianza nasaha zake mzee J4 kwa kijana wake huyu ambaye alionesha waziwazi kuwa pesa ilimpa kiburi.
Watu wenye uwezo wa kifedha(matajiri) wana mambo mengi sana nyuma yao ambayo sisi raia wengine hatuyajui..sasa unapotaka kushindana na mtu wa aina ile, wewe mwenyewe uwe umejipanga, na sio kujipanga kwa pesa, bali ujipange kwa mambo mengine.. Bado mzee j4 aliendelea kufunguka kwa mwanae huyu..
Sasa kwa mfano kama sio mimi kukuokoa pale, wewe ulikua unaharisha mpaka kifo chako, unafikiri ingekuaje? Alihoji Mzee J4 kumuuliza Kulwa ambaye kwa muda wote huo alikua anatafuta haswa Mzee J4 anataka kuongea kipi haswa, na sasa anaonekana kupata picha ya nini Mzee J4 anamaanisha..
Kama mtu anaweza kumuua mkewe, atashindwa kukuua wewe? Ndivyo alivyozidi kugongelea msumari wa moto Mzee J4 katika kichwa cha Kulwa.. Mzee J4 aliongea maneno haya mfululizi akiwa hataki kumpa nafasi Kulwa kuchangia.. Kisha akamalizia kwa kumwambia..Jambo ambalo limeshatokea kama hivi, usipende sana kwenda kinyume na utaratibu uliozoeleka, hutaonekana SHUJAA bali KICHAA.. sasa kwa mfano ungegundua kuwa Sauda alipewa sumu akafa, na aliyemuua ni mumewe, wewe si ungetengeneza uhasama na Khatib? Na unahisi ungekua na mwisho mzuri? Hebu saa zingine weka mbali MATAMANIO ya nafsi yako, na uangalie UHALISIA ukoje, nakutakia safari njema Alimalizia maneno hayo Mzee J4 akampa mkono Kulwa kisha yeye akawa ndiye wa kwnza kutangulia ndani..
Kulwa alibaki pale nje akitafakari kwa kina maneno aliyoambiwa na Mjomba wake, ambaye hakumpa hata nafasi ya kujieleza au kuuliza swali.
*******************************
Hello My lovely Husband..
I miss you so much my..
I wish I could see you this weekend..
It has been a long time now..
I love you so much..bye
Ilikua ni short and clear e-mail ambayo ilikua imetumwa kwenye e-mail address ya Mr Khatib 26th May, siku tano kabla ya Arobaini ya Sauda.. aliisoma barua pepe hii na kushika kichwa, kwani hiyo ilikua ni siku ya Jumatano, na email ilitamani ndani ya weekend waonane..Alijikuta katika wakati mgumu sana..Jumapili ilikua ndio siku ya 40 tangu Sauda kufariki, na maandalizi ya kumalizia huu msiba yalishafanyika yote na kila kitu kikiwa tayari, yeye kama Mume wa marehemu aligharamia kila kitu kinachohusu chakula kwa ajili ya siku hiyo. Alianza kujiuliza itakuaje endapo hatoonekana katika 40 ile..zaidi ya kuonekana msaliti na penginepo zile hisia za kuwa amemuua mkewe huenda zikaibuka upya. Na vipi kuhusu mtumaji wa ile email??!! Ambaye anaonyesha ni mkewe?..
Hisham, mi naona uniwakilishe tu ifikapo Jumapili, kila kitu nimetoa, na kwa asilimia 85 za hiyo shughuli nzima ni pesa zinazotoka mfukoni mwangu, sasa kama bado wataendlea kunilaumu waache tu Maneno yaliyotoka kinywani kwa Khatib akiongea na Hisham usiku wa Ijumaa kwani Khatib alipanga kuondoka Jumamosi asubuhi kuelekea nchini Canada kuonana na mama Camilla Hellen, Manager wa Camihel Bank of Commerce (CBC) iliyokuwepo Jijini Vancouver.
Kusema ni kawaida ya waswahili, we nenda tu boss, mi niache nao tu hawa waswahili nitamalizana nao.. Maneno ya Hisham Omar Mikidad akimtoa wasiwasi Khatib ili afanye kama alivyotakiwa kufanya.
Kitu ambacho kilionekana hapa ni kuwa email ile haikuwa inaomba kukutana na Khatib, bali ilikua ni 'order' ya kuonana na Khatib. Kwani kama si hivyo Khatib asingekubali kuacha shughuli ya mkewe na kupanda ndege kuelekea Canada kipindi kile..lazma palikua pana zaidi ya ambavyo wtu wote wanawez kufikria.
Sawa kaka, nashukuru sana, kila la kheri na tutaonana tena baada ya wiki mbili nadhani ndivyo alivyoaga Khatib kwa Hisham..
Ila kabla hawajaachana, Khatib alionekana kukumbuka kitu, Hisham ambaye wakati huu alishafungua mlango wa gari yake tayari kwa kuondoka, alimuona Khatib akimnyemelea kama anayetaka kumwambia kitu..
Vipi boss, kuna kitu umesahau??
Yeah Hisham, unajua ni wewe pekee ndiye unayejua siri zangu nyingi, nakuamini kama ndugu yangu, maana kwa sasa sisi tumekua si marafiki tu, au watu tunaoshirikiana kwenye biashara, bali tumekuwa ndugu kabisa.. Khatib kwanza alianza kueleza ukaribu wao kati yake yeye na Hisham ili kumueka tayari aweze kupokea atakaloelezwa.
Mimi naamini hakuna siku wewe Hisham utakuja kunisaliti, na ndio maana nakutumia wewe zaidi katika mambo yangu mengi kuliko Haroun..na hata malipo yako ni makubwa zaid kuliko ya Haroun.. Khatib aliendelea kuiweka sawa akili ya Hisham kabla hajaongea kile alilolikusudia haswa..
Can't you see? Wewe ni Manager wa Pub na unakula pesa nyingi zaid kuliko Manager wa Hotel kubwa kiasi kile..!?? Hii inadhihirisha imani yangu kwako..nakukubali sana bro
Boss,mi nashkuru sana kwa kunikubali, wewe ndiye rafiki pekee uliyefanya Hisham akawa mtu aliye hivi sasa..sipati picha kama si wewe mi ningekua na maisha gani sasa..hawa jamaa wajinga si wangeendelea kunifanya 'punda' mpaka leo,? Nawaingizia wao pesa nyingi mimi nakula hela ya mbuzi, kila siku nikiwa na hamu ya kurudi tena kuwakusanyia wao mzigo..Jambo baya zaidi nilikua nawaza siku hiyo vitakaponipasukia tumboni..sijui ingekuaje?.. Kaka, mi nakushukuru sana, kukusaliti wewe ni sawa na kuisaliti nafsi yangu mwenyewe..SIWEZI KUFANYA HIVYO Hisham aliongea maneno haya kwa hisia, akimueleza Khatib umuhimu wake kwake..
Hebu nambie boss, ni kitu gani hicho haswa unataka kunieleza boss wangu, mi ndo mtu wako pekee wa kunieleza kuhusu habari zako nyeti..
Kuna siri moja nzito sana nataka kukueleza kaka, maana mi nasafiri na sijui huko ninakoenda patakuaje..na huku nyuma naacha mambo mengi sana ambayo yananihitajia..majukumu yamekua mengi, mambo mengine ambayo yalikua siri yangu tu, sina budi kukupunguzia, ili kwa kipindi kama hiki ambacho sipo basi unaweza ukasimamia na ukasaidia pale panapohitajia msaada.. Alianza kufunguka Mr Khatib, kisha akaendelea..
Mtu ukiwa maarufu na tajiri, unakua na siri nyingi sana ambazo usingependa watu wazifahamu, ni kwa sababu ya kulinda ile REAL IDENTITY yako..kwa sababu mimi binafsi naishi kwa FAKE HISTORY hapa duniani..na kama itatokea jamii ikajua historia yangu halisi, basi nitakua katika wakati mgumu sana..
Naelewa boss, nami naahidi kuwa pamoja na wewe mpaka kufa Hisham alikuwa akipenda sana jinsi Khatib anavyomuheshimu na kumchukulia kama ndugu yake, hakuwa na malipo kwa Khatib zaid ya kufanya vile anavyovihitaji tu..
Hivi mbali na umbea umbea ambao alikua analeta, unafikiri sababu nyingine ya mimi kumuua Sauda inaweza kuwa ni nini? Khatib aliamua kuanza kile anachotaka kumwambia Hisham kwa swali lile..
Hisham akainamisha kichwa chini akitafakari nini kinaweza kuwa sababu ya kifo cha Sauda zaidi ya ile ambayo anaifahamu yeye, kuwa Sauda alihoji uhalisia wake. Alitafakari kwa muda kidogo kisha akanyanyua kichwa na kumwangalia Khatib kisha akasema Hapana, sifahamu boss..
Khatib akamuangalia Hisham usoni ambaye alionekana kuwa na shauku ya kujua ni nini haswa undani wa kifo cha Sauda..
Sasa nisikilize kwa makini sana, ila kabla sijaanza kukueleza, hebu save hii namba katika simu yako.. Aliongea Khatib akimkabidhi simu yake Hisham ambayo alikua ameandika namba za simu ambazo Hisham alitakiwa kusave..
Ok, boss..niandike Jina gani?
Kwani namba yangu ya simu umesave kwa jina gani?
Nimeandika Boss
Basi hiyo andika Khatib
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Unakosaje Episode 12??
Unajua ni siri gani nzito ipo hapo?..
Follow IG:
Sir_mdharubajk
Maoni: +255718274130