Mdharuba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2011
- 824
- 522
- Thread starter
- #21
STORY: Historia Batili-Fake History.
MTUNZI:Jumaa Khatib Mdharuba
+255 718 274 130
SEASON 01-EPISODE O4
★★★★★★★★★★★★★★
Alice, dada anayekuwa reception katika zamu ya mchana hapa Euler Hotel alikua akijiuliza maswali mengi sana juu ya huyu bwana Khatib ambaye alionekana wazi kutoeleweka..Alipendelea kuja hapa na mkewe Sauda mara kwa mara na kulala naye mpaka wakawa wamemzoea, lakini baada ya Alice kupafahamu nyumbani kwa Khatib ndo akaanza kupata mashaka nae..Nyumba ilikua kubwa ya kifahari ambayo ilikua na kila kitu au zaidi ya vile alivyokua anapata pale Euler Hotel..Sasa kwanini aache kulala nyumbani kwake na aje alipie laki 1.5 kwa Executive room per day na alikua anakaa zaidi ya wiki moja pale hotelini sometymz..
Kingine kilichompa mawazo zaidi ni kwanini Haroun ambaye ndiye Manager wa hii hoteli alikua akimuheshimu sana Khatib, na mara zote alipokuja alikua na kawaida ya kumkaribisha ofisini kwake na walikua wakiongea kwa zaidi ya dakika 30!!
Maswali haya ya Alice hakuna aliyeweza kuyajibu zaidi ya kujaribu kupotezea tu..ila leo alishtuka zaidi kwa maana hakumuona Khatib siku nyingi pale hotelini halafu pia amekuja peke yake wakati si kawaida yake. Kama hiyo haitoshi, moja kwa moja ameenda ofisini kwa Manager pale ghorofa ya tano.. Akaamua kumshirikisha Florah, ambaye walikua wote reception zamu ya mchana..!!
"Huyu Khatib ww unamuelewa Florah?"
"Kivipi Alice wee..mbona utakua mmbea mtoto wa kike wee..mi namuona kawaida tu"
"Ana dili gani na boss, mbona wanajifungia kila siku pale ofisi ya juu halafu hatujui wanaongea nini?" Alice alionekana ni mfuatiliaji mzuri sana kwa mujibu wa maelezo haya..
"Babu wee..wote hao wana mapesa yao..usishindane nao, itakua wana dili zao.." Florah alijibu kimkato tu wala hakuwa na mda wa kufatilia kwa undani juu ya kile alichoelezwa na Alice..Ila moyoni kwa Alice bado alitamani kufahamu uhusiano uliopo kati ya Haroun na Khatib..
Akaamua amsubiri Mr.Khatib akitoka ajaribu kumdodosa huenda akapata mwanga juu ya ayawazayo.
Na baada ya dakika 27 Khatib alipita reception akielekea nje alikopark gari yake..
"Samahani boss" Ilikua ni sauti ya Alice akimuelekea Khatib akionekana kutaka kumuuliza kitu..
"Yes Alice Nemhina Tupa, una tatizo?" Aliitika Mr.Khatib na kumfanya Alice ashtuke kidogo, Ni kwel anajua kuwa Khatib anamfahamu, lakin sio hadi jina la babaake na la ukoo..akabaki mdomo wazi hajui huyu mtu kajuaje jina lake kamili wakati hapa kazini yeye alijulikana kwa jina moja tu la Alice.
"Sijakuona siku nyingi boss ulikua waapi? Afu naona wife nae hujaja nae leo..nashangaa umeongea tu na boss Haroun afu unatoka, vipi kwema?" Aliuliza maswali haya Alice ambayo cdhani hata kama angejibiwa angepata faida gani..
Khatib alisimama kidogo akamwangalia sana Alice kisha akamjibu kifupi "Ntarudi baadae" akaingiza mkono mfukoni na kumkabidhi Alice sh elf 80, "Naomba tukutane Mambo pub leo saa 3 usiku" Ndio maneno yaliyofuatia baada ya kukabidhiwa pesa ile kisha akatoa business card na kumkabidhi.
Alice Kabla hajajibu chochote Khatib alishavuta hatua hadi katika mlango wa gari lake na kuzama ndani akawasha gari na kuondoka kwa kasi sana.
★★★★★★★★★★★★★★ "MORO 9pm URGENT" Ndivyo ilivyosomeka sms aliyoipata Noor A Mdharuba soon baada ya Khatib kutoka pale hotelini. Ilijieleza vizuri kuwa alitakiwa awepo Moro kabla ya saa 3 usiku na ilikua ni muhimu sana. Noor alishaelewa..na hakuchukua muda sana akawa yuko barabarani akitokea Dar kwenda Moro..
Alifika Morogoro majira ya saa 1 usiku na moja kwa moja akafikia Euler Hotel akapata chakula cha jioni kisha akazama chumbani kujipumzisha.
Khatib alikuwa nyumbani kwake muda huu akijaribu kumpa maelekezo Noor juu ya nini cha kufanya kwa kutumia sms..
"0714261861; Alice; P-Wp;Mb;21😀c" Hiyo ndiyo ilikua msg yenye maelekezo yote juu ya kipi Noor alitakiwa kufanya hapa Moro, hakukuwa na haja ya kuonana na Khatib sababu kila kitu kilijieleza katika msg ile.
0714261861 ilikua ni namba ya simu ya mkononi ya Hisham Omar Mikidadi Manager wa Mambo pub ambayo ilikua ikimilikiwa na Mr.Khatib na siri hii alikua akiijua Hisham peke yake, Hisham pia alifaham uhusiano uliopo kati ya Noor na Khatib ingawa hawakuwahi kuonana ana kwa ana hata siku moja, ilikua ni lazima Hisham atambue uwepo wa Noor Mambo pub jioni ya leo.
Alice ndo mtu ambaye alitakiwa kudeal nae.
P-Wp: Ni maelekezo kuwa picha ya Alice ataituma kupitia whatsap.
Mb: Ni initial waliotumia kuashiria Mambo Pub ambayo ndio sehemu aliyoambiwa Alice akutane na Khatib.
21: Inaashiria tatu usiku kuwa ndo muda wa promise.
Dc; Ni maelekezo kuwa Noor alitakiwa afanye nae mahojiano ya kina sana..
★★★★★★★★★★★★★★
"Vipi kazi yako mke wangu? Umeianza vizuri?" Alihoji Mr.Khatib wakati huu wakiwa kitandani na mkewe Sauda.
"Yeah, nashukuru..ila umenisuprise sana, daah siamini yani"
"Kawaida tu, mpango huo nlikua nao tangu siku nyingi ila nilikua navuta subra kwnza.."
"Ok, sawa.. thanks kwa kutambua umuhimu wangu, mi nilikua nachukia sana kukaa nyumbani muda wote, atleast now ntakua na amani kidogo"
"Ok sawa, nakupenda saana.."
"Huna lolote, ungenipenda sana ungeniwekea ratiba??" Sauda alianza utani wa kweli na kumfanya Khatib awe mpole..
Maneno haya yaliashiria leo huduma ilitakiwa hapa ndani ingawa haikuwa ratiba yake. Lakin kwa jambo alilokusudia kulifanya usiku ule, ilibidi abadili msimamo wake..
"Ucjal, usiku wa leo lazima uukumbuke"
Na baada ya ahadi hii ndipo Khatib alipoanzisha purukushani za hapa na pale katika kuhakikisha panakua na dibaji ya maana kabla ya kuanza chapter ya kwnza na kuendlea.
Ni siku ambayo bwana huyu alitoa vitu adimu sana kwa bi mdogo yule na kumfanya kupayuka mijineno mengi isiyo na maana. Usiku ukaisha vizuri kabisa wote wakiwa hoi lakini kwa furaha.
"Ikiwa hivi kila siku hata ukiondoka mwezi usipoaga mi sina neno, ila ww hunipi huduma kama hizi kwa ukamilifu halafu waondoka, mi napata wivu najua unaenda kuwapa wengine huko"
Maneno yaliyomtoka bi Sauda asubuhi baada ya kumuamsha mumewe ili akaoge.
Mr.Khatib alimwangalia kisha akatabasamu bila kuongea neno lolote.
★★★★★★★★★★★★★★
"Haya nambie boss, ni kazi gani maalum iliyokuleta hapa leo, maana najua wewe Khatib anakutumia kwa kazi maalum tu." Hisham aliongea baada ya kufahamiana na Noor kwa sura sasa, wakiwa katika meza fulani iliyozungukwa na viti vitatu ndani ya Mambo pub, ilikua ni majira ya saa 2:19 usiku.
"Kuna bint anaitwa Alice nimekuja kufanya mahojiano nae maalum".
"Vipi ameleta kujifanya kujua?" Alihoji Hisham akiwa na hamu ya kujua nini kinaendelea hapa.
"Yaah alijaribu kumuuliza boss nahis kuhusu vtu flan vilivyoashiria kumfuatilia, maana amenambia nifanye nae deep conversation."
"Okay, kama ameanza kuleta kidomodomo poteza tu" Alisema Hisham ambaye alionekana kuwa hakua hata na chembe ya huruma.
"Ntaangalia mahojiano yetu yatakavyokua maana sometymz lisilo budi hutendwa" Aliongea kwa busara kidogo Mr.Khatib.
"Wewe unaremba sana, watu hawa ni hatari sana zaidi ya Ebola, wanatakiwa kufa mapema kabla ya kuambukiza wengine.." Bado aliendelea kusisitiza Hisham Omari Mikidadi, safari hii akigonga meza na ngumi na kunyanyuka kuelekea ofisini kwake ndani ya pub ile.
★★★★★★★★★★★★★★
Don't Miss Episode O5
MTUNZI:Jumaa Khatib Mdharuba
+255 718 274 130
SEASON 01-EPISODE O4
★★★★★★★★★★★★★★
Alice, dada anayekuwa reception katika zamu ya mchana hapa Euler Hotel alikua akijiuliza maswali mengi sana juu ya huyu bwana Khatib ambaye alionekana wazi kutoeleweka..Alipendelea kuja hapa na mkewe Sauda mara kwa mara na kulala naye mpaka wakawa wamemzoea, lakini baada ya Alice kupafahamu nyumbani kwa Khatib ndo akaanza kupata mashaka nae..Nyumba ilikua kubwa ya kifahari ambayo ilikua na kila kitu au zaidi ya vile alivyokua anapata pale Euler Hotel..Sasa kwanini aache kulala nyumbani kwake na aje alipie laki 1.5 kwa Executive room per day na alikua anakaa zaidi ya wiki moja pale hotelini sometymz..
Kingine kilichompa mawazo zaidi ni kwanini Haroun ambaye ndiye Manager wa hii hoteli alikua akimuheshimu sana Khatib, na mara zote alipokuja alikua na kawaida ya kumkaribisha ofisini kwake na walikua wakiongea kwa zaidi ya dakika 30!!
Maswali haya ya Alice hakuna aliyeweza kuyajibu zaidi ya kujaribu kupotezea tu..ila leo alishtuka zaidi kwa maana hakumuona Khatib siku nyingi pale hotelini halafu pia amekuja peke yake wakati si kawaida yake. Kama hiyo haitoshi, moja kwa moja ameenda ofisini kwa Manager pale ghorofa ya tano.. Akaamua kumshirikisha Florah, ambaye walikua wote reception zamu ya mchana..!!
"Huyu Khatib ww unamuelewa Florah?"
"Kivipi Alice wee..mbona utakua mmbea mtoto wa kike wee..mi namuona kawaida tu"
"Ana dili gani na boss, mbona wanajifungia kila siku pale ofisi ya juu halafu hatujui wanaongea nini?" Alice alionekana ni mfuatiliaji mzuri sana kwa mujibu wa maelezo haya..
"Babu wee..wote hao wana mapesa yao..usishindane nao, itakua wana dili zao.." Florah alijibu kimkato tu wala hakuwa na mda wa kufatilia kwa undani juu ya kile alichoelezwa na Alice..Ila moyoni kwa Alice bado alitamani kufahamu uhusiano uliopo kati ya Haroun na Khatib..
Akaamua amsubiri Mr.Khatib akitoka ajaribu kumdodosa huenda akapata mwanga juu ya ayawazayo.
Na baada ya dakika 27 Khatib alipita reception akielekea nje alikopark gari yake..
"Samahani boss" Ilikua ni sauti ya Alice akimuelekea Khatib akionekana kutaka kumuuliza kitu..
"Yes Alice Nemhina Tupa, una tatizo?" Aliitika Mr.Khatib na kumfanya Alice ashtuke kidogo, Ni kwel anajua kuwa Khatib anamfahamu, lakin sio hadi jina la babaake na la ukoo..akabaki mdomo wazi hajui huyu mtu kajuaje jina lake kamili wakati hapa kazini yeye alijulikana kwa jina moja tu la Alice.
"Sijakuona siku nyingi boss ulikua waapi? Afu naona wife nae hujaja nae leo..nashangaa umeongea tu na boss Haroun afu unatoka, vipi kwema?" Aliuliza maswali haya Alice ambayo cdhani hata kama angejibiwa angepata faida gani..
Khatib alisimama kidogo akamwangalia sana Alice kisha akamjibu kifupi "Ntarudi baadae" akaingiza mkono mfukoni na kumkabidhi Alice sh elf 80, "Naomba tukutane Mambo pub leo saa 3 usiku" Ndio maneno yaliyofuatia baada ya kukabidhiwa pesa ile kisha akatoa business card na kumkabidhi.
Alice Kabla hajajibu chochote Khatib alishavuta hatua hadi katika mlango wa gari lake na kuzama ndani akawasha gari na kuondoka kwa kasi sana.
★★★★★★★★★★★★★★ "MORO 9pm URGENT" Ndivyo ilivyosomeka sms aliyoipata Noor A Mdharuba soon baada ya Khatib kutoka pale hotelini. Ilijieleza vizuri kuwa alitakiwa awepo Moro kabla ya saa 3 usiku na ilikua ni muhimu sana. Noor alishaelewa..na hakuchukua muda sana akawa yuko barabarani akitokea Dar kwenda Moro..
Alifika Morogoro majira ya saa 1 usiku na moja kwa moja akafikia Euler Hotel akapata chakula cha jioni kisha akazama chumbani kujipumzisha.
Khatib alikuwa nyumbani kwake muda huu akijaribu kumpa maelekezo Noor juu ya nini cha kufanya kwa kutumia sms..
"0714261861; Alice; P-Wp;Mb;21😀c" Hiyo ndiyo ilikua msg yenye maelekezo yote juu ya kipi Noor alitakiwa kufanya hapa Moro, hakukuwa na haja ya kuonana na Khatib sababu kila kitu kilijieleza katika msg ile.
0714261861 ilikua ni namba ya simu ya mkononi ya Hisham Omar Mikidadi Manager wa Mambo pub ambayo ilikua ikimilikiwa na Mr.Khatib na siri hii alikua akiijua Hisham peke yake, Hisham pia alifaham uhusiano uliopo kati ya Noor na Khatib ingawa hawakuwahi kuonana ana kwa ana hata siku moja, ilikua ni lazima Hisham atambue uwepo wa Noor Mambo pub jioni ya leo.
Alice ndo mtu ambaye alitakiwa kudeal nae.
P-Wp: Ni maelekezo kuwa picha ya Alice ataituma kupitia whatsap.
Mb: Ni initial waliotumia kuashiria Mambo Pub ambayo ndio sehemu aliyoambiwa Alice akutane na Khatib.
21: Inaashiria tatu usiku kuwa ndo muda wa promise.
Dc; Ni maelekezo kuwa Noor alitakiwa afanye nae mahojiano ya kina sana..
★★★★★★★★★★★★★★
"Vipi kazi yako mke wangu? Umeianza vizuri?" Alihoji Mr.Khatib wakati huu wakiwa kitandani na mkewe Sauda.
"Yeah, nashukuru..ila umenisuprise sana, daah siamini yani"
"Kawaida tu, mpango huo nlikua nao tangu siku nyingi ila nilikua navuta subra kwnza.."
"Ok, sawa.. thanks kwa kutambua umuhimu wangu, mi nilikua nachukia sana kukaa nyumbani muda wote, atleast now ntakua na amani kidogo"
"Ok sawa, nakupenda saana.."
"Huna lolote, ungenipenda sana ungeniwekea ratiba??" Sauda alianza utani wa kweli na kumfanya Khatib awe mpole..
Maneno haya yaliashiria leo huduma ilitakiwa hapa ndani ingawa haikuwa ratiba yake. Lakin kwa jambo alilokusudia kulifanya usiku ule, ilibidi abadili msimamo wake..
"Ucjal, usiku wa leo lazima uukumbuke"
Na baada ya ahadi hii ndipo Khatib alipoanzisha purukushani za hapa na pale katika kuhakikisha panakua na dibaji ya maana kabla ya kuanza chapter ya kwnza na kuendlea.
Ni siku ambayo bwana huyu alitoa vitu adimu sana kwa bi mdogo yule na kumfanya kupayuka mijineno mengi isiyo na maana. Usiku ukaisha vizuri kabisa wote wakiwa hoi lakini kwa furaha.
"Ikiwa hivi kila siku hata ukiondoka mwezi usipoaga mi sina neno, ila ww hunipi huduma kama hizi kwa ukamilifu halafu waondoka, mi napata wivu najua unaenda kuwapa wengine huko"
Maneno yaliyomtoka bi Sauda asubuhi baada ya kumuamsha mumewe ili akaoge.
Mr.Khatib alimwangalia kisha akatabasamu bila kuongea neno lolote.
★★★★★★★★★★★★★★
"Haya nambie boss, ni kazi gani maalum iliyokuleta hapa leo, maana najua wewe Khatib anakutumia kwa kazi maalum tu." Hisham aliongea baada ya kufahamiana na Noor kwa sura sasa, wakiwa katika meza fulani iliyozungukwa na viti vitatu ndani ya Mambo pub, ilikua ni majira ya saa 2:19 usiku.
"Kuna bint anaitwa Alice nimekuja kufanya mahojiano nae maalum".
"Vipi ameleta kujifanya kujua?" Alihoji Hisham akiwa na hamu ya kujua nini kinaendelea hapa.
"Yaah alijaribu kumuuliza boss nahis kuhusu vtu flan vilivyoashiria kumfuatilia, maana amenambia nifanye nae deep conversation."
"Okay, kama ameanza kuleta kidomodomo poteza tu" Alisema Hisham ambaye alionekana kuwa hakua hata na chembe ya huruma.
"Ntaangalia mahojiano yetu yatakavyokua maana sometymz lisilo budi hutendwa" Aliongea kwa busara kidogo Mr.Khatib.
"Wewe unaremba sana, watu hawa ni hatari sana zaidi ya Ebola, wanatakiwa kufa mapema kabla ya kuambukiza wengine.." Bado aliendelea kusisitiza Hisham Omari Mikidadi, safari hii akigonga meza na ngumi na kunyanyuka kuelekea ofisini kwake ndani ya pub ile.
★★★★★★★★★★★★★★
Don't Miss Episode O5