Historia batili: Riwaya mpya na JK episode 02

Historia batili: Riwaya mpya na JK episode 02

Jiandae kusoma kitabu soon ..

Hopefully hicho kitabu hakitakuwa compillation ya hizi series zako!! Kama utakusanya hizi series tulizokwisha kusoma na ndio kiwe kitabu hakutakuwa na haja ya sisi kukinunua!!
 
Ni mojawapo ya simulizi tamu nilizowahi kuzisoma. Miongoni mwa vitu ninavyofurahia katika hii simulizi ni
1.Mpangilio mzuri wa visa na matukio
2. Uhalisia wa mambo hasa uhai unaojionesha katka mazungumzo ya wahusika
3.na kubwa kuliko yote ni kiswahili maridhawa kinachotumika na hata kiingereza hukaa mahali sahihi.
OMBI: Jitahidi utukarimu episodes kwa wakati na ikiwezekana uunganishe threads.
 
SEASON O1-EPISODE O5
★★★★★★★★★★★★★★
"Haloo, kama zali yani, Khatib amenipa pesa na kunambia tukutane Mambo pub saa 3 usiku wa leo.." Ni sauti ya Alice katika sikio la bwana Ahmed Khamis Hamad.
"Mwanzo mzuri huo" Aliongea Ahmed na kuongeza.."Nenda nipo nyuma yako" kisha akakata simu.
Ahmed Khamis alikua kijana mmoja shupavu aliyekuwa anafundisha Somo la Stadi za kazi katika shule ya Msingi Mazimbu na pia alikua ndio Mwalimu wa Michezo katika shule hii.
Ila Ahmed alikua akifanya kazi pia kama Afisa usalama wa serikali ya Tanzania. Aliifanya kazi hii kwa miaka saba sasa lakini hakuna aliyekuwa anatambua hilo.
Baada ya kukabidhiwa jukumu la kufuatilia juu ya utajiri wa Mr.Khatib, ndipo alipokutana na Alice na njia pekee ya kumrubuni Alice ilikua ni kumtongoza awe mpenzi wke ili aweze kumtumia vizuri katika harakati zake.
Alishampa HISTORIA BATILI Alice kuhusu yeye(Ahmed) na Khatib na kudai kuwa Khatib aliwahi kutumia pesa zake nyingi kumrubuni mkewe mpaka wakafikia hatua ya kuachana. Kwahy kwa sasa alitaka kujua undani wake ili amchongee polisi aje amkamatishe katika mikono ya dola. Alice, kwa sababu ya uaminifu aliokuwa akionyeshwa na Ahmed na jinsi alivyokuwa akipewa pesa kila alipohitaji na saa zngne hta kabla hajaomba, alijikuta akimpenda sana mwalimu yule wa michezo. Akawa anafanya vile ambavyo Ahmed alimtuma kufanya.
Alice alikua akifanya mambo kwa upande mmoja akiwa hajui kuwa alikua akitumika vibaya. Upofu wake katika kupenda ulimfanya awe ----- sana na hakuwa hata na muda wa kufikiria katika alichoambiwa. Mwenzie Ahmed alishajua kuwa Khatib ni mtu hatari na anaweza kufanya chochote, kwahyo Alice akishindwa kumsaidia kufanikisha kazi angetafuta mtu mwengine ambaye angemtumia kama msaada. Hata kama Alice angeuawa hilo si jambo geni kwake, alishazoea..
********************
Alice alifika pale Mambo pub majira ya saa 2:56 usiku na moja kwa moja akatafuta meza ambayo ilikua haina mtu akafika na kukaa kwenye kimoja kati ya viti vilivyoizunguka meza ile.
"Unatumia kinywaji gani?" Swali lililotoka kwa mmoja kati ya wahudum wa pub ile..
"Naomba Kuku nusu"
Akakaa pale kwa muda wa dakika 6 na kushika simu yake na kuanza kupiga namba za Khatib. Simu haikupokelewa na badala yake ilikatwa kisha meseji ikaingia ikisomeka "Am driving, on my way to Mambo Pub, plz wait for me..i'll be there within 15 minutes" . Baada ya kusoma msg hii akaifoward kwa Ahmed kisha akaweka simu katika pochi yake ndogo na kuendlea kugonga kuku wake bila hata woga.
"Naweza kukupa kampani,? naona upo peke yako" Aliulza bwana Noor baada ya kufika katika meza ya bi Alice huku akimuangalia vizuri usoni kuhakikisha"
"Mmmh...aaaah.. kuna mtu namsubiria bado hajafika, unaweza kunipa kampani mpka atakapokuja" Alijibu Alice, tatizo lake kubwa Alice alikua hajui kukataa hasa pale anapoona dalili za pesa.
"Ok, asante sana.."
Alikaa pale bwana Noor na kuanza story za hapa na pale na bi Alice.
"Umesema unamsubiri nani vilee maana nshasahau eti mara moja hii.." Noor aliuliza swali la kimtego akijidai kama vile aliyetajiwa jina mwanzoni..hapa alikua anatafta pa kuanzia..
"Yaani nina promise na Mr.Khatib yule wa Saukhat Investment Company.. si unamjua??" Aliingia mzima mzima Alice pale alipokusudiwa kufika.. akiwa hajui kuwa maongezi haya yanasikika moja kwa moja katika sikio la Khatib kupitia earphone alizovaa akiwa kitandani na mkewe.
"Nasikia yule bwana ana pesa vibaya sana ila watu hawajui anafanya biashara gani haswa" Alianza kuchochea Noor.
"Yule ni balaa..kama sio unga sijuuii.. , maana nina waswas ile Euler hotel pia anamiliki yeye" Alijiachia Alice akiwa hana hili wala lile.
"Labda alirithi mali nyingi sana, maana nasikia babaake alikua tajiri mkubwa sana halafu alizaa watoto wawili tu" Noor Alijaribu kuigusia fake history kuangalia Alice anaichukuliaje..
"Sidhani, hata kama ni hivyo itakua bdo ana kitu cha ziada yule..Unajua kwanin nakwambia hvyo?? Yule anaweza akapotea hata mwezi nasikia hajulikani yuko wapi? Afu mbaya zaid hadi mkewe hajui..Naskia anapata tabu kweli mtoto wa watu anatafta mpka anakoma" Maelezo haya ya Alice yalianza kumpa picha flani Noor..lakin bdo akaendelea kuchimba zaid..
"Kwahyo unataka kunambia hyu mtu anaweza kuwa ni mafia?"
"Inawezekna maana nasikia pia ni mbabe, akitaka lake ndo hilo hlo..kwa mfano mi yule boyfriend wangu alishamgombanisha na mkewe..halafu baadae yule mwanamke alimtumia watu wamuue.." Maneno haya ya Alice yakampa picha Noor kuwa huyu Alice yupo nyuma ya mtu flani..Sababu Historia hii anayompa sasa ni ya kutunga-FAKE HISTORY. Mpaka hapa hakukuwa na sababu ya kumuacha Alice mzima, ingawa alitakiwa kufanikisha kumjua nani hyo yuko nyuma ya Alice..
"Yaaah nshawahi kusikia kitu kama hicho, ila huyo jamaa tu ndo simjui..na nasikia yupo Morogoro hii hii.." Noor aliongea kwa kujiamini na kuonyesha kuwa si mgeni na hizi habari ili apate kujua undani wa habari hii..wkati huu Noor alishamnunulia Alice pombe kali na kujikuta ameshasahau pia kuwa alikuja pale kwa madhumuni yapi.!!
"Boyfriend wangu ni mwalimu wa Michezo shule ya Msingi...." Kabla hajamalizia sentensi hii Alice alianguka pale alipokuwa amekaa huku damu nyingi zikimtoka kichwani..
★★★★★★★★★★★★★★
Mama Mdharuba, alianza kutilia mashaka juu ya mwanae Khatib kuhusu mambo anayoyafanya hivi karibuni. Na kabla mambo hayajawa mabaya aliamua kumuita mwanawe na kumpa onyo.
Pamoja na ubabe wke wote, Khatib hakuwahi kumdanganya mama yake kitu chochote..hivyo alipouliza kitu chochote na mama yake alikua hana option zaid ya kuongea ukweli!!.
Jumapili hii aliamua kuja kumuuliza maswali mawili matatu yahusuyo maisha yake kwa ujumla na mwenendo wke wa sasa.
"Nasikia sasa hivi umeanza kujiingiza katika biashara haramu mwanangu, ni kweli?" Aliuliza Mama Mdharuba wkat wako mezani wakipata chakula cha mchana..wakiwa na mdogo wake Khatib, Hawa ambaye alikua akiishi na mama yake katika jumba lile kubwa lililopo maeneo ya Mbezi.
Khatib alikaa kimya kana kwamba hajasikia swali hili..
"Siku zote nimekuwa nikikwmbia kuwa mimi sipendi niongee halafu ukae kimya..Naomba unijibu, unafanya biashara haramu au hufanyi?" Mama Mdharuba alianza kufoka.
"Mama nisikilize, hizo biashara sio zangu, ni za watu, mimi sina hata fungu katika hizo biashara mama!" Alijaribu kujitetea Mr.Khatib huku mamaake akimsikilza kwa makini.
"Siku zote nakwambi kuwa sitaki ushirikiane na watu wanaofanya biashara za haramu, sipendi na sitaki!! Kwanini hunisikilizi?? Mali zote hizo ulizokuwa nazo unatafuta nini tena mwanangu??"
Hapa Khatib alikuwa kama aliyemwagiwa maji ya baridi.
"Sasa ni hivii..ukirudi tena hapa nisikie umeacha hizo biashara zako za kipuuzi, la sivyo mimi na mwanangu tutakuachia nyumba yako turudi kuleee tulipotoka, nadhani unapakumbuka vizuri".Aliweka kituo kikubwa Mama Mdharuba na kumfanya Khatib azidi kutahayari.
"No mama plz usiseme hvyo.."
"Nasema hivyo sababu ya ujinga wako, mtoto mdogo namna hyo hata miaka 30 hujatimiza umekua na tamaa ya pesa kiasi hicho mpka unafanya biashara haram?? Sasa mi ntakukimbia..nakwambia hivyo.."
"Nimekuelewa mama, ntaachana nayo".
"Huyo mwenzio wa Canada ndo alokushawishi mfanye hiyo biashara??" Aliuliza swali la kizushi mama Mdharuba.
"Hapna mama, yeye hata hajui"
"Sasa ni nani mwengne mwenye uwezo wa kukushawishi?? kumbe wewe umekua mpuuzi siku hizi eeh?? Pumbaaavu" Alipatwa na hasira mama Mdharuba na kumzaba Khatib kibao cha shavu la kushoto.
★★★★★★★★★★★
 
Hopefully hicho kitabu hakitakuwa compillation ya hizi series zako!! Kama utakusanya hizi series tulizokwisha kusoma na ndio kiwe kitabu hakutakuwa na haja ya sisi kukinunua!!

Nina story nyingi sana kaka.. Hii nayo pia ni ndefu sana..hata nikiandka vitabu viwili bado siwezi kumaliza story..kwahy nikitoa kitabu hata nikirudia hii bado kuna haja ya kukisoma kwani hata niandke epsode 200 hapa story haitaisha..
Ila kitabu kitakua na story zngne mbili tofauti na hizi..
 
Ni mojawapo ya simulizi tamu nilizowahi kuzisoma. Miongoni mwa vitu ninavyofurahia katika hii simulizi ni
1.Mpangilio mzuri wa visa na matukio
2. Uhalisia wa mambo hasa uhai unaojionesha katka mazungumzo ya wahusika
3.na kubwa kuliko yote ni kiswahili maridhawa kinachotumika na hata kiingereza hukaa mahali sahihi.
OMBI: Jitahidi utukarimu episodes kwa wakati na ikiwezekana uunganishe threads.

Thanks for appreciation..
Nitajitahidi niwape episode 2 kwa siku..kila baada ya saa 12 natoa moja..

Bila shaka umesoma episode ya 6 mkuu..naleta ya 7 sasa hivi
 
Thanks for appreciation..
Nitajitahidi niwape episode 2 kwa siku..kila baada ya saa 12 natoa moja..

Bila shaka umesoma episode ya 6 mkuu..naleta ya 7 sasa hivi

Hiyo ya sita mbona haionekani?
 
STORY: HISTORIA BATILI(Fake History)
MTUNZI: Jumaa Khatib (Jk)
+255 718 274 130
+250 726 023 140

EPISODE O7
★★★★★★★★★★★★★★★
Baada ya kujihakikishia kuwa mumewe ni mtu tofauti na wengi wanavyomjua, Sauda aliamua kutunza maswali yake ili aje amuulize mumewe 'live' atakaporudi..
“Kwanini ananifichaficha vitu??” Alijiuliza swali hili moyoni mwake, akiamini alistahili kujua kila kitu kuhusu mumewe..
“Leo lazima atanieleza, au sivyo anipe talaka yangu, nimechoka mi, mwanaume gani asiyeeleweka?, kila siku nagundua mambo mapya tu..aaaghh” Bado alizidi kujipa tabu za mawazo bi Sauda akiupa tabu sana ubongo wake na kutaka kujua undani haswa wa mumewe..
*******************************
Kifo cha Alice kiliwashangaza wengi sana, kwa maana hakuna maelezo yoyte yaliyotolewa polisi juu ya nani aliyempiga risasi na kwanini apigwe risasi.. Kila mtu alibaki kuduwaa tu na kukosa kujua nini hasa kisa na mkasa..
Shoga yake Alice, Flora, alikua akilia saana pale msibani, akiwaza mambo mengi sana yaliyotokea jana tu alipokua na shoga yake Alice pale Euler Hotel, na mpaka wanaagana akimwambia kuwa ana promise na Mr.Khatib, akakumbuka pia maongezi yao mchana wa jana kuhusu Mr Khatib na jinsi Alice alivyomtilia mashaka, alibaki kulia tu!!. Wazo la haraka kichwani mwake ni kuwa Mr Khatib alihusika na kifo cha Alice, lakini atamwambia nani maneno haya?? Khatib alikua mpole sana mbele za watu, na alikua mtu wa watu haswa,, nani atakuelewa kuwa yeye alihusika na mauaji ya Alice wakati hata hakuepo kwenye tukio usiku ule..!!
Ukweli kuhusu kifo cha Alice waliufahamu askari, kwani aliyewapigia simu alikua ni Ahmed Khamis, afisa usalama wa Taifa,, na aliwaeleza pale ambapo Alice alifikia kutaka kutoa siri za Ahmed baada ya kulewa!! Kwa Ahmed, Alice alishakua useless, maana alifika pabaya, na dawa wakati ule ilikua moja tu-Kifo!! Na ndo kilichotokea, huo ukawa mwisho wa safari ya uzima wake aliyoianza miaka 25 iliyopita, “RIP Alice” ni maneno aliyoyatamka Ahmed kabla hajamfyatulia Alice risasi ya kichwa usiku ule..
Hakuna aliyehoji sana, kila mmoja alionekana si mhusika juu ya kifo cha Alice Tupa Nemhina, ni Florah pekee ndiye aliyeteseka na mawazo ya kila siku, na kila alipomuona Mr Khatib alikua akikumbuka maneno ya mwisho ya Alice juu ya promise ya kukutana na Mr Khatib na ndo ukawa mwisho wa Alice.. Aliteseka sana kimawazo, ila baadae alizoea, akibaki na siri ile moyoni mwake.
★★★★★★★★★★★★★★★★★
“Nataka unieleze ukweli, kuhusu hivi vitambulisho vyako” Alihoji Sauda baada ya kutoa vitambulisho kabatini na ile pasi ya kusafiria akimuonyesha Mr Khatib aliyekua amekaa mbele ya 'screen' ya Computer pale ndani ya chumba chao..
Khatib alionekana kushtushwa sana na taarifa hii, akaangalia vizuri documents zile za siri, kisha akamuangalia saana Sauda pasi na kumjibu chochote, akageukia screen ile na kuendelea na kazi zake..
“Khatib, naomba uniambie hivi vitambulisho mbona vina majina tofauti wakati sura ya kwako,?? Vipi haya mambo??.” aliendelea kuhoji Sauda alipoona Khatib hajangea kitu mwanzoni..
“Vitambulisho vina sura ya nani??” Alihoji Khatib baada ya 'kupata moto'
“Sura yako” Alijibu Sauda ambaye alikua haelewi kuwa kufahamu kuhusu vile vitambulisho ni kosa ambalo haliwezi kumbakiza tena duniani, yeye alikua anaona ana haki tu ya kuhoji chochote kuhusu mumewe..
“Sasa kama vina sura yangu wewe vinakuhusu nini mpaka kutaka kujua?”
“Mimi ni mkeo, nina haki ya kujua kila kitu kuhusu wewe, sababu ni mume wangu”..
“Pole sana, haki hiyo hapa kwangu umeikosa”
“Khatib naomba unieleze vizuri, sababu unavyoendelea kunificha utanifanya niondoke hapa bila kuaga”
“Nisikilize vizuri wewe mwanamke, tena nisikilize vizuri sana..” Alianza kuongea kwa msisitizo Mr Khatib na kufanya Sauda akodoe macho huku akitega masikio yake vizuri kutaka kujua Khatib anataka kuongea nini!!
“I was born ME, I and MySelf, you are now trying to change the word "ME" to be "US" something that will NEVER happen..”
“Anhaaa, kwahiyo mimi unanichukuliaje? Unanichukulia mimi mwehu, mwendawazimu, mpuuzi au malaya tu nsiyejielewa hapa?” Alihoji Sauda ambaye alishapanic wakati huu..
“Mimi nakuchukulia vyote vinne ulivyotaja, na cha tano ni kuwa wewe ni ---- pia, hiyo umeisahau”
Majibizano haya makali yaliendelea na kumfanya Sauda aone kuwa mumewe amebadilika saana siku hiyo tofauti na alivyomzoea.. Alipata tabu sana, alijitahidi 'kuchimba biti' vya kutosha lakini Khatib wala hakujali.. Akabaki analia tu. Mwishoni akanyamaza akapanda kitandani akiwa na hasira na mawazo tele, baadae akapitiwa na usingizi, akalala akimuacha Khatib katika kioo cha Computer pale chumbani..
Khatib alifikiria sana juu ya hatma ya yule mwanamke pale kitandani, akaanza kumuonea huruma, akakumbuka maneno ya babaake mdogo Noor akawa hana option.. Kulibaki jambo moja tu kutekelezwa mda ule, Sauda auwawe..
Alikaa pale mezani kwa mda mrefu sana akitafakari..baada ya muda mrefu kupita akanyanyuka na kufungua kabati, akazama chini kabisa akatia mkono akapapasa papasa akatoka na kikaratasi kidogo kilichofungwa vizuri..akakifungua akatoa unga uliokuwemo mle ndani, akikamata na vidole vyake viwili,cha gumba na kinachofuatia..akaenda kumpaka Sauda karibu na tundu zake za pua..
*******************************
Kosa kubwa ambalo alilifanya sauda ni haraka ya kutaka kujua mambo yanayomuhusu huyu mumewe..Licha ya kuwa alishaona dalili za wazi kuwa huyu si mtu wa kawaida..hakujali, alidhani anaweza kucontrol maisha yao na wakaishi kama mke na mume wanaopendana sana..Kumbe alikosea..kwa Khatib haikua hivyo, ni tofauti sana..,, Khatib alikua anamuona kila mtu ni adui yake, yeyote anayetaka kujua undani wa maisha yake basi hakuwa na mwisho mzuri, na ndo kinachomkuta Sauda kwa sasa..Khatib aliona dalili za wazi za Sauda kutaka kufuatilia maisha yake, na ndio maana kwa miaka yote miwili aligoma kabisa kuzaa nae..Angewezaje kumuua mama wa mtoto wake?? Baadae atajibu vipi maswali ya mwanae kuhusu mama yake??!! Aliamua kumchunguza kwa undani kwanza.. Na haya ndo matokeo ya uchunguzi..ameamua kumuua..kwa sumu ya unga ambayo anaivuta kupitia pumzi anazoingiza mwilini..ndani ya dakika 10 tu tangu kupakwa ule unga Sauda alishafariki
★★★★★★★★★★★★★★★★★★

Dont Miss Episode O8
 
Nina story nyingi sana kaka.. Hii nayo pia ni ndefu sana..hata nikiandka vitabu viwili bado siwezi kumaliza story..kwahy nikitoa kitabu hata nikirudia hii bado kuna haja ya kukisoma kwani hata niandke epsode 200 hapa story haitaisha..
Ila kitabu kitakua na story zngne mbili tofauti na hizi..

Nakutakia kila lililo la kheri katika uandishi wako.
 
STORY: HISTORIA BATILI(Fake History)
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba (Jk)
+255 718 274 130
+250 726 023 140


EPISODE O8
★★★★★★★★★★★★★
"Kaka, nimepokea sms hapa kutoka kwa boss, hebu isome" Aliongea Hisham akimpa simu Haroun na kusoma ile sms ilotumwa na Mr Khatib kwenye simu ya Hisham..
“Duuuh..kaka, hatari.., sasa tunafanyaje hapa?” Haroun ambaye alionekana kuduwaa zaidi aliuliza..
“Tufanye kama alivyotuelekeza, vitu vingine tutajua baadae..” Aliongea Hisham na kuongozana na Haroun kuelekea maeneo ya Alhaj Hospital kuonana na Dokta Mwinyi Moh'd, daktari maarufu wa magonjwa sugu hasa kwa akina mama..
Dokta Mwinyi alimiliki hospitali yake mwenyewe licha ya kuwa alikua pia ameajiriwa katika hospital ya serikali..
Walifika, wakaongea nae kwa muda wa takriiban dakika 24 na kuonekana kukubaliana jambo.
Kisha baadae ikaonekana Ambulance ikiingia kwa kasi hospitalini hapo akishuka Mr Khatib na mgonjwa aliyekuwa kwenye machela akiongozwa na wahudumu wawili wa kike wote wakazama ndani hospitali.
******************************
“Dokta, nini hasa sababu ya kifo cha mwanangu??” aliuliza mama Sauda baada tu ya kufika hospitali na kuonana na Dokta Mwinyi ambaye ndiye haswa aliyehusika na mgonjwa yule. Dr Mwinyi alishatoa taarifa juu ya kifo cha Sauda.
“Kumbe wewe ndo mama Sauda, kwanza pole sana mama, usihuzunike sana licha ya kuwa nafahamu jinsi unavyojiskia kwa sasa, kifo hakikwepeki, kwahiyo yapaswa uushinde moyo wako ili uweze kukubaliana na ukweli kuwa Sauda ameshafariki na hakuna namna ya kuirudisha pumzi yake tena...” Aliongea Dr Mwinyi kisha akaweka pozi kabla ya kuendelea,...
“Naaa...kuhusu sababu ya kifo chake, ni kuwa Sauda alipata saratani ya shingo ya kizazi, ambao huu ni ugonjwa hatari sana, kwa hapa kwetu Tanzania kila mwaka wanawake zaidi ya 40,000 wanaambukizwa ugonjwa huo. Naaa..ugonjwa huu unasababishwa na virusi ambavyo kitaalamu vinajulikana kama Human Papilloma Virus (HPV). Tatizo kubwa ni kuwa ugonjwa huu hauna dalili za mwanzoni, mpaka mtu awe na kawaida ya kucheki afya yake mara kwa mara ndo atagundua, ila baadae dalili kuu mbili tu ndo huwa zinajitokeza ambazo ni uvimbe katika kinena na maumivu makali wakati wa kujamiiana, hizi ni dalili za mwishoni. Ilaaa..kwa mujibu wa maelezo ya Mr Khatib mwenyewe ni kuwa alikua hafanyi mapenzi na mke wake mara kwa mara, yaani alikua akikaa mda mrefu saana.. Hivyo ni ngumu kugundua dalili hii ya maumivu katika tendo, na dalili hii ya uvimbe katika kinena mara nyingi ni ngumu kugundua sababu wanawake wengi wanaona aibu kuongea tatizo hli kwa watu wao wa karibu.. Kwahyo mama, Sauda anaonekana aliugua huu ugonjwa kwa mda mrefu saana, lakin alikua HAJUI.., Pole sana, Mungu atawapa wepesi katika msiba huu mzito..” Alimaliza maelezo Dr Mwinyi na kumfanya Mama Sauda kukosa hata swali la kumuuliza..
Akanyanyuka na kushika kitasa cha mlango akaufungua na kutokomea..
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
“Mama, kwa sasa nimeshakua mkubwa, nakuomba plzzz..niambie baba yangu ni nani!!”
“Mwanangu, kusema ukweli kutomjua babaako ni salama zaidi kuliko kumjua, mi namfahamu vizuri yule babaako, sio mtu mzuri kabsaa..licha ya kuwa machoni kwa watu anaonekana mwema”..
“Mama, mi nishakwambia kuwa ili uwe na amani na mimi kwa sasa ni kunionesha tu babaangu, nina miaka 9 sasa, kwanini bado tu unaniona mtoto?, mi namtaka babaangu” Aliendelea kusisitiza Abdul-mtoto wa darasa la 4, ndo kwnzaa akiwa na miaka 9, umahiri wa akili yake ndio ulifanya aandikishwe darasa la kwnza akiwa na miaka 6 badala ya 7, alikua ana akili ya ziada.. akilelewa na Mama yake bi Hamida Hassan aliyekua akimpenda sana mwanawe huyu wa pekee..
Alijitahidi kuhangaika sana kutafuta kuhakikisha mwanawe anaishi katika mazingira salama na anakua na furaha.
Baba wa mtoto, Mr Khatib, hakugombana na Hamida bali Hamida alijitenga nae baada tu ya kuzalishwa mtoto huyu sababu alihisi Mr Khatib atakua ana nyodo sana na anaweza kumnyanyasa na mtoti wake..
Hamida Hassan alikutana na Khatib miaka 11 iliyopita wakati Hamida alipoenda na wazazi wake kutembelea Hifadhi moja ya wanyama kijijini Kiwavu, Khatib akiwa kama ndio muongozaji mkuu wa eneo lile kwani alibahatika kusoma na kuelewa vizuri kuzungumza Kingereza pamoja na Kifaransa..
Hamida alimpenda sana Khatib na wakawa wakiwasiliana kutokea hapo mpka ambapo Hamida alipata mimba ya Abdul, wakiwasiliana vizuri mpaka mtoto alipozaliwa hadi alipofikia miaka miwili. Baada ya maisha ya Khatib kubadilika ndipo Hamida alipoamua kujitenga nae.
*******************************
“Haloo..”
“Yes, haloo”
“Habari za huko?”
“Nzuri tu, nani anaongea?”
“Mama Abdul”
“Ooooh Hamida, za siku tele mama watoto? Ukaaamua kunisusa, nimekutafta weee sijui uko wapi, vipi Abdul anaendleaje??” Aliropoka maneno mengi sana Mr Khatib baada ya kujua anaongea na Mama wa mtoto wake.
“Mi niko poa, mwanao huyu ongea nae” Alijibu kiufupi Hamida na kumkabidhi simu Abdul, hakutaka mazoea tena na Khatib, sababu zake alikua anazijua mwenyewe..
“Shikamoo dady..” Abdul alianza baada tu ya kupewa simu..
“Marahaba, hujambo mwanangu?”
“Sijambo, eti daddy wewe unaitwa Khatib nan?”
“Hahhaaahaa..mimi ni Khatib Mdharuba mwanangu..”
“Waoooh daddy i know you, wewe ndo yule tajiri kumbee.. ”
“Aaaaaaaghhhhh....” Ni sauti iliyotokea upande wa Baba Abdul na kumfanya Abdul ahamaki sana na kuanza kumuita babaake...
“Daddy..daddy..daddy....” Abdul aliita mara kadhaa bila ya majibu upande wa pili.. Hamida akachukua simu na kuiweka sikioni, bado ilikua haijakatwa lakini upande wa pili alikua haongei..
“Baba Abdul.., Baba Abdul..,,..iiishhhh...baba Abdul...Baba Abduliiiiiii...” Aliita mara nyingi Hamida lakini hakukua na majibu yoyote..
★★★★★★★★★★★★★★★★★
Watch Out Episode O9
 
STORY: HISTORIA BATILI(Fake History)
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba (Jk)
+255 718 274 130
+255 756 274 130

EPISODE O9
★★★★★★★★★★★★★★★★★
“Ila Mama, tunazika leo ndio, ila hiki kifo cha mdogo wangu mimi nina wasiwasi nacho sana.. Sidhani kama ugonjwa tulioambiwa ndio kweli aliokufa nao, nahisi kuna kitu zaidi ya hivyo” Alianza kuhoji bwana Kulwa Yassini-kaka mkubwa wa Sauda upande wa mamaake, wakiwa wamezaliwa mama mmoja lakini kila mtu na baba yake..akiwa anajaribu kumshauri mamaake kutokubaliana na Dokta Mwinyi..daktari bingwa wa magonjwa sugu, hasa yanayowahusu wanawake..
Kulwa Yassin alikua akiishi nchini Rwanda akifanya kazi kama afisa mikopo katika benki moja iliyopo katika Mtaa wa Kabuye Jijini Kigali..Alikua akiishi maisha mazuri sana, yeye ndiye aliyekua tegemeo pekee la mama yake..na aliitendea haki nafasi yake haswaa..Alimuenzi sana mama yake akiwa anamtumia pesa karibu kila baada ya wiki moja..
Kifo cha Sauda kilimshtua sana, aliharakisha sana ili awahi mazishi na kujua kiundani haswa nini sababu ya kifo hicho..
Wakati akijadili haya na mama yake watu walikua tayari wamekusanyika nyumbani kwao tayari kwa ajili ya mazishi yaliyopangwa kufanyika saa 10 jioni, na muda huo ilikua yapata saa 8:45 mchana..
“Mwanangu, mimi nimechanganyikiwa hapa, sielewi hata ni nini unachokiongea, naomba tuangalie haya ya mazishi kwanza halafu hizo hoja zako zingine utazileta baadae..” Aliongea mama Sauda machozi yakimbubujika usoni..
“Hapana mama, huu mwili ni lazima tukaufanyie uchunguzi katika hospitali nyingine, maana mazingira ya kifo cha mdogo wangu mimi siyaelewi..!!”. Kulwa aliona atoe yale ya moyoni, japo alijua fika kuwa muda umeenda sana na mwili wa marehemu ulishalala hospitali siku moja, na taratibu za waislam ni kuwahisha kuzika, hivyo kwa kuzikwa leo saa 10 tayari Sauda alikua amechelewa sana kuzikwa tangu alipofariki. Anapoleta wazo la kwenda kufanyia uchunguzi mwili wa marehemu anamaanisha anamsogezea zaidi siku za kuzikwa, na vilevile ni jambo gumu kwani watu wote walishakua na taarifa za mazishi kuwa yatafanyika leo saa 10.
Ila, Kulwa bado aliendelea kusisitiza kuwa alitaka kwenda kuufanyia mwili ule uchunguzi kwenye hospitali tofauti na Alhaj Hospital ili ajiridhishe na kifo cha mdogo wake..
Kama wasemavyo pesa ina nafasi kubwa katika maamuzi kwa maisha ya leo kuliko hata umri, Kulwa alishinda hoja yake na akakubaliwa aupeleke mwili kwa ajili ya uchunguzi kwenye hospitali nyingine.
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Wakati anaongea na mwanae Abdul, Mr Khatib alisikia beep tone katika simu yake ikiashiria kuna ujumbe mfupi (sms) imeingia katika simu yake..Akaitoa simu yake sikioni na kuweka 'loudspeaker' kisha akaanza kusoma ule ujumbe aliotumiwa..
Ndipo hapo alipojikuta akitoa sauti kubwa ya kushangaa.."Aaaaaaaaaghh" akawa ameduwaa hajui nini afanye. Akaiacha simu ikiwa bado hewani kwa dakika kadhaa kisha akaikata, na kurudia tena kuisoma ile sms iliyokua imetumwa katika simu yake na Hisham Omari Mikidadi iliyosomeka..
"Boss, Yule ---- Kulwa analazimisha auchukue mwili wa Sauda akaufanyie uchunguzi katika hospitali tofaut na Alhaj Hosptal, tunafanyaje hapo boss?”.
Khatib hakuwa anaamini hiki anachokisoma katika simu yake,ila haraka sana akaamua kuifoward ile sms kwa mama yake Mama Mdharuba ambaye naye alikuwepo pale msibani..
Baada ya takriiban dakika mbili simu yake ikaingia ujumbe mwingine kutoka kwa mama yake, “0726023140 piga hiyo namba halafu mwambie mimi ni mtoto wa Mama Mdharuba kisha umueleze hili jambo, fanya hivyo sasa hivi”.
Khatib hakuwepo eneo la msiba muda huu licha ya kuwa yeye ndiye Mume wa marehemu, ingawa hakuna aliyekuwa anahoji kwani kabla ya hapo alishakuja mara nyingi sana pale msibani akiwa anawajibika kwa kila jambo, kwahiyo 'kuchomoka' kwa dakika kadhaa pale msibani hakukuwashtua watu kwani walimjua vizuri Khatib kuwa ni mtu mwema tu hana tatizo haswa ukizingatia bado muda wa kuzika haukuwa umefika..
“Haloo, Khatib Mdharuba, mtoto wa Mama Mdharuba” aliongea Khatib baada ya simu yake kupokelewa..
“Oooh, mama yako amenitumia ujumbe tayari na amenambia kuwa utanitafuta..” Aliongea bwana yule ambaye alijulikana kwa jina la Sheikh Lesangwa kwa watu wote waliomfahamu.
“Sasaa..Khatib sheikh wangu huyo mzembe anataka kutafuta umaarufu kupitia jina lako, sasa usiwe na wasiwasi, hakuna atakachofanya, naomba uniamini na uniachie mimi hiyo kazi, ila nitakuomba ufanye kitu kimoja kwa sasa, nenda haraka sana hapo msibani na umpe mkono kwa kusalimiana nae, kabla hajatoka na marehemu, wahi” Aliongea sheikh Lesangwa ambaye alionekana kulijua vizuri jambo linavyoendlea. Haikuhitaji maswali mengi kwa bwana Khatib zaidi ya kuitikia “Sawa” na kukata simu, maelezo yalishajitosheleza.
Akatoka haraka sana na kuchukua gari yake aina ya Land Cruiser-Prado TX na kuelekea moja kwa moja msibani. Ndani ya dakika 5 tayari alishafika msibani kwani palikua si mbali na nyumbani kwake. Moja kwa moja hadi ndani ambapo alikutana na bwana Kulwa na kumuomba waje waongee mara moja..
Alitoka bwana Kulwa na wakasalimiana kwa kupeana mikono kisha mazungumzo yakaendelea..
“Nambie kaka, nilitoka kidogo hapa, vipi kuna chochote ambacho kinaenda tofauti? Maana na muda wenyewe umekaribia sana huu..” Aliongea Khatib akijifanya hajui chochote kuhusu uchunguzi wa mwili ambao Kulwa alipanga kwenda kuufanya.
“Yeah mabadiliko yapo, maana nipo katika maandalizi ya kwenda hospitali kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa mwili wa marehemu, sijaridhika bado na maelezo ya Dokta Mwinyi” Alifunguka bwana Kulwa.
“Oooh, oky sawaa.. Ila sasa shem kama umeamua kufanya hivyo ni vyema ukawaambia hawa watu waliokusanyika hapa nje mapema, maana hayo mazishi hayatakuwa ya leo tena” Alishauri Khatib, moyoni bado akiwa na wasiwasi mkubwa.. Kwanza hajui kwanini aliambiwa aje ampe mkono Kulwa, pia hajui kuwa huyo Sheikh Lesangwa ana kipi haswa cha kufanya katika hili ili hili tukio lisitokee..Kwa muda mfupi sana alishawaza mambo mengi mno huku akimuona bwana Kulwa akiwa anamaanisha alichokisema..
“Itakuaje endapo atauchunguza huu mwili na kugundua kifo chake kimetokana ma kuvuta sumu??” “Nani atakua wa kuulizwa kuhusu hiyo sumu zaidi ya mimi mumewe?” “Na nikigundulika kuwa nimempa sumu kwa njia ya hewa mke wangu, jamii itanichukuliaje?” Maswali yote hayo yalizunguka kichwani kwa Khatib, lakini hakuna hata moja liliokuwa na jibu wakati huo.
*******************************
“Mwanangu, hilo jambo unalotaka kufanya ni gumu sana, na utatafuta uhasama na watu, hivi unafikiri shemeji yako Khatib atakuchukuliaje?? Sauda ameshakufa, acha tu aende akapumzike kwa amani huko mwanangu, una lazima gani ya kufanya uchunguzi? Hivi wewe unafikiri una uchungu zaidi na Sauda kuliko mimi niliyemzaa mwenyewe? Hao watu hapo nje wote wanasubiri wakazike, sasa ni saa 9:15, bado nusu saa tu waende na mwili msikitini kwa ajili ya kuuswalia, hivi unawaambiaje mazishi yameahirishwa?? Mbna watoto wa siku hizi mnakua hivyo jamani??” Mama Sauda alilalama sana kumlalamikia mwanae ambaye alionekana amekua mbishi na analazimisha kufanya jambo gumu bila hata kuhofia chochote,..Ndio, hakuhofia kitu, na ndio kawaida ya pesa, ukiwa na pesa na uoga unaondoka, kinachoongezeka ni confidence tu!!.
“Mama mi acha tu nipate ukweli wa hiki kifo, wewe nione mkorofi au vyovyote tu, lakini mimi lazima nikachunguze kwa makini kifo cha Sau....” Kabla hajamalizia sentensi hii ghafla alishtuka akashikilia tumbo lake na kukimbilia chooni.
★★★★★★★★★★★★★★★★★★

Watch Out Episode 10
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom