Hints za January Makamba kuhusu mafuta na Gesi Tanzania

Contents za Mh. Waziri Makamba

1. Utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia nchini ulianza mwanzoni mwa miaka ya 1950. Mafanikio makubwa yalipatikana yakiwemo ugunduzi wa gesi asilia katika kisiwa cha Songo Songo mwaka 1974 na Mnazi Bay mwaka 1982. Aidha, Katika miaka ya 2010 na 2012 utafiti uliendelea katika maeneo ya kina kirefu cha Bahari ya Hindi. Hadi kufikia mwezi Mei 2022, jumla ya Futi za Ujazo Trilioni (TCF) 57.54 za gesi asilia ziligunduliwa katika maeneo ya nchi kavu na kina kirefu cha bahari. Kati ya kiasi hicho Futi za Ujazo Trilioni 47.13 zimegundulika katika Vitalu vilivyopo katika kina kirefu cha bahari ya Hindi, na Futi za Ujazo Trilioni 10.41 zimegundulika kutoka maeneo ya nchi kavu.

2. kutokana na ugunduzi huo wa kiasi kingi cha gesi asilia, Serikali ilifanya maamuzi ya uanzishwaji wa Mradi wa Kusindika na Kuchakata Gesi Asilia (Liquefied Natural Gas -LNG) kama njia bora ya kuendeleza rasilimali hiyo kwa ajili ya kuuzwa katika masoko ya Kimataifa na sehemu nyingine ya gesi hiyo kutengwa kwa ajili ya matumizi ya ndani ya nchi

3. Serikali kupitia TPDC itashiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mradi huu. Ushiriki, katika ubia na ushirika wa uendeshaji wa mradi, utasaidia kujenga uwezo wa Shirika hili ili miaka ijayo liweze kufanya shughuli hizi lenyewe na kwa tija na ufanisi kwa manufaa makubwa zaidi kwa taifa. Safari ya kuisuka upya TPDC kama Shirika mahiri na la kimkakati imeanza kwa wewe kutupatia Mwenyekiti wa Bodi mzito na sisi tumeunda Bodi mpya yenye kutoa mwelekeo wa dira mpya tunayoitaka kwa TPDC.

4. Manufaa yatakayopatikana katika utekelezaji wa mradi huu ni pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi; kujenga uzoefu wa TPDC kupitia ushiriki wake; kuongeza mapato ya Serikali yatakayotokana na mauzo ya gesi; upatikanaji wa gesi asilia iliyochakatwa kwa ajili ya matumizi ya ndani ya nchi; ushiriki wa watanzania katika uuzaji wa bidhaa na utoaji huduma; na fursa nyingi za ajira kwa watanzania hususan katika kipindi cha ujenzi na hata katika kipindi cha uendeshaji wa mradi.

5. pia tumefanya uamuzi wa kuanzisha Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone) kwenye eneo la mradi ambapo kutakuwa na vivutio mbalimbali, ikiwemo bei nafuu ya umeme, ili kuvutia viwanda na shughuli za kiuchumi katika mikoa ya Kusini.
Twambie kwanza, mradi wa umeme wa Mwl. Nyerere utakamilika lini. Hatutaki maswala ya gesi kwani Rais Magufuli aliishatwambia kuwa huko tushapigwa.
 
Katika ku summarise speech ya kiazi yule umeacha hoja ya msingi kwenye maeneo ya majadiliano.

Anadai wanatumia consultant kwenye key four areas kwa ushauri;
Kifedha (commercial)
Biashara (economic)
Kiufundi (technical)

Sheria (hii sio technical issue ya kibiashara).

Hizo tatu za juu kweli ni key issues lakini sio hizo tu zipo sita.
Mazingira (hii ni key issue kwenye dunia ya leo katika majadiliano).

Mbili zingine za jamii na siasa wameparaza paraza tu lakini sijasikia emphasis katika majadiliano hayo mambo yanatakiwa kuwa kwenye maandishi pia especially ushiriki wa jamii.

Ushauri wa kisheria ni muhimu lakin unakuja kivingine sio key issue ya namna mradi utakavyoendeshwa kila siku.

Sheria ni muhimu katika kukadhia makubaliano; sasa makubaliano yenyewe bado ushauri wa sheria wa nini at this stage unless hao negotiators are clueless ata kwenye basic issues za majadiliano ya awali.

Mambo yenyewe awayaelewi halafu wanayakimbiza.

Huo mradi eleweni wanaenda kutoa mali za Tanzania sandakalawe wao wanachofikiria ni hizo $30 za uwekezaji wa awali not sure even those sums are justifiable, let alone wanajua madhara ya interest kubwa kwenye kugawana mapato huko mbeleni bila kuuliza source za hizo funds.

Yaani chief negotiator anampigia simu waziri kwa ushauri, Makamba huyu huyu ambae ukimsikiliza akiongelea hayo mambo hajui lolote; sasa sijui ana mshauri nini.

Hakuna shughuli hapo zaidi ya kugawa maliasili kwa mabeberu kwa bei chee.
Kuna wapuuzi wata like hii comment ya mchawi mwenye chuki Sana
 
At least they should seek local input kwanza by poking ideas on what direction the government should pursue.

Kama wanaweza anzisha zoom meetings kila siku za kumsifia raisi; kipi kinawashinda kuanzisha mjadala wa mikataba ya mafuta na gesi wadau wachangie kushauri serikali ijikite na mambo gani kupata mawazo ya watu mbali mbali.
Majadiliano ya mkataba wa biashara sio sawa na majadiliano ya katiba
 
Mkataba huu wa awali sijui kama ulikuwa sahihi kuukimbiza kwa haraka kwetu wananchi Na kuhudhuriwa Na mheshimiwa rais kwani bado haujaweka manufaa ya moja kwa moja kwa serikali yetu ukiacha qualitative information kama vile Ajira Na gharama ya uwekezaji iliyotajwa.

Watanzania wanahitaji kuelezwa faida za Ziana za mkataba ikiwemo hisa za serikali na gawiwo kutokana Na projections za Mauzo Na kodi..

Naamini bado watarudi tena kwetu Na kuweka hadharani manufaa ya mradi kwa taifa letu ukiacha Ajira kwa watu wetu pekee ambayo ndo imetajwa leo.
Wewe una shida kichwani,ulifuatilia majadiliano ya mradi wa Bomba la mafuta la Uganda? Yameshuhudiwa na Marais mara ngapi?

Ilivyokuwa kule ndivyo na huku itakuwa.
 
Nafaham ya kwamba imekuwa ikitumika kwa matumizi ya nyumbani lkn kwa njia ya mabomba,hoja yangu ni kama imeweza kusindikwa kwenye mitungi na kutumika kwenye magari,je inashindakana nini kujazwa kwenye mitugi hii tunayotumia majumbani?
Gesi asilia ya kwenye mitungi inayouzwa Tanzania kwasasa inaitwa compressed natural gas (CNG) kwa kiswahili ges asilia iliyoshindiliwa. Huwezi pikia gesi asilia ikiwa kwenye mtungi wa CNG, pressure yake inakua kubwa mno.

Gesi asilia tunachotumia kupikia inaitwa gesi asilia ya bomba (PNG).

Huna haja ya kukandamiza gesi asilia ili uweze kuitumia kwenye jiko kwa kupikia kwasababu pressure itakua kubwa. Kama pressure yake ni kubwa Utalazimika kupunguza ili uweze kupika.

Kwa kupikia chakula kwenye majiko ya kawaida ya nyumbani, tunahitaji pressure ya 21 mbar. Na hii ndogo sana kuliko hata atmospheric pressure. Kwa hiyo utalazimika kutumia pressure regulator ili kupunguza pressure hadi 21 mbar ndipo uweze kupika.

CNG inatumika zaidi katika magari, ambayo yana pressure kati ya 200 na 250 bar.

Hivyo ikiwa utapunguza pressure ya gesi asilia kwenye silinda mpaka 21 mbar, utajaza kiasi kidogo sana cha gesi. Hivyo nishati itakayopatikana itakua ndogo sana.

Lakini kwa hiyo, kwa pressure hiyo ya 21 mbar, unaweza kupata kiasi kingi zaidi na nishati iliyohifadhiwa kwenye silinda yenye LPG.

Hivyo ili kupata nishati ya CNG ya kutosha ya kupikia, utahitaji kubadilisha silinda mara nyingi zaidi, na zitakua nzito zaidi kwa sababu ya mahitaji ya juu ya pressure.
 
Majadiliano ya mkataba wa biashara sio sawa na majadiliano ya katiba
Wewe ata nikikwambia ‘unitisation agreement’ ya mafuta na gas ni kitu gani. Hiyo terminology ndio utakuwa umeisikia hapa kwa mara ya kwanza.

Kwa ivyo sitarajii uweze ku analyse limitations za Makamba kwenye maswala ya mikataba ya mafuta kwa kumsikiliza na wala uwezi kuona mantiki ya kuanzisha mijadala ikibidi tofauti kuzungumzia different aspects za contract negotiations ya oil and gas wahusika kupata ideas.

Stick na ushambenga wa mambo ya katiba hayo yanahitaji makelele yasiyo na kichwa wala miguu ndio unayoyaweza, huku kwenye mafuta kunataka uwe na foundation ya mambo kadhaa.
 
Wewe ata nikikwambia ‘unitisation agreement’ ya mafuta na gas ni kitu gani. Hiyo terminology ndio utakuwa umeisikia hapa kwa mara ya kwanza.

Kwa ivyo sitarajii uweze ku analyse limitations za Makamba kwenye maswala ya mikataba ya mafuta kwa kumsikiliza na wala uwezi kuona mantiki ya kuanzisha mijadala ikibidi tofauti kuzungumzia different aspects za contract negotiations ya oil and gas wahusika kupata ideas.

Stick na ushambenga wa mambo ya katiba hayo yanahitaji makelele yasiyo na kichwa wala miguu ndio unayoyaweza, huku kwenye mafuta kunataka uwe na foundation ya mambo kadhaa.
Hata ningekuwa ndio naisikia saizi,google ipo kwa Kazi gani Kwa mfano?

Narudia kukwambia majadiliano ya biashara sio sawa na majadiliano ya katiba kwamba ni public,kule msingi ni nipe nokupe..

Kama unaona timu ya majadiliano haijui wewe ndio unajua Sana omba Kazi wakuweke huko..
 
Hii gesi asili nmeona inawekwe kwenye mitungi na kufungwa kwenye magari kama nishati mbadala wa petroli,kwa ufahamu wangu mdogo niliju gesi asili sio raisi kuwekwe kwenye mitungi ndio maana yanatumka mabomba kwa ajili kuisambaza kwa wahitaji,kama hilo limewezekana kwenye magari ni kwa nini isijziwe kwenye mitungi kwa ajili ya matumizi ya majumbani?
mkuu tofautisha COMPRESSION na LIQUIFICATION, ya kwenye magari ni compressed natural gas aka CNG na ya kwenye mitungi ni liquified natural gas aka LNG sasa hii LNG mchakato wake ndio complex sana.
 
Ni jambo jema,waharakishe kujenga Ili tuwapige BAO Msumbiji.
Yaani mbulukenge kama hizi zimejazwa JF kwa ajili ya kusifu na kuabudu. Hana hoja, hana knowledge wala hana skills. Rasilimali kama gesi sio ishu za kukimbiza ili umshinde Jirani yako, ukimshinda then what's next?

Mikataba ya rasilimali inatakiwa iwe shirikishi, ya kizalendo kweli kweli, ikihusisha utaalamu wa ndani kwanza, majadiliano ya kina nk. Tusirudie makosa yaliofanyika kwenye uwekezaji wa madini na nchi kupigwa mchana kweupe.
 
Back
Top Bottom