Nigeria ilianza kuchimba mafuta 1956, bado inauza mafuta ghafi nje na kununua yaliyosafishwa. Tanzania tutatoboa na gesi?

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,446
7,821
Nigeria ni nchi ya pili kwa uzalishaji mafuta barani nyuma ya Angola, ilianza rasmi uchimbaji mafuta na kuyauza nje kibiashara mwaka 1956, kufikia mwaka 2000 mapato ya mafuta ghafi yalikuwa 98% ya mapato yote Nigeria iliyopata kwa kuuza bidhaa na huduma nje ya nchi.

Pamoja na mafuta ghafi kuwa chanzo kikuu cha mapato ya fedha za kigeni Nigeria bado iliingia gharama kubwa kuagiza mafuta yaliyosafishwa kwa miaka yote.

Kiwanda cha Dangote kimeanza rasmi uzalishaji lakini bado kina safari kuelekea kuzalisha kwenye uwezo wake unaotarajiwa ili kutosheleza mahitaji ya ndani.

Ni safari ya zaidi ya miaka 68 kwa nchi hii iliyo magharibi mwa Afrika, tutegemee safari hii kwa gesi yetu kuweza kuifanya kimiminika(LPG) ili iweze kutumiwa kwa matumizi mbalimbali? Tanzania tunanunua gesi ya kupikia inayojazwa kwenye mitungi kwasababu tumeshindwa kuweka mitambo ya kuifanya LPG huku yetu tukiiuza nje!

Nchi za kiarabu ziliwezaje kutumia mafuta yake mapema na kuwatoa kwenye lindi la umasikini kufikia utajiri wa kiwango cha juu!
 
Nigeria ni nchi ya pili kwa uzalishaji mafuta barani nyuma ya Angola, ilianza rasmi uchimbaji mafuta na kuyauza nje kibiashara mwaka 1956, kufikia mwaka 2000 mapato ya mafuta ghafi yalikuwa 98% ya mapato yote Nigeria iliyopata kwa kuuza bidhaa na huduma nje ya nchi.

Pamoja na mafuta ghafi kuwa chanzo kikuu cha mapato ya fedha za kigeni Nigeria bado iliingia gharama kubwa kuagiza mafuta yaliyosafishwa kwa miaka yote.

Kiwanda cha Dangote kimeanza rasmi uzalishaji lakini bado kina safari kuelekea kuzalisha kwenye uwezo wake unaotarajiwa ili kutosheleza mahitaji ya ndani.

Ni safari ya zaidi ya miaka 68 kwa nchi hii iliyo magharibi mwa Afrika, tutegemee safari hii kwa gesi yetu kuweza kuifanya kimiminika(LPG) ili iweze kutumiwa kwa matumizi mbalimbali? Nchi za kiarabu ziliwezaje kutumia mafuta yake mapema na kuwatoa kwenye lindi la umasikini kufikia utajiri wa kiwango cha juu.
Mkuu Replica , una hoja ya msingi ila hujaiweka vizuri. Nchi za kiarabu zimetumia mafuta kujenga uchumi wake sasa baadhi ya nchi hizo hazitegemei tena mafuta. Nigeria na Angola zina mafuta lakini mafuta hayo hayajaweza kujenga nchi hizo. Tanzania sasa ina gesi, jee LNJ itaisaidia Tanzania kujenga uchumi imara?.

Jibu.
Uchumi wa dunia japo unatawaliwa na nguvu soko, marked forces, nchi mabeberu ndio wana influence hizo market forces.

Mfano Africa, South Africa, Angola, Ghana, Tanzania, tunachimba sana dhahabu, lakini bara la Africa lote hatuna gold smelter hata moja, wakati nchi ya Uswiss haina hata pune moja ya dhahabu ina gold smelters 6!. Mabeberu wamefanya hivyo ili gold inayochimbwa Afrika ipelekwe huko.

The same applies to crude oil, Africa tuna mafuta hata Uganda, mafuta inayoyachimba, japo yanatosha kuifanya Uganda ijitegemee isiagize mafuta, Manmade market forces ziko designed in such a way Uganda haiwezi kujenga oil refinery yake, ikasafisha mafuta yake, lazima yapelekwe kwa nchi mabeberu kusafishwa ili Uganda iendelee kununua mafuta.

Hata Tanzania, tutayapokea mafuta ya Uganda pale Chongoleani na kuyasafirisha yote, badala ya kujenga refinery, ili tuendelee kuagiza mafuta.

The same applies to LNG gas yote ni for export, huku tukiendelea kuagiza LPG kwa matumizi ya majumbani!.

Huo ndio uchumi wa dunia.
P
 
Mkuu Replica , una hoja ya msingi ila hujaiweka vizuri. Nchi za kiarabu zimetumia mafuta kujenga uchumi wake sasa baadhi ya nchi hizo hazitegemei tena mafuta. Nigeria na Angola zina mafuta lakini mafuta hayo hayajaweza kujenga nchi hizo. Tanzania sasa ina gesi, jee LNJ itaisaidia Tanzania kujenga uchumi imara?.

Jibu.
Uchumi wa dunia japo unatawaliwa na nguvu soko, marked forces, nchi mabeberu ndio wana influence hizo market forces.

Mfano Africa, South Africa, Angola, Ghana, Tanzania, tunachimba sana dhahabu, lakini bara la Africa lote hatuna gold smelter hata moja, wakati nchi ya Uswiss haina hata pune moja ya dhahabu ina gold smelters 6!. Mabeberu wamefanya hivyo ili gold inayochimbwa Afrika ipelekwe huko.

The same applies to crude oil, Africa tuna mafuta hata Uganda, mafuta inayoyachimba, japo yanatosha kuifanya Uganda ijitegemee isiagize mafuta, Manmade market forces ziko designed in such a way Uganda haiwezi kujenga oil refinery yake, ikasafisha mafuta yake, lazima yapelekwe kwa nchi mabeberu kusafishwa ili Uganda iendelee kununua mafuta.

Hata Tanzania, tutayapokea mafuta ya Uganda pale Chongoleani na kuyasafirisha yote, badala ya kujenga refinery, ili tuendelee kuagiza mafuta.

The same applies to LNG gas yote ni for export, huku tukiendelea kuagiza LPG kwa matumizi ya majumbani!.

Huo ndio uchumi wa dunia.
P
Nadhani umeongea vizuri sana, kuna external forces huwezi kuzikwepa kwenye uchumi wa dunia.
 
Nigeria ni nchi ya pili kwa uzalishaji mafuta barani nyuma ya Angola, ilianza rasmi uchimbaji mafuta na kuyauza nje kibiashara mwaka 1956, kufikia mwaka 2000 mapato ya mafuta ghafi yalikuwa 98% ya mapato yote Nigeria iliyopata kwa kuuza bidhaa na huduma nje ya nchi.

Pamoja na mafuta ghafi kuwa chanzo kikuu cha mapato ya fedha za kigeni Nigeria bado iliingia gharama kubwa kuagiza mafuta yaliyosafishwa kwa miaka yote.

Kiwanda cha Dangote kimeanza rasmi uzalishaji lakini bado kina safari kuelekea kuzalisha kwenye uwezo wake unaotarajiwa ili kutosheleza mahitaji ya ndani.

Ni safari ya zaidi ya miaka 68 kwa nchi hii iliyo magharibi mwa Afrika, tutegemee safari hii kwa gesi yetu Tu kuweza kuifanya kimiminika(LPG) ili iweze kutumiwa kwa matumizi mbalimbali? Nchi za kiarabu ziliwezaje kutumia mafuta yake mapema na kuwatoa kwenye lindi la umasikini kufikia utajiri wa kiwango cha juu.
Tujifunze kwa waarabu. Unajua tungeweza kupata hata umoja wa wauza korosho, cobalt, duniani.
 
Nchi za magharibi zina nguvu sana hasa katika kuendesha masoko ya kimataifa.

Hapo kiwanja cha Julius Nyerere Int. Airport: Wazungu walikataa kuwa kiwanja hakina hadhi ya kuwa airport ya kimataifa kwa sababu hakina magari ya zimamoto. Kumbuka walimkatalia Nyerere kumuuzia hizo gari za zimamoto.

Nyerere akajimwambafai ajitoe kwenye hiyo matrix, akaunda magari ya zimamoto (nafikiri ndio hiyo nyumbu kwa sasa). Walivyoona anapandisha mabega wakaamua kumpatia sasa hizo gari za zimamoto asije akaanza kujitegemea.

Kiufupi nchi yoyote ya kiafrika ikitaka ijitegemee kwa kilaa kitu lazima itakutana na upinzani mkubwa wa hali ya juu.

Pia na system yetu tuliyoachiwa na wazungu ni ngumu sana kutoboa.

Mfano:
Mtu kakamatwa na bunduki ya kutengeneza kwa mkono, akikamatwa mtu huyu ataishia kufungwa tu badala ya kumchukua na kuendeleza hiki kipaji, pengine anaweza akawa asset kwa taifa.

Au
Ajitokeze mtu avumbue dawa ya UKIMWI au Kansa, mtu wa hivi ngumu kumaliza mwaka kuna uwezekano mkubwa wakalala nae mbele.
 
Nchi za magharibi zina nguvu sana hasa katika kuendesha masoko ya kimataifa.

Hapo kiwanja cha Julius Nyerere Int. Airport: Wazungu walikataa kuwa kiwanja hakina hadhi ya kuwa airport ya kimataifa kwa sababu hakina magari ya zimamoto. Kumbuka walimkatalia Nyerer kumuuzia hizo gari za zimamoto.

Nyerere akajimwambafai ajitoe kwenye hiyo matrix, akaunda magari ya zimamoto (nafikiri ndio hiyo nyumbu kwa sasa). Walivyoona anapandisha mabega wakaamua kumpatia sasa hizo gari za zimamoto asije akaanza kujitegemea.

Kiufupi nchi yoyote ya kiafrika ikitaka ijitegemee kwa kilaa kitu lazima itakutana na upinzani mkubwa wa hali ya juu.

Pia na system yetu tuliyoachiwa na wazungu ni ngumu sana kutoboa.
Mfano:
Mtu kakamatwa na bunduki ya kutengeneza kwa mkono, akikamatwa mtu huyu ataishia kufungwa tu badala ya kumchukua na kuendeleza hiki kipaji, pengine anaweza akawa asset kwa taifa.

Au
Ajitokeze mtu avumbue dawa ya UKIMWI au Kansa, mtu wa hivi ngumu kumaliza mwaka kuna uwezekano mkubwa wakalala nae mbele.
Mwafrika ndio kiumbe ambaye ameshindwa kutatua matatizo yake mwenyewe, mwisho anatafuta kwa kupeleka lawaza zake ili kupata kisingizio.

Nchi za Asia zilikuwa chini ya utawala wa wazungu Kama ilivyo kuwa kwa Afrika,Leo hii zimepiga hatua kubwa ya maendeleo kushinda hata wazungu na mwisho zinatunishiana mbavu na wazungu katika nyanja zote.

Wakati huo huo bara la Afrika likiwa limezama zaidi kwenye dimbwi la ufukara,sababu ya rushwa za kipumbavu huwezi Kuta nchi serious zinaiba pesa ya umma kwa ajili ya maendeleo na kwenda kugharamia kampeni za chama huu ni upumbavu wa mwafrika na sio mzungu.

Leo hii watawala wa kiafrika Kutwa kusaini mikataba ya kuuza rasilimali za nchi kwa gawio la 10% sasa hili nalo unawapa wazungu lawama.

Ni ukweli mchungu na ulio thabiti pasi kutia shaka,kwamba Mwafrika hawezi jitawala. Ukitaka mfano angalia South Africa ya Makaburu na ya ANC,Zimbabwe ya walowezi na Zimbabwe ya Mwafrika Robert Mugabe.
 
Nigeria ni nchi ya pili kwa uzalishaji mafuta barani nyuma ya Angola, ilianza rasmi uchimbaji mafuta na kuyauza nje kibiashara mwaka 1956, kufikia mwaka 2000 mapato ya mafuta ghafi yalikuwa 98% ya mapato yote Nigeria iliyopata kwa kuuza bidhaa na huduma nje ya nchi.

Pamoja na mafuta ghafi kuwa chanzo kikuu cha mapato ya fedha za kigeni Nigeria bado iliingia gharama kubwa kuagiza mafuta yaliyosafishwa kwa miaka yote.

Kiwanda cha Dangote kimeanza rasmi uzalishaji lakini bado kina safari kuelekea kuzalisha kwenye uwezo wake unaotarajiwa ili kutosheleza mahitaji ya ndani.

Ni safari ya zaidi ya miaka 68 kwa nchi hii iliyo magharibi mwa Afrika, tutegemee safari hii kwa gesi yetu kuweza kuifanya kimiminika(LPG) ili iweze kutumiwa kwa matumizi mbalimbali? Nchi za kiarabu ziliwezaje kutumia mafuta yake mapema na kuwatoa kwenye lindi la umasikini kufikia utajiri wa kiwango cha juu.
Uchumi wa Tanzania na Nigeria upo sawa?
 
Nigeria ni nchi ya pili kwa uzalishaji mafuta barani nyuma ya Angola, ilianza rasmi uchimbaji mafuta na kuyauza nje kibiashara mwaka 1956, kufikia mwaka 2000 mapato ya mafuta ghafi yalikuwa 98% ya mapato yote Nigeria iliyopata kwa kuuza bidhaa na huduma nje ya nchi.

Pamoja na mafuta ghafi kuwa chanzo kikuu cha mapato ya fedha za kigeni Nigeria bado iliingia gharama kubwa kuagiza mafuta yaliyosafishwa kwa miaka yote.

Kiwanda cha Dangote kimeanza rasmi uzalishaji lakini bado kina safari kuelekea kuzalisha kwenye uwezo wake unaotarajiwa ili kutosheleza mahitaji ya ndani.

Ni safari ya zaidi ya miaka 68 kwa nchi hii iliyo magharibi mwa Afrika, tutegemee safari hii kwa gesi yetu kuweza kuifanya kimiminika(LPG) ili iweze kutumiwa kwa matumizi mbalimbali? Nchi za kiarabu ziliwezaje kutumia mafuta yake mapema na kuwatoa kwenye lindi la umasikini kufikia utajiri wa kiwango cha juu.
Hapo kuna, wanaigeria, tena viongozi wananufsika na huo uozo, ili nchi ya Afrika, inufaike na rasilimali zake,lazima uanzishe Vita na UK, ulaya, America, maana Hawa wajomba hawapo tayari kuona Rasilimali zinanufsisha wazawa, wataua, watatoa rushwa,watawakamata makenge watatu wa kiafrika,wawape mpunga, na Hao watauza nchi,
Mkapa alijiuzia mgodi!kikwete aliuza gesi yetu kwa wanzungu, Ukitqka Uwe kama Iran, south Afrika, au, china, lazima ujipange kupambana na mabepari!
 
Nigeria ni nchi ya pili kwa uzalishaji mafuta barani nyuma ya Angola, ilianza rasmi uchimbaji mafuta na kuyauza nje kibiashara mwaka 1956, kufikia mwaka 2000 mapato ya mafuta ghafi yalikuwa 98% ya mapato yote Nigeria iliyopata kwa kuuza bidhaa na huduma nje ya nchi.

Pamoja na mafuta ghafi kuwa chanzo kikuu cha mapato ya fedha za kigeni Nigeria bado iliingia gharama kubwa kuagiza mafuta yaliyosafishwa kwa miaka yote.

Kiwanda cha Dangote kimeanza rasmi uzalishaji lakini bado kina safari kuelekea kuzalisha kwenye uwezo wake unaotarajiwa ili kutosheleza mahitaji ya ndani.

Ni safari ya zaidi ya miaka 68 kwa nchi hii iliyo magharibi mwa Afrika, tutegemee safari hii kwa gesi yetu kuweza kuifanya kimiminika(LPG) ili iweze kutumiwa kwa matumizi mbalimbali? Nchi za kiarabu ziliwezaje kutumia mafuta yake mapema na kuwatoa kwenye lindi la umasikini kufikia utajiri wa kiwango cha juu.
Mmmmm! Hatari sana. Yani 68 years ndio leo wameanza kusafisha. Ukiona umeruhusiwa kusafisha just mabwenyenye wana mkakati mwingine.
 
Nchi zilizojaa rushwa haziwezi piga hatua yoyote ya maendeleo. Sababu zitakuwa kulalamika kuhusu wazungu kwamba wanakwamisha maendeleo kumbe ukweli ni kwamba hatuna akili ya kujitawala.
Huu ndiyo ukweli...watu ambao can't even call Mwizi kuwa ni mwizi instead they water it down to Mpigaji...hawawezi kufanya lolote la maana hata wakiwa na raslimali zote za dunia which Africa has: madini, good land, water bodies, oil and gas etc.
 
Huu ndiyo ukweli...watu ambao can't even call Mwizi kuwa ni mwizi instead they water it down to Mpigaji...hawawezi kufanya lolote la maana hata wakiwa na raslimali zote za dunia which africa has: madini, good land, water bodies, oil and gas etc.
Rasilimali muhimu iliyo johari hapa duniani ni akili, ambayo ndo huipa kitu au vitu thamani kutokana na akili kufanya vumbuzi zenye matumizi ya hicho kitu/ vitu.

Mwafrika Kutwa hasa Watanzania, kujimwambafai tuna rasilimali ambazo ni utajili bla bla kibao, anashindwa kufahamu kwamba hana akili ya kutumia hizo rasilimali kuleta tija au ustawi na hii ni kwa sababu hana akili ya kufanya mang'amuzi kujua kwamba hana pakutumia hizo rasilimali.
 
Sera ya mabeberu ni kutufanya tuwewazalishaji wa malighafi tu.

To never produce anything.

Wanatulazimisha mikopo kwa fedha zao na wanatupangia bei ya mauzo ya raw materials.
 
Utajiri wa Angola nusu umeishia kwa raisi wa nchi hio kupitia binti yake kama mwanamke tajiri kuliko wote Africa,mapato ya Nigeria yameishia kunufaisha mafisadi wakubwa wa nchi hio ambao wengi ni viongozi huku mamilioni wakitopea kwenye umasikini mkubwa.
 
Back
Top Bottom