.
Sky, sometimes huwa unaongea mambo mazito. Kikanuni shule zote ambazo sio seminari zinapaswa kuheshimu uhuru wa kuabudu wa kila mwanafunzi.
Kama Ali ni mwislamu anasomea St. Anthony's Sec School, siku ya JUmatano ya Majivu haimhusu. Kusali sala za asubuhi katika paredi moja kwa kutumia Biblia au Misale ya Waumini Katoliki hakuruhusiwi.
Hata hivyo, haya yanafanyika kwa kuwa serikali haijayawekea katazo lenye mkazo. In fact, niliwahi kufundisha shule moja, ambako nilisikia Headmaster anasema Baba Askofu amemwambia walimu wote wawe wanasali na wanafunzi Jumapili.
Nilimcheka sana HM na Askofu wake, tena huyu askofu ni PhD holder. Haki zinapiganiwa....