Kuna swahiba yangu mkuu yeye ni Mpemba aliniambia amesikia shule za Roman Catholic zina elimu bora hivyo anaomba nimsaidie watoto wake wawili wapate nafasi, basi tulipigania kumwambia baba paroko hawa ni watoto wa kaka yangu kabisa. Watoto walipewa mtihani na walifauli na kupata nafasi, kaka yangu alifurahi sana na zawadi tele nililetewa, shule ni boarding, baada ya miezi sita watoto wamerudi wanajua mpaka novena. Kaka aliniambia "dada sasa hawa wakimaliza shule si nitakuwa nimewapoteza kabisa".
Watoto hawakurudi tena shuleni kule, walitafutiwa shule nyingine. Jitihada zangu ziliishia hapo.