Hijab kwenye shule za kikristo

Hijab kwenye shule za kikristo

Nenda kasome petro 5:7 ili ujue nani wakumkabidhi huo wasiwasi wako ikiwa hujui pa kuupeleka halafu urudi hapa tujadili.
Polisi ufaransa wakilazimisha mama wa \kiislaam avue Hijjab !
Hijabu Polisi wakilazimisha kuvua.png
 
Kaka akaogopa ''salaamu maria umejaa neema bwana u nawe umebarikiwa kuliko wanawake wote na yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa, maria mtakatifu mama wa Mungu utuombee sisi wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu Amina''.

Mwambie KAKA aache uoga aache watoto wapate cha kula cha kiroho
Mbona Maria mama wa Mungu sijaiona hapo?
 
Kwanza kabla ya kuendelea na suala hili la kwanini kuna double standards. Mie naona suala kubwa hapo ni hijabu. wengi wetu labda hatujui maana hata ya hijabu ila tunakurupuka tu kuanza ubishi. HIJABU ni vazi analovaa mwanamke ili kuficha uchi wake. Sehemu zinazotakiwa kuonekana ni uso na viganja vya mikono.
kwa kifupi hijabu haina dini fulani wala fulani. Hijabu ni wajibu wa kila mwanamke au mkristo ama muislamu. Sasa hizo shule zinazojiita za kikristo kwanini haziwalazimishi watoto wa kikistro kuvaa hijabu? Nadhani hilo mdio swali muhumu kujiuliza
 
Acha udini. Tuishi kama siku zote.
siyo udini, issue ni kuwa upande mmoja hauthamini upande mwingine kwa kuuona hauna haki, mimi mdogo wangu alisoma Thaqaafa ya mwanza, alikuwa anavaa hijabu kwa lazima, kwa kuwa ni shule inayomilikiwa na taasisi ya kiislamu, lakini ukienda pale SAUT, bado waislamu wanaruhusiwa kuvaa baibui kama kawa, sasa hapo nani ana udini?
 
Hakuna muisilamu anasoma seminary za kikristo. Bali wapo waisilamu wanao soma Shule za binafsi zinazomilikiwa na wakristo
Jk alisoma wapi? Makamba alisoma wapi? Salim Ahmed Salim alisoma wapi?
 
Nashangaa sana mtu anachukia muislam kuvaa hijab eti kisa yeye ni Mkiristo! Inakuhusu nini wewe hijab mpaka uchukie! Ni chuki za kidini tu mangapi waislamu hawayapendi Ila wakristo wana yapenda je waislamu wasimame waseme hatuyataki haya mtajisikiaje ni chuki na udini tu
 
siyo udini, issue ni kuwa upande mmoja hauthamini upande mwingine kwa kuuona hauna haki, mimi mdogo wangu alisoma Thaqaafa ya mwanza, alikuwa anavaa hijabu kwa lazima, kwa kuwa ni shule inayomilikiwa na taasisi ya kiislamu, lakini ukienda pale SAUT, bado waislamu wanaruhusiwa kuvaa baibui kama kawa, sasa hapo nani ana udini?
Kama mdogo wako kweli ni mkristo anatakiwa afurahie kabisa. Maana anavaa vazi takatifu. Vazi bora. Vazi la bikra Mariaa!!
 
Enyi mlioamini! Msiwafanye kuwa marafiki Mayahudi na Manaswara.
 
Nimeshuhudia mara mbili:Tukio la kwanza nikisafiri toka Morogoro kwenda DSM,abiria kama watatu hivi wakimlalamikia dereva wa basi abadilishe "stesheni" ya redio baada ya kusikia yakitolewa mawaidha ya kiislamu.Dereva yule kwa busara aliamua kuzima kabisa redio.Tukio la pili nikisafiri toka Arusha kwenda Moshi,abiria kadhaa walimfokea abiria mwenzao aliefungulia nyimbo ya kaswida kupitia simu yake ya mkononi,malumbano yalikuwa makali.Nilimsihi yule dada atumie "earphone" ili kutowakera wengine wasiopenda kusikia hiyo kaswida yake.Lakini sijawahi kushuhudia tafrani ikitokea pale unapopigwa wimbo/kwaya katika mazingira hayo hayo ya chombo cha usafiri,taaizo ni nn hasa? Kwa nini upande mmoja unashindwa ustahamilivu wa kiimani kwa mwenzie????
Kama hujashuhudia haimaanishi haijawatokea, Mimi nimeshashuhudia.

Hapa inatakiwa tu watu kuwa wastaarabu, huwezi kuweka nyimbo/mawaidha ya dini flank kwenye chombo cha public. Sio dini tu, kuna watu wengine wanaweka nyimbo za kilugha kwenye simu zao na zinaimbwa kwa loudspeaker. Huo Si uungwana hata kidogo
 
Back
Top Bottom