Hii ndio Orodha ya makundi ya watu wanaohitaji Katiba Mpya na wasiohitaji

Umetumia methodology gani kubaini makundi hayo? Mawazo binafsi si tafiti

Nimehoji watu wa makundi niliyoyataja Mkuu.

Nimefanya kautafiti kadogo.

Sample niliyoichukua ni participants 100 Kwa mikoa ya Morogoro, Dar, Iringa, Mbeya NK.

Wapo niliowahoji,
Wapo Kwa kuwatazama tuu nikiwa kijiweni nk
 
Kwa mujibu wa tathmini hii ambayo si haba akisikika mtu anapinga katiba mpya bila shaka ni:

1. Mwanamke,
2. Mzee,
3. Boda boda, machinga, sungu sungu, mpiga debe, vibaka vibaka na wa namna hiyo,
4. Wana CCM, wasijijitambua, wanafiki na wenye Maslahi binafsi.

Hiiiiii bagosha!

Iko hivyo
 
Katiba inaumhimu wake ila si kwa kila kitu,

Mwanadamu si wa kudhibitiwa na katiba pekee, Ni nidhamu na kupenda haki ndiyo tunu kwa kila taifa

Ukitaka kufahamu kwamba katiba sio mwarobaini, Jifunze kwa vitabu vya Mungu vilivyoahidi adhabu kali kuliko katiba zote za duniani, lakini wanadamu wanazivunja kila siku amri na katiba ya maisha ya baada ya haya, sembuse katiba isiyoziba mianya yote, la mwanadamu haliwezi kuwa Perfect 💯, Mtatengeneza katiba, lakini kutapatikana tu watu watakaoona mianya ya katiba hiyo na watajinufaisha kupitia udhaifu huo, hii ni lazima,

Katiba inahitajika, ila siyo dawa ya wavunja katiba, na wala haitasababisha tuishi kama peponi, Kwani Africa nzima hakuna nchi zenye katiba nzuri na bora?

Je kwao kukoje?

Tuitafuteni katiba kwa maelewano, Wale wanaoitaka, wasiitake kwa nguvu, wale wasiopenda wasiwazuie wanaoitaka kwa nguvu

Tujadiliane kwa upendo, ingawa kwangu mimi siiwekei umhumu na kuipa matumaini makubwa mno

Tujifunze kwa katiba za vyama vyetu,

Mungu Ibariki Tanzania
 
HII NDIO ORODHA YA MAKUNDI YA WATU WANAOHITAJI KATIBA MPYA

Na, Robert Heriel

Mjadala unaoendelea katika Siasa mitandaoni ni ishu ya Katiba.

Wanaohitaji Katiba Mpya wamegawanyika katika makundi Yafuatayo;

1. Wanasiasa hasa wa vyama vya Upinzani

2. Wanasiasa upande wa Zanzibar.

3. Wanaharakati wa mrengo wa kiliberali.

4. Wasomi wenye elimu kuanzia stashahada mpaka uzamivu. Wenye exposure ya dunia na wenye kutaka mabadiliko kwenye nchi.

Kiuchunguzi makundi hayo ukiyajumlisha ili upate idadi kamili basi ni wazi ni asilimia 20% tu ya Watanzania wote.

Makundi yasiyohitaji Katiba mpya na wala yasiyojishughulisha kama kujua kinachoendelea;

1. Wanawake wengi hapa nchini hawana mpango na ishu za Katiba mpya wala hawalijui Katiba ya zamani.

2. Vijana wa umri chini ya miaka 40 ambao wanaelimu ya chini na Hali zao za kimaisha ni duni. Hawa ukiwakuta kijiweni ukileta mambo ya Katiba mpya ndio utavuruga kila kitu. Kwanza hawatachangia mada. Kundi hili mada zake ni Udaku, mpira, kisha Diamond na Ally Kiba

3. Wana CCM
Kundi hili lipo lipo, hili ni Kama bendera, Inategemea serikali itakapoegemea. Serikali ikisema Katiba mpya ndio, nalo linasema Katiba mpya ndio, serikali ikisema hapana, nalo linasema hapana.

4. WAZEE Hasa wenye miaka kuanzia 60+
Kundi hili litasimama upande serikali ilipo. Kundi hili sio la kulaumiwa Kwa sababu wengi wao elimu Yao ni duni, exposure ya dunia iendavyo pia ni hafifu.

Kundi hili lisilohitaji au kujishughulisha na masuala ya Katiba ndilo kundi lenye watu wengi zaidi, karibu 80% hawana mpango wa Katiba mpya wala hawajihusishi na Siasa.

Uchunguzi wangu unaonyesha kuwa Watanzania wengi wanaamini katika serikali iliyopo madarakani, wanaiheshimu na kuigopa.
Hivyo serikali ikisema No! Basi watu nao watasema No!

Hata hivyo, uchunguzi wangu umebaini kuwa Watanzania wengi ni WANAFIKI, Unafiki wa Watanzania waliowengi unachangiwa kwa kiasi kikubwa cha Umasikini,
Ulimbukeni,
Elimu duni,
Woga na kujikomba Kwa wenye mamlaka.

Aidha Kama nilivyoeleza kwenye andiko langu lililopita ni kuwa, wanaodai Katiba mpya ni Kwa sababu ya mapungufu ya Katiba hii ambayo yanawafanya wasinufaike na Nchi yao.

Na wanaccm wengi wao hasa watawala, hawaoni Upungufu wa Katiba iliyopo hivyo inawanufaisha.

Kundi la mwisho ambalo ni wananchi ambao hawapo upande wowote hawa ni Bora liende, maisha yasonge, mauti ije, kaburini wafukiwe.

Binafsi, ninahitaji Katiba mpya itakayonufaisha makundi yote ya wananchi wa TANZANIA.

Hata hivyo, Siwezi kataa kuwa ndani ya jamii yangu, wananchi wengi hawana habari na Katiba mpya kwani wao ni Bora maisha siku ziende.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Uko sahihi. Ila, pamoja na wengi kutojua maana ya katiba na wengine kunufaika na katiba iliyopo; mazingira ya kijamii, kiuchumi na kisiasa Tanzania kwa sasa yanadai katiba mpya. Hii ninaifananisha na enzi za kudai uhuru. Ni aslimia ndogo sana ya raia wakati ule (Nyerere na raia wachache wengine) walijua maana na umhimu wa uhuru. Kwa uchache wao walipambana hadi uhuru ukapatikana. Hivyo hivyo, kwa uchache wetu, tuendelee kupambana hadi katiba mpya ipatikane. Tusichoke kupayuka: TUNATAKA KATIBA MPYA!!!?
 
Katiba inaumhimu wake ila si kwa kila kitu,

Mwanadamu si wa kudhibitiwa na katiba pekee, Ni nidhamu na kupenda haki ndiyo tunu kwa kila taifa

Ukitaka kufahamu kwamba katiba sio mwarobaini, Jifunze kwa vitabu vya Mungu vilivyoahidi adhabu kali kuliko katiba zote za duniani, lakini wanadamu wanazivunja kila siku amri na katiba ya maisha ya baada ya haya, sembuse katiba isiyoziba mianya yote, la mwanadamu haliwezi kuwa Perfect 💯, Mtatengeneza katiba, lakini kutapatikana tu watu watakaoona mianya ya katiba hiyo na watajinufaisha kupitia udhaifu huo, hii ni lazima,

Katiba inahitajika, ila siyo dawa ya wavunja katiba, na wala haitasababisha tuishi kama peponi, Kwani Africa nzima hakuna nchi zenye katiba nzuri na bora?

Je kwao kukoje?

Tuitafuteni katiba kwa maelewano, Wale wanaoitaka, wasiitake kwa nguvu, wale wasiopenda wasiwazuie wanaoitaka kwa nguvu

Tujadiliane kwa upendo, ingawa kwangu mimi siiwekei umhumu na kuipa matumaini makubwa mno

Tujifunze kwa katiba za vyama vyetu,

Mungu Ibariki Tanzania

Umenena
 
Hata kipindi cha Nyerere waliotaka vyama vingi walikuwa 20% tu ,haijalishi wanaotaka ni asilimia ngapi hata kama ni mmoja tu anataka na akawa na hoja zenye mashiko basi ana haki yake.

-Kuna mambo mengi sana ya hovyo yaliyopo kwenye katiba hii ambayo yanahitaji kuondolewa,eg kuna ulazima wa kuwa na utitiri wa RC,RAS,DAS,DC etc na kuongeza gharama kwa taifa? Rasimu ya Warioba ilikuwa nzuri maana ilikusanya maoni ya wananchi.
 
Pengine niwakumbushe, kupata Katiba nzuri ni kitu kimoja na kuheshimu Katiba ni kitu kingine. Katiba hii mbovu ya sasa yule Mwendazake alikuwa anaivunja anavyotaka. Tumpongeze kwanza huyu Samia ambaye anaiheshimu pamoja na mapungufu yake.

Kuna haja ya elimu ya Katiba kwa wananchi na kujenga utamaduni wa kuheshimu Sheria na taratibu. Maana tukipata Katiba mpya na ikashindwa kuheshimiwa, tutakuwa tumevikosea vizazi vijavyo
 
Hata kipindi cha Nyerere waliotaka vyama vingi walikuwa 20% tu ,haijalishi wanaotaka ni asilimia ngapi hata kama ni mmoja tu anataka na akawa na hoja zenye mashiko basi ana haki yake.

-Kuna mambo mengi sana ya hovyo yaliyopo kwenye katiba hii ambayo yanahitaji kuondolewa,eg kuna ulazima wa kuwa na utitiri wa RC,RAS,DAS,DC etc na kuongeza gharama kwa taifa? Rasimu ya Warioba ilikuwa nzuri maana ilikusanya maoni ya wananchi.
Ndiyo mkuu, lakini kipengele hiko ni sehemu ya mtu kuwa na ajira!! kumbuka hilo mkuu
 
Mazuzu mengi ya ccm hayajui hata faida ya katiba wao wanachojua ni mwenyekiti kasemaje yenyewe utasikia ndiiiiiiiooooooooooooo hata yakiambiwa leo kunya hapana yataitikia hivyo hivyo sababu yamekalili!
 
Uko sahihi. Ila, pamoja na wengi kutojua maana ya katiba na wengine kunufaika na katiba iliyopo; mazingira ya kijamii, kiuchumi na kisiasa Tanzania kwa sasa yanadai katiba mpya. Hii ninaifananisha na enzi za kudai uhuru. Ni aslimia ndogo sana ya raia wakati ule (Nyerere na raia wachache wengine) walijua maana na umhimu wa uhuru. Kwa uchache wao walipambana hadi uhuru ukapatikana. Hivyo hivyo, kwa uchache wetu, tuendelee kupambana hadi katiba mpya ipatikane. Tusichoke kupayuka: TUNATAKA KATIBA MPYA!!!?

Uko sahihi kabisa
 
Zote ni nchi
Ndugu Crimea kinachowaumiza Kenya pamoja na katiba yao nzuri ni zaidi issue ya ukabila (ambayo haikuletwa na katiba) lakini ni aina ya mfumo wa uchumi waliorithi kutoka kwa Muingereza (ubepari) ulisababisha land grubbing hivyo kuwaacha wengi wakiwa hawana ardhi na kutegema matajiri wachache! Lakini hii katiba yao inawapa nguvu ya juu ya kuwawajibisha viongozi wao! kitu ambacho tunakosa hapa Kwetu!
 
Pengine niwakumbushe, kupata Katiba nzuri ni kitu kimoja na kuheshimu Katiba ni kitu kingine. Katiba hii mbovu ya sasa yule Mwendazake alikuwa anaivunja anavyotaka. Tumpongeze kwanza huyu Samia ambaye anaiheshimu pamoja na mapungufu yake.

Kuna haja ya elimu ya Katiba kwa wananchi na kujenga utamaduni wa kuheshimu Sheria na taratibu. Maana tukipata Katiba mpya na ikashindwa kuheshimiwa, tutakuwa tumevikosea vizazi vijavyo

Upo sahihi Mkuu
 
Back
Top Bottom