Hii inamaanisha nini, BUNDI kukaa nje ya Nyumba zaidi ya Mwezi kila Usiku na haondoki?

Hii inamaanisha nini, BUNDI kukaa nje ya Nyumba zaidi ya Mwezi kila Usiku na haondoki?

VERBOSE

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
8,145
Reaction score
12,743
Wakuu wa Jukwaa, leo na mimi nina swali ambalo linakua linanitatiza sana kichwani kwangu kwa muda kidogo sasa.

Nimekua napitia hali ya kujiuliza maswali mengi sana juu ya kiumbe hiki kinachoitwa BUNDI. Bundi ni ndege mwenye sifa kede wa kede. Sitaki kuzungumzia sifa za ndege huyu, leo nimeona niwaulize km mimi ninavyojiuliza imewezekanaje ndege huyu kuishi tunapoishi kwa zaidi ya Mwezi?

Yaan anakuja kila usiku unapoingia kuanzia majira ya saa 4 - 6 mpaka 7 usiku BUNDI anakua kashafika tayari kwenye mazingira yake na anakaa palepale anapokaa siku zote kwenye mti ule ule anaosimamaga siku zote na anatazama uelekeo ule ule anaotazama siku zote (anatazama mlangoni watu wanapotokea na kuingia) yaan ukifungua mlango kwa ajili ya kutoka nje unakutana na BUNDI yupo juu ya mti anakutazama na anakukazia macho haswa, na haondoki hapo mpaka kunaenda kupambazuka saa 11 kuelekea 12 asubuhi ndio BUNDI anaondoka ni km amekuja kulinda nyumba au sielewi, ukimpita anageuza shingo, hapo kabla sikua najua nilikua nasikia tu na kujionea kwenye video za kule Utube km BUNDI anao uwezo wa kugeuza shingo yake kwa jinsi anavyotaka, hii nimejionea mubashara yaani nimejionea bure kabisa bila kwenda kwenye Mbuga au Hifadhi fulani na kulipa kiingilio ili nione.

Sasa basi leo naomba tujiulize kwa pamoja au km yupo mwenye kufahamu atufahamishe inawezekanaje BUNDI kukaa sehemu moja kila unapoingia usiku kwa zaidi ya Mwezi? Na anapofika BUNDI watu waliopo ndani ya nyumba hata waliopo nyumba za jirani usiku wanaweweseka sana, utasikia mtu anaweweseka huko unajua tu tayari BUNDI yupo nje hapo kashaweka kambi, na ukisikia mtu kaweweseka ukitoka tu nje ile kufungua geti tu unamuona bundi yule pale kwenye mti anakutazama, hii ina maana gani wakuu? BUNDI kuweka kambi kila usiku anatutazama nje wakati sisi tumelala ndani, hii inamaanisha nini?
 
Kuna mgonjwa hapo mnapoishi?
Mgonjwa wa nini? Ungefafanua vizuri mkuu kumbuka ni zaidi ya Mwezi yupo tena haji mmoja sasa wamekua wanakuja na wenzake watatu km sio wawili, sema huyo mmoja ndio anakua front line yeye ndio anasimama kwenye huo mti anatazama mlango kwa sana na anapenda sana kukaa kwenye huo mti na haogopi hata ukimsogelea (nimethubutu kufanya hivi) labda uonyeshe ishara za kutaka kumrushia kitu ndio anaruka (nilifanya hivyo pia) kisha anazunguka na kurudi tena kwenye ule ule mti
 
Wakuu wa Jukwaa, leo na mimi nina swali ambalo linakua linanitatiza sana kichwani kwangu kwa muda kidogo sasa.

Nimekua napitia hali ya kujiuliza maswali mengi sana juu ya kiumbe hiki kinachoitwa BUNDI. Bundi ni ndege mwenye sifa kede wa kede. Sitaki kuzungumzia sifa za ndege huyu, leo nimeona niwaulize km mimi ninavyojiuliza imewezekanaje ndege huyu kuishi tunapoishi kwa zaidi ya Mwezi?

Yaan anakuja kila usiku unapoingia kuanzia majira ya saa 4 - 6 mpaka 7 usiku BUNDI anakua kashafika tayari kwenye mazingira yake na anakaa palepale anapokaa siku zote kwenye mti ule ule anaosimamaga siku zote na anatazama uelekeo ule ule anaotazama siku zote (anatazama mlangoni watu wanapotokea na kuingia) yaan ukifungua mlango kwa ajili ya kutoka nje unakutana na BUNDI yupo juu ya mti anakutazama na anakukazia macho haswa, na haondoki hapo mpaka kunaenda kupambazuka saa 11 kuelekea 12 asubuhi ndio BUNDI anaondoka ni km amekuja kulinda nyumba au sielewi, ukimpita anageuza shingo, hapo kabla sikua najua nilikua nasikia tu na kujionea kwenye video za kule Utube km BUNDI anao uwezo wa kugeuza shingo yake kwa jinsi anavyotaka, hii nimejionea mubashara yaani nimejionea bure kabisa bila kwenda kwenye Mbuga au Hifadhi fulani na kulipa kiingilio ili nione.

Sasa basi leo naomba tujiulize kwa pamoja au km yupo mwenye kufahamu atufahamishe inawezekanaje BUNDI kukaa sehemu moja kila unapoingia usiku kwa zaidi ya Mwezi? Na anapofika BUNDI watu waliopo ndani ya nyumba hata waliopo nyumba za jirani usiku wanaweweseka sana, utasikia mtu anaweweseka huko unajua tu tayari BUNDI yupo nje hapo kashaweka kambi, na ukisikia mtu kaweweseka ukitoka tu nje ile kufungua geti tu unamuona bundi yule pale kwenye mti anakutazama, hii ina maana gani wakuu? BUNDI kuweka kambi kila usiku anatutazama nje wakati sisi tumelala ndani, hii inamaanisha nini?
Chunguza vizuri.
Kwako au kwa majirani ikiwa ni pamoja na nje ya nyumba kuna panya, fuko na vyakula vingine vinavyopendwa na bundi.
 
Nimeuliza BUNDI anakula Popo?
Ndio.


Many species of owls are opportunistic predators that hunt and eat bats. Due to shared nocturnal habits, owls like the Great Horned Owl, Barn Owl, and Tawny Owl often catch bats in flight or near roosting sites. While rodents are a more common food source, owls will readily prey on bats, sometimes waiting at entrances to snatch them as they emerge.
 
Ndio.


Many species of owls are opportunistic predators that hunt and eat bats. Due to shared nocturnal habits, owls like the Great Horned Owl, Barn Owl, and Tawny Owl often catch bats in flight or near roosting sites. While rodents are a more common food source, owls will readily prey on bats, sometimes waiting at entrances to snatch them as they emerge.
Basi nimeshajua kwanini BUNDI wameweka kambi hapa na hawaondoki kuna Popo nadhani ndio wanaowawinda kila siku usiku, yes hapa Popo wapo kila siku usiku lazima Popo waje, je Popo wanakula nini kingine ukiondoa Mapapai?
 
Back
Top Bottom