Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe

Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe

Kuna wakati alikuwa anawaambia watu kujipamba ni dhambi,
akawavua dhahabu zao shingoni na vikuku vyao miguuni;
......... swali
  • Ziko wapi zile dhahabu?


  • Na je hizo sadaka mnazotoa ina maana halipwi mshahara?
Unakumbuka maneno haya:
1.Waumini wa kakobe ni masikini
2.Kakobe anavua dhahabu za waumini
3.Viongozi wa dini wasishiriki siasa
4.Viongozi wa dini waombee amani
 
mtoto wake Eze kakobe anendesha noah new model na ana video studio yenye vifaa vya kisasa and expensive
1.Kakobe ametoroka kuelekea Marekani na familia yake
2.Mtoto wa kakobe anaendesha Noah new Model
3.Mtoto wa Kokobe ana miliki studio ya kisasa.

Nataka utueleze je unasahau uongo uliopita??
 
Ninyi washirika wa Kakobe kweli hamumtakii mema Kakobe wenu... Sasa tutaenda hata kwenye Mavazi yake Kakobe... Mbona Kakobe Suti anazovaa ni ghali sana?? Nionavyo ni kwamba jumla ya pesa au gharama ya nguo anazovaa Kakobe ni kama gharama ya Gari.... Sasa kuwa na gari au magari, nini ishu??
Hizo suti kapewa kule aliko enda kuhubiri na waliompa wameonekana wakifanya hivyo.

hata hivyo ni vigumu gharama za suti zilingane na gari labda kwa wajinga wanweza kuamni
 
Mmh ndugu yangu, imani ni kitu cha kipekee sana. Unakumbuka kesi ya Kibwetere? Kuna mtu alienda polisi kushitaki kuwa wanakaribia kuchomwa? Nimetoa mfano tu wa imani, sihusishi habari ya dhahabu na baba Askofu kwa kuwa si mshirika wa kanisa hilo hivyo siwezi kuyajua ya humo.

Kibwetere alifanya utapeli ule kupitia kanisa Katoliki na Utawala wa katoliki hapa nchini ulikemea sana hilo na kuwatahadharisha waumini wake .Muulize Pengo atakwambia!!
 
Nani aje kuyumbishwa mimi simuabudu mtu namuabudu mungu nyie endeleeni kumtafutia huyo jamaa maisha bora kwa sasa hana mpya tena ndio anatafuta pa kuanzia ndo mana unaona yote haya yameanza. Zite ni promo tu wasio na akili waende imani gani ya kujitajirisha mchungaji huku waumini wakizidi kudhoofika siku hadi siku.
Hata mimi naamini kuwa unamwabudu mungu!!
Staili ya maneno yako tangia mwanzo yameonekana!!
 
Baada ya kuona watu hawaitaji tena kuibiwa naona umekuja na mpya ili upate tena wakuwavua midhahabu yao.
1.Waziri Ernest alikuja na agenda ya upuuzi kama huu kuwa kakobe anaiba dhahabu wakati yeye yuo serikalini
2.Hijawahi kuripotiwa na mtu yoyote kuwa ameibiwa dhahabu zaidi sana Rais Mwinye kwa wakati ule mkewe alikamatwa na dhahabu uwanja wa ndege akisafirisha nje ya nchi
3.CCM walifuatilia na kusema waumini wa Kakobe ni masikini

Naona wewe humwamini mtu ila unamuabudu mungu!!
 
Pesa huwa haijifichi kiukweli. Huyu mtu yamkini ni mwema.
 
Hii ni mbinu mpya ya kuwachokoza watumishi wa Mungu waanike utajiri wao. Asante kwa mbinu yako lakini sidhani hii inatosha kumfanya huyo mtumishi tajwa aje humu JF. Pole, tafuta mbinu mbadala.
Weye , unapokuja na mbinu hizi unataka kutuambia kuwa kila mtu ana malengo ya kufanana na weye? Kwani lazima ajenge nyumba ya kifahari hapa Dar? Mbona unamdhalilisha mtumishi wa Mungu tena mwenye matawi mpaka USA??
Mwambiye awafundishe waumini wake kutoa na kuwajali wahudumu wao, huenda hilo ndo tatizo.
 
Turudi na kuijadili mada yenyewe, "Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe".Ukweli umewekwa hapa na mwenye kuukanusha ukweli huu alete ushahidi usio na shaka hapa JF.Uongo na uzushi sikuzote haulipi!
 
Sikuzote penye ukweli uongo hujitenga, "Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe".Ukweli umewekwa hapa na mwenye kuukanusha ukweli huu alete ushahidi usio na shaka hapa JF.Uongo na uzushi sikuzote haulipi!Ukweli ndio unaoweza kutuweka huru.Nathibitisha bila unafiki wowote ndani yangu kwamba ni kweli kwa asilimia zote hii ndiyo nyumba pekee ya Askofu Kakobe.
 
Unafahamu umiliki wa hiyo gari uliyotaja ??

Kama upo TRA au serikalini kabla hujajibu hili yueleze tujue, mimi najua sasa wewe unapotukana watu huku ukiwa hujui sasa hapa ni kazi!!
Mimi nakuambia mtu yule hana Acount katika benki yoyote na hata alipokwenda DRC watu wote waliochangia michango yao iliwekwa wazi kwenye TV jambo lililo washangaza wengi sasa usiwafanye watu wajinga wakati upo ushahidi wa maandishi

kwahyo amekutuma kuwa utuelezee sifa zake?? Mungu wake ndio najua yote huo utenda mema wake au mabaya sisi hautuhusu. Tatizo wanadamu tunapenda kujionesha mbele ya watu kama watenda mema ila tunasahau kuwa Mungu huona yote yaliyogizan na kwenye nuru......... Mtu wa Mungu watamtambua tu, kwamaneno na kwa matendo lakin hata hvyo tukumbuke haya" kuwen makin wala msidanganywe, siku za mwisho wengi watakuja kwa jina langu na kusema mm ni kristo, na watafanya miujiza ya kila aina watawaponya watu magonjwa na watawaombea wenye shida mbalimbali lakin nyinyi msiende huko". Kwahyo ww bwana kama kakobe ni mtu wa mungu bas aongezewe baraka zaidi lakin kama ni nabii wa uwongo Mungu ndiye atatenda yote.
 
Heeeeee sasa anawaombea wenzie waendeshe ma-benz kumbe yeye hana ni wehu huu anasema watapata majumba ya kifahari wakati yeye anaishi kwenye kibanda ni uwendawazimu basi,waibieeeee kaka Zaka.
 
Halafu unaponiambia nirudi kwenye MADA na kuniletea mistari ya kwenye Biblia ndio sikuelewi kabisa ni
NANI ALIYETOKA kwenye MADA mm na wewe?
mbona mnatudanganya hana nyumba wakati ana mahekalu kwa kukusanya sadaka na vidani vya kina-Mama?
\

Soma Isaya 42;1-4 kuhusu Mtumishi wa MUNGU
Isaya 42;2 Hatalia wala kupiga kelele wala hatapaza sauti yake barabarani

au Mathayo 12;15-21 Mtumishi mteule wa MUNGU
Mathayo 15;18Tazama Mtumishi wangu niliyemteua .......................nitaiweka Roho yangu juu yakenaye atatangaza hukumu yangu kwa mataifa yote
Mathayo 15;19 hatakuwa na ubishi wala kupiga kelele wala sauti yake haitasikika barabarani


(Kakobe hana sifa hizo asilani kwani ni mropokaji na ni mtu anayeshindana na Dola (Ikulu, Siasa, Tanesco, Uchangzi kumpigia debe Mrema)

ASKOFU KAKOBE AKIMBIA NCHI - Global Publishers

Hili Jengo ni mali ya nani?
na ni kwanini alilibadilisha jina na ninyi Waumini wake (Walokole wa FGBH
) na kuliita "Bishop Zacharia Kakobe International Ministry"
Acheni kutudanganya ana kajumba kamoja

Exposed From The Source.....Askofu Kakobe Kuhamia America? | Sam Sasali Ze Blogger

Huduma za Kimataifa za Injili bado ni jambo geni sana katika nchi yetu ya Tanzania kwa sababu tuna Wahubiri wachache sana wa Kimataifa walio na neema ya kufanya Mikutano ya Injili ya malaki ya watu katika nchi nyingine duniani kama ilivyo kwa wahubiri wengine wa Kimataifa kwa mfano, Reinhard Bonnke, Benny Hinn n. k. Kwa sababu hii watu wasioelewa jinsi Huduma hizi zinavyofanya kazi, ndiyo wanaoweza kufikiri kwamba Kanisa la FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP limebadili jina na kuwa BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES, kutokana na kukosa uelewa.


Kanisa la FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP halijawahi kubadili jina lake wala halitabadili jina lake, na waumini wa FGBF, wote tunajua jambo hili. Hata hivyo ni muhimu kufahamu kwamba wito wa mwasisi wa Kanisa hili, Askofu Mkuu Zachary Kakobe sio kuhubiri Tanzania tu bali kuhubiri kote ulimwenguni. Katika maono hayo, Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship linahubiri Injili Tanzania na kufungua makanisa kote nchini. Hata hivyo katika kuenenda ulimwenguni kote, huko hatuendi kuanzisha Makanisa ya Full Gospel Bible Fellowship kila nchi, kwasababu muda uliosalia kabla ya Yesu kurudi ni mchache mno. Biblia inasema katika WAEBRANIA 10:37, "Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye anakuja, wala hatakawia. " Kwa sababu hii, badala ya kufungua makanisa ya FGBF nchi nyingine ulimwenguni, Mtumishi wa Mungu, Askofu Kakobe hushirikiana na madhehebu yote ya Kiinjili ya nchi hizo katika kuwaleta watu wengi kwa Yesu. Hufanya hivyo, kwa kufanya Mikutano Mikubwa ya Injili, inayokwenda sambamba na Konferensi za Wachungaji, ambao hufundishwa jinsi ya kukuza Makanisa yao, na kuwekewa mikono, ili kuchochea karama zilizomo ndani yao.


Mikutano hii Mikubwa ya Injili, katika baadhi ya nchi hizo, hukusanya makumi elfu elfu ya watu mahali pamoja, kama picha mbili hizi hapa chini zinavyoonesha sehemu ya umati wa watu waliokuwa wakihudhuria kila siku, na pia kukata shauri kuokoka, katika Mkutano alioufanya Askofu Kakobe, Oktoba mwaka jana 2013, huko Congo (DRC), katika Jiji la LUBUMBASHI:

attachment.php



attachment.php



Sasa basi, ni muhimu kufahamu kwamba, ni vigumu kwa Kanisa moja kutoka nje ya nchi kuandaa Mkutano unaoweza kukusanya watu wengi kiasi hiki, katika nchi nyingine. Kwa mfano, Mkutano huu wa Lubumbashi uliandaliwa na Makanisa tofauti zaidi ya 300. Mamia ya Maaskofu na Wachungaji hukusanya nguvu, na kuunda kamati mbalimbali za maandalizi. Mambo mengi huhitajika kufanikisha Mkutano wa Injili kama huu, ikiwemo upatikanaji wa maelfu ya Wahudumu, kutoka katika mamia ya Makanisa.


Ni muhimu pia kufahamu kwamba, kama Mhubiri atakwenda katika Jiji fulani, lililoko nchi fulani, kwa jina la dhehebu au Kanisa lake, kwa mfano FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP, halafu akataka mamia ya Maaskofu na Wachungaji pamoja na Makanisa au madhehebu yao tofauti tofauti, kumpa ushirikiano kuandaa Mkutano Mkubwa wa Injili, ni vigumu kwa Watumishi hao kumpa ushirikiano. Hofu yao kubwa, huwa ni Mhubiri huyo kutaka kuanzisha Kanisa lake katika mji huo, kwa kutumia mgongo wa Watumishi hao wa Mungu, na Makanisa yao. Mamia ya Makanisa, huwa tayari tu kumpokea Mhubiri kama watajua kwamba siyo tu karama mbalimbali hutenda kazi ndani yake, bali pia Mhubiri atahakikisha kwamba haendi huko kuanzisha Kanisa, bali anakwenda kuyasaidia Makanisa yao kuimarika, na kwamba waumini wapya katika Mkutano huo, watajiunga na Makanisa yao. Watumishi wa Mungu, hupenda kuipokea huduma ya yeye Mhubiri kama yeye tu, na siyo Kanisa au dhehebu lake.


Kwa sababu hiyo, kote ulimwenguni, Wahubiri wakubwa wa Kimataifa, huenda wao kama wao, kuhubiri katika nchi nyingine, na hawaendi huko kwa jina la Makanisa au madhehebu yao, ili wakubalike kwa Wachungaji wa madhehebu yote. Kwa mfano, Mhubiri wa Kimataifa kutoka Marekani, BENNY HINN, ni Mchungaji wa Kanisa lake linaloitwa WORLD HEALING CENTER CHURCH, lakini anapoenda kuhubiri ulimwenguni, haendi kwa jina la Kanisa lake, bali huenda kwa huduma ya yeye kama yeye, BENNY HINN MINISTRIES. Asipofanya hivyo, hawezi kupewa ushirikiano na Watumishi wa madhehebu tofauti. Vilevile Mhubiri mwingine wa Kimataifa kutoka Marekani, ERNEST ANGLEY, huyu ni Mchungaji wa Kanisa lale la GRACE CATHEDRAL, lakini anapoenda ulimwenguni kote kuhubiri, huenda kwa huduma ya yeye Mhubiri kama yeye, ERNEST ANGLEY MINISTRIES, ili apokewe na madhehebu yote, n.k. Miezi michache iliyopita alikuja Tanzania, Mhubiri wa Kimataifa, REINHARD BONNKE. Huyu naye hakuja kama Kanisa, angefanya hivyo, isingekuwa rahisi kukubalika kwa madhehebu yote. Wahubiri wa Kimataifa kote duniani, hufanya hivihivi.


Kwa msingi huu sasa, Askofu Kakobe anapokwenda kuhubiri kote ulimwenguni, mbali na Tanzania, huenda kwa huduma ya yeye Mhubiri, kama yeye, BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES. Likienda kama Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, haliwezi kupokelewa na madhehebu mengi tofauti. Yadhuru nini, hatuko hapa kujenga ufalme wa dhehebu, bali Ufalme wa Mungu. Furaha yetu ni kuona wengi wanampokea Yesu kila mahali duniani, na wengi wakiongezeka katika Ufalme wa Mungu. Huduma ya BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES imesajiliwa Marekani na pia Canada. Kutokana na sheria za nchi hizo, mambo mengi ya Injili hayawezi kufanyika mpaka huduma husika ya Injili iwe inatambulika kwao kisheria. Nchi hizo, na hata nchi nyingi nyingine zilizoendelea, huwa ni vigumu kuipokea huduma iliyosajiliwa katika nchi za Afrika, kwa sababu huidharau Afrika, na kujiona wao ndiyo watawala wa dunia. Unaweza kupata mengi zaidi kuhusu utendaji wa huduma ya BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES, kwa kutembelea http://www.bishopzacharykakobe.org
 
Huduma za Kimataifa za Injili bado ni jambo geni sana katika nchi yetu ya Tanzania kwa sababu tuna Wahubiri wachache sana wa Kimataifa walio na neema ya kufanya Mikutano ya Injili ya malaki ya watu katika nchi nyingine duniani kama ilivyo kwa wahubiri wengine wa Kimataifa kwa mfano, Reinhard Bonnke, Benny Hinn n. k. Kwa sababu hii watu wasioelewa jinsi Huduma hizi zinavyofanya kazi, ndiyo wanaoweza kufikiri kwamba Kanisa la FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP limebadili jina na kuwa BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES, kutokana na kukosa uelewa.


Kanisa la FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP halijawahi kubadili jina lake wala halitabadili jina lake, na waumini wa FGBF, wote tunajua jambo hili. Hata hivyo ni muhimu kufahamu kwamba wito wa mwasisi wa Kanisa hili, Askofu Mkuu Zachary Kakobe sio kuhubiri Tanzania tu bali kuhubiri kote ulimwenguni. Katika maono hayo, Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship linahubiri Injili Tanzania na kufungua makanisa kote nchini. Hata hivyo katika kuenenda ulimwenguni kote, huko hatuendi kuanzisha Makanisa ya Full Gospel Bible Fellowship kila nchi, kwasababu muda uliosalia kabla ya Yesu kurudi ni mchache mno. Biblia inasema katika WAEBRANIA 10:37, "Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye anakuja, wala hatakawia. " Kwa sababu hii, badala ya kufungua makanisa ya FGBF nchi nyingine ulimwenguni, Mtumishi wa Mungu, Askofu Kakobe hushirikiana na madhehebu yote ya Kiinjili ya nchi hizo katika kuwaleta watu wengi kwa Yesu. Hufanya hivyo, kwa kufanya Mikutano Mikubwa ya Injili, inayokwenda sambamba na Konferensi za Wachungaji, ambao hufundishwa jinsi ya kukuza Makanisa yao, na kuwekewa mikono, ili kuchochea karama zilizomo ndani yao.


Mikutano hii Mikubwa ya Injili, katika baadhi ya nchi hizo, hukusanya makumi elfu elfu ya watu mahali pamoja, kama picha mbili hizi hapa chini zinavyoonesha sehemu ya umati wa watu waliokuwa wakihudhuria kila siku, na pia kukata shauri kuokoka, katika Mkutano alioufanya Askofu Kakobe, Oktoba mwaka jana 2013, huko Congo (DRC), katika Jiji la LUBUMBASHI:

attachment.php



attachment.php



Sasa basi, ni muhimu kufahamu kwamba, ni vigumu kwa Kanisa moja kutoka nje ya nchi kuandaa Mkutano unaoweza kukusanya watu wengi kiasi hiki, katika nchi nyingine. Kwa mfano, Mkutano huu wa Lubumbashi uliandaliwa na Makanisa tofauti zaidi ya 300. Mamia ya Maaskofu na Wachungaji hukusanya nguvu, na kuunda kamati mbalimbali za maandalizi. Mambo mengi huhitajika kufanikisha Mkutano wa Injili kama huu, ikiwemo upatikanaji wa maelfu ya Wahudumu, kutoka katika mamia ya Makanisa.


Ni muhimu pia kufahamu kwamba, kama Mhubiri atakwenda katika Jiji fulani, lililoko nchi fulani, kwa jina la dhehebu au Kanisa lake, kwa mfano FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP, halafu akataka mamia ya Maaskofu na Wachungaji pamoja na Makanisa au madhehebu yao tofauti tofauti, kumpa ushirikiano kuandaa Mkutano Mkubwa wa Injili, ni vigumu kwa Watumishi hao kumpa ushirikiano. Hofu yao kubwa, huwa ni Mhubiri huyo kutaka kuanzisha Kanisa lake katika mji huo, kwa kutumia mgongo wa Watumishi hao wa Mungu, na Makanisa yao. Mamia ya Makanisa, huwa tayari tu kumpokea Mhubiri kama watajua kwamba siyo tu karama mbalimbali hutenda kazi ndani yake, bali pia Mhubiri atahakikisha kwamba haendi huko kuanzisha Kanisa, bali anakwenda kuyasaidia Makanisa yao kuimarika, na kwamba waumini wapya katika Mkutano huo, watajiunga na Makanisa yao. Watumishi wa Mungu, hupenda kuipokea huduma ya yeye Mhubiri kama yeye tu, na siyo Kanisa au dhehebu lake.


Kwa sababu hiyo, kote ulimwenguni, Wahubiri wakubwa wa Kimataifa, huenda wao kama wao, kuhubiri katika nchi nyingine, na hawaendi huko kwa jina la Makanisa au madhehebu yao, ili wakubalike kwa Wachungaji wa madhehebu yote. Kwa mfano, Mhubiri wa Kimataifa kutoka Marekani, BENNY HINN, ni Mchungaji wa Kanisa lake linaloitwa WORLD HEALING CENTER CHURCH, lakini anapoenda kuhubiri ulimwenguni, haendi kwa jina la Kanisa lake, bali huenda kwa huduma ya yeye kama yeye, BENNY HINN MINISTRIES. Asipofanya hivyo, hawezi kupewa ushirikiano na Watumishi wa madhehebu tofauti. Vilevile Mhubiri mwingine wa Kimataifa kutoka Marekani, ERNEST ANGLEY, huyu ni Mchungaji wa Kanisa lale la GRACE CATHEDRAL, lakini anapoenda ulimwenguni kote kuhubiri, huenda kwa huduma ya yeye Mhubiri kama yeye, ERNEST ANGLEY MINISTRIES, ili apokewe na madhehebu yote, n.k. Miezi michache iliyopita alikuja Tanzania, Mhubiri wa Kimataifa, REINHARD BONNKE. Huyu naye hakuja kama Kanisa, angefanya hivyo, isingekuwa rahisi kukubalika kwa madhehebu yote. Wahubiri wa Kimataifa kote duniani, hufanya hivihivi.


Kwa msingi huu sasa, Askofu Kakobe anapokwenda kuhubiri kote ulimwenguni, mbali na Tanzania, huenda kwa huduma ya yeye Mhubiri, kama yeye, BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES. Likienda kama Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, haliwezi kupokelewa na madhehebu mengi tofauti. Yadhuru nini, hatuko hapa kujenga ufalme wa dhehebu, bali Ufalme wa Mungu. Furaha yetu ni kuona wengi wanampokea Yesu kila mahali duniani, na wengi wakiongezeka katika Ufalme wa Mungu. Huduma ya BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES imesajiliwa Marekani na pia Canada. Kutokana na sheria za nchi hizo, mambo mengi ya Injili hayawezi kufanyika mpaka huduma husika ya Injili iwe inatambulika kwao kisheria. Nchi hizo, na hata nchi nyingi nyingine zilizoendelea, huwa ni vigumu kuipokea huduma iliyosajiliwa katika nchi za Afrika, kwa sababu huidharau Afrika, na kujiona wao ndiyo watawala wa dunia. Unaweza kupata mengi zaidi kuhusu utendaji wa huduma ya BISHOP ZACHARY KAKOBE INTERNATIONAL MINISTRIES, kwa kutembelea http://www.bishopzacharykakobe.org
****************************************************************************************
Huu ni ufafanuzi mzuri sana na mtu yeyote mwenye nia safi na anayetaka kuelewa anaelewa kama nilivyoelewa.Safi sana!
 
da hii habari imekaa kiumbea umbea hivi na kusafishana aisee sasa we ni mke,dada, kaka, shemeji, mfaidikaji wa sadaka, ndugu tu au muumini???
 
".......kama maskini, bali tukitajirisha wengi...." (2WAKORINTHO 6:10).

kama hayo maswali yote hapo umejibu kwa mstari mmoja!! nisaidie kitu kimoja hebu nipe hilo fungu lako kuanzia 6:4-12, wewe ubandike hapa. Kwa msaada wa walio wengi!

Haya mtumishi wenye akili tumekuelewa, mpe salam baba Askofu Kakobe

SP
 
Kama hayo unayosema na kuandika hapa ni kweli basi mimi binafsi natilia shaka huduma ya askofu Kakobe.
Mungu ni tajiri sana, kila kitu anacho, na mtumishi wake yeyote akiomba lolote atapata, leo Askofu kakobe amejenga nymba kabla ya kuwa mchungaji kisha askofu, na tangu apate ufunuo na kumtumikia Mungu wake amempa nini? na je anamtumikia huyu mungu mwenye nguvu mwenye kila kitu? je yeye amemuomba nini huyo mungu wake?
Labda pia unisaidie, kujua hili Je kuna sifa gani kwa mtumishi wa Mungu mwenyewe kuwaombea waumini wake na kupata mafanikio kutoka kwa huyo mungu ili hali yeye hana mafanikio? au ina maana yeye hana uwezo wa kuwaombea waumini/wafuasi wake wakapata mafanikio?

Pengine labda utuambie Askofu kakobe kuishi nyumba hiyo na wewe kuwa muumini wake wa miaka 25, inatufundisha nini?, au wewe umejifunza nini kutoka kwa askofu wako huyo? unaposema hana Hela wala nyumba (hivo hana mali zingine) zaidi ya hiyo nyumba unataka sisi tuelewe nini?, hapokei sadaka kanisani? au ana matumizi mabaya ya fedha za kanisa?, mtu wa anasa asiye penda maendeleo? hebu tuelezee kwa mapana

nakutakia ibada njema mlokole wa FGBF
SP

Ahsante baba/ mama..... Mungu akuzidishie Rehema na akili ya kuuliza
 
Kwa nini useme "mbona kama", si utembelee eneo hilo ukajionee mwenyewe, mbona ni hapahapa Bongo!

picha zinaonyesha hakuna sababu ya kutembelea. Au labda zilipigwa kipindi kile kazamia nje ya nchi.
 
picha zinaonyesha hakuna sababu ya kutembelea. Au labda zilipigwa kipindi kile kazamia nje ya nchi.

Zaidi ya saa 24 sasa zimepita tangu uzi huu uwekwe hapa, na hakuna hata mtu mmoja duniani aliyeweka hapa vielelezo vya majumba ya kifahari na maisha ya kifahari ya Askofu Kakobe. Zilizoko hapa tu muda wote ni blabla tu za "labda". Baadhi ya Watanzania, wanapenda kukaririshwa tu maneno ya mitaani ya "redio mbao"! Tujifunze kutokuamini kila jambo na kulisambaza kwa wengine, bila sisi wenyewe kulifanyia utafiti. Matokeo ya uongo, siku zote ni fedheha!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom