Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe

Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe

Mara nyingi hawa watumishi feki wanaweka pesa zao ndani,wanachimba chini kisha wanatunza madola tu.Nadhani Kakobe atakuwa na dola bilioni 1.Msanii Gwajima atakuwa na dola bilioni 2 kwa maana yeye sadaka zote anatia kwapani,hataki hata kununua eneo ajenge.mama rwakatare atakuwa na bilioni 3,Yule mwenye bank atakuwa na bilioni 5,lusekelo nae yuko nyuma yao na anawakimbiza kwa hasira atakuwa na milioni 7.Waacheni wajinga waliwe,hawajazimishwa.

akizichimbia ardhini yeye zinamsaidia nini hizo pesa? ifikie hatua tusiwe tunakubalikubali tu maneno ya mtaani bila kuangalia japo tu kama yana logic
 
Kwa nini useme "mbona kama", si utembelee eneo hilo ukajionee mwenyewe, mbona ni hapahapa Bongo!

Mimi namjuwa Kakobe tangu anauza kanda za kaseti Temeke lakini nilikuwa mdogo kiumri, nyumbani kwake kakobe anaishi maisha ya Mtanzania wa kawaida kabisa wala hana chembe ya ufahari ndani ya sitting room yake au nyumbani kwake kiujumla.

Mwisho mtumishi huyu hana account yoyote kwenye benki yoyote hapa duniani yeye kama Kakobe.
Je unalijuwa hili?
 
I have research & I have right to speak too.
Am christian lakini kuhusu Kakobe nilichosema ndio ukweli wenyewe na kama si kweli basi Jaji aliyekuwa au anayesikiliza shauri la kakobe kuhusu ubadhirifu ndio muongo.

Bahati mbaya hapa natumia simu ningekushushia vitu ungeshaa mwenyewe incase kama ulikuwa huujui ukweli.

Sina sababu wala maslahi yoyote ya kumzushia mtumishi huyu na mimi ni mmoja ninayevutiwa na mahubiri yake lakini hainibani kusema ukweli.

Kakobe anatembelea gari aina ya Nissan Patrol ambayo inamilikuwa na kanisa, na mwisho wa siku kanisa ni kakobe.

Jaji alikuwa anapiga porojo tu wakati wa Mediation. Hiyo haikuwa "hearing"! Kumbe hujazijua porojo za Jaji Augustine Shangwa, kwenye "mediation". Kaulize Mahakama Kuu, watakuambia!
 
Jaji alikuwa anapiga porojo tu wakati wa Mediation. Hiyo haikuwa "hearing"! Kumbe hujazijua porojo za Jaji Augustine Shangwa, kwenye "mediation". Kaulize Mahakama Kuu, watakuambia!

Pasco naomba unisaidie hapa maana nilikuwa sijui kama majaji wanaporojo kazini.
 
Last edited by a moderator:
Siyo kweli kwamba anawavua watu dhahabu. Ajitokeze hapa hata mtu mmoja aliyewahi kuvuliwa dhahabu zake, na Kakobe,halafu akazichukua. Hayo ndiyo hayohayo ya kusikia tu! Kweli inawezekana akawavua watu dhahabu, asiwepo hata mmoja wa kwenda kumshitaki Polisi, miaka yote 25? Tembea vituo vyote vya Polisi, hakuna taarifa yoyote iliyopelekwa ya mtu kuvuliwa dhahabu na Kakobe. Anachofanya Kakobe ni kufundisha Neno la Mungu linalosema kujipamba kwetu hakupaswi kuwa kwa dhahabu, bali kwa utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani roho ya upole na utulivu, kama wanawake watakatifu wa zamani, kwa mfano Sara (1PETRO 3:1-6; 1TIMOTHEO 2:9). Mtu aliyedhamiria kuongozwa na Neno la Mungu (ZABURI 119:9), akijifunza hivyo, akifika nyumbani kwake, kwa hiari yake hukongoroa mapambo yake, na kujua mwenyewe pa kuyapeleka. Je, anapata mshahara? Bila shaka anahudumiwa na Kanisa, ndiyo maana anapata chakula na mahitaji mengine ya kawaida ya maisha.

Mmh ndugu yangu, imani ni kitu cha kipekee sana. Unakumbuka kesi ya Kibwetere? Kuna mtu alienda polisi kushitaki kuwa wanakaribia kuchomwa? Nimetoa mfano tu wa imani, sihusishi habari ya dhahabu na baba Askofu kwa kuwa si mshirika wa kanisa hilo hivyo siwezi kuyajua ya humo.
 
Watu wengine ni wapuuzi sana. Eti mtu amefanya kazi ya injili karibu miaka 30 mtaka asiwe na mafanikio?. Yaani nilitegemea awe hata kaghorofa kadogo kwani watu wanaohitaji huduma yake ni wengi na wapo matajiri na maskini hivyo kuimarika kwake kiuchumi lingekuwa jambo la kheri tu. Au mlitaka mbanane naye kwenye dalala au watoto wake waende st kayumba bila viatu wakati anao waumini wanamiliki shule za kimataifa ambo wamesaidiwa naye.
 
Unataka wanakondoo waliokimbia warudi harudi mtu huko kwa msanii huyo wamerudi kundini
 
Ni uongo usiopingika mnapiga nani mchanga wa macho hiyo nyumba hatukatai kama si yake ila kwa sasa labda inafugia mambo yake yale anayofataga nigeria, ehee endelea kutudanganya sasa tupia na picha ya ka mark 11 ambako atakuwa anatembelea kuingia nayo humu alafu cheza na kila kitu sio jf utaletewa mambo ya huyo kakobe wako hapa ni vithibitisho utafute pa kuweka uzi wako we subiri kama huamini.
 
Mkuu kwan umetumwa kumsafisha KAkoBE? Kama c hvyo bas anaeleta huu uzi n hyo mtumishi mwenyewe ambae anataka kujua atmosphere ya watu.
Kunavitu ambavyo huwezi kuacha kujiuliza hivi wakati anasema Lazima mLEMa awe rais hakuwa na huyu!? Je siasa na din vinawiana? Majengo aliyojenga ya kuabudia ni nguvu za waumin wa maeneo husika,au mchango kidogo,
Njoo na hoja mpya kumsafisha,na kama anaajenda ya kugombea ubunge/urais umekula kwake!
 
Ni uongo usiopingika mnapiga nani mchanga wa macho hiyo nyumba hatukatai kama si yake ila kwa sasa labda inafugia mambo yake yale anayofataga nigeria, ehee endelea kutudanganya sasa tupia na picha ya ka mark 11 ambako atakuwa anatembelea kuingia nayo humu alafu cheza na kila kitu sio jf utaletewa mambo ya huyo kakobe wako hapa ni vithibitisho utafute pa kuweka uzi wako we subiri kama huamini.

Porojo hizi, hapa siyo mahali pake, kinachotakiwa hapa ni kwamba kama huu ni uongo, wenye ukweli ulio na vithibitisho, waumwage hapa. Kama wewe unajua mambo hayo ya Nigeria, yaweke hapa na uthibitisho. Kama unadanganywa, basi lete ukweli halisi hapa, siyo propaganda hizi nyepesi. Njia ya mwongo ni fupi!
 
Ni uongo usiopingika mnapiga nani mchanga wa macho hiyo nyumba hatukatai kama si yake ila kwa sasa labda inafugia mambo yake yale anayofataga nigeria, ehee endelea kutudanganya sasa tupia na picha ya ka mark 11 ambako atakuwa anatembelea kuingia nayo humu alafu cheza na kila kitu sio jf utaletewa mambo ya huyo kakobe wako hapa ni vithibitisho utafute pa kuweka uzi wako we subiri kama huamini.
Mkuu hapo ndio nyumbani kwake kijitonyama hilo wala halina mjadala na hata kijijini kwao mama yake anaishi maisha na nyumba ya kawaida tu au unaweza kuiita duni.
 
Mkuu kwan umetumwa kumsafisha KAkoBE? Kama c hvyo bas anaeleta huu uzi n hyo mtumishi mwenyewe ambae anataka kujua atmosphere ya watu.
Kunavitu ambavyo huwezi kuacha kujiuliza hivi wakati anasema Lazima mLEMa awe rais hakuwa na huyu!? Je siasa na din vinawiana? Majengo aliyojenga ya kuabudia ni nguvu za waumin wa maeneo husika,au mchango kidogo,
Njoo na hoja mpya kumsafisha,na kama anaajenda ya kugombea ubunge/urais umekula kwake!

Baki kwenye mada, acha porojo. Njia ya mwongo ni fupi!
 
Unataka wanakondoo waliokimbia warudi harudi mtu huko kwa msanii huyo wamerudi kundini

Hii siyo hoja! Wanakondoo walimkimbia Yesu mwenyewe, sembuse Kakobe? Yesu alipofundisha Neno gumu, tunasoma katika YOHANA 6:66,"Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena." Hata hivyo, pamoja na kuwa wako wanaoikimbia kweli, lakini wako wanaoipenda kweli. Njoo Jumapili moja uone wanaoipenda kweli walivyojazana, usisikie ya kuambiwa.
 
Ni kweli kabisaa, hata rizi1 anamiliki MarkII ya mwaka 94, na hana nyumba hata moja anaishi kwa babaake.
 
Unafikiri kila anayeendesha gari, anakuwa ndiye mmiliki wa gari? Eze huendesha magari mengi tu ya watu wengine,lakini hana gari analolimiliki. Yeye ni mahiri katika Video/Computer Technology, na anafanya consultancy za kifundi kwenye taasisi kubwakubwa. Fanya utafiti kabla hujasema!

jisheshimu, utachekwa wewe
 
Lèo ndio nimeamin ukweli kuhusu huyu mchungaji kumbe yaliyokuwa yanasemwa juu ni uongo na uzandiki mtupu, tatizo la wabongo kukalilishwa vitu nao kuvipokea bila kuvifanyia utafiti matokeo yake wanapinga tu bila kuleta ushahidi, mbona hao wachungaji wengine mmeweza kuzitaja mali wanazomiliki hata bila hii thread kuwahusu. Achen ujinga
 
Back
Top Bottom