Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe

Hii hapa nyumba pekee ya Askofu Kakobe

tuambie kwanza dhaka na sadaka zinaenda wapi afu ndyo ulete prnpangada zako

Nafikiri zinatumika kujengea kanisa hamlioni lilivyo kubwa na zuri? Sidhani kama anafuja mali yoyote.
 
Wala Askofu Kakobe asitegemee huruma za Watanzania kumpa utajiri wa Duniani... Wengine wanataka apande hata Daladala au bodaboda... Ndio maana hata washirika wakampa Gari used "mtumba".... Ndio washirika wake wanaona ndio vinamfaa....
 
Washirika wa Kakobe hasa huyu Mhabarishaji na Smirna.. Aidha ni washirikina au wana mashetani.... Nami Nawasilisha...
 
mtoto wake Eze kakobe anendesha noah new model na ana video studio yenye vifaa vya kisasa and expensive
 
Kwa hiyo mnamsafisha kwamba yeye sio mlafi wa sadaka kama wale wengne mfano yule wa ubungo

Naona kilichowekwa hapo ni ukweli kuhusu hali halisi ya maisha ya Kakobe, hayo mengine itakuwa mtazamo wako binafsi.
 
Mtumishi wa mungu achafuriki wala kuchafuliwa.. unajua LUSEKELO MZEE WA UPAKO anaaishi wapi na anaendesha gari gani?

Hapa naona mimi ni kuwekana sawa tu.

Huyo Mzee wa upako kaingiaje hapa au ilikuwa ndiyo gear yenu ya kumuingia?
 
Kuna wakati alikuwa anawaambia watu kujipamba ni dhambi,
akawavua dhahabu zao shingoni na vikuku vyao miguuni;
......... swali
  • Ziko wapi zile dhahabu?


  • Na je hizo sadaka mnazotoa ina maana halipwi mshahara?
 
Kwa hiyo wewe GBBS unafurahia kabisa sana Umasikini wa Kakobe?? -------- wewe.... Mimi sio mshiriki lakini sio mara moja ninakuja pale kanisani... Naanza kutiwa shaka...

Hapa nipo kuthibitisha ukweli wa mambo ulivyo ili kuondoa uongo na uzushi ambao huwa unaenezwa na watu kwamba Kakobe amejilimbikizia mali nyingi sana ili kudanganya uma.
 
mtoto wake Eze kakobe anendesha noah new model na ana video studio yenye vifaa vya kisasa and expensive

Unafikiri kila anayeendesha gari, anakuwa ndiye mmiliki wa gari? Eze huendesha magari mengi tu ya watu wengine,lakini hana gari analolimiliki. Yeye ni mahiri katika Video/Computer Technology, na anafanya consultancy za kifundi kwenye taasisi kubwakubwa. Fanya utafiti kabla hujasema!
 
Ninyi washirika wa Kakobe kweli hamumtakii mema Kakobe wenu... Sasa tutaenda hata kwenye Mavazi yake Kakobe... Mbona Kakobe Suti anazovaa ni ghali sana?? Nionavyo ni kwamba jumla ya pesa au gharama ya nguo anazovaa Kakobe ni kama gharama ya Gari.... Sasa kuwa na gari au magari, nini ishu??
 
Wengine wanaweza kuhoji anakula nini?? Analalia kitanda gani?? Anaogea sabuni ya gharama gani?? Huu ni ujinga au utoto...
 
Unafikiri kila anayeendesha gari, anakuwa ndiye mmiliki wa gari? Eze huendesha magari mengi tu ya watu wengine,lakini hana gari analolimiliki. Yeye ni mahiri katika Video/Computer Technology, na anafanya consultancy za kifundi kwenye taasisi kubwakubwa. Fanya utafiti kabla hujasema!

Sasa naye huyo mwanaye eze atakuwa MJINGA kupitiliza kama ana elimu hizo za Computer na hata kagari hana? Magari siku hizi ni yamechukua nafasi ya Baiskeli tu... Ndio maana bodaboda haziendi mjini... Wanataka magari ndo yaende...
 
Kuna wakati alikuwa anawaambia watu kujipamba ni dhambi,
akawavua dhahabu zao shingoni na vikuku vyao miguuni;
......... swali
  • Ziko wapi zile dhahabu?


  • Na je hizo sadaka mnazotoa ina maana halipwi mshahara?

Siyo kweli kwamba anawavua watu dhahabu. Ajitokeze hapa hata mtu mmoja aliyewahi kuvuliwa dhahabu zake, na Kakobe,halafu akazichukua. Hayo ndiyo hayohayo ya kusikia tu! Kweli inawezekana akawavua watu dhahabu, asiwepo hata mmoja wa kwenda kumshitaki Polisi, miaka yote 25? Tembea vituo vyote vya Polisi, hakuna taarifa yoyote iliyopelekwa ya mtu kuvuliwa dhahabu na Kakobe. Anachofanya Kakobe ni kufundisha Neno la Mungu linalosema kujipamba kwetu hakupaswi kuwa kwa dhahabu, bali kwa utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani roho ya upole na utulivu, kama wanawake watakatifu wa zamani, kwa mfano Sara (1PETRO 3:1-6; 1TIMOTHEO 2:9). Mtu aliyedhamiria kuongozwa na Neno la Mungu (ZABURI 119:9), akijifunza hivyo, akifika nyumbani kwake, kwa hiari yake hukongoroa mapambo yake, na kujua mwenyewe pa kuyapeleka. Je, anapata mshahara? Bila shaka anahudumiwa na Kanisa, ndiyo maana anapata chakula na mahitaji mengine ya kawaida ya maisha.
 
Mimi nataka kufahamu Mhabarishaji alikuwa na lengo gani kuleta hii mada... Na wewe Smirna una matatizo gani na Askofu Kakobe wako?? Mpaka aje kuomba pesa nyumbani kwako ndio utafurahi??
 

Vipi kuhusu Mwingira, Gwajima, Lusekelo na Rwakatare, nao wanaishi nyumba za design gani?

Nimebahatika kuiona nyumba ya mama lwakatare iliyopo pembezoni ya bahari ana hekalu la maana limezungukwa na nyumba ndogo ndogo kama tatu hiyo fensi ya ukuta wa nyumba yake unajenga nyumba tatu za heshima mbagala chezea mlima wa moto wewe .
 
Back
Top Bottom