Haya sasa hawa ndo ACACIA!

Haya sasa hawa ndo ACACIA!

Soma na haya maneno ya mwenzenu hapo kwenye blue hivi wakala ni yule anayesema kutetea uhalisia wa tukio au yule aliyeweka saini kwenye sheria na mikataba ili hao wezi waibe? Duhh!! nalaani sana kuzaliwa Tanzania

WAZIRI NCHEMBA ATOA SIRI SABABU YA MKAPA NA KIKWETE KUHUSISHWA SAKATA LA MAKINIKIA

KITAIFA

BY RABI HUME

JUNE 18, 2017

Ikiwa zimepita siku chache tangu Rais Magufuli kuzuia watu kuwahusisha Marais wawili wastaafu wa Tanzania Jakaya Kikwete na Benjamin Mkapa katika sakata la mchanga wa dhahabu (makinikia) kwani katika ripoti zote mbili hakuna sehemu ambayo imewataja wastaafu kuhusika.

Waziri wa Mambo ya ndani na Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba amesema wezi hao walitafuta kichaka cha kutaja viongozi waliostaafu ili kuzia serikali iache kufatilia sakata hilo.

“Viongozi wetu hawajawai kuwa mawakala wa wale wanao tuibia, mawakala tumewabaini ni wale wanao watetea wezi,” alisema Waziri Nchemba.


Waziri Mwigulu ameongeza kusema sifa ambayo inafanya viongozi walioko madarakani wasing’ang’anie madaraka ni viongozi wastaafu kuheshimiwa baada ya muda wa uongozi.

Waziri Mwigulu ameyaongea hayo akiwa katika kijiji cha Zinzirigi katika Tarafa ya Ndago katika mwendelezo wa ziara jimbo kwake Iramba Magharibi kuongea na wananchi kuwaeleza alipofikia kuhusu ahadi ambazo walikubaliana kutekeleza hasa suala la umeme kutokufika katika vijiji vingi akieleza kuwa sababu ni mkandarasi aliyekuwepo mkoa wa Singida aliyetolewa baada ya kushindwa kazi lakini sasa ameambiwa na watu wa wizara ya nishati kuwa wakandarasi wawili wameshapatikana hivyo kuanzia sasa zoezi la kuunganisha umeme vijijini utaendelea kwa kasi hasa wa REA awamu ya Tatu.

Kuhusu ujenzi wa zahanati amesema mpaka sasa zahanati katika vijiji vingi alipopita zimefika hatua nzuri ya kupaua na kuwahidi kuwa pelekea mabati na mbao na mifuko ya saruji 100 ili zahanati hizo zikamilike na kuanza kutoa huduma mapema sana.
Mkuu Mwigulu Nchemba unaujua ukweli hata kama umeamua kupiga siasa huko Singida. CCM na viongozi wake ndio wametufikisha leo hapa. tatizo hampendi kuelezwa ukweli.unaanzaje kusema uwachukulie hatua wote waliohusika huku ukisema Kikwete na Mkapa wasisumbuliwe? Hakuna kesi hapo hao wote mtakaowahoji ( kama mtafanya hivyo) watawaambia ni maelekezo kutoka kwa bosi na hamtakuwa na la kuwafanya. Simple and clear
 
Lete CVs zao tuwajue. Mlianza kutabiri Acacia kukimbilia mahakamani, mkashindwa. Sasa mmehamia kwenye psychological warfare, Nakuhakikishia mamluki ninyi mtashindwa pia.
Screenshot_20170618-212901.png
 
Watanzania wananiangusha sana jamani. Tulishaambiwa mmiliki wa Acacia ni Mossad lakini hakufua dafu, eti wataalamu waliobobea ushit, na hao tukiwamaliza, mtakuja kutwambia Acacia wamemleta Referee Collina kuja kuzungumza na JPM na mijitu itakuja kuweka post ikiuliza "mara hii tutatoka kweli?" Nasema ivi, tutatoka mara zote kwa hawa majambazi. Anyways hio bodi haiji hapa kutaka kuitetea Acacia, hio bodi ni kama washauri tu.
Nani kakwambia mmiliki wa acacia ni mossad? Unajua mossad ni nini? Acheni stori za kwenye kashata vijana.
 
Nani kakwambia mmiliki wa acacia ni mossad? Unajua mossad ni nini? Acheni stori za kwenye kashata vijana.
e e e eeeeee..... kulikuwa na mada humu ililetwa tukaambiwa jamaa ni mossad, sijui mwengine mmarekani kwenye defence bla bla zilikuwa nyingiiii na vitisho visivofua dafu. kwaio tulia usichapie mchango.... wacha magu ashughulikie ili swala. wakati tulipokuwa tunaibiwa makelele mengi sasa tunajitahidi kutetea chetu mnaanza kuiombea dua serikali ibume.
 
e e e eeeeee..... kulikuwa na mada humu ililetwa tukaambiwa jamaa ni mossad, sijui mwengine mmarekani kwenye defence bla bla zilikuwa nyingiiii na vitisho visivofua dafu. kwaio tulia usichapie mchango.... wacha magu ashughulikie ili swala. wakati tulipokuwa tunaibiwa makelele mengi sasa tunajitahidi kutetea chetu mnaanza kuiombea dua serikali ibume.
Israel huwa hawaishi kitapeli mkuu...trust me. Au kama huamini muulize Papa Msofe atakwambia
 
Wanabodi kuna hiyo kitu hapo. Je, tutachomoka wakituletea hao wataalamu kwenye mazungumzo?
95b74b177c2be5a1b1edae75c7117160.jpg
Uwoga wenu, umaskini wenu BINAFSI NINAWAHESHIMU WAbongo kwa kuwaogopa wazungu duh...lakini ninachojua ni kwamba tuna wasomi wenye weledi Tz juu ya madini subili uone!
 
Boss Kipapatiro Wadau naombeni maana na utofauti kati ya Ubobezi na Uelewa. Na je unaweza ukawa Mbobezi na Usiwe Muelewa?

My Take: Hii kitu tusiikuze kihivyo. Makanikia ni asilimia ndogo sana kuliko wanachozalisha. Wao wakileta hao sijui Wabobezi au Wataamu sijui mbinu hizi na zile. Sisi tupeleke Wataalamu wenye Uelewa. Ukubwa wa Pua si Wingi wa Makamasi.
Pia si mtaalamu sana maana Mimi ni Advocate tu. But anyway, Mimi siwaamini wataalamu wabobezi wetu hata siku moja mkuu maana hawa ndo wametufikisha hapa tulipo.

Mf: Chenge ni mbobezi
Karamagi
Kabudi (Sasa hivi amesaliti kaulizake)
Ngeleja
Kafumu n.k
 
Hapana mzee. Si kweli! Yaani wewe na ccm yenu msaini mikataba mahotelini huku mnakula bagger Leo hii niwaonee huruma Mzee? Sijawa zuzu kiasi hicho Mzee

Sent from my VFD 500 using JamiiForums mobile app
KWAKUWA TULISAINI SISI HIYO MKATABA KWA HYO TUKAE KIMYA TU MPAKA NABII ISSA ARUDI AU TULIANZISHE KAMA HIVI MAANA MNACHOSHUPALIA NI SAWA NA KUTAKA MAREHEMU ARUDI
 
Dawa ya hao watu ni kujikita kwenye hoja, watu wetu wasikubali kuingiza maswala ya democrasia, utawala wa sheria,ukimwi,umasikini, n.k kwenye mjadala.

Hoja ni moja tu wamekuwa wana underestimate kiwango cha dhahabu na madini mengine yaliyo kwenye mchanga wanaosafirisha.

Na ikiwezekana njia ya kwanza ya kupima kiwango hicho iwe ni ile iliyotumiwa na akina profesa mruma na osolo.

Kama watataka itumike njia ingine tuite warusi waverify accuracy yake.

Huo ni uzuZu na u.chizi!
Yaani CCM mnashangilia makiniikia wakti dhahabu halisi inaondoka moja kwa moja tokea kwene migodi pasi na kurekodiwa popote! Ama kweli mmerogwa na aliyewaroga kesha kufa kitaambo. Mungu tusaidie utuokoe na hawa watawala waovu wa Chama cha Makinikia-CCM!
 
WA TZ bhn nchi ya kwenu, Mali za kwenu, Acacia wako kwenu, Wameiba mali yenu, Nashangaa sana mnavyosambaza woga kwa wananchi., Ili iweje..?? Kama mtu kaamua na kasema anaweza mpeni walau support bhas....

Sipati picha km TZ leo hii ikiingia vitani sidhani kama kutakua na wazalendo wa kufia nchi hii....!?? Yaan hatuna umoja hata kidogo..!! Muda mwingine hua naona bora chama kimoja tu kingebaki, Upinzani walifanya vizuri lkn kwa hii sumu walowapa wananchi nawalaumu sana..!!
Western walileta upinzani sio kwa maendeleo ndugu bali kwa interest zao na wasomi wetu waliokaririshwa ulaya wakakubali tu kwa kigezo cha democracy
 
Tumejipanga kimkakati kukabiliana nao...vita ni vita tu muraaa!
 
magufuli ni mchumia tumbo km walivoccm wote....ameshindwa na ama amedanganya kila alichowahi kusimamia
1. Samaki wa magufuli alishindwa na kuliinhizia taifa hasara kubwa
2. Lugumi hiyo yeye yumo na imemshinda hawezi kujichukulia hatua
3. Kivuko kibovu alileta yeye wala hajajikamata na kujishitaki
4. BASHITE tu amemshinda sembuse Marais waliopita ambao alishasalimu amri hadi kuteua mke wa rais kuwa mbunge
5. Hajaweka mezani mkataba wa chatointernational airport???!!
6. Yeye binafsi hajaweka wazi mkataba wa bormberdier watz wanajua dili alizofanya yeye binafsi....
7. Hajaonesha hata nukta ya uzalendo kwa yale ambayo yeye binafsi ameshinikiza na kupazimishwa yafanyike.
8. Watz mtachezeshwa sn shere na ccm hukumnawalaumu wazungu na wachina kwa kiwaibia wkt wezi wenu ni ccmmnaowachekea
 
Back
Top Bottom