Naunga mkono kufufua shirika letu la ndege lakini haya hapa chini ni uongo.
1. Ndege hii ni kubwa kuliko zote africa.
Watanzania mmesahau kwamba ile boeng 787 ninkubwa hata kqa bei kuliko hii a220-300. Hii ni ndege ya kawaiada tuu inayo beba watu kati ya 130 hadi 160.
2. Tanzania ni nchi ya kwanza kumiliki ndege hii.
Si kweli ndege hizi kabla ya kununuliwa na airbus zilikua zinatengenezwa na bombardier zilisha nunuliwa na kutumika toka mwaka 2016.
3. Hakuna nchi africa yenye uwezo wa kununua ndege hii. Ni uongo pia kwa sababu , bei yake i ya kawaiada sana. Dreamliner 787 moja ni sawa na a200'-300 kama 3 hivi. Ethiopia wana dreamliner 787 kama 29 hivi.
Hivyo kuaema hakuna nchi africa yenye uwezo wa kununua hizi ndege ni kujidanganya. Kujiona ni simba wakati kila mtu anakuona ni paka.
Tanzania kuwa ya kwanza africa ni sawa na kuwa wa kwanza kuingia chumba cha mtihani. Baada ya miezi michache kuna nchi Africa zitanunua ndege nyingi aina hii kupita tz. ( nyongeza), egypt imeweka order ya ndege 14.
Waandishi wa habari Tanzania nao wamekua wanasiasa. Someni mitandaoji kabla ya kuandika mambo yenu.