Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

inasikitisha kuona tuna rais ambaye haendeshi nchi kwa sheria , kama kweli masauni kagushi yeye ndio angehakikisha sheria inafuata mkondo lkn haishangazi hata mafisadi waliokwapua bot c'aliwapa muda warudishe fedha halafu akacheka, ila kumbuka ukiua kwa upnga nawewe kifo chako ni upanga huohuo .

Rais apeleki mtu mahakamani,hapo sheria ndio itakayofata mkondo na usishangae ukaambiwa masauni ameshitakiwa na jamhuri
 
Jk tangu awali alijua kuwa masauni aligushi vyeti lakini alimpa uenyekiti huo ili wamtumie watakavyo. Mpango mzima ni kuwa ajue kuwa wao wanajua kuwa amegushi vyeti hivyo yeye akose ujasiri wa kusimamia kile anachoamini.ilifika mahali masauni akakataa kuburuzwa ndiyo ugomvi ulipoanzia.wote masauni na waliompa kazi ni wahalifu tu wanatakiwa kushitakiwa. Jk anashangaza kweli masauni ametenda kosa la jinai lakini yeye anasema atampa kazi nyingine, hivi kweli kikwete anajua maana ya utawala wa sheria? Ndiyo maana ana chukuwa jukumu la mahakama kuamua kuwa mgomo wa tucta ni batili, na ndiyo maana anadharau hata maamuzi ya mahakama juu ya takrima kuwa ni rushwa. Watanzania tuko motoni kwa kutawaliwa na rais asiyeheshimu utawala wa sheria

DOUGLAS SALLU: JK hamna kitu mle
 
Huyu kijana napenda alivyo na mmisimamo yake lakini kwa kweli mwanzoni alipojiunga
na hii uvccm nililaalama sana kwamba amewekwa kwa makusudi mule ndani bayazaidi
yuko radhi kumwaga damu kama uko against na msalahi ya babake....

Hivi sasa ni wengi sana wataongea kuhusu kujiuzulu kwa masauni lakini ukweli utabaki
RIDHIWANI akishirikiana na BENO MALISA walijitahidi kufanya uchafu na upumbavu wao
huko iringa kwa garama zot ehata kuhonga wenyeviti wamtimue huyu bwana

hakika naweza kusema aikuwa kitu cha kushangaza kuona kikwete akisema masauni
kajimaliza mwenyewe nasema hivi nikiwa na maana wangapi wenmye makosa kama yake
bungeni kuna mawaziri vihiyo walioteuliwa na huyu huyu bwana kama si Bw msemakweli
kutufungua macho sijui tungejuaje tuna mawaziri wabunge vihiyo....

Mh rais bado nasema masauni na wenzake walikubana vilivyo na mikataba yenu
ya ul;aji wa kipuuzi UVCCM na swala la kumuondoa ni kutokana na kuwa kinyume na msalahi\
yenu kutaka kuuza ama kuangamiza kila kilicho mbele yenu

Ninachosema haki ya mtu aipotei tusubiri yapo mengi yanaibuka na yataendela kuibuka
SIKUSHANGA KUSIKIA MAKAMBA AKISEMA MASAUNI AJIUZULKU ATTI KATUMWA NA DOLA
HUU NI UPUUZI NILISHASEMA HUYU BABU ATAJIBU DHAMBI ZA WENGI SAA NA NAMWONEA
HURUMA NA UMSKINI WAKE....ANYWAY.....

INNALILAH NA MASWABRINA....KILA MWENYE KUSUBIRI YU PAMOJA NA MWENYEZI MUNGU

mkuu umechanganya mawili

masauni kuondoka ni sawa kwani forgery ni kosa kubwa!

hili la pili la ridhiwani na malisa, nadhani ni kubwa kidogo na kama wana matatizo basi vijana wanatakiwa waungane kwani ingawa leo wana mamlaka, inaweza kutokea very soon wakawa chanzo cha mparaganyiko wa UVCCM

natumai viongozi wao wanafikiria outside the box!!
 
Na bado kipindi cha pili ndo mtashangaa sana labda mjiandikishe kama mimi tumnyime kura. Mimi nimejiandikisha mwaka huu kwa ajiri ya kuwanyima kura zangu watu wawili tu: Makongoro na JK potelea mbali hata kama kura yangu ni moja.
 
Ni kweli hakuna haja ya kutafuta mchawi kuhusu jambo hili lakini inatubidi kujiuliza maswali kadha.
Kwanza , kulikuwa na sababu gani kwa katibu mkuu (CCM) kusema kujiuzulu kwa Masauni haikutokana na kugushi/kudanganya umri wake wakati hiyo ndiyo sababu kuu ambayo ilikuwa inajulikana kwa viongozi wakuu wa CCM na Mwenyekiti ame confirm hilo.
Pili, kwa system yetu (shule, vyombo vya dola, kamati ya ulinzi na usalama (ya CCM), ndugu, jamaa na marafiki) kushindwa kujua miaka halisi ya huyu kijana. Katika mchakato wa kupata mwenyekiti wa Vijana, issue ya age ilitawala sana. Sasa inakuaje watu wote walishindwa kulijua hilo na kuacha mpaka inakuwa issue miaka miwili ijayo.

Mpwaa kumbuka kwanza kabla ya uchanguzi au kabla ya kupitisha majina ya mgombea UVCCM yaani majina ya wenyeviti watakao gombea tiali kulikuwa na zengwe kubwa na sio kidogo na kulikuwa na makundi na mpaka leo yapo amini usiamini nakwambieni sasa basi katika ulemchakato wa kuchuja majina ya na kumtaka mwenyekiti walimtoa mapema Nape walikuwa wakijua fika moto wake ulikuwa ni upi ni kuisafisha UVCCM na kutengana na mafisadi na mafisadi walikuwa na vibaraka wao huko UVCCM dawa ni kumbwaga nje wakafanikiwa kuja kwa Beno wakajua huyu ni rafiki ya Ridhwani watu wakahisi panaweza pakawa na midomo mingi sana ya watu ikabidi M/kiti CCM taifa aseme mwaka huu UVCCM M/kiti atokee Zanzibar wataka kuniambia hili halikujulikana walilijua lazi tu kuna jambo ndani ya UVCCM au CCM huyu Masauni alishaanza kuwageuka baadhi ya hao viongozi wakubwa na kuwa upande fulani na wakaamua kumtibulia sasa uwezi ukaniambia usalama wa Taifa hauna original file la Masauni sikubali hata kidogo this is Politics bwana watawadanganya wajinga kuna mchezo mchafu hapo ni kuwa wameamua kuepushia mbali na liwalo na liwe. na ndio maana umeona hakuna hata hatua yoyote inayochukuliwa katika kugushi?

Jana JK alitamka wazi ati hakuna kumtafuta mchawi jamani sasa mlimwacha Nape huko na yeye alikuwa na 30 na mwezi mmoja si bora angechaguliwa yeye hapo hamjiulizi kuwa kuna mchawi tu mpaka sasa kwa nini walimpiga chini NAPE??? Na bado akawaambia hao wana UVCCM nyie ni vijana mwapaswa isimamia sheria ipasavyo sasa sijui huwa kuna jinamizi lawapitia hat hawa vijana na kujisahau kuwa wao ndio tegemeo la kesho mkipewa rungu mwashindwa litumia na ndio maana kila kukicha nawambia UVCCM ni kuna unafki fitna mezengwe chuki na kuchafulianan majina hakuna hata mtu wa kufikilia wapi TAIFA tulipeleke ni kila mtu kirwake lini UVCCM itakuja kuwa IMARA?

 
Yaani, mimi sijawahi kulalamika kuhusu huu ugonjwa wa Malaria Sugu lakini nadhani sasa imefika kikomo.

Ni jambo la msingi kabisa, hata kama mtu si muandishi, kufahamu kuwa kichwa cha habari ni utangulizi wa habari yenyewe; lazima kuwe na muendelezo na uhusiano!

Kwa hiyo Ridhwani Kikwete kaitisha kamati kuu ya CCM, au?

Mzee si '' Malaria Sugu'' , imepanda kichwani :confused3:
 
MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani Kikwete, sasa anatajwa waziwazi na kuhusishwa na mpango wa mapinduzi ndani ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Tanzania Daima Jumatano imeelezwa. Baadhi ya vyanzo vya habari kutoka ndani ya UVCCM vimeliambia gazeti hili kuwa mtoto huyo ndiye anayevuruga umoja huo.
Wakati huohuo, Rais Kikwete amelazimika kuitisha kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya dharura kesho (leo), pamoja na mambo mengine, kujadili kashfa na mzozo ulioibuka ndani ya UVCCM.

Kwa kuwa siku za karibuni umekuwa ukiongoza kwa kuanzisah topic nyingi hapa JF, na kwa kuwa Topics zako nyingi huwa hazina Miguu wala kichwa, na Kwa kuwa watu wanatumia Megabytes zao kufungua topic zako zisizo na kichwa wala miguu, na kwa kuwa hizo MB watu tunazilipia kwa ISP. Ili nisiendelee kuona topic zako na kushawishika kuzifungua basi LEO nimekuweka/nimekutupia kunako Ignore list yangu and I woulld like to call upon other member wenye mapenzi mema na JF waitumie hii Functionality
 
Mungu wetu Mungu wetu.
Vumbi jingi latimka
Nchi yetu yavamiwa
Mungu wetu tuepushe


Mafisadi tuepushe Mungu
Shime tunyanyue Mungu
Turudishe enzi zile
Mungu wetu tuepushe

Wapeana vyeo tele
Vyeti feki kutumia
Masikini hawapati
Mungu wetu tuepushe

Haki zetu wazitwaa
Mikwara Mingi tunapewa
Masikini Kuufyata
Mungu wetu tuepushe

Usultani wauleta
Baba, mama mwana pia
Uwaziri wapeana
Mungu wetu tuepushe

Na vikao wavifanya
Kuchaguana kama kawa
wenye nchi wameachwa
Mungu wetu tuepushe

Juzi juzi Masauni
Sifa Nyingi amwagiwa
Leo tena yupo wapi
Mungu wetu tuepushe

Watudanganya hakika
Wafikiri hatujui
Sasa HATUDANGANYI-KI
Mungu wetu tuepushe
 
Hivi Lowassa na RA wako wapi na wanafanya nini? Hawa watu ni balaa....
 
Jk tangu awali alijua kuwa masauni aligushi vyeti lakini alimpa uenyekiti huo ili wamtumie watakavyo. Mpango mzima ni kuwa ajue kuwa wao wanajua kuwa amegushi vyeti hivyo yeye akose ujasiri wa kusimamia kile anachoamini.ilifika mahali masauni akakataa kuburuzwa ndiyo ugomvi ulipoanzia.wote masauni na waliompa kazi ni wahalifu tu wanatakiwa kushitakiwa. Jk anashangaza kweli masauni ametenda kosa la jinai lakini yeye anasema atampa kazi nyingine, hivi kweli kikwete anajua maana ya utawala wa sheria? Ndiyo maana ana chukuwa jukumu la mahakama kuamua kuwa mgomo wa tucta ni batili, na ndiyo maana anadharau hata maamuzi ya mahakama juu ya takrima kuwa ni rushwa. Watanzania tuko motoni kwa kutawaliwa na rais asiyeheshimu utawala wa sheria

Ndugu zangu Raisi wetu hayuko makini..Maneno yake mwenyewe yanamfunga..Jamani kwanini watu kama hawa tuna wa-entertain? Inaumiza sana..
 
Acha jazba hoja iliyopo jamaa KAGHUSHI au la? Hivi sheikh wangu mtu akikuuliza kwa nini unakula kiti moto ukamjibu mbona Mapdri wanalawiti watoto litakuwa jibu sahihi? kosa halihalalishwi kwa kosa!! kama jamaa kafoji aondoke kama kuna waliofumbiwa macho basi nao waandamwe sio eti aachiwe kisa kuna wengine kama yeye.unda taifa lako ndo uweke utaratibu huo, cha kumbana JK ni ilikuwaje vyombo vya usalama vilishindwa kutambua hilo mapema. T unachosubiri ni kuona jamaa anapandishwa kizimbani sio SIASA zenu mpauko.

Mtume anasema kila mwenye kughushi makazi yake motoni
 
wale wabunge waliogushi wako wapi??
then utajua masauni anaenda wapi!!!1!hii ndio serikali wakati mh nyanganyi alipoaribu kivuko cah kigamboni akaenda kuwa balozi usishangae jamaa kupewa ubalozi wa afghanistan soon...nchi hii!!!naipenda tanzania yangu
 
Yap hii ndo TANZANIA YA jk, kwani mmesahau kosa la wizi wa EPA liligeuzwa kosa la Deni eti walioshitakiwa ni wale waloshindwa kurudisha pesa as if walikopa bila riba.leo kihiyo anaitwa mchapakazi sio mhalifu,

"BURIANI TANZANIA YA JULIUS, MAFISADI WAMEKUTWAAA"
 
sasa kama Masauni ameghushi umri matokeo yake ni nini:

Mbona Nchimbi, Lukuvi, Makongolo Mahanga na Kamala walijipachika degree feki na mpaka sasa jamaa katia pamba masikioni? Hii ya kumshinikiza Masauni kujiuzuru ni mbinu za mkwere na mwanae; hiyo sio siri!!
 
kweli mkuu bulesi niliuliza hilimmbona wale wabunge na mbaya zaidi mawaziri wanaotuongoza wana degree feki embu fikiria
unaundiwa bajeti na waziri feki unatarajia nini rais nae naitaji kuhoji elimu yakle ukiona mtu anatetea wahalifu ujue nae mhalifu

HUYU RAIS MSANII MTUPU..UNAJUA WAKATI ULE ALIKUWA ANASHINDA BENO NA ALIPOSIKIA MWANAE AMEIJIINGIZA AKAJIFANYA KUOGOPA KASHFA AKAPANGUA LAKINI ALIJUA MWISHO ATAMRUDISHA BENO NA WIZI WAO UNAENDELEA KAMA KAWAIDA...YAANI KADI YANGU YA UVCCM
NIMETOKA KUICHANA SASAHIVI
 
sasa kama Masauni ameghushi umri matokeo yake ni nini:

Mbona Samuel Chitalilo alighushi vyeti vya shule na hajachukuliwa hatua yoyote? Na Mwaka huu anagombea pia!
The case of Double Standards?
 
"...
Amesema hafurahishwi na njama chafu zinazofanywa na baadhi ya vijana ndani ya CCM kwa kuendesha makundi ya kuwachafua wenzao na kuchochea fujo ndani ya umoja huo, na kuwa kamwe wenye tabia kama hiyo hawatavumiliwa na wasitegemee kupata nafasi za uongozi daima hata kama watagombea.
"Nasema Umoja wa Vijana ni tegemeo kubwa kwa CCM, hivyo vijana wagomvi tokeni wenyewe...nasema acheni kabisa vijana kuishi maisha ya kujengeana chuki na kuendesha makundi ya kuwang'oa wenzenu kupitia vyombo vya habari.
"Ni vizuri penye tatizo kutumia vikao, kulumbana na kumalizana ndani ya vikao badala ya kuita waandishi na kueneza chuki," alisema Rais Kikwete. (Source: Tanzania daima, 20 May 2010)


Ninaposoma sehemu hii ya hotuba ya Mwenye Enzi, napata shida, naona ihitimisho la hoja niliyowahi kuisikia hapo nyuma kuwa mheshimiwa ana michiririzi ya udikteta katika damu yake. Itawezekana vipi yeye kuzuia kijana asichaguliwe kama akigombea nafasi! Isije ikawa ni kweli kwamba demokrasia yetu imefungushiwa ndani ya mwanakondoo mwenye kuonekana mpole na mnyenyekevu kumbe sivyo
 
Ridhiwan na Beno ni chanda na pete, damu damu!!! Ila atakuwa amepata ushindi maana wakati wa kampeni waziwazi alimtaka Benno ila Baba akataka apooze uzenji!!! Na baba alibariki kutumia upenyo wa umri kufikia ndoto za kijana wake!!! Lo umoja ni nguvu!!! Baba na mwana wana nguvu sana!! Bado tena mama mdogo naona anakuja kwa kasi!! Bado mama mkubwa any time akitaka kiti tena cha kuchagulia atakipata! Dogo naye Chipukizi, yaani familia yote!!! Ila dada Salama low political profile, anajitahidi sana! So culm our Dr.!!!
 
Back
Top Bottom