Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

mtu gani hapatii hata siku moja, na huyo masauni alimteua mwenyewe baada ya songombingo za huku bara akina nape. Hajawahi kupatia hata chembe.
 
Mnashangaa ya Masauni? Je Mwilima yule aliyekuwa katibu wa CCM(WANAWAKE), Sasa yuko wapi ni mkuu wa wilaya na anatembelea VX V8. Huyo ndo JK bwana Mkwere halisi a.k.a King'ota(Ng'ong'ona) aliyewadanganya Mambayuwayu (wafanyakazi). Nchi hiiiii full Rose Muhando (NIBEBE).
 
yaani wewe unadhani mtu mwongo ndio hana nafasi kwa CCM huyo ndio anawafaa zaidi,na ndio maana rais kakwambia atampangia kazi ingine.anajua pa kumuweka we ulie tu.yana mwisho haya:angry:
 
Wadau ninanukuu kile ambacho kinadaiwa kusemwa na rais wetu kuhusu sakata la kujiuzulu kwa Masauni:

Nanukuu: Hata hivyo, Rais Kikwete alimfariji kijana huyo mpole na mzito kufanya maamuzi magumu na haraka, akisema kwakuwa ni makakamavu na mchapakazi atapangiwa kazi nyingine hapo baadaye. mwisho wa kunukuu (Source: Gazeti la mwananchi la leo 20 May 2010)

Jamani naomba mnisaidie huenda mimi ndo sielewi vizuri mambo haya. Hivi kama ni kweli huyu kijana amegushi umri rais anapata wapi ujasiri wa kusema atampangia kazi nyingine? Hivi ni kazi gani nyingine ambayo haiitaji mtu kuwa mwadilifu? Kama mtu ameweza kudanganya umri na hilo likajulikana na "akalazimishwa" kujiuzulu atashindwa vipi kufanya udanganyifu mwingine kwenye hiyo kazi nyingine atakayopewa? Au atawekwa kwenye kamati ya "saidia CCM ishinde" ili afanikishe udanganyifu wa kura?

Nisaidieni mwenzenu, napata shida kuamini kuwa viongozi wetu wamefikia hapo. Au nchi hii haina kabisa watu wanaoweza kuwa viongozi hivyo inabidi wale wachache waliopo tung'ang'ane nao hata wanapoonyesha upungufu mkubwa kama wa kudanganya. Ni jambo gani ambalo mtu akilifanya ktk nchi hii linamnyima nafasi ya kuwa kiongozi wa umma?

Alikuwa ANATANIA tu wewe huujui UTANI wa rais wala usimchukulie Seriaous maana hata Tendwa ameshatwambia kwamba Mkulu wetu ni Mtu wa UTANI sana hata kwenye mambo ya Msingi
 
Niloposoma hii habari nilishtuka sana...hakika tuna hitaji mabadiliko....mabadiliko ni lazima imetosha sasa.
Kwanza kugundua kuwa ameanza la kwanza 1979 leo ni ajabu! Masauni hatoki peponi anatoka mahali ambapo kuna watu wanamjua toka kuzaliwa na isitoshe walikuwepo pale alipogombea.....najiuliza walikuwa wapi kusema haya? au aliwekwa makusudi ili aje atolewe baadae? huu ni mfumo gani wa uongozi?
Haya amejiuzulu kama JK alivyosema mchawi ni yeye mwenyewe lakini bado anafikiria kumpa post nyingine kwa kweli inasikitisha
Lakini labda jambo moja la kujifunza hapa....wakoloni walipanda mbegu ya kujiharibia wenyewe Fank Fanon kama sikosei bila shaka sasa ndipo tulipo ccm .....for its own destruction....
 
Ridhiwani: Huyu kijana napenda alivyo na misimamo yake lakini kwa kweli mwanzoni alipojiunga na hii uvccm nililaalama sana kwamba amewekwa kwa makusudi mule ndani baya zaidi yuko radhi kumwaga damu kama uko against na msalahi ya babake....

Hivi sasa ni wengi sana wataongea kuhusu kujiuzulu kwa masauni lakini ukweli utabaki RIDHIWANI akishirikiana na BENO MALISA walijitahidi kufanya uchafu na upumbavu wao huko iringa kwa garama zot ehata kuhonga wenyeviti wamtimue huyu bwana

hakika naweza kusema aikuwa kitu cha kushangaza kuona kikwete akisema masauni kajimaliza mwenyewe nasema hivi nikiwa na maana wangapi wenmye makosa kama yake bungeni kuna mawaziri vihiyo walioteuliwa na huyu huyu bwana kama si Bw msemakweli kutufungua macho sijui tungejuaje tuna mawaziri wabunge vihiyo....

Mh rais bado nasema masauni na wenzake walikubana vilivyo na mikataba yenu ya ul;aji wa kipuuzi UVCCM na swala la kumuondoa ni kutokana na kuwa kinyume na msalahi yenu kutaka kuuza ama kuangamiza kila kilicho mbele yenu

Ninachosema haki ya mtu aipotei tusubiri yapo mengi yanaibuka na yataendela kuibuka SIKUSHANGA KUSIKIA MAKAMBA AKISEMA MASAUNI AJIUZULKU ATTI KATUMWA NA DOLA. HUU NI UPUUZI NILISHASEMA HUYU BABU ATAJIBU DHAMBI ZA WENGI SAA NA NAMWONEA HURUMA NA UMSKINI WAKE....ANYWAY.....

INNALILAH NA MASWABRINA....KILA MWENYE KUSUBIRI YU PAMOJA NA MWENYEZI MUNGU
 
Ingekuwa naamini katika nguvu za giza basi ningesema kunamkono wa mtu haiwezekani kabisa kinywa cha raisi kikatoa kauli tata kila kukicha bila hata ya kujishtukia...Waliosema JK ni Chagua la Mungu Mpoo ? na alikuwa ni mungu gani huyo maana kunamiungu mingi sana.
 
CCM hii si ile ya MKAPA, naweza kusema hii ya sasa ni ya kifamilia zaidi
 
Naona kuna wakati inabidi tuwe na mipaka hii tabia ya wazazi kuongoza nchi na watoto kupewa madaraka humo humo matokeo yake tunajimaliza wenyewe....hivi karibuni tumeona ridhiwani kikwete anapogeuza uvcmm kuwa ya babake na mama yake..na kuamua kuweka watu anaotyaka yeye...wangapi wasiojua ridhiwani alitumika kwa garama zote kumsaidia beno achaguliwe..sasa baada ya rais kuamua kuwapiga mchanga wa macho watanzania sasa naona wamefanikiwa kuweka punga lao beno malisa ili waweze kuiba vizuri

sasa kwa style hii nihisi kuwepo na mipaka ya uongozi ....naona mwanae mwingine kapewa uenyekiti uvccm chipukizi bagamoyo..mama mjumbe wa h....jamani si mbadilish e na jina liwe chama cha familia ya kikwete..(.ccfk).....na makao makuu muyapeleke huko bagamoyo kabisa
kama kuuana kwa uchawi mkapambane huko huko sipendi kabisa kuona chama kikiongozwa na ukoo ama amilia

ingekuwa vipi nyerere nae angeweka watoto wake..mbona ninyi wahuni amjifunzi kwa nyerere meeona wapi nyerere alimdumbikiza mwanae kwenye uongozi sasa...mwinyi rais mtoto waziri...
Amos makala kiongozi ccm ati mwanae mwenyekiti uvccm chipukizi huu ni upuuzi atutakiwi kuukubali..anyway poelni watanzania tushauzwa nchii
 
Wadau ninanukuu kile ambacho kinadaiwa kusemwa na rais wetu kuhusu sakata la kujiuzulu kwa Masauni:

Nanukuu: Hata hivyo, Rais Kikwete alimfariji kijana huyo mpole na mzito kufanya maamuzi magumu na haraka, akisema kwakuwa ni makakamavu na mchapakazi atapangiwa kazi nyingine hapo baadaye. mwisho wa kunukuu (Source: Gazeti la mwananchi la leo 20 May 2010)

Jamani naomba mnisaidie huenda mimi ndo sielewi vizuri mambo haya. Hivi kama ni kweli huyu kijana amegushi umri rais anapata wapi ujasiri wa kusema atampangia kazi nyingine? Hivi ni kazi gani nyingine ambayo haiitaji mtu kuwa mwadilifu? Kama mtu ameweza kudanganya umri na hilo likajulikana na "akalazimishwa" kujiuzulu atashindwa vipi kufanya udanganyifu mwingine kwenye hiyo kazi nyingine atakayopewa? Au atawekwa kwenye kamati ya "saidia CCM ishinde" ili afanikishe udanganyifu wa kura?

Nisaidieni mwenzenu, napata shida kuamini kuwa viongozi wetu wamefikia hapo. Au nchi hii haina kabisa watu wanaoweza kuwa viongozi hivyo inabidi wale wachache waliopo tung'ang'ane nao hata wanapoonyesha upungufu mkubwa kama wa kudanganya. Ni jambo gani ambalo mtu akilifanya ktk nchi hii linamnyima nafasi ya kuwa kiongozi wa umma?


Hakuna Mkuu. Na ndiyo sababu tunahitaji kubadili hali hii kwa bidii zote!
 
hehehe kichekesho huyo rais wenu eti anasema kwa kuwa masauni kijana mchapa kazi na mwenye msimamo atatafutiwa kazi nyingine.... hv jamani kughushi nyaraka c kosa la jinai.. sasa rais anautangazia umma kuwa anayedaiwa kughushi na kufukuzwa anatafutia kazi nyingine na sio kushtakiwa.....

Ukishangaa ya MUSA utayaona ya Firauni... ila ukiyaona ya FIRAUNI ukadhani ndio umemaliza basi HUJASIKIA NA KUONA YA KIKWETE
 
Jk tangu awali alijua kuwa masauni aligushi vyeti lakini alimpa uenyekiti huo ili wamtumie watakavyo. Mpango mzima ni kuwa ajue kuwa wao wanajua kuwa amegushi vyeti hivyo yeye akose ujasiri wa kusimamia kile anachoamini.ilifika mahali masauni akakataa kuburuzwa ndiyo ugomvi ulipoanzia.wote masauni na waliompa kazi ni wahalifu tu wanatakiwa kushitakiwa. Jk anashangaza kweli masauni ametenda kosa la jinai lakini yeye anasema atampa kazi nyingine, hivi kweli kikwete anajua maana ya utawala wa sheria? Ndiyo maana ana chukuwa jukumu la mahakama kuamua kuwa mgomo wa tucta ni batili, na ndiyo maana anadharau hata maamuzi ya mahakama juu ya takrima kuwa ni rushwa. Watanzania tuko motoni kwa kutawaliwa na rais asiyeheshimu utawala wa sheria
 
Kweli CCM inaelekea pabaya hivi wakati wa kumpitisha Masauni hawakuona hivyo vyeti? Nchi inaelekea wap jamani si ndio tunauzwa tukiwa tunaona?
Wa tanzania tubadilike la sivyo tutakuja kujuta hali si nzuri ni blah blah kila kukicha!!!
 
3]mtu gani hapatii hata siku moja[/B], na huyo masauni alimteua mwenyewe baada ya songombingo za huku bara akina nape. Hajawahi kupatia hata chembe.

Mh... sikuwahi kujiuliza kwa namna hii!!!
 
inasikitisha kuona tuna rais ambaye haendeshi nchi kwa sheria , kama kweli masauni kagushi yeye ndio angehakikisha sheria inafuata mkondo lkn haishangazi hata mafisadi waliokwapua bot c'aliwapa muda warudishe fedha halafu akacheka, ila kumbuka ukiua kwa upnga nawewe kifo chako ni upanga huohuo .
 
Huu upuuzi (nepotism) wa akina Ghadaffi, Museveni na Mubarak kwa bahati mbaya sana naona umeingia TZ. ....ee Mungu uliye juu tunakuomba utunusuru
 
Back
Top Bottom