Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Kuna haja uanzishwe mpango wa kupitia thread na kuhakiki zote kabla ya kuwekwa hadharani...tuna watu malaria imepanda kichwani!!
 
Nadhani neno Kung'atuka limetumiwa pasipo stahili....hili neno asili yake ni unazanaki maana yake kuachia madaraka kwa hiyari....sidhani kama huyu dogo wa miaka 36 alifanya vile...
 
Hata hivyo, Rais Kikwete alimfariji kijana huyo mpole na mzito kufanya maamuzi magumu na haraka, akisema kwakuwa ni makakamavu na mchapakazi atapangiwa kazi nyingine hapo baadaye.
Masauni kafanya kosa la jinai badala apelekwe ktk vyombo vya sheria JK anasema atapangiwa kazi nyingine...............
 
Kamati kuu ya ccm wamekubalina kila mwezi watakuwa wanakutana mpaka mwisho wa uchaguzi!Hicho sio cha dharura!Acha porojo zako
 
Kwa hiyo Malisa atakaimu uenyekiti? Nasikia wazee wao wa CC wanakutana leo pamoja na mengine ku-deliberate juu ya hali hii. FMES uko wapi? Tunakumiss sana kwenye suala hili.
FMES Nadhani naye alikuwa Iringa. Sasa hivi yuko buzy Mtera akijinadi kwa wapiga kura.
 
Ni kweli hakuna haja ya kutafuta mchawi kuhusu jambo hili lakini inatubidi kujiuliza maswali kadha.
Kwanza , kulikuwa na sababu gani kwa katibu mkuu (CCM) kusema kujiuzulu kwa Masauni haikutokana na kugushi/kudanganya umri wake wakati hiyo ndiyo sababu kuu ambayo ilikuwa inajulikana kwa viongozi wakuu wa CCM na Mwenyekiti ame confirm hilo.
Pili, kwa system yetu (shule, vyombo vya dola, kamati ya ulinzi na usalama (ya CCM), ndugu, jamaa na marafiki) kushindwa kujua miaka halisi ya huyu kijana. Katika mchakato wa kupata mwenyekiti wa Vijana, issue ya age ilitawala sana. Sasa inakuaje watu wote walishindwa kulijua hilo na kuacha mpaka inakuwa issue miaka miwili ijayo.
 
nimepata fununu kuwa Malaria Sugu ni ndugu wa mmojawapo wa MODS hivyo kupigwa Bann ni ndoto.
 
This is what we call "invitation to treaty"

kama konda wa daladala vile anaposema njoo kuna siti za kulala....na huku abiria wananing'inia mlangoni ---- Utamshtaki?
 
ni kweli hakuna haja ya kutafuta mchawi kuhusu jambo hili lakini inatubidi kujiuliza maswali kadha.
Kwanza , kulikuwa na sababu gani kwa katibu mkuu (ccm) kusema kujiuzulu kwa masauni haikutokana na kugushi/kudanganya umri wake wakati hiyo ndiyo sababu kuu ambayo ilikuwa inajulikana kwa viongozi wakuu wa ccm na mwenyekiti ame confirm hilo.
Pili, kwa system yetu (shule, vyombo vya dola, kamati ya ulinzi na usalama (ya ccm), ndugu, jamaa na marafiki) kushindwa kujua miaka halisi ya huyu kijana. Katika mchakato wa kupata mwenyekiti wa vijana, issue ya age ilitawala sana. Sasa inakuaje watu wote walishindwa kulijua hilo na kuacha mpaka inakuwa issue miaka miwili ijayo.

jibu: Hio ndio tanzania yetu ilipoletwa chini ya ccm
 
Ili changa la macho, why Masauni ajiuzuru nearly uchaguzi? wanatafuta huruma za wapiga kura wasanii hawa, kwani ni juzi ndio wamejua mtu kughushi cheti cha kuzaliwa? na displinary measures toka lini zinasubiri vikao? hii ni hapa kwetu tu ndio inatokea na kwa wateule fulani fulani wakichemka ndio tume zitaundwa kutafuta ukweli. Nashangaa hawakuunda tume kuchunguza tuhuma za Masauni. By the way Ridhwan si alikua lawyer IMMMA aliyedeal na issue ya Deep Green ile nyingine (msaada kwenye tuta) :angry:
 
Yanayoshangaza:

1. Hawa vijana mazuzu kabisa, yaani m'kiti wao anajiuzulu wao hata sababu hawaijui na wala hawaulizi mpaka mkutano unafungwa.

2. Mwenyekiti badala ya kusema mkondo wa sheria utachukua mkondo wake kuhusu kughushi kwa Masauni anamwahidi kazi nyingine. Is this guy serious???????

3. Mwenyekiti anawataka wanaccm kujiandaa na mashambulizi ya tuhuma za ufisadi badala ya kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua mafisadi. Huyu mkulu anajua anachofanya lakini???[/QUOTE]

Ni kweli umenena:
Namba 1, ni tatizo ni kuwa wengi wanadhani kwa upotofu kuwa MAAMUZI na KAULI za viongozi ni LAZIMA yakubaliwe, hata kama ni MABOVU na ni kinyume na MADARAKA yao.
Namba 2, the guy is never serious. Masauni amewekwa kando ili Ridhiwani atawale vizuri UVCCM. Kudanganya umri kwenye nyaraka ni kosa la jinai, na kwa CCM na hasa UVCCM ni kitu kilichoenea sana.
Namba 3, Mwenyekiti hataki kuwachukulia hatua mafisadi kwa kuwa 'birds of the same feather fly together'.
 
nashangaa tena nitaendelea kushangaa ndg. zangu kuona Machauni wa watu, aliyepewa nafachi na MKULU WA NCHI, anaachishwa uleadership hivihivi, wajameni Chi Chi eM wamemuonea Machauni, wajameni, mbona huko Chi Chi Em kufoji ni kitu cha kawaida tu. Basi hata wale wabunge wake walio foji vyeti vya kitaaluma wawajibike, tuone kama kweli Chi Chi Em wana mean business.

anyway sijui wanajisikiaje. mambo si shwari:target::mad2:
 
Wadau ninanukuu kile ambacho kinadaiwa kusemwa na rais wetu kuhusu sakata la kujiuzulu kwa Masauni:

Nanukuu: Hata hivyo, Rais Kikwete alimfariji kijana huyo mpole na mzito kufanya maamuzi magumu na haraka, akisema kwakuwa ni makakamavu na mchapakazi atapangiwa kazi nyingine hapo baadaye. mwisho wa kunukuu (Source: Gazeti la mwananchi la leo 20 May 2010)

Jamani naomba mnisaidie huenda mimi ndo sielewi vizuri mambo haya. Hivi kama ni kweli huyu kijana amegushi umri rais anapata wapi ujasiri wa kusema atampangia kazi nyingine? Hivi ni kazi gani nyingine ambayo haiitaji mtu kuwa mwadilifu? Kama mtu ameweza kudanganya umri na hilo likajulikana na "akalazimishwa" kujiuzulu atashindwa vipi kufanya udanganyifu mwingine kwenye hiyo kazi nyingine atakayopewa? Au atawekwa kwenye kamati ya "saidia CCM ishinde" ili afanikishe udanganyifu wa kura?

Nisaidieni mwenzenu, napata shida kuamini kuwa viongozi wetu wamefikia hapo. Au nchi hii haina kabisa watu wanaoweza kuwa viongozi hivyo inabidi wale wachache waliopo tung'ang'ane nao hata wanapoonyesha upungufu mkubwa kama wa kudanganya. Ni jambo gani ambalo mtu akilifanya ktk nchi hii linamnyima nafasi ya kuwa kiongozi wa umma?
 
Ingelikuwa nchi za wenyewe tayari polisi walishaanza kumtembelea! Maswali kidogo unaachwa.....Kesho tena wanakuja! Bongo ndio kwanza...... tutampangia kazi nyingine. Nashukuru umeliona hilo mleta hoja.
 
wanasheria mnasemaje kuhusu hili kosa la masauni kughushi umri? Je anaweza kushitakiwa? na kama atatiwa hatiani, adhabu yake ni nini?

Kifungo kisichopungua miaka 4 au 9
 
Usihangaike naye huyo siku hizi namuangalia tu. Huku nikiwa na fundo la hasira kinywani mwangu. Anachemsha kila kitu.
 
Back
Top Bottom