Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Natanguliza pole zangu kwa watakaopangiwa DC ambaye amedanganya kuhusu umri wake.

Mkuu hii naiita statement ya mtanzania halisi - yaani uwape wengine pole lakini ushindwe kujipa pole kwa kuwa na mpangaji ambaye ameweza kukudanganya... no I mean kuongoza kwa miaka yote minne !

Sijui atawadanganya mambo mangapi mengine hao atakaokabidhiwa dhamana ya kuwadanganya... no I mean kuwaongoza

Kama watanzania wote tumeweza kudanganywa... no I mean kuongozwa na huyu msanii na bado tunamtaka atudanganye.....oops, atuongoze kwa miaka mingine mitano, kazi ipo ! Yaani sisi kama taifa la wadanganyika, tushangae nini ? Mkuu, tuhurumie !
 
Jamani,kwani mtu akikosea upande mmoja hawezi kufanya upande mwingine?Mimi sioni tatizo kama atapewa majukumu mengine lakini sio ya vijana...

..The same old politics, ungekuwa kiongozi wa CCM nisingeshangaa lakini CHADEMA!?..ndio maana CCM bado inaendelea kupeta pamoja na upuuzi wao kwa sababu vyama vya upinzani bado havionyeshi tofauti kwa wanachi, more of the same.
 
Nimefutalia debate ya UVCCM... nadhani tunwapa umuhimu usiostahili... Masauni na Moyo wanaumuhimu gani katka uchumi wetu. Wangekuwa Ma CEO fulani wa Kampuni zenye tija kwa uchumi wetu then tungewaza juu yao. UVCCM ni nondo waharibifu wa uchumi... kazi yao kama raisi alivyowaagiza ni kutetea na kulinda mafisadi na kugawa fedha za kifisadi wakati wa uchaguzi fullstop. Tufike mahali tuichukulie CCM kwa kiwango inachostahili kama genge la mafisadi.
 
headline_bullet.jpg
Asema alijitakia mwenyewe



Kikwete%201%2810%29.jpg

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.



Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amesema kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha mapinduzi (UVCCM), Hamad Yusuf Masauni, hakuonewa wala kufanyiwa fitina bali alijiuzulu kutokana na kudanganya kuhusu umri wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu wa jumuiya hiyo mwaka 2008.
Rais Kikwete alisema kuwa Masauni alitamka kuwa alizaliwa mwaka 1979 wakati uchunguzi ulibaini kuwa alizaliwa Oktoba 5, 1973.
Akizungumza jana jioni baada ya kufungua kambi ya wiki moja ya UVCCM kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu katika Kijiji cha Ihemi, wilayani Iringa Vijijini, mkoa wa Iringa, Rais alisema Masauni hakuwa mkweli na kwamba uamuzi wake wa kujiuzulu usingeepukika.
Alisema kuwa suala la umri sio tukio la kwanza katika UVCCM kwa kuwa kuna baadhi ya wanachama wake waliozuiwa kugombea nafasi fulani za uongozi kutokana na kuzidi umri.
Ingawa hakuwataja kwa majina baadhi ya vijana waliokumbana na kikwazo hicho, lakini mmoja wao ni Nape Nnauye, ambaye katika uchaguzi wa mwaka 2008 aliomba kugombea uenyekiti wa Taifa, lakini juna lake likaondolewa.
Mwenyekiti huyo wa CCM alisema:”Hakuna uchawi, ni kanuni na ni lazima kusimamia sheria na kanuni, hatutafumba macho.”
Rais Kikwete alisema kwa kuwa Masauni ni kijana, atatafutiwa kazi nyingine inayolingana na umri wake.
Aidha, Rais alikemea makundi ndani ya jumuiya hiyo na kwamba makundi yasiyo na tija hayana nafasi ndani ya CCM.
Alisema alisikia kuna magenge ndani ya UVCCM akiwa mbali na kwamba sio vizuri kuwa nayo kwa kuwa hayakisaidii chama hicho.
Alisema njia pekee ya kumaliza tofauti ni vikao badala ya kuunda makundi.
Masauni na Naibu Katibu Mkuu UVCCM Zanzibar, Mohamed Moyo walitangaza uamuzi wao wa kujiuzulu nyadhifa zao katika kikao cha Baraza Kuu la jumuiya hiyo mjini Iringa juzi usiku.
Kabla ya kujiuzulu, Masauni alikuwa akituhumiwa kuwa uwezo wake wa kuiongoza jumuiya hiyo ni mdogo.
Masauni na Moyo waliwasilisha barua za kujiuzulu katika kikao cha Baraza Kuu ya UVCCM baada ya vikao vya sekretarieti na Kamati ya Utekelezaji.
Awali jana, Nipashe ilipomuuliza Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, kuhusu tuhuma kwamba Masauni aligushi vyeti na kudanganya umri, Makamba alisema:
“Sijalisema mimi, hilo ni la kwako wewe. Katika chama hiki, kinachozingatiwa ni heshima na kuheshimu maamuzi yanayoamuliwa.”
Makamba alisema kuwa kitu ambacho wajumbe walizingatia ni pamoja na heshima ya chama, jumuiya yao, na familia zao.
Katika hatua nyingine, UVCCM imesema itajaza nafasi ya Masauni na Moyo ambazo zilibakia wazi kufuatia uamuzi wao wa kujiuzulu.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za CCM mkoa wa Iringa jana, Katibu wa Umoja wa CCM mkoa huo, Roda George, alisema kwa sasa nafasi hizo ziko wazi kutokana na viongozi hao kujiuzulu kwa ridhaa yao wenyewe.
Alisema kuwa katika kikao cha juzi Masauni, aliandika barua na kuomba kujiuzulu rasmi uongozi huo.
Aidha, alisema kuwa katika barua hiyo, Masauni aliahidi kutoa ushirikiano na kukitumikia chama hicho kwa moyo.
Katibu huyo alisema Masauni katika barua hiyo, alieleza kuwa alifikia uamuzi huo bila kushinikizwa na mtu yeyote.
Roda alisema ombi hilo lilipokelewa na wajumbe baada ya kutangaziwa rasmi majira ya saa nne usiku katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo.
Masauni alipoulizwa kuhusiana na kujiuzulu, alikataa kuzungumza.
Migogoro ndani ya UVCCM imekuwa ikizuka mara kwa mara wakati wa michakato ya chaguzi, zikiwemo chaguzi zake.
Mwaka 1995 wakati wa mchakato wa uteuzi wa mgombea urais kupitia CCM, UVCCM iliitisha kikao na kuwapendekeza makada kadhaa kuwa ndio waliokuwa na sifa za kuteuliwa.
Hatua hiyo iliilazimisha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kuipangua safu nzima ya uongozi wa taifa wa UVCCM.
Katika uchaguzi wa mwaka 1997 yaliibuka makundi ndani ya jumuiya hiyo yaliyowahusisha Emmanuel Nchimbi na Frank Uhahula.
Aidha, katika uchaguzi wa 2002 yalizuka makundi na mivutano ikiwa ni pamoja na kushutumiana hadharani miongoni mwa waliokuwa wakiwania nafasi ya uenyekiti.
Kadhalika, katika mchakato wa uchaguzi wa mwaka juzi, yalizuka makundi na kampeni chafu. Miongoni mwa matukio makubwa ni kuenguliwa kwa Nape Nnauye na vikao vya juu vya CCM kuengua majina ya waliogombea uenyekiti wa taifa na kuyaweka katika nafasi ya makamu mwenyekiti.
Miongoni mwa walioenguliwa katika nafasi ya uenyekiti ni Benno Malisa na Hussein Bashi wakati Masauni aliyekuwa ameomba kugombea umakamu mwenyekiti, jina lake lilihamishiwa nafasi ya uenyekiti na kuwa mgombea pekee.
Wachambuzi kadhaa wamekuwa wakiihusisha mivutano ndani ya UVCCM na mikakati ya wanasiasa ndani ya chama tawala kuitumia jumuiya hiyo nyeti kusaka uongozi wa juu wa dola.
Mvutano ulioibuka ndani ya jumuiya hiyo kabla na baada ya uchaguzi wa mwaka 2008, unachukuliwa kuwa ni mikakati ya wanasiasa kuanza mikakati ya kujipanga kutafuta uongozi wa dola katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.



CHANZO: NIPASHE
 
Kikwete%201%2810%29.jpg


Rais alisema Masauni hakuwa mkweli na kwamba... Rais Kikwete alisema kwa kuwa Masauni ni kijana, atatafutiwa kazi nyingine inayolingana na umri wake .

Kasema mtu hakuwa mkweli halafu unasema atamtafutia kazi nyingine, huyu Rais wetu sijui ana majini?
 

Kasema mtu hakuwa mkweli halafu unasema atamtafutia kazi nyingine, huyu Rais wetu sijui ana majini?

Tindikali ndugu yangu hiyo ndiyo Tanzania

JK ndiye mkuu wa nchi,kwa nafasi yake alipaswa kuiamuru Polisi imkamate Masauni na imchunguze,kwani kujaribu kughushi ni kosa la jinai na linakuwa kosa kubwa zaidi kama ulizogushi ni documents zozote genuine toka serikalini.Cheti cha kuzaliwa kinatolewa na serikali na ni kos ala jinai kukirekebisha kw asababu zozote zile uzijuazo wewe,Masauni kama akipatikana na hatia anaweza kufungwa hadi miaka 14 jela!

Sasa JK badala ya kumlaani Masauni kwa kitendo chake cha kugushi yeye anamsifia kwa kusema "ni kijana msikivu na mchapakazi na atapangiwa kazi ingine"

Masauni anapaswa kufikishwa mahakani kwa kosa analotuhumiwa kulitenda la jinai,ni mahakama tu itakayomsafisha na wala sio JK!
 
UVCCM ndio CCM ya kesho, CCM ya leo ilikuwa UVCCM ya jana; sasa tutegemee nini kwao? 'Mtoto wa nyoka ni nyoka'. Hawa vijana wanafanya wanayoyaona kwa wakubwa wao wa chama kuanzia umoja wao wa wanawake mpaka wazazi! JK hana uwezo wa kufikiri wala kumbukumbu, na wala hajishughulishi na kusoma mambo ya serikali yake!
 
Malafyale kama JK ataamua kuchukua huo uamuzi mgumu wa kuamuru polisi kaukata waliogushi nyaraka ndani ya serikali na chama , CCM habaki mtu!
 
hapo sasa wazanzibar hawatakubali kwani kwenye urais wa jamhuri wamepoteza na huku kwa vijana nako, nadhani ndio mwisho wa wazanzibar kuwa viongozi katika CCM. mambo yanaelekea kule kule walikotoka
 
mfumo mzima wa CCM pia una bidi ujiuzulu.. kwani Masauni hakujichagua mwenyewe.kumshinikiza Masauni ajiuzulu ni sawa na CCM kujivua nguo......wahenga walisema ukivuliwa nguo chutama ......lakini naona CCM imejivua yenyewe halafu inasemama watu wote waione aibu yake........Tunaelekea Wapi ?
 
Ingekuwa naamini katika nguvu za giza basi ningesema kunamkono wa mtu haiwezekani kabisa kinywa cha raisi kikatoa kauli tata kila kukicha bila hata ya kujishtukia...Waliosema JK ni Chagua la Mungu Mpoo ? na alikuwa ni mungu gani huyo maana kunamiungu mingi sana.

Atakuwa ni Beelzebuli, Mkuu wa mashetani. Maana huyu Mungu wetu wa ukweli ni MUNGU wa utaratibu. Lakini labda hii inamlinda " Ya Kaisari mpe Kaisari" "Ya JK mwachie mwenyewe JK" Ya kwet sisi watanzania tuondoke nayo nyumbani hapo Oktoba 29 zis yia!!! hapo vp!.....
 
Natanguliza pole zangu kwa watakaopangiwa DC ambaye amedanganya kuhusu umri wake. Sijui atawadanganya mambo mangapi mengine hao atakaokabidhiwa dhamana ya kuwadanganya... no I mean kuwaongoza

Kwa mujibu wa report ya uchunguzi wa mahusiano ya wanadamu wanaume wanadanganya zaidi -mara zaidi ya 1000 kwa mwaka- kuliko wanawake -mara si zaidi ya 750 kwa mwaka-(Source: TBC Jambo sehemu ya pili 22/05/2010). Ni kwanini basi tunakuwa wakwanza kumtupia jiwe Masauni, JK na wengine wakati ni sehemu yetu tu Watanzania? Tukumbuke wale watu wala hawakuchukua yale madaraka kwa risasi ni hiari yetu. So walaumiwa wa kwanza ni sisi wenyewe humu JF na wengineo. Na mwaka huu tutawapa tena despite ya makelele yoooooote ya humu ndani. Watanzania bwana, Mbona tunasubiri vitu vitoke Jupiter wakati tunaofanya maamuzi ni sisi wenyewe!!! Kama humwelimishi mwenzio akaelewa kwanini asimchague A na amchague B si kwa misingi ya chama bali uwezo wake wa kufanya kazi, na yule mtu akachagua ***** hapo nani alaumiwe!???
Lakini hatujachelewa sana tuna nafasi nyingine baada ya miezi mitano ijayo, KAZI KWETU WA-TZ!!!!
 
Hao UVCCM hawana umuhimu kwa maslahi ya Taifa letu...imejaa vijana walio-compromise taaluma zao,short sighted,hawana future wala vision ya nchi hii huko baadaye

Ni club ya wafuata upepo tu,hawajui Taifa letu linahitaji nini.Kwa kifupi wamedumaa akili..sorry kama nimewakwaza but jitazameni upya!
 
Kama Tanzania inahitaji kuwa katika nafasi decent infuture basi UVCCM ni muhimu kuangamizwa au kutumia mbinu za kijasusi kuiporomosha pamoja na chama.Kwa ajili ya maslahi ya taifa in future
 
Ridhiwani na Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Kikwete wasihusishwe na sakata la kumwondoa Masauni asema mwenyewe amejichongea



Picha ni ni katibu mkuu wa UVCCM Taifa Bw.Martine Shigella (kulia) katika ofisi za CCM mkoa wa Iringa jana na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na sakata la kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti wa UVCCM Hamad Yusuph Masauni , kulia kwake ni katibu wa idara ya uhamasishaji na chipukizi Taifa Estar Bulaya.


BAADA ya sakata la kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UV-CCM) Hamad Yusuph Masauni kuzidi kuchukua sura mpya na baadhi ya makundi ya vijana kumhusisha mtoto wa mwenyekiti wa CCM Taifa Ridhiwan Kikwete na mwenyekiti mwenyewe kuwa wanahusika katika kumwondoa Masauni katika nafasi hiyo ,utata zaidi umezidi kuibuka katika sakata hilo baada ya katibu mkuu wa UV-CCM Taifa Martine Shigella kwa mara ya kwanza kujitokeza mbele vyombo vya habari kutolea ufafanuzi juu ya mwenendo mzima wa sakata hilo na kudai kuwa Rais Kikwete na Ridhiwani wasihusishwe katika sakata hilo ambalo mhusika mkuu ni yeye mwenyewe Masauni na si mtu mwingine.

Asema mkakati wa UV-CCM ni kukiomba chama cha mapinduzi kumpitisha Rais Kikwete kuwa mgombea pekee katika uchaguzi mkuu na wanaomhusisha yeye na mtoto wake Ridhiwani na tuhuma za kumwondoa Masauni ni vizuri wakapeleka ushahidi kwake ili kuwajibishwa vinginevyo hawatamwajibisha kwa maneno ya mitaani.

“…Hatuwezi kumwondoa Ridhiwani kwa tetesi za mitaani na kama yupo mtu mwenye ushahidi wa tuhuma zake kuuvuruga umoja huo apeleke kwake ili hatua zichukuliwe ila vinginevyo itakuwa ngumu kumwajibisha” Pia katibu huyo amesema kuwa pamoja na kuwepo na watu wanaohusisha sakata hilo na mbio za uchaguzi mkuu huko Zanzibar ni kutomtendea haki kwani hata katika maelezo yake na yale ya mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Kikwete hajapata kuzungumzia hilo.

Alisema kuwa yapo maneno kuwa tuhuma za Masauni zimetoka Zanzibar ambako kuna mwanamke ambaye mume wake anataka kugombea nafasi ya juu ya uongozi huko aliondolewa katika nafasi ya uongozi ndani ya UV-CCM kutokana na fitina za Masauni jambo ambalo halina ukweli kwani hakuna kiongozi wa UV-CCM Zanzibar aliyeenguliwa nafasi yake toka Masauni achaguliwe katika nafasi hiyo.

Shigella ambaye aliongozana na wajumbe nane wa umoja huo akiwemo naibu katibu mkuu (bara) Mfaume Kizito,katibu wa idara ya uhamasishaji chipukizi Taifa Ester Bulaya, katibu wa idara ya fedha na uchumi Issa Hajji Gavu, mkuu wa utawala Augustino Mbogo,katibu idara ya usalama na maadili Suttan Mipiko ,Mohamed Nalinda na Deo Daffi ambaye ni mwasibu mkuu alitoa kauli hiyo jana katika kikao chake na waandishi wa habari katika ofisi za. CCM mkoa wa Iringa.

Alisema kuwa ndani ya UV-CCM baada ya kujiuzulu kwa Masauni na naibu katibu mkuu visiwani Mohamed Moyo hakuna mpasuko wowote na wala hakuna mpasuko unaotegemewa kutokea kutokana na vijana kuelewa vizuri suala hilo isipo kuwa UV-CCM umejipanga kuhakikisha CCM inashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu octoba mwaka huu.

Hata hivyo alisema kutokana na udanganyifu huo wa umri ambao Masauni ameufanya kuanzia sasa mkakati unawekwa kwa ajili ya kuepusha hali kama hiyo mbeleni na kuwa moja kati ya makati huo ni kuweka utaratibu wa kuhakiki vizuri umri wa wagombea na majina yao ili kupata uhalali wa wagombea wa nafasi mbali mbali.

“Tuna mikakati kabambe kupitia kamati ya maadili ili kujiridhisha na CV za wagombea na kuziba mwanya wa udanganyifu wa umri na majina ya wagombea “
Kuhusu sababu za msingi za kujiuzulu kwa Masauni Shigella aliendelea kufanya siri pamoja na mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Kikwete kueleza wazi kuwa kujiuzulu kwake ni kutokana na kudanganya umri wake .

Huku katibu huyo akiungana na katibu mkuu wa CCM Taifa Yusuph Makamba kugoma kueleza sababu za msingi za kujiuzulu kwake na kudai kuwa sababu za kujiuzulu kwake ambazo amezitoa Masauni mwenyewe ni nne kuwa amejiuzulu kwa nia njema ya kulinda heshima yake ,kulinda heshima yake ya familia yake,kulinda heshima ya chama na sababu ya nne kulinda heshima ya UV-CCM Taifa.
Hivyo alisema hizo ndizo sababu ambazo wao wanazitambua na ndizo zimo katika barua yake ya kujiuzulu na sababu ya umri haipo katika barua yake ya kujiuzulu.

“Nataka kusema kuwa ni kweli mwenyekiti wa chama Taifa Rais Kikwete alishiriki kuchuja majina ya wagombea ila nyaraka ambazo zilionyeshwa na Masauni ni zilikuwa zikionyesha anazo sifa kuwa mgombea na nafasi hiyo ….ila kama alionyesha na sasa kuja kubainika hili haituzuii kumwajibisha ila kabla ya kuwajibisha alijiuzulu mwenyewe baada ya kubaini kunyaraka nyingine halali nyumbani ila nasema alichokifanya Masauni ni ukomavu wa kiasiasa”

Kuhusu nafasi mbili alizokuwa nazo Masauni katika ujumbe wa baraza kuu la UV-CCM Taifa alisema kuwa ni kweli kabla ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa UV-CCM Taifa alikuwa ni mjumbe wa baraza aliyechaguliwa kupitia halmashauri kuu ya CCM Taifa kupitia kundi la vijana na nyingine ni ile aliyopitia UV-CCM uenyekiti wa UV-CCM Taifa.

Hivyo alisema akiwa kama katibu mkuu wa UV-CCM nafasi zinazomhusu Masauni ambazo amejiuzulu ni uenyekiti na ujumbe wa baraza kuu la UV-CCM kupitia nafasi yake ya uenyekiti na sio vinginevyo na kuwa ile nafasi ambayo aliipata kupitia chama ipo chini ya katibu mkuu wa CCM Makamba na mwenye uwezo wa kulisemea ni chama chenyewe si vinginevyo.

Shigella alikanusha madai ya kuwepo kwa ajenda ya kumng’oa Masauni kupitia kikao hicho cha baraza kuu UV-CCM Taifa ni kuwa ajenda hiyo haikuwepo na kabla na baada ya kufika Iringa ajenda kuu ilikuwa ni moja pekee ambayo ni ile ya hali ya siasa na hali ya vijana nchini .Hata hivyo alisema kuwa kabla ya Masauni kujiuzulu aliweza kukieleza kikao hicho juu ya taarifa ya kujiuzulu kwa naibu katibu mkuu (visiwani) Moyo ambaye aliandika barua yake mapema zaidi na baada ya taarifa hiyo ndipo mwenyewe alipotangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake hiyo.

Hivyo alisema baada ya zoezi la kujiuzulu kwa mwenyekiti huyo kukamilika aliyekuwa makamu mwenyekiti UVCCM Taifa Beno Malisa ndie alichukua nafasi yake kwa kuendesha kikao hicho hadi mwisho kwa mujibu wa kanuni ya UVCCM ibara ya 97(a) inayotamka wazi kuwa makamu mwenyekiti atakuwa msaidizi mkuu wa mwenyekiti wa UVCCM Taifa na atafanya kazi zote za mwenyekiti endapo mwenyekiti hayupo kwa sababu yoyote ile.

Pamoja na katibu huyo kuonyesha kugoma kuelezea sababu ya msingi ya Masauni kujiuzulu zaidi ya ile ya kulinda heshima ya familia yake na nyingine ambazo bado si chanzo kikuu cha kujiuzulu kwake ,bado aliwataka viongozi wengine wa UVCCM ambao wamedanganya umri wao kuanza kujiengua wenyewe badala ya kusubiri kuumbuliwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom