Hatimae Pedeshee Ndama akiri kutakatisha fedha

Hatimae Pedeshee Ndama akiri kutakatisha fedha

Duh! What do you "ukabaki nayo!? " simply ni kuwa Pesa itayotokana na hiyo hotel itakuwa imetakatishwa!


Ukabaki nayo meaning ukaendelea kuimiliki hoteli.

Elewa ninaejadiliana nae kasemaje. Kasema umenunua asset, hoteli, umeiuza, ndio utakatishaji. Usipoiuza?
 
Kutumia njia ya udanganyifu ili kuzihalalisha fedha zilizopatikana kwa njia haramu.

Kwa mfano:-
Unauza ngada, mapato yatokanayo na ngada unafungulia bureau de change. Sasa mapato yatokanayo na biashara ya bureau de change yatakuwa halali yenyewe pamoja na mtaji wake.

Wengine ongezeeni mifano.
Mfano mwingine ni; Unafanya ujambazi kwa kupora pesa na mali za watu,pesa unayoipata kwa njia hiyo unanunua au kujenga majumba na kuyapangisha,pesa ya kodi ya pango unayoipata toka kwa wapangaji inaonekana kama ni halali pamoja na kwamba mtaji wake haukuwa halali.Mtu anapokuja kuhoji ukwasi wako unakuwa na maelezo ya kuridhisha kwamba pesa yako ni matokeo ya kodi unayoipata kutoka kodi za pango za majumba yako (so inakuwa ngumu kuona kwa macho ya kawaida kwamba wewe ni mhalifu)
 
Maana yake ni money laundering

Kauliza maana yake sio tafsiri yake kwa kizungu. Mtu akiuliza maana ya baiskeli unajibu ni chombo cha uchukuzi chenye matairi mawili humwambii tafsiri yake in English (bicycle). Huko shuleni umesomea ujinga
 
Mfano mwingine ni; Unafanya ujambazi kwa kupora pesa na mali za watu,pesa unayoipata kwa njia hiyo unanunua au kujenga majumba na kuyapangisha,pesa ya kodi ya pango unayoipata toka kwa wapangaji inaonekana kama ni halali pamoja na kwamba mtaji wake haukuwa halali.Mtu anapokuja kuhoji ukwasi wako unakuwa na maelezo ya kuridhisha kwamba pesa yako ni matokeo ya kodi unayoipata kutoka kodi za pango za majumba yako (so inakuwa ngumu kuona kwa macho ya kawaida kwamba wewe ni mhalifu)
Kweeli kabisa!
Lakini mamlaka zikihoji mapato ya ujenzi wa nyumba hizo yalikuwaje ndipo mmiliki anajikuta anaikana mali yake.
 
Amekubali kutakatisha 1.18Bln

Adhabu kwa mujibu wa sheria hilo kosa
a) Kifungo kati ya miaka 5 kisichozid miaka 10 AU
b) Faini ya kati ya mili 100 mpaka 500

Hapo ndio nnapoipenda sheria.
Hapo kesi imeisha mkuu atalipa faini asepe zake!
 
Timu ya ndama ni kubwaa sana kuliko inavyojulikana.Hao mapedeshee miongoni mwao sijui niseme ni vipaji asilia au kuna University wamesomea.Ila habari zao uzisome kama humu tu ukija kuingia kwenye 18 zao hao jamaa ndiyo utajua ni wa aina gani.Na hawachezi madili ya pesa ndogo hao,ila vitu kama hivi siku zote mwisho mbaya. Kuisambaratisha A.Team ngumu kuisambaratisha huyu ndama hayupo peke yake.
 
Hapo kesi imeisha mkuu atalipa faini asepe zake!
Shida ni kwamba inategemea alitakatisha kutokea uhalifu upi,inaweza ikapita hukumu ya kutakatisha halafu baadae jamhuri ikampin na kesi nyingine,mathalan kama mtu alitakatisha baada ya kuwa ameuza "sembe" au ujambazi wakimrudisha kwa kesi ya "sembe"(na itauwa rahisi kama atakuwa amekiri) adhabu itakuwa ni kubwa zaidi mbali na hiyo ya kutakatisha.
 
Walimu wana kazi sana.

Maswali ya Mtihani wa Taifa wa kidato cha nne hujibiwa na wanafunzi laki tatu. Lakini mwisho wa siku division Zero, Four na Three zinakuwa laki mbili na nusu.

Kwa hiyo usinambie "watu watano wametoa majibu mbona huelewi"?

Mwingine anasema fomu ya kufungulia akaunti ndio itakufunga kwa sababu benki wanauliza pesa umepata wapi. Benki gani duniani inakuuliza umepata wapi pesa? Umetembea duniani lakini wewe? ATM machine nazo huwa zinakuhoji uki deposit pesa? Hilo jibu sio ridiculous?

And what if ume deposit pesa chafu kwenye akaunti ya mkeo, na wewe huna mkataba wala ahadi na benki hiyo kwamba utaweka fedha halali, atafungwa mkeo? Na wewe utapona?

Mwingine anasema ukinununua asset kwa pesa chafu ukaja ukaiuza ndio kosa. Kwa hiyo ukinunua hoteli ukaihodhi, ukala faida ya huduma za hoteli, sio utakatishaji?

Mwingine anasema ni kuweka benki au kuwekeza. Kwa hiyo ukiituma kwa Western Union kutoka TZ kwenda UK hujatakatisha? Hivi mnajua transactions anazoshutumiwa amezifanya Kitilya wa TRA kufanya atiwe ndani bila dhamana mpaka leo?

Haya, kwa ma definition tuliyopewa yoooote hayo, Ndama Shabani kafanya lipi kwa pesa chafu, kafungua Islamic Missonary School?
 
Kutumia njia ya udanganyifu ili kuzihalalisha fedha zilizopatikana kwa njia haramu.

Kwa mfano:-
Unauza ngada, mapato yatokanayo na ngada unafungulia bureau de change. Sasa mapato yatokanayo na biashara ya bureau de change yatakuwa halali yenyewe pamoja na mtaji wake.

Wengine ongezeeni mifano.
Asante mkuu hata Mimi ilikuwa inanipa utata kwel
 
Nakupa mfano mdogo tu " upo kitaani huna kazi wala biashara, ila gafla unapeleka madawa ya kulevya south unarud unalipwa milion mia tatu, cha kwanza huwez kaa nazo ndani pili utumiaji wake watu watauliza umepata wapi pesa? Maana hela haijifichi!
Sasa walichokuwa watu wanafanya anafungua kiduka cha kuuza nguo/boutique kisha anaweka mzigo, then anaanza kutumia fedha sasa ukimuuliza anakuambia duka la nguo linalipa sana, anachukua hela anaingiza bank mfano kwa siku 40 milion akifatiliwa na vyombo vya usalama anawaonyeshea duka la nguo kwamba ndio chanzo cha mapato yake! Kuumbe lahaula.
Na hii style kipindi cha kikwet ilikuwa common sana vuduka vya nguo vikawa vingii na watu wana hela mbayaa....ila ww ukichukua hela yako ya shamban ukawekeza unashanhaa huoni biashara
yaan umeielezea kirahisi na kivichekesho na imeeleweka![emoji2] [emoji2]
 
Back
Top Bottom