Hatimae Pedeshee Ndama akiri kutakatisha fedha

Hatimae Pedeshee Ndama akiri kutakatisha fedha

Mfanyabiashara, Ndama Shabani Hussein (Pichani katikati) maarufu kama Ndama mtoto ya Ng'ombe amekiri mahakamani kosa la kutakatisha zaidi ya billioni 1.2.

Ndama anadaiwa kuwa Februari 20, 2014 jijini Dar es Salaam, alighushi nyaraka ya kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited iliruhusiwa kusafirisha maboxi manne ya dhahabu yenye kilogramu 207 yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000.00 kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.

Chanzo: Nipashe

Nikiiangalia tena ile Live Show ya Fally Ipupa ya Dar es Salaam na kumwona Pedeshee Ndama Mtoto wa Ng'ombe jinsi alivyokuwa anamwagia Pesa tena ' Midola ' mitupu Fally Ipupa na wale Dancers wake wote pale ' Stejini ' halafu leo namwona akiwa ' Lupango ' nasema kuwa ama kweli dunia haina dhamana na ' Sifa ' ni mbaya mno na hakuna maisha mazuri kama kuishi zako tu simple life kama GENTAMYCINE kwani utakuwa na amani sana na furaha siku zote.
 
A
Amekubali kwa sababu hilo kosa halina dhamana , sasa hata kama anakataa si anaendelea kusota mahabusu tu , si bora haukumiwe ajue moja
Kwa hiyo Mkuu mtu akikubambika kesi tu kwamba umetakatisha fedha hata kama unashinda porini au shamba inabidi ukubali tu ili ufungee yaishe!! Ndicho unachomaanisha?
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Google money laundering
Laundering linatokana na laundry, sehemu ya kufulia nguo zitakate. Ni slang ya kizungu kuwa hela ambayo siyo halali ni ni hela ambayo ina uchafu, haikupatikana kihalali. Hela chafu na sheria inaikataza. Ina adhabu kubwa. So, unachofanya unaifua, kuitakatisha ili sheria isikuandame. Unaiweka kwenye biashara halali ionekane uliipata kwa njia halali! then from hiyo biashara halali unaizalisha bila kuandamwa na sheria.... something of tha nature ( though in a nutshell for a beginner)
Mchambuzi ongeza nami huwe siyaelewi vizuri haya mambo...
 
Kwa hiyo Mkuu mtu akikubambika kesi tu kwamba umetakatisha fedha hata kama unashinda porini au shamba inabidi ukubali tu ili ufungee yaishe!! Ndicho unachomaanisha?
Ushahidi pia umembana
 
Naombeni mnisaidie maana ya hili neno "kutakatisha fedha"
Laundering linatokana na laundry, sehemu ya kufulia nguo zitakate. Ni slang ya kizungu kuwa hela ambayo siyo halali ni ni hela ambayo ina uchafu, haikupatikana kihalali. Hela chafu na sheria inaikataza. Ina adhabu kubwa. So, unachofanya unaifua, kuitakatisha ili sheria isikuandame. Unaiweka kwenye biashara halali ionekane uliipata kwa njia halali! then from hiyo biashara halali unaizalisha bila kuandamwa na sheria.... something of tha nature ( though in a nutshell for a beginner)
 
Naombeni mnisaidie maana ya hili neno "kutakatisha fedha"

Kutakatisha Fedha ni utaratibu wa kihalifu kufanya Fedha zillizopatikana kihalifu kuingia kwny Mfumo na Mzunguko rasmi wa Fedha na kuonekana Kama ni Pato halali!

Mfano umepata Fedha unanunua Nyumba halafu baada ya Muda unaiuza na kumuelekeza alienunua afanye Malipo kwny Account yako Bank ikieleza ni Fedha za Mauzo ya Nyumba hivyo Fedha yako itatambulika ni malipo yako halali ya Mauzo ya Nyumba Kumbe source yake sio hiyo!

Wengine wanajifanya kujenga Hotel au Guest House Kama Jambazi anaemiliki zile atajifanya Hotel zake zipo busy kwny Kupata Wateja hivyo kila siku watakuwa wana deposit bank Mamilion Kumbe yamepatikana kwa Njia haramu lakin wanajifanya ni Mapato ya Biashara zao
 
Kutumia njia ya udanganyifu ili kuzihalalisha fedha zilizopatikana kwa njia haramu.

Kwa mfano:-
Unauza ngada, mapato yatokanayo na ngada unafungulia bureau de change. Sasa mapato yatokanayo na biashara ya bureau de change yatakuwa halali yenyewe pamoja na mtaji wake.

Wengine ongezeeni mifano.
Umemaliza sina cha kuongeza.
 
Naombeni mnisaidie maana ya hili neno "kutakatisha fedha"
Money laundering.
kuingiza pesa chafu katika mzunguko halali
Pesa chafu ni pesa ya wizi,utapeli,madawa ya kulevya halafu uingize katika akaunti yako,au ukanunulie mali kama nyumba au gari.
Sheria hii imewekwa kuwabana majizi kama huyo Ndama,ili akinunua nyumba nayo itaifishwe au akiingiza kwenye akaunti hata kama ina mkopo itaifishwe
 
Back
Top Bottom